CHADEMA/UKAWA: Uwekezaji usiotabirika

Wanajukwaa uchaguzi wa mwaka huu una changamoto kubwa kwa chama tawala na wapinzani.

Tumeambiwa kuwa leo lowassa anachukuwa fomu ya kugombea urais kwenye ofisi ya makao makuu ya chadema ufipa DSM, swali, je anachukua fomu kupambanishwa na nani? kama kuna kushindanishwa kwa mchujo je atakuwa tayari kukubali matokeo endapo yatakuwa tofauti na ilivyotegemewa? na kama inajulikana wazi kuwa yupo upinzani ili kupeperusha bendera ya urais kupitia ukawa kwanini achukue fomu?
Mkuu, hii ni "deal" imeishapangwa na Mbowe, Lowassa ndiyo mgombea urais wa Chadema hamna watu wa kumkata hayo ni makubaliaano kinachofanyika sasa hivi ni utelekezaji tu.

CHADEMA imetumia miaka tisa ikimwandaa-Dk. Slaa na familia yake-katika maisha ya taasisi ya Rais wa Tanzania kutokana na trends za kisiasa nchini. Ametembelea nchi nyingi duniani kujifunza kazi za Rais na mahitaji ya nchi. Amehudhuria mikutano na makongamano yenye shabaha ya kupanua mitazamo na fikra za kiutendani katika ofisi ya Rais.Mpaka wiki iliyopita, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, Ezekiah Wenje alinukuwa na Stav TV akisema Kamati Kuu ya CHADEMA ilimpitisha Dk. Slaa kuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA.

Kama hiyo haitoshi, alikuwa mbioni kutangazwa kuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CHADEMA au UKAWA.Matarajio na ndoto yake imefutika ghafla-baada ya ujio wa Edward Lowassa kwenye ulingo wa siasa za upinzani na kukabidhiwa kadi ya CHADEMA, na kama hiyo haitoshi, Edward Lowassa kimantiki anamtaka apeleke vielelezo vya ufisadi wake mahakamani au akae kimya!Kwa sasa hata wale waliokuwa wanadai ni Rais wa moyoni, hawaonekani tena!This is a sad ending for Dk. Slaa and his family!Kweli siasa hazina huruma na mbaya zaidi, hazina rafiki wa kudumu na adui wa kudumu!Politics is a brutal business!Ama kweli, tenda wema uende zako, usisubiri shukrani!.

Dr.Slaa hana sauti mbele ya Chadema yeye mwenyewe alikaribishwa tu inabidi afuate maagizo ya Mbowe, zaidi ya hapo atatangazwa msaliti, kaambiwa akagombee ubunge Karatu ndiyo maana yule mbunge wa Karatu safari hii kajitoa kugombea kumpisha Dr.Slaa.
 
Hippocratesocrates
Tunaposema investment yenye risk tunamaanisha baadhi ya uliyosema.

Uwekezaji wa wapinzani umechukua muda mrefu

Je, kulikuwa na tathmini ya kutosha ya mwekezaji vs time and resources zilizotumika?

Kulifanyika risk assessment ya kutosha?

Sidhani kama hili lilitegemewa. Na hapa ndipo naposema kama kuna jambo/mambo hayakutarajiwa lakini yametokea(pengine kutokana na historia) ilifaa kukaa chini kutafakari kwa kina kabla ya kudhani 'Fursa ndiyo hii'

Unajua waswahili husema "Si kila king'aacho ni dhahabu", Sidhani na kama tathmini ilifanyika ilikuwa ya kutoa majibu wanayotaka na si uhalisia. Ninaamini hili jambo ni kubwa kuliko lionekanavyo na lidhaniwavyo.
 
Nguruvi3;

Wapinzani rasmi Tanzania hawana nguvu. Wapinzani rasmi nikiwa na maana wale waliokuwa kwenye vyama viliyosajiliwa.

Naomba nilielewe kitu kimoja. Kutokuwa na nguvu haina maana kuwa viongozi wa vyama hivyo hawafanyi juhudi. Wanafanya juhudi za kutosha sana. Lakini hili wapate nguvu ni lazima sehemu kubwa ya umma ikubali kuwafuata na kusimama nao kidete.

Nimerudi kutoka Tanzania. Pima joto zangu zinaonyesha kuwa personality za watu na sio juhudi za yale wanayosema au kutenda ni sehemu kubwa ya siasa za Tanzania.

Kwa mfano,tunapiga longolongo kwenye nafasi ya uraisi. Lakini ukichuguza jinsi maendeleo ya kampeni za uchaguzi nafasi za ubunge zinavyoendelea, utaona watu wanaopitia CCM wanapoteza pesa nyingi wakati hakuna gharama zozote kugombea kupitia upinzani.

Gharama alizotumia Lowassa kupata nafasi CCM zilikuwa nyingi wakati hatumii gharama yoyote wa kupitia CDM/UKAWA. Na anachokileta CDM ni personality yake lakini sio track record.
 
Kuna mantiki na yale unayosema kama siasa ingekuwa static and stable system au kitu kinacho tabirika. Ukweli wa mambo siasa follows chaotic behavior. Hivyo ni lazima kwa vyama upinzani kutumia nafasi zinazojitokeza.

Miaka minne iiyopita, CDM walitegemea uchaguzi kufanyika kwa kutumia katiba mpya. Katiba hiyo labda ingeruhusu mgombea huru. Kwa mtaji wa mgombea huru, Lowassa asingejiunga na chama cha upinzani. Angekuwa mgombea huru ambaye angegawa kura za CCM na kutoa nafasi kwa CDM.

Kama Lowassa angepeperusha bendera ya CCM, CDM wangetumia Richmond na kashfa kuigawa CCM na DR. Slaa angekuwa mpinzani wa kutosha.

Wapinzani ni lazima wakuze na kudumisha capabilities zao. Ni lazima mtu yoyote anashika nafasi ya juu awe presidential material. Hivyo sioni sababu kwanini unashangaa Dr. Slaa kuandaliwa. Je wewe ulitaka akaye kishambashamba? Hakuna mtu aliyeandaliwa kwa gharama kubwa kama Membe.
 
Ni vema umeliona hili ambalo wengi either hawajaligundua ama kwa makusudi hawataki kulisemea.

Tunapaswa kutambua kuwa CHADEMA/UKAWA wameingia katika mtihani ule ule ambao kwa muda sasa tangu mfumo wa siasa za vyama vingi uanze CCM imekuwa ikikabiliana nao. Hii ni kuingia katika uchaguzi kwa changamoto kwanza ya kujisafisha then kuomba kura kwa mara moja. Kwa haya yaliyotokea na yanayoendelea kutokea shughuli pevu imehamia upande wa wapinzani ambao ghafla wanaonekana ni kigeugeu hivyo hawawezi kuaminika na mbaya zaidi muda si rafiki tena. Ukifanya comparison analysis utaona kuwa CCM wako safe side zaidi ya CHADEMA/UKAWA katika uchaguzi wa mwaka huu.

Kwa hali hii na kwa kadri niwajuavyo watanzania basi uamuzi wao ni ule wa heri zimwi likujualo. Kwangu mimi CCM wanawajua zaidi wapiga kura wa Tanzania kuliko wapinzani ambao ni kama vile wanashiriki siasa za nchi ya ugenini.
 
Mkandara,

..lakini wewe ulishapata kusema kwamba ukawa watashindwa ikiwa watamsimamisha Dr.Slaa. sababu ulizotoa ni kwamba cuf hawawezi kumpigia kura Dr.Slaa.


..mimi nashangaa leo umebadilika na kuwa mtetezi mkubwa wa Dr.Slaa.

Jokakuu;

Ngoja nikuulize. Je unaunga mkono hatua za CDM kama strategic move au in a long term we can bet that Lowassa is a game changer?
 
Nguruvi3,
Mkandara #12 Kwamba kuna ushahidi na anacheza na upanga, sidhani kama upo ushahidi wa kutosha
Hata hivyo, alipokuwa waziri mkuu alikula kiapo cha nafasi hiyo ikiwa ni pamoja na kutunza siri za serikali.

Hofu, akiendelea kuongea bila wanasheria kumshauri, hoja ndogo kama hii inaweza kutumika katika 'tech knock out' hapo ndipo tunaposema uwekezaji huu ni risk na usiotabirik
hakuna kiapo cha kulinda siri za UFISADI na kibaya zaidi huyu ndiye Fisadi haswa akiitwa PAPA la baharini ama tumuulize Dr. Slaa alikuwa na maana gani kuliweka jina lake katika list of Shame! Na kama mnaweza kumsafisha Lowassa basi bila shaka hata JK msafi na CCM wasafi kwani sio nyie mlokuwa mkilia na Nape CCM wajivue magamba? hao magamba kina nani? Leo feza ya Rostam ndio imekuwa mkombozi wa kuinunua IKULU! - Ati Regime change? jamani kumbukeni maneno ya mwalimu bado yapo sana kichwani mwa wananchi haswa mwaka huu hotuba zake zimetembea sana mitandaoni na karibu zote zilimgusa mtu kama Lowassa na kundi lake.

Halafu nyie Chadema hamna hata chembe ya aibu kabisa, yaani kusema kweli nimewatoa maanani kabisa. Huyu Lowassa ndiye alikuwa Mwenyelkiti wa kamati ya bunge ya USALAMA.,wakati wake Chadema wamepigwa na polisi wamedhalilishwa kwa kila baya na hakuna hata siku moja huyu mtu kaingia Bungeni kutaka uchunguzi ufanywe ama tume iundwe kuchunguza kupigwa kwa Dr.Slaa ama wanachama wa Chadema wengine waliuawa chini yake akiwa mwenyekiti, leo kweli mnakuja mkumbatia yule yule!. Mko tayari mkumpaka Zitto na kamati yake alofanya mambo mazito kwa maslahi ya Taifa aonekane mbaya halafu huyu nduli ndiye mwokozi wenu? Mungu pitishia mbali kabisa! Still ile Picha ya Dr.Slaa na mkewe na mauaji ya Arusha imejaa ninayo kichwani..

Poleni sana na sijui mtaweza vipi kumtetea katika majukwaa maana watu watataka kujua ule Ufisadi wake umefia wapi? maana fisadi sio lazima awe mwizi ama mtaka rushwa (hongo) bali mharibifu..Na kama alishingiziwa Je, nyie mnao ushahidi? isiwe tena hadith zile zile kuwa ati amri ilitoka juu wakati yeye ndiye alokuwa juu mwaka mzima na miezi minane yote ya Utawala wa mwanzo wa JK na sote tunajua kwamba Lowassa ndiye alikuwa kama rais wa nchi hii akiwafukuza hadi makatibu wakuu, wakurugenzi na hata kuvunja mikataba ya kitaifa leo iwe JK ndiye alokuwa na deal la Richmond halafu ajisifie Lowassa!.

Poleni sana rangi zenu haswa zimeonekana na bila shaka CUF na NCCR wamekubali ili kuuweka uwanja sawa na kuanzia mwaka kesho Chadema, CUF na NCCR wote watakuwa wachovu kila mmoja atamhitaji mwingine (Kwa sisi tunaoona mbali). Na read my lips.. Lowassa atashindwa vibaya vibaya na UKAWA kwa ujumla watapoteza majimbo kuliko jumla waloipata mwaka 2010..
 
Mkandara,

..lakini wewe ulishapata kusema kwamba ukawa watashindwa ikiwa watamsimamisha Dr.Slaa. sababu ulizotoa ni kwamba cuf hawawezi kumpigia kura Dr.Slaa.


..mimi nashangaa leo umebadilika na kuwa mtetezi mkubwa wa Dr.Slaa.
Nilisema hivyo kweli lakini kushindwa kuna kipimo maana hapakuwa na uwezekano wowote wa UKAWA kushinda uchaguzi huu baada ya kuvurunda toka mwanzo kutoungana. nadhani nilieleza kwa kirefu huko nyuma kwa nini UKAWA hawawezi mkushinda uchaguzi huu..Ila kuna unafuu wa kupata japo wabunge wengi..

Fikria kitu kimoja, kwa dhana yenu wenyewe japokuwa miye nilisema UKAWA hawawezi kushinda uchaguzi huu - Period. Nanyi mkaweka tumaini na tumaini lenyewe ni kwamba hakuna mgombea anayeweza mshinda Dr.Slaa isipokuwa Lowassa!. Okay, sasa ikiwa CCM wamemtupa nje Lowassa na kumweka Magufuli, ina maana Dr.Slaa hakuwa na mshindani tena saizi yake hivyo nilitegemea pengine yale matumaini yenu mngeyatumia maana Lowassa katupwa nje. sasa watupe sababu ya kumtupa nje Dr.Slaa basi, utasikia wengine wakidai kuwa kazeeka, ni mgonjwa, Slaa ni mzoga kisiasa hii toka lini? Yaani Lowassa ana afya bora kuliko dr. Slaa..Ama kweli Chadema kwa UNAFIKI hawajambo!

Ghafla wakamchukua Lowassa ambaye mimi miaka yote husema Lowassa hawezi kuwa rais wa nchi hii hata kidogo. Huyu mtu anaopogopwa kwa sababu ya watu walokuwa nyuma yake ( Kundi lake la usalama) na nguvu ya feza alokuwa nayo kama SCARFACE! na ndicho alichotumia kutaka kununua IKULU kupitia Chadema. Haya ni makosa mengine makubwa ambayo bora Dr.Slaa angeweza kusimama na kura chache za wananchi walompenda ukawaacha CUF ambao sii wengi kihivyo lakini tungepata ushindani mzuri kuliko Lowassa, haswa kwenye wabunge.

Ikumbukwe mwaka 2010 Chadema walitumia feza kidogo sana ukilinganisha na CCM na waliweza kushinda majimbo mengi tu na hata Dr.Slaa kufanya vizuri zaidi ya ilivyotangazwa ila mchezo mkubwa ulifanyika. Na kilichowapa kura Chadema ilikuwa kuibomoa CCM kisiasa, wananchi waliyataka kweli mageuzi wakaweka matumaini kwa Dr, lakini safari hii utaibomoa vipi CCM wakati itabidi kuna baadhi ya maneno UKAWA wayaweke kando? Huwezi kuzungumzia mfumo tawala pasipo kumtaja Lowassa alokuwa Waziri mkuu na baadaye Mwenyekiti wa bunge kamati ya USALAMA and he did nothing hata to prevent vifo vya Albino!

Uliwahi kumsikia Lowassa Bungeni? ati maamuzi magumu ni maamuzi gani mnayoyafahamu alowahi kuyafanya ya aina hiyo on record! Ni sifa gani basi alokuwa nayo Lowassa ambayo mtaweza kuitumia kumtangaza! kama ni mchapakazi hata huyo Magufuli mchapakazi na hamuwezi kwa namba - he can prove!.
 
Mkandara #28 ni vema kuwa objective kuliko innuendos

Tunajadili mustakabali wa taifa hili si kwa ajili yetu bali vizazi visivyojua nini kinaendelea

Hakuna siyejua taifa limekwama wapi na nani yupo nyuma ya mkwamo huo

CCM kurudi madarakani kuendeleza uhuni wa serikali na Bunge ni jambo la kusikitisha

Kudhoofu kwa upinzani kutatupa yale yale ya mtu asiyejua kwanini sisi ni masikini

Itatuzalishia Makkindaa's wengi kiasi cha kuwa taifa la wendawazimu

Ukifanya analysis yako si lazima ipingwe au ikubaliwe, na una haki ya kuwa biased au impartial, muhimu ni kujenga hoja na kuzisimamia kwa weledi, mantiki na hekma

Ndio maana tupo hapa
 
Jokakuu;

Ngoja nikuulize. Je unaunga mkono hatua za CDM kama strategic move au in a long term we can bet that Lowassa is a game changer?

..nawaunga mkono chadema.

..ila sina uhakika kama Lowassa ataweza kuleta ushindi kwa nafasi ya uraisi.

..wanadai uamuzi huu wameufanya based on research iliyofanywa na wataalamu wa mambo ya uchaguzi including pollsters.

..kwa kweli inabidi cdm/ukawa wapige hatua kubwa zaidi kuliko hapa walipo.

Nb:

..pollsters wakishaingia ktk chama hupelekea kufanyika kwa maamuzi ambayo yanaweza yasiwafurahishe baadhi ya wanachama, especially wale wakereketwa.
 
Nguruvi3,hakuna kiapo cha kulinda siri za UFISADI na kibaya zaidi huyu ndiye Fisadi haswa akiitwa PAPA la baharini
..
Mkuu , kwavile umekuja ukiwa na prejudice, umekosa pointmuhimu sana.

Kuna mipaka ya viongozi kuongea. Kiapo kina maana yake namoja ni hiyo ya kutoongelea baadhi ya mambo hovyo bila kujali ni kitu gani

Hakuna mtu anayesema mambo ya serikali yasioongelewe, lakinikuna mipaka ambayo inaweza kutumiwa vizuri au vibaya. Tumeonyesha tu mfano

Hivyo, elewa mada, elewa hoja za wenzako, zijadili kwamuktadha wake na si kupandikiza maneno au kuyageuza
Simple as that
 
..nawaunga mkono chadema.

..ila sina uhakika kama Lowassa ataweza kuleta ushindi kwa nafasi ya uraisi.

..wanadai uamuzi huu wameufanya based on research iliyofanywa na wataalamu wa mambo ya uchaguzi including pollsters.

..kwa kweli inabidi cdm/ukawa wapige hatua kubwa zaidi kuliko hapa walipo.

Nb:

..pollsters wakishaingia ktk chama hupelekea kufanyika kwa maamuzi ambayo yanaweza yasiwafurahishe baadhi ya wanachama, especially wale wakereketwa.
Mkuu siasa za Tanzania ni ‘fluid’ sana. Analysis inawezakutoa majibu tofauti na hali halisi on the ground.
Hao wakereketwa ndio tunawaita ‘base’ ni core ya chamachochote na sifa yao, ndio ‘infrastructure’
Inapotokea wakawa upset ni sawa na kuwa na meli nzuri sanatena kubwa , injini zake zikiwa hazifanyi kazi
Pollster sijui kama ilifanya analysis ya kutosha. Hili sijambo la namba tu, nadhani lipo zaidi ya hapo
 
Wanaduru ninatoka nje ya mada kidogo..

Habari za uhakika hali ya mambo si nzuri kati ya Dr. Slaa, Mbowe na Lowassa. Kama zisipofanyika jitihada za hali na mali uwezekano wa Dr. Slaa kuachia nganzi ni mkubwa.

Ila kwa vile ndani ya Chadema kuna watu wenye busara na Dr. Slaa ni mtu mwenye busara hivyo ni mategemeo yangu kuwa hii hali ya sintofahamu wataisawazisha.

Ndugu wana duru Taifa letu linapita katika kipindi kigumu, ni kipindi ambacho si wanaccm au wanaukawa au vyama vingine wanafahamu ni lipi litatokea kesho.

Mbowe na viongozi wengine angalieni Chadema hisipasuke kwa ajili ya Lowassa.. Uwamuzi wenye hekima na busara unatakiwa kwa wakati huu ila kumbuka Dr. Slaa ni muhimu katika Chadema kuliko Lowassa maana bila Chadema imara Lowassa hasingetia mguu huku na Chadema Imara imetokana na mchango mkubwa na Dr. Slaa.
 
Wanaduru ninatoka nje ya mada kidogo..

Habari za uhakika hali ya mambo si nzuri kati ya Dr. Slaa, Mbowe na Lowassa. Kama zisipofanyika jitihada za hali na mali uwezekano wa Dr. Slaa kuachia nganzi ni mkubwa.

Ila kwa vile ndani ya Chadema kuna watu wenye busara na Dr. Slaa ni mtu mwenye busara hivyo ni mategemeo yangu kuwa hii hali ya sintofahamu wataisawazisha.

Ndugu wana duru Taifa letu linapita katika kipindi kigumu, ni kipindi ambacho si wanaccm au wanaukawa au vyama vingine wanafahamu ni lipi litatokea kesho.

Mbowe na viongozi wengine angalieni Chadema hisipasuke kwa ajili ya Lowassa.. Uwamuzi wenye hekima na busara unatakiwa kwa wakati huu ila kumbuka Dr. Slaa ni muhimu katika Chadema kuliko Lowassa maana bila Chadema imara Lowassa hasingetia mguu huku na Chadema Imara imetokana na mchango mkubwa na Dr. Slaa.
Alinda
Wamefikaje katika hatua hiyo kama si kutawaliwa na maamuzi ya pupa na tena yasiyo shirikishi? Kwa akili ya kawaida tu hilo la kuketi na kuridhiana lilipaswa kufanyika kabla na si sasa. Wengine tunafikia hatua ya kuwaogopa hawa watu maana tunapata shaka hatima ya nchi itakuwaje kwa uongozi wa hili kundi na maamuzi ya namna hii. Hivi think tank ni kina nani haswa huko?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu siasa za Tanzania ni ‘fluid’ sana. Analysis inawezakutoa majibu tofauti na hali halisi on the ground.
Hao wakereketwa ndio tunawaita ‘base’ ni core ya chamachochote na sifa yao, ndio ‘infrastructure’
Inapotokea wakawa upset ni sawa na kuwa na meli nzuri sanatena kubwa , injini zake zikiwa hazifanyi kazi
Pollster sijui kama ilifanya analysis ya kutosha. Hili sijambo la namba tu, nadhani lipo zaidi ya hapo

..kuna kitu nadhani wachangiaji wengi wa hapa JF hatukielewi.

..bado hatuelewi kwanini ccm inashinda uchaguzi tena na tena.

..cdm imeendesha kampeni dhidi ya rushwa, dhuluma, ufujaji, na ufisadi, kwa miaka 10 sasa, but they really dont have that much to show for it.

..bado hakuna uhakika wa ushindi, pamoja na kwamba kampeni hiyo imedumu kwa miaka 10+ sasa.

..kwa hiyo this time nimeamua kuangalia huu muelekeo mpya utaifikisha wapi cdm. I hope ushauri waliopata ni mzuri na watafikia malengo yao ya kushinda uchaguzi.

Cc Zakumi
 
Last edited by a moderator:
Wanajukwaa uchaguzi wa mwaka huu una changamoto kubwa kwa chama tawala na wapinzani.

Tumeambiwa kuwa leo lowassa anachukuwa fomu ya kugombea urais kwenye ofisi ya makao makuu ya chadema ufipa DSM, swali, je anachukua fomu kupambanishwa na nani? kama kuna kushindanishwa kwa mchujo je atakuwa tayari kukubali matokeo endapo yatakuwa tofauti na ilivyotegemewa? na kama inajulikana wazi kuwa yupo upinzani ili kupeperusha bendera ya urais kupitia ukawa kwanini achukue fomu?
Hoja nzuri sana ambayo wengi hawaelewi kwanini tunasema lipo tatizo.
Hata kama watu wanakataa, tatizo lipo

Huko nyuma tetesi zilipoanza, tulisema Lowassa kama Mtanzania ana haki ya kujiunga na chama chochote cha siasa
Hakuna chama chenye haki ya kumkataa bila sababu za msingi, kufanya hivyo ni kuua demokrasia

Baada ya kusema hayo, EL akienda kama mwanachama mwingine, chama chohote atakuwa na haki ya kugombea nafasi

Hapo ndipo Wapinzani (Ukawa) walipocheza fyongo. Leo angekuwa mwanachama , angechukua fomu kama kama mwanachama mwingine na wanachama ndio wangeamua kwa njia ya ishiriki na ushindanishi.

Kupitia njia hiyo kungekuwa na kile kinachoitwa maridhiano na ndipo umoja ungetawala

Kwa hali ilivyo, inaonekana tayari makubaliano yapo miongoni mwao.

Ikumbukwe kuwa uendeshaji wa chama ni 'business' na inahitaji Business plan.

Moja ya misingi ya business plan ni ushiriki wa wadau' stake holder'
Ndipo tunarudi kwenye hoja ya je, business plan yao ilizingatia hayo?

Kama haikuzingatia, ndio hasa tunachosema 'high risk investment'
 
Wanaduru ninatoka nje ya mada kidogo..

Habari za uhakika hali ya mambo si nzuri kati ya Dr. Slaa, Mbowe na Lowassa. Kama zisipofanyika jitihada za hali na mali uwezekano wa Dr. Slaa kuachia nganzi ni mkubwa.

Ila kwa vile ndani ya Chadema kuna watu wenye busara na Dr. Slaa ni mtu mwenye busara hivyo ni mategemeo yangu kuwa hii hali ya sintofahamu wataisawazisha.

Ndugu wana duru Taifa letu linapita katika kipindi kigumu, ni kipindi ambacho si wanaccm au wanaukawa au vyama vingine wanafahamu ni lipi litatokea kesho.

Mbowe na viongozi wengine angalieni Chadema hisipasuke kwa ajili ya Lowassa.. Uwamuzi wenye hekima na busara unatakiwa kwa wakati huu ila kumbuka Dr. Slaa ni muhimu katika Chadema kuliko Lowassa maana bila Chadema imara Lowassa hasingetia mguu huku na Chadema Imara imetokana na mchango mkubwa na Dr. Slaa.
Alinda, tunafahamu watu hawapendi kusikia ukweli, lakini ukweli una tabia moja, hujidhihiri wakati ukitimia
Hili ni suala linalohusu utaifa na hatma yetu sote, lijadiliwe kwa uwazi na ukweli ili tusijsononeka tutakaposikia watu hawajui kwanini sisi ni masikini

Naweza kusema CCM wapo wodini wanaendelea na matibabu ya dawa za maumivu.
Kama ni jeshi basi wapo katika hatua inayoitwa 'mobilization' Pamoja na majeraha waliyo nayo, lakini wanapumua

Ukawa wapo kati disarray. Muda na rasilimali haziwapi nafasi ya mobilisation na kurudi katika uwanja wa mapambano wakiwa imara. Hawakujifunza , hawakuisikiliza
 
Yale yaliyoitokea ccm ndio yanaanza kuinyemelea cdm. Kuna kipindi baadhi ya watu walikuwa wanasema mtandao wa kisiasa wa EL ni mkubwa kiasi kwamba endapo ccm itamuweka kando kwenye kupeperusha bendera ya urais basi ccm ingekuwa katika wakati mgumu sana kisiasa hasa kwa kile kilichoitwa ni mpasuko wa chama utakaopelekea kuvunjika vipande vipande hatimaye kushindwa kwenye uchaguzi mkuu huu wa oct 2015.

Madai yaliyokuwa yanatolewa ni lawama ya kwa viongozi wa ccm kutochukua hatua ya kumdhibiti EL mapema, matokeo yake ndio yanaonekana sasa japo kuna dalili za ccm kutotikisika kwa kile kinachoonekana ni mgogoro unaoweza kujitokeza muda wowote ndani ya cdm/ukawa hasa kutokana na kutoridhishwa na ujio wa EL kwenye chama chao na kupewa ridhaa ya kupeperusha bendera ya kuwania urais huku akiwa na tuhuma za ufisadi.

Tayari kumekuwa na tetesi zinazotolewa na baadhi ya watu hasa walioko cdm/ukawa kuwa Dr.slaa na mnyika wamesusa kushiriki shughuli za chama kwa sababu ya uwepo wa EL ambaye walikuwa mstari wa mbele kumtuhumu kuwa ni miongoni mwa mafisadi papa walioufirisi nchi, hivyo hawataki kula matapishi yao na kuonekana vigeugeu.

Sasa lile waliloambiwa ccm kuwa wakimsimamisha kugombea urais EL itakuwa ni dhida na wasipomsimamisha pia itakuwa ni shida limeanza kuonekana cdm/ukawa kwa maana tayari wamempokea EL na kukiri kuwa waliibiwa fikra na kwamba EL ni mtu safi wakati ccm wanasema kuwa wamemtosa kwa kuwa na tuhuma za kimaadili.

Upepo umeanza kuwageuka wapinzani na hawana chaguo lingine maana kumfukuza itawaletea shida na akiendelea kuwepo itakuwa ni shida pia.

Hapa kinachoonekana ni kuwa tatizo hasa lipo kwa cdm kwani wakati viongozi wake wakimsema EL kuwa ni fisadi EL yeye alikuwa kimya hivyo kauli ya juzi iliyorolewa na EL kuwa mwenye ushahidi wa tuhuma za ufisadi aende mahakamani ni kuwafunga kamba akina slaa na mnyika ambao hadi sasa hawajatengua kauli zao.

Je uwepo wa Dr.slaa na mnyika nje ya cdm/ukawa kutaleta matokeo gani kwa wapinzani wanategemea kushika dola baada ya uchaguzi kuisha na matokeo kutangazwa?

Binafsi naona ujio wa EL cdm/ukawa umewafunga kamba miguu na midomo ili wasiweze kushika wala kuongea. Dr. slaa na mnyika wakiendelea kuwepo cdm ni lazima kutakuwa na tatizo tu hasa wakati wa kampeni maana watatakiwa kula matapishi yao ili kuuaminisha umma kuwa mtu waliyrmtuhumu ni safi kitu ambacho ni kigumu kuiaminisha jamii, vile vile wakitoka cdm/ukawa mambo yatakuwa vile vilr tena maana kutakokea mgawanyiko utaopelekea kusambaratika kwa chama .na hatimaye umoja wao wa ukawa jambo ambalo litasababisha ccm ishinde bila kupata upinzani mkali.

Pia dalili za EL kuwekewa pingamizi la kugombea urais linaweza kuwepo kutoka kwa watu kama mtikila ambaye alithubutu kusema kuwa ataenda kufungua kesi ya kupinga EL kuwania urais kwa kuwa ana tuhuma za ufisadi kama ccm na baadhi ya wana cdm/ukawa wanavyosema, je ikitokea akawekewa pingamizi na kuzuiwa asigombee cdm/ukawa watafanya nini? kwa kuwa waliamini kuwa bila EL hawataweza kuingia ikulu watakubali kushindwa mbele ya ccm? na kwa kumsimamisha EL wako tayari kukabiliana na mpasuko wa ndani ya chama?

Hoja iliyowabeba wapinzani ndio itakayowashusha, kama sio tuhuma za ufisadi kwa baadhi ya makada wake wapinzani wasingepata hoja ya kuwaaminisha wananchi kuwa ccm haifai.

Viongozi wa cdm/ukawa hawana muafaka wa pamoja kati yao na EL kwa sababu kila upande unataka kumtumia mwenzake kama ngazi kufanikisha malengo yake

EL anachotafuta ni urais tu huku cdm/ukawa wakitafuta fursa ya kushinda tu kwa kutumia mtu yeyote. Kila mmoja anamuhitaji mwenzake kwa maslahi binafsi. Makubaliano ya aina hii hayadumu kwa sababu kila mmoja anaangalia fursa iliyopo ni kwa namna gani atanufaika kwa mwenzake.
 
Tuanze na kwenye red: Unaamini kwa sasa Wapinzani wana nguvu? Ndani ya week mbili Lowassa kabadili karibu kila kitu - unchallenged! Huoni kama sasa ni mfalme?

Kwenye blue: Ni kweli hatumii gharama yoyote CDM/UKAWA?
 
Back
Top Bottom