CHADEMA, uislam na waislam!

Status
Not open for further replies.
Mmmmhhhh haya bana
 
Wadau

kama mngetumia walau chembe ndogo ya hekima na busara mjadala huu ungekuwa na maana.

Kila mmoja wetu shulti aheshim imani ya mwingine pia kuheshim uwepo wa wasiomin (wapagani)

Watanzania wana dini na iman zao. Lazima uislam uheshimiwe, lazima ukristu uheshimiwe, lazima imani zingine pia waheshimiwe.

Kuchangia mjadala kwa kejeli kwa iman yoyote ni kumkosea mungu na kuwakosea adabu watanzania wanaoamin na wasiomini.

Utu wa mtu ni kauli na matendo yake, hivyo nidham na utulivu unahitajika katika kujadili mambo yanayohusu imani za watanzania.
 

ahaa ha haaa! yule mama mkuu wa wilaya mfuga kitimoto maarufu pale mbezi beach!! kumtetea bi fatuma kimario hapo watu wazima mlichambia steelwire...lol!
 
Katika uchaguzi wa 2010 zilichapishwa fulana kwa kuandikwa VOTE FOR PEDRO na watu kuzivaa makanisani. Kuvaa barghashia na kula nao futari pamoja haitoshi! kuna jambo zaidi la kufanywa nalo ni sera itakayozingatia mawazo yao.

"Sera itakayozingatia mawazo yao" safi sana kwa kuanzia unaweza kutupa mawazo mawili matatu labda ili wenyewe wayaone maana viongozi wa chadema wapo humu,so ni wakati muafaka wa kusema nini waislam wanahitaji ambacho pengine cdm ikikifanya hali ya kuaminiana itarudi na kukiona cdm kama ni chama cha siasa tu na si vinginevyo

Nitawatolea mfano,hapo kwa jirani zetu kenya,kuelekea uchaguzi mkuu wao ule uliozaa vurugu na mauaji makubwa,waislam wa kenya walipanga mikakati kabambe ya kuhakikisha kura zao kwa umoja wao wanazitumia vizuri,walichofanya waliorodhesha madai yao yote ambayo wanayataka na kuyaweka hadharani huku wakitoa tamko kwamba wao hawana mgombea kwenye uchaguzi mkuu wa rais ila wanayo madai yao ambayo wangependa yatekelezwe hivyo mgombea yeyote atakaekua tayari kutekeleza madai yao wao ndio watakaempigia kura bila kujali dini yake,mwai kibaki akaenda mombasa akakutana na masheikh akakubaliana nao masheikh wakamwambia hatutaki makubaliano ya maneno tunataka makubaliano yetu tuyasajili kisheria mahamani ili ukitugeuke tujue pa kuanzia,kibaki maji yalikua shingoni laila alikua anaelekea kuishika pwani kwa kuwa alikua sambamba na na najib balala ambae ni mwenyeji wa pwani na mtoto wa sheikh maarufu huko,hivyo ili kuikabili nguvu ya Raila pwani kibaki akaingia agreement na waislam kupitia masheikh!hii ni changamoto kwa chadema na waislam wa tanzania ili kuondoa sintofahamu baina yenu tumieni mfano huo,hakuna linaloshindikana pakiwepo nia njema mioyoni
 
Vyama vya siasa vinapokumbatia dini ni hatari sana
 
Tofauti ni kubwa CHADEMA NI CHAMA CHA KIKROSTO na kikanda pia ni wanafiki waislamu hawapendi unafiki na ukanda hivyo basi chadema hawawezi kukaa meza moja na waislamu wakaaminiana.

Mwenye busara na kuitakia mema nchi ni yule anayeona kosa na akasema kosa ni hili hapa bila kumung'unya maneno, badala ya kusema ukanda, ukristo nadhani tungesema ukanda wenu unatokana na moja mbili tau, badala ya kusema udini kijumlajumla tuainishe matendo yanayoashiria kukumbatia dini moja na kuitenga nyingine, vilevile tutofautishe mtu mmoja mmoja na msimamo wa chama
 
Matusi hayo wewe unafuga naye kiti moto. Chadema nasema tena mwislam yeyote atakae ichagua atakuwa ameusaliti uwislam na hakika hastahili msamaha mbele ya mola wake.
 
Hayo yaliletwa na sultani kikwete kuitenganisha chadema na Uislamu lakini sasa yameanza kumtokea puani Waislamu wa Mtwara wameshaligundua sasa wanampa za USO

chadema haiwezi kuingia misikitini na makanisani kuomba waumini waiunge mkono. Kila mtu ana utashi wake na kutambua lipi jema na lipi baya. Propaganda wote tunazisikia lakini wengine tunafia nafsi zetu na sio dini. Kwa hiyo kila watakachongea viongozi wa dini tunalinganisha na hali halisi na kufanya maamuzi. Hatuwezi kufuata upuuzi wa wachache wanaotetea matumbo yao!
 

Wakati mwingine waislam yabidi wawe consistent katika hoja zao. Kuna wakati wanamwita Dr. Slaa padre hivyo ni mdini, na kuna wakati wanamtuhumu kwamba alilisaliti kanisa hivyo haaminiki. Kipi ni kipi sasa kwa Dr. Slaa?

Mimi bado nasisitiza kwamba ni makosa kwa mwanasiasa yoyote kujipeleka kimbele mbele kwenye mambo ya dini ili kukubalika na watu wa dini hiyo. After all -- kukubalika kwa watu hakumaanishi kukubalika kwa Mungu.

Taifa letu ni kubwa, yatosha tu kumtambua Kikwete kwamba ni Mtanzania aliyetokea kuwa mwislam kwa kuzaliwa na sasa ni rais wa Tanzania. Dr. Slaa ni mtanzania aliyetokea kuwa mkristo kwa kuzaliwa, akawa padre, akastaafu upadre, akaamua kuwatumikia watanzania kwa njia ya siasa.

Kama ilivyokuwa kwa Mkapa mkristo, itawashangaza sana waislam nadhani iwapo Dr. Slaa atatokea kuwa Rais halafu maisha yao nchini yakaneemeka chini ya uongozi wa Dr. Slaa. Na nadhani inawashangaza pia kwamba Kikwete ni mwislam, na makamu wake, lakini maisha ya waislam kama ilivyo kwa wakristo bado ni mpigiko tu.

Somo kubwa hapa ni kwamba dini ya rais haviusiahani kabisa na maisha ya kawaida ya mtanzania.
 
ahaa ha haaa! yule mama mkuu wa wilaya mfuga kitimoto maarufu pale mbezi beach!! kumtetea bi fatuma kimario hapo watu wazima mlichambia steelwire...lol!

yah pia lipo tatizo la kutafsiri na kutofautisha kati ya muislam na mtu mwenye jina la kiislam!
 
Mimi nadhani tuingalie zaidi CCM na uhusiano wake na waislam hasa tukianzia TANU ilivyoanzishwa, viongozi wake, na wanachama wake alafu tuangalie ilivyobadilishwa kutoka TANU mpaka kuwa CCM na uongozi wa CCM ilipoanzishwa mpaka sasa, majibu yote utayapata hapo ndani ya TANU mpaka kuzaliwa kwa CCM. Someni HISTORIA kwa makini.
 
Udini mnaousema upo kwenye Media tu, kwetu bado tunazikana waislam na wakristu, kuoana ndio kama kawa na mambo mbalimbali tunasidiana... Udini upo wap!? Mitandaoni? Mapovu ya nini!
 
Tatizo hapa si Chadema wala uislamu wala ukristo; tatizo ni CCM
 
Nakubaliana na wewe kabisa. Lakini kosa lingine kubwa lililofanyika ni ule waraka wa kanisa kuelekea uchaguzi wa 2010 na hata pale kanisa jijini Arusha lilipojiingiza kutomtambua meya wa Arusha ilijipambanua wazi kuwa kanisa linaiunga mkono chadema na hilo huwezi kulikanusha. Hivyo, CCM wanatumia kosa hilo kwa faida yao na hiyo ndio Siasa.
 

Hata mimi bado naamini kwamba CUF ni cha waislam maana mpaka sasa hawajatuambia kilichomfukuzisha uongozi na uanachama bwana Mapalala, Lwakatare sijaona wa dini nyingine wakiondolewa uanachama bila kutolewa sababu kwa umma. Nitaamini vinginevyo kama CUF watakuwa wawazi kuhusu haya, lakini pia ndo chama cha kwanza kupigiwa debe katika nyumba za ibada hasa misikitini mfumo wa vyama vingi ulipoanza nchini bila kukemewa na viongozi wa chama husika sasa kwa nini tusiamini ni chama kwa ajili ya waislam na wa dini nyingine waliopo huko ni wasindikizaji?
 
Mkuu naomba nitoe mtazamo tofauti na huo wako, waislamu pia wameenda shule wala hawaitaji upendeleo maalum kwa sababu ikiwa hivyo itafanyika kwa gharama ya nani kama sio ya upande wa pili na kuleta kitu chenye sura ilieile ya gharama za kuendesha mahakama ya kadhi, isipokuwa wale wachache wasioenda elimu dunia ndio wako na sauti sana na pia wana nyadhifa za juu kwenye taasisi za dini. nashauri walioenda shule waingie kwenye taasisi zao na kuwaelimisha wenzao wachache ambao wanachafua sura nzuri ya dini yao.
 
Wewe utashi wako uko vipi katika hili?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…