Tindo
JF-Expert Member
- Sep 28, 2011
- 58,989
- 103,373
Sawa Mimi ngoja tutazame endless progress ,
Kuitoa ccm ni tofauti na kuanzisha chama ni process ndogo zenye , kuvaa uchungu wanaopitia watanzania , na sio kuvizia Ruzuku na kuomba maridhiano ,
Nimeshawatumia uongozi wa CHADEMA Taarifa lakini wanakataa eti sisi vijana tunabidi kufata utaratibu ambao utapatikana kwa Rais niseme tu .
Hawa nyie mnaowaona Kama mashujaa ni wabinafsi Sana that way wamewa-blind ili msijitambue mbaki na jicho moja la kuona kuwa Ccm itatolewa kwa maridhiano au ballots box .
Haitokaa itokee watu Kama Mbowe and so called wanaharakati mkitoe hiki chama chakavu endapo mkawa na hizi Ego zenu za kuona nyie ni Bora .
Mimi nimecheza sabotage mbalimbali huko Ccm so I don't want to find my self guilty that way nilitaka CHADEMA watupe nafasi na sisi tuweze kufanya kitu .
Mkuu narudia tena, mimi ni shabiki wa kutupwa wa Cdm, ila sio mwanachama wa CDM, wala chama chochote cha siasa. Sina popote ninapounga mkono hayo maridhiano ya kitapeli ya kina Mbowe. Na post zangu zote sijawahi kuunga mkono huo utapeli uitwao maridhiano, na uchaguzi ninasema kabisa kwa sasa Tanzania hakuna uchaguzi, bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Njia ninazopendekeza za kuitoa CCM madarakani, namba moja ni machafuko, au 2, mapinduzi ya kijeshi. Mbinu hizi sisubiri kuitwa na viongozi wa CDM, au Kuremba kwenye kuzitaja. Ndio maana nimekuambia kama una mbinu weka hapa hadharani, hayo mambo ya kutaka kuitwa na viongozi wa CDM ni kupoteza muda. Viongozi wa CDM waache wafuate njia wanayoamini maana wako kisiasa zaidi. Ww weka mbinu hapa kwenye mahakama ya umma inayotegemea nguvu ya umma.