Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 58,894
- 132,245
Mkuu Oscar, japo umetumia jokes kuwasilisha mada yako, but hoja hii ni ya msingi sana and its long overdue, hivyo naunga mkono hoja.Kwa yanayo endelea humu Nchini ni bora Tuanze mchakato wa Kuanzisha kituo chetu cha Tv na Radio .
Tutachangia ujenzi na uanzishwaji,kwani kuna shida gani mbona mengi tumechangia.
Kwanza ile 2012 niliwashauri Elections 2015 - Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni ... hapo niliwaambia
17. Sasa ili kuwafikia Watanzania wote -haswa hawa grassroots level na kuwaamsha waliolala, Chadema haiwezi kuwafikia Watanzania wote kwa kutegemea maandamano na mikutano ya hadhara na mass media za wengine. Chadema lazima wawe na mass media yake ambayo ita propagate the message of "changing the mindset" ya Watanzania. Chadema wana all the resource kumiliki media yake lakini very unfortunately they are myopic, hawana vision ya kuona mbali kuangalia nje ya box and see a bigger picture. Hawajui kupanga priorities zao. Bei ya gari moja tuu la M4C linatosha kununua transmitter ya Digital ya redio na TV and convert chumba kimoja pale Ufipa into a modern studio! na kuwa na YouTube Channel yake ya live stream na active interactive social media pages, Chadema bila media yake, ni kutwanga maji kwenye kinu! CCM ina media yake na TV yake ya TBCCM, radio zake na magazeti yake, Chadema bila media yake, ikulu wataendelea kuisikia tuu kwenye bomba, 2015 ni CCM tena! .
Wasalaam.
Pasco
Enzi zile za ule upepo wa kisulisuli cha Kaskazi ulipoipiga Chadema, nikajua Chadema itamiliki media yake Elections 2015 - Mabadiliko Chanya ya Ujio wa Lowassa: CHADEMA Kuhama Ufipa!, Kuwa Makao Yake, Kituo cha TV na Redio! hapa nilishauri
Wanabodi,
Ukipiga hesabu ya jumla ya ruzuku yote ambayo Chadema imekuwa ikipokea, ukajumlisha na zile fedha za Sabodo alizoipa Chadema kujenga ofisi za makao makuu zenye hadhi, na kulinganisha ruzuku hiyo imekuwa ikifanyia nini, utakubaliana na mimi, kuwa fedha hiyo, ingetosha kabisa kujenga jengo jingine la maana na lenye hadhi kwenye eneo la kutosha. Hali hii imetokana na upangaji mbovu wa vipaumbele vyake, hali iliyopelekea matumizi mabovu ya ruzuku, kama yalivyofafanuliwa kwenye ripoti ya CAG.
Mabadiliko hayo chanya ya ujio wa Lowassa sio tuu kwa Chadema kumiliki jengo lake lenyewe, bali pia Chadema itamiliki media zake yenyewe kikiwepo kituo chake cha Redio na Televisheni pamoja na magazeti yake yenyewe, kwa sababu Lawassa hapo alipo tayari anamiliki by proxy, familia kubwa ya media, yenye vituo vya Redio, TV na magazeti lukuki!, hivyo sasa pia vitatumiwa kuisupport Chadema kwa kuanzia tuu, wakati mchakato wa umiliki rasmi wa vyombo vyake yenyewe ukiendelea!.
Ama kweli mgeni njoo, mwenyeji apone!.
Hongera sana Lowassa!.
Hongera Chadema.
Ikulu 2015 ni ya UKAWA!.
Mungu Ibariki Tanzania.
Paskali
Ni muhimu sana Chadema iwe na media yake, huwezi kushika inchi kwa kutegemea media za wengine!, kila kipindi cha uchaguzi, media huwa zinafanya endorsement, Kuelekea Octoba 2015: Je, Sasa ni Wakati wa Media Zetu Kufanya Endorsement ya Wagombea?
most media za Bongo zina endorses CCM kwasababu...!
P