CHADEMA Special Thread

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepiga fataki katika Makao Makuu yake, Edwin Mtei House, Mikocheni jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kumbukizi ya miaka 20 tangu kufanyika kwa mabadiliko makubwa ya chama mwaka 2006.

Shughuli hiyo imefanyika usiku wa leo huku wanachama na viongozi wa chama wakishiriki katika kumbukizi hiyo inayorejea kipindi kinachoelezwa kuwa kilikuwa na umuhimu mkubwa katika historia ya CHADEMA.

Kwa mujibu wa chama hicho, maadhimisho hayo yanalenga kukumbuka hatua za mageuzi zilizofanyika mwaka 2006 na mchango wake katika safari ya kisiasa ya CHADEMA ndani ya Tanzania.

Fataki hizo zimepigwa katika eneo la Makao Makuu ya chama kama ishara ya kuadhimisha miaka 20 ya mabadiliko hayo ya kihistoria.

https://www.facebook.com/
View: https://www.facebook.com/share/v/1W4drie9e1/
 
#BREAKINGNEWS

Wakili wa Serikali mkuu Nassoro Katuga anaiambia Mahakama kuwa upande wa Jamhuri umeoana ushahidi ambao umekwishatolewa unajitosheleza hivo basi hakuna sababu ya kuongeza ushahidi mwingine. Jamhuri wanaomba kufunga ushahidi wao kwa idadi ya mashahidi hao 17. Tundu Lissu
 
TAARIFA

Mwalimu John Ngoni (kushoto pichani) ameachiwa huru leo baada ya kuchukuliwa na Polisi takribani wiki mbili.
simu zake zote zinashikiliwa kwa uchunguzi na hizo hazirudi tena.

Polisi sasa wamejigeuza mahakama wanakamata MTU wanakaa nae Mpaka siku 40 wengeni wiki tatu wengine wiki 2.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…