CHADEMA, serikali tatu na serikali ya majimbo

CHADEMA, serikali tatu na serikali ya majimbo

EMT kwa kuanzia napenda kukuuliza Serikali ya Zanzibar sasa inafanya nini?

Ni sawa na na mimi kukuuliza kama kutakuwa na utawala wa majimbo, then serikali za bara na Zanzibar zitakuwa zinafanya nini? Huoni kuwa kwa kuwepo kwa serikali ya majimbo na serikali tatu, bado utaendelea kuuliza swali ulilouliza?

Halafu nigekuuliza tena ulioona wapi nchi ikawa haina serikali? Yaani Tanganyika iwe ni nchi pekee katika uso wa dunia ambayo haina haja ya kuwa na serikali?

Muungano wa Tanzania ni muungano wa nchi mbili na hivyo inawajibika kila upande uwe na serikali yake iwapo makubaliano sio kufanya muungano wa nchi moja kama ulivyo wetu wa Tanzania.

Usawa uko wapi kama nchi moja inakuwa na serikali yake, usawa uko wapi ikiwa wananchi wa upande mmoja wanajihudumia kupitia serikali yao, huku upande mmoja unaongozwa na mchanganyiko wa pande mbili na wananchi wake wakitumia pato la jumla la pande mbili?

Inawezekana mtu alie nje ya taifa hili asifahamu huo mchakachuo uliopo na akashangaa huu ni mseto wa namna gani. Kuondowa mtafaruku huu ndio kunapohitajika kuwa na serikali ya Tanganyika.

That was not my point. Sisemi kuwa iwepo serikali ya Zanzibar, isiwepo serikali ya Tanganyika, lakini iwepo serikali ya majimbo.

Sasa nikujibu Serikali ya Tanganyika itakuwa inafanya nini. Serikali ya Tanganyika itakuwa inashughulikia mambo ya kiutawala wa Tanganyika na itakuwa haiingiliwi katika mamdo ya Watanganyika kama vile inavyofanyika kule zanzibar. Tanganyika itaamuwa iwe na wabunge wangapi na si lazima iwe wabunge wawe wengi kama sasa eti kila wilaya kuwa na mbunge. Pengine hayo majimbo yatatowa wabunge kwa bunge la Tanganyika. Kuulizia mfumo na gharama ni jambo la kipuuzi kwani tangu tulikpopata uhuru tumekuwa na mfumo mmoja? Mfumo wa utawala ni kitu cha kupangwa kulingana na mazingira na matakwa.

Na serikali ya jimbo itakuwa inafanya nini? The way ulivyoeleza ni kama vile unataka kuendeleza tawawa za mikoa za sasa kupitia back door ya utawala wa majimbo.
 
CHADEMA wanataka kuwe na serikali tatu. Wakati huo huo wanataka kuwe serikali ya majimbo. Kwa maana hiyo, kutakuwa na Rais wa Muungano na wakuu wawili wa serikali za Bara na Zanzibar. Pia kutakuwepo na gavana katika kila jimbo ambao watakuwa na mamlaka kamili kwenye majimbo yao.

Ukiondoa suala la gharama ambalo kwa demokrasia ni vyema kuzipitia kiutawala hii imekaa sawa? Utawala wa majimbo chini ya serikali tatu unawezekana? Dhana kuu ya sera ya serikali ya majimbo ni kuhamisha madaraka ya maamuzi kutoka kwa watu wachache na kuyarejesha mikononi mwa wananchi vijijini.

Kama ni hivyo, hizo serikali mbili za Bara na Zanzibar zitakazokuwa zinaongozwa na wakuu wawili zitakuwa zinafanya nini? Madaraka ya wakuu wa serikali hizo mbili hayatagongana na madaraka ya magavana wa majimbo? Kama serikali moja chini ya utawala wa majimbo haiwezekani, solution ni kuwa na utawala wa majimbo chini ya serikali tatu?

Hivi kwa akili zako hujui kwamba kinachojadiliwa sasa ni rasimu ya katiba, na kwamba rasimu hii ilishakataa suala la majimbo (hivyo suala hili si sehemu ya mjadala wala hitaji la Chadema?)
 
Mkuu EMT, haya maswali yako hayatakiwi kwenye siasa za Tanzania!.

Nchi kwa sasa iko kwenye usingizi na wananchi wake hawafahamu siku ya kesho itakuwaje kwa maana kuwa kwa sasa hatujui muundo wa serikali kesho utakuwaje huku vyama vya siasa kama CHADEMA wao tayari wana muundo wao kinadharia lakini ukiuleta na kuutingisha kwenye serikali tatu ambazo pia CHADEMA wamezipendekeza, utakumbana na mapungufu mengi ya kiutendaji achilia mbali matumizi ya raslimali na mapato ya taifa. Hili swala la majimbo kwa CHADEMA liko kisiasa sana wakati linatakiwa liwe limechambuliwa hasa kiuchumi na kijamii.

Hoja ya CHADEMA kuhusu serikali za majimbo itakuwa na maana zaidi katika kupambana na hoja za muundo wa serikali uliopo kwa sasa, lakini inakuwa ni kaput katika kupambana na hoja za serikali tatu ambazo zimependekezwa CHADEMA, vile vile na tume ya Jaji Warioba.

CHADEMA wanaongelea swala la majimbo kwa kuitazama katiba ya 1977 wakati baada ya miaka miwili itakuwa ni kaput halafu kikubwa kabisa, haijulikani kama hii sera itakuwa ni sehemu ya katiba ya Tanganyika au itatokana na sheria zinazokuwa ni matokeo ya katiba. Kama ndivyo hivi, CHADEMA wana uhakika gani wa kuifanya kuwa ni sheria kupitia katiba ya Tanganyika ndani ya bunge la Tanganyika ikichukuliwa hata hawana uhakika wa kupata idadi kubwa ya wabunge wa 'Tanganyika' ikichukuliwa kuwa siasa za Tanzania zinachagizwa winner-take-all.

Hizi ninaziona ni kama zilezile porojo za kila siku za kisiasa na wanasiasa wetu ambazo kwa kiasi kikubwa ndiyo mzizi wa siasa za Tanzania.

Kama kweli Watanzania wanataka serikali tatu, basi katiba ya Tanganyika ni muhimu sana zaidi ya katiba ya muungano, na kwa maana hii, ni lazima kwanza wananchi wangefahamu muundo wake kwa sababu wananchi wanataka kufahamu hatma za raslimali zao kama madini, ardhi, gesi, mafuta na pia elimu kwa wananchi wake na siyo mambo saba ya Muungano.

Ndiyo maana nikasema, kulikuwa na umuhimu sana wa kuwepo kwa kura ya maoni kabla ya kuwepo Rasimu ya Katiba ili kufahamu kama wananchi wengi wanataka muungano uwepo au usiwepo, na kama wanataka uwepo, basi wangepewa tena fursa ya kusema ni serikali ngapi wanazitaka. kufanya hivyo kungefanya hata zoezi la kuandika rasimu ya katiba kuwa straight foward kutokana na kupata political legitimacy and defined political context kwa maana kuwa tume ingefahamu kama rasimu niya serikali moja, mbili, tatu au nne na hiyo serikali nyingine/zingine zitakuwa vipi.

Kilichofanyika kwa sasa ni sawa na kuanza kununua nguo za mtoto wa kiume kwa sababu tunapenda kupata kupata mtoto wa kiume wakati hatufahamu hata jinsia ya mtoto zaidi ya kutambua kibailogia, mtoto lazima atakuwa mwanamke au mwanamme bila hata kudhani kama mimba inaweza kutoka au kukazaliwa mapacha.

Kila siku ninasema kuwa fikra za Watanzania walio wengi katika maswala ya kisiasa na kiuchumi ziko chini sana kiasi kwamba hata swala muhimu la katiba kwa sasa linaendeshwa kwa ushabiki wa kisiasa ambapo hata siasa zenyewe zinazoshabikiwa zimejengwa kwa mawazo na mitazano duni.

Ningeelewa angalau kidogo kama hizi siasa zingekuwa zimejengwa kwa mawazo na mitazamo ya hali ya juu kwa maana kuwa, vyama viwe chini ya utaifa na siyo vyama kuwa juu ya utaifa.

Wananchi lazima waamue mwelekeo wa taifa lao na vyama lazima vikubaliane na mwerekeo huo na kama vikishindwa kukubaliana au kuusimamia, basi nguvu ya wananchi itumike kuviweka kando kwa njia ya kura na kingine kipewe fursa hiyo.

Hatari ya chama kuwa juu ya utaifa ni wananchi kukosa nguvu katika maamuzi ya mwerekeo wao kitaifa na hivyo kushindwa kuvishinikiza vyama kufanya kile wanachokitaka na matokeo yake ni wananchi kuwajibika kwa vyama badala ya vyama kuwajibika kwa wananchi.

Kinachoonekana kwa sasa nchini ni wananchi kuwajibika kwa vyama vya siasa ambapo vyama vina-dictate matakwa ya wananchi badala ya wananchi ku-dictate matakwa yao mpaka hata asasi zingine za kiraia ambazo kwenye sheria ya mabadiliko ya katika vinaangaliwa kisheria kuwa sawa na vyama vya siasa lakini kwa sasa zimekuwa ni sehemu ya vyama katika mchakato wa katiba mpya.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
EMT , labda tuanzie hapa: Hivi hata kwa katiba ya sasa CDM wangewezaje kutekeleza sera yao ya majimbo?
 
Kiwi, ameeleza vizuri sana.lakini kwa Tanzanian ni shida kuelewa. Chadema walipaswa kutekeleza mfumo huu kwenye sehemu ambazo wanaongoza council ili kutoa picha jinsi ambavyo wananchi wanavyoshiriki ktk kutoa maamuzi juu ya maendeleo yao ili uwe mfano,

Alichofanya Kiwi ni kujaribu kueleza dhana ya utawala wa majimbo na faida zake dhidi ya tawala za mikoa.

Ambacho hakugusia ni mahusiano kati utawala wa majimbo na serikali tatu zilizopendekezwa na kuungwa mkono na Chadema.

Nchi moja inakuwa na serikali kuu ikiongozwa na Rais na labda makamu wa rais.

Nchi hiyo inakuwa pia na serikali nyingine mbili zikiongozwa na Marais, au mawaziri wakuu or whaterver names you would like to call them.

Nchi hiyo pia inakuwa na utawala wa majimbo chini ya magavana.

How would you reconcile all these political administrations?
 
Hivi kwa akili zako hujui kwamba kinachojadiliwa sasa ni rasimu ya katiba, na kwamba rasimu hii ilishakataa suala la majimbo (hivyo suala hili si sehemu ya mjadala wala hitaji la Chadema?)

Labda kinachojadiliwa ni rasimu ya katiba lakini dhumuni la mimi kuanzisha hii thread haikuwa kujadili rasmi rasimu ya katiba bali sera ya Chadema ya utawala wa majimbo na jinsi inavyoweza kufit kwenye muundo wa serikali tatu ambao unaungwa mkono pia na Chadema.

Unless uniambie basi sera ya chadema ya utawala wa majimbo imekufa kama kifo cha mende ili mjadala ufungwe.
 
Hoja ya CHADEMA kuhusu serikali za majimbo itakuwa na maana zaidi katika kupambana na hoja za muundo wa serikali uliopo kwa sasa, lakini inakuwa ni kaput katika kupambana na hoja za serikali tatu ambazo zimependekezwa CHADEMA, vile vile na tume ya Jaji Warioba.

Hapo ndipo ilipo hoja yangu. Kama moja ya misingi ya sera ya Chadema ya utawala wa majimbo ni kushusha na kugawanya madaraka, kuwa na muundo mpya unaosaidia utekelezaji wa majukumu na kupunguza ukubwa na gharama za uendeshaji wa serikali, basi hii inaweza isifanikiwa kama tutakuwa na siyo tuu na serikali mbili kama ilivyo sasa, bali serikali tatu.
 
EMT , labda tuanzie hapa: Hivi hata kwa katiba ya sasa CDM wangewezaje kutekeleza sera yao ya majimbo?

Wasingeweza kwa sababu they are not in power. Hata hivyo, mimi naongelea mbele zaidi.

Chadema inadai is the opposition party in waiting kuchukuwa madaraka.

In doing so, Chadema imekuja na sera za kiutawala mojawapo ikiwa ni sera ya mfumo mpya wa utawala maafuru kama sera ya utawala wa majimbo.

Tayari Chadema imeshaanza kuitumia sera hii ya utawala wa majimbo ndani ya chama.

Plan ni kwamba kama Chadema ikiingia madarakani basi itaanzisha utawala wa majimbo.

Kwa hiyo, sera ya majimbo ni moja ya alternatives za tawala za mikoa ambayo Chadema imejaribu kuiuza kwa wapiga kura.

Wakati huo huo, Chadema inaunga mkono muundo wa serikali tatu kama ilivyopendekezwa na Tume ya Warioba.

Ina maana kama katiba ikiamua kuwa na serikali tatu na Chadema ikafamikiwa kuchukuwa madaraka, then Tanzania itakuwa na utawala wa serikali tatu na pia utawala wa majimbo?

If so, how would you reconcile these administrations? In particular, demarcation ya mamlaka kati ya serikali ya Tanganyika na serikali za majimbo itakuwaje?

Wapo watu wanadai kuwa suala la muhimu sasa ni serikali tatu kwa sababu tume ya Warioba imetupilia mbali pendekezo la utawala wa majimbo.

If that is the case, sera ya Chadema ya utawala wa majimbo halina tena mantiki na hivyo litupiliwe mbali au mfumo huu wa utawala utakuwa unatumika ndani ya Chadema pekee lakini siyo kwa taifa hata kama kitachukuwa madaraka?
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Shida ni kwamba pamoja na wananchi kukataa mfumo wa majimbo kama ulivyosema wewe mwenyewe, bado Chadema inatumia mfumo uliokataliwa na wananchi. Maana huwezi kuweka jambo pending wakati huo huo unalitekeleza.

Kama mfumo wa serikali tatu ndiyo ulikubaliwa basi Chadema waachane na utekelezaji wa sera yao ya majimbo.

Na serikali ifunge office zote bara na visiwani kisa mswada unataka serikali 3?? Uvivu wa kufikiri ndio huu.. Basi. Hata hivyo mimi binafsi nilimsikiliza zitto akifafanua kuhusu msimamo wa cdm ndani ya hoja hii ya idadi ya muundo wa serikali, nilihisi msimamo wa chama cha cdm ni serikali moja na sio tatu ama mbili.. labda msikilizeni wenyewe hapa. https://www.youtube.com/watch?v=JbV1eC_ztuw&feature=youtube_gdata_player
 
Alichofanya Kiwi ni kujaribu kueleza dhana ya utawala wa majimbo na faida zake dhidi ya tawala za mikoa.

Ambacho hakugusia ni mahusiano kati utawala wa majimbo na serikali tatu zilizopendekezwa na kuungwa mkono na Chadema.

Nchi moja inakuwa na serikali kuu ikiongozwa na Rais na labda makamu wa rais.

Nchi hiyo inakuwa pia na serikali nyingine mbili zikiongozwa na Marais, au mawaziri wakuu or whaterver name you would like to call them.

Nchi hiyo pia inakuwa na utawala wa majimbo chini ya magavana.

How would you reconcile all these political administrations?

Nakubaliana na wewe EMT. Sikuwa na muda mrefu wa kuingia kwa mapana zaidi kuhusiana na jinsi ya ku- 'reconcile' hizo tawala mbalimbali. Nashukuru kwa kuliona hilo, bado tuna kazi kubwa ya kuchanganua na ninaamini ya kuwa kwenye hili jukwaa tunaweza kumpata mtu atakayeweza kufafanua zaidi. Binafsi nimeliona hilo tatizo, na nipo kwenye kuandaa mada kwenye semina itakayofanyika wiki ijayo, kwa hiyo bado ninachanganua. Nikipata wasaa nitajaribu kuja kuliweka wazi baadaye humu jamvini, lakini kwa kuwa hili ni jukwaa la 'Great Thinkers' nami pia ningeomba maoni ya wengine ili tupanue upeo wetu na kukuzana kitaaluma. Shukrani za dhati wanajamvi, tunapata darasa zuri sana! Ninaamini mawazo haya hayatabaki jukwaani tu, bali yanakwenda kufanyiwa kazi. Tanzania ni yetu sote, pamoja tunaweza. Mwalimu alisema, 'Inawezekana, timiza wajibu wako!'
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Na serikali ifunge office zote bara na visiwani kisa mswada unataka serikali 3?? Uvivu wa kufikiri ndio huu.. Basi.

Wewe utakuwa na uvivu hata wa kusoma. Wapi nimeandika kuwa serikali ifunge office zote bara na visiwani kisa mswada nataka serikali tatu?

Serikali ifunge office zote bara na visiwani kwani sana kuna utawala wa majimbo?

Hata hivyo mimi binafsi nilimsikiliza zitto akifafanua kuhusu msimamo wa cdm ndani ya hoja hii ya idadi ya muundo wa serikali, nilihisi msimamo wa chama cha cdm ni serikali moja na sio tatu ama mbili.. labda msikilizeni wenyewe hapa. https://www.youtube.com/watch?v=JbV1eC_ztuw&feature=youtube_gdata_player

Kwenye hiyo link ya video uliyotoa Zitto hajaongelea kabisa kuhusu sera ya Chadema ya utawala wa majimbo.
 
Akili za kinapenape ni rojorojo kabisa.Bila kuwa na serikali za majimbo katika nchi hii, maendeleo yasahaulike kabisa kwa miaka mingi ijayo.
 
Still, how would you reconcile serikali kuu ya Mungano, serikali ya Tanganyika na serikali za majimbo?

To me this type of muungano is an illusion I am living with. I mean it is an imposed Mungano so it does not contribute nor attract any aspiration from the type of me. I think there are also some like me.
 
Laiti tungekuwa na serikali za majimbo serikali kuu isingewaburuza watendaji kutii amri kutoka juu. .
upo sahihi mkuu, Top-Down leadership methodology ime-prove failure kwa changamoto za dunia ya leo, naikubali sera ya Majimbo na dhana nzima ya uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi iliyomo ndani ya sera hii.
 
Hapo ndipo ilipo hoja yangu. Kama moja ya misingi ya sera ya Chadema ya utawala wa majimbo ni kushusha na kugawanya madaraka, kuwa na muundo mpya unaosaidia utekelezaji wa majukumu na kupunguza ukubwa na gharama za uendeshaji wa serikali, basi hii inaweza isifanikiwa kama tutakuwa na siyo tuu na serikali mbili kama ilivyo sasa, bali serikali tatu.
Kwa watu wanaoiangalia CHADEMA wakiwa nje ya jiko lake wanaona mapungufu mengi tu kuhusiana na utendaji wake. Mapungufu hayo inakuwa ni vigumu sana kuyaona walio ndani ya jiko na hata kama wakiyaona, inakuwa ni vigumu sana kuyatafutia majibu iwapo yanawagusa wafanya maamuzi katika hali hasi.

Ni taasisi chache sana zinazojitadhimini kila wakati kwa kutumia wataalamu ambao wako nje ya jiko na kufanya marekebisho kwa muda mwafaka.

Tatizo kubwa moja ambalo ninaliona ndani ya CHADEMA ni kuendelea kuwa na mentality ya uanaharakati hata katika mazingira ambayo kama chama kilichokamilika 'kupewa nchi' wanatakiwa ku-set agenda na pia kuwa pre-emptive.

Kwangu mimi ninaona hata hii agenda ya serikali ya majimbo CHADEMA iliileta ili kupambana na hoja za CCM zinazotokana na katiba ya 1977 katika sehemu ya tatu, kipengele cha 51-61 kinachohusu Waziri Mkuu, Baraza la Mawaziri, serikali na wakuu wa mikoa na pia katika Sura ya nne, kwenye kipengele cha 145-146 kuhusu madaraka ya umma (Serikali za mitaa), bila kufikiria kuwa by the end of 2014, katiba ya 1977 itakuwa ni historia na wakati ikitafutwa hiyo historia, agenda yao itakuwa ni serikali tatu. Kwa sasa hivi CHADEMA wako kwenye mishmash.

Kama chama 'kilichokamilika', jambo kama hili walitakiwa walifahamu mapema na ku-set agenda badala ya kukaa na kusubiri ku-react baada ya CCM kuleta hoja.

Kwa sasa hawaongei tena kuhusu Majimbo kwa sababu wako busy kujibu mashambulizi yanayoanzishwa na CCM, cha kushangaza hata kujibu mashambulizi hawafanyi mapema na kwa muda mwafaka kudhihirisha kama wako tayari kwa lolote kama agenda hawakui-set wao.

CHADEMA wanatakiwa kwa sasa waonyeshe kile wanachokisimamia na jinsi kitakavyofanya kazi siyo kwa leo tu bali kwa maisha ya vizazi vijavyo na siyo muda wote waonyeshe kile wanachokipinga kutoka CCM.

Kusimama jukwaani na kusema chama kinaachana na siasa za uanaharakati haitoshi bali matendo ndiyo yanatosha.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
..Plan ni kwamba kama Chadema ikiingia madarakani basi itaanzisha utawala wa majimbo..
Mkuu hapa ndio ilikuwa kiini cha swali langu.

Hata kama katiba ya sasa ikiendelea na CDM ikashika madaraka, hawawezi kuweka serikali za majimbo kwa sababu itakuwa ni kinyume cha katiba. Kama tunaamini kuwa wazo lao ni kubadili katiba - wakiwa madarakani- ili kuwapo na serikali za majimbo then katiba yoyote itakayokuwepo si wanaweza kuibadili?

Kama wazo lao ni kubadili katiba kama watashika madaraka ili kuruhusu serikali za majimbo, then katika hali ya sasa sioni kama kuna ubaya wowote strategically kwa wao kukubali serikali tatu kama wanaamini hiyo itajenga mazingira mazuri zaidi wa kuweza kuitoa CCM madarakani (na bila shaka maslahi bora zaidi kwa wananchi?). Then wakishashika madaraka, wakaaminika, pengine inaweza kuwa rahisi zaidi kwao kuwashawishi wananchi juu ya suala la serikali za majimbo na accordingly kubadilisha katiba.

Katika mchakato wa kidemokrasia ni kawaida kufuata njia/chaguo la wengi hata kama ni tofauti na chaguo lako. Tumeona hata Zanzibar (Uamsho na makundi mengine) ambayo mwanzoni walikuwa na msimamo wa muuungano wa makataba (whatever that is!) lakini baada ya kuona hilo sio suala rahisi, nao pia wame soften na sasa naona wanakubali serikali tatu (kimsingi) lakini wanataka mambo ya muungano yapunguzwe zaidi.

Lakini suala la muhimu ni haya yote pamoja na misimamo/sera zao (iwe CCM, CDM, CUF, Uamsho etc) yanafanywa kwa maslahi ya nani? Wananchi, Chama, ama Kikundi cha watu fualani tu? Hili ni tatizo kubwa sana (nimeona mdau Ng'wamapalala ameligusia hapo juu).
 
  • Thanks
Reactions: EMT
CHADEMA wanataka kuwe na serikali tatu. Wakati huo huo wanataka kuwe serikali ya majimbo. Kwa maana hiyo, kutakuwa na Rais wa Muungano na wakuu wawili wa serikali za Bara na Zanzibar. Pia kutakuwepo na gavana katika kila jimbo ambao watakuwa na mamlaka kamili kwenye majimbo yao.

Ukiondoa suala la gharama ambalo kwa demokrasia ni vyema kuzipitia kiutawala hii imekaa sawa? Utawala wa majimbo chini ya serikali tatu unawezekana? Dhana kuu ya sera ya serikali ya majimbo ni kuhamisha madaraka ya maamuzi kutoka kwa watu wachache na kuyarejesha mikononi mwa wananchi vijijini.

Kama ni hivyo, hizo serikali mbili za Bara na Zanzibar zitakazokuwa zinaongozwa na wakuu wawili zitakuwa zinafanya nini? Madaraka ya wakuu wa serikali hizo mbili hayatagongana na madaraka ya magavana wa majimbo? Kama serikali moja chini ya utawala wa majimbo haiwezekani, solution ni kuwa na utawala wa majimbo chini ya serikali tatu?

Rudi tena darasani!!!!!! sasa hivi kuna Mikoa hiyo ni serikali,kuna wilaya hiyo ni serikali. Utawala wa majimbo maana yake ni scope ya maeneo mfano mikoa ya morogoro,dodoma,sindida ikaunda jimbo la kati na mkuu wa jimbo ni gavana na hapa maana yake tayari umeondoa wakuu wa mikoa 3 na pia umeondoa uteusi wa wakuu wa mikoa 3 na kurudisha mamlaka kwa raia. yaani unakubali akili ndogo ikatawala akili kubwa,pole sana
 
Back
Top Bottom