CHADEMA, serikali tatu na serikali ya majimbo

CHADEMA, serikali tatu na serikali ya majimbo

umeuliza maswali ya msingi sana kwenye hoja yako hii EMT. lakini kwanza hebu tujaribu kutafakari kwa undani ni kitu gani ambacho wanachi wanataka wka sasa??

wananchi wanataka serikali 3 wao hawataki moja wala mbili wala serikali za majimbo, kama ndivyo wananchi wanavyotaka ni wazi kwamba matakwa yao ndio yatimie.

lakini kwa upande mwngine CDM walilenga gavana wa jimbo ndiye atakaye mreplace mbunge by so doing wabunge wapewe meno ya kuwawajaibisha watendaji wa serikali. to me hii ilikuwa inaniwia ngumu sana sana kuipatia picha itakavyokaa manake niliwaza kiutendaji wabunge wetu kwanza sio wachapa kazi ni watu wa maneno mengi pasipo utekelezaji na hapo hapo pia wabunge wetu zaid ya kujineemesha kwa kutaka maposho makubwa hawana jingine wanalo tusaidia sisi kama wananchi sasa leo hii wakipewa hayo mamlaka ya kiutedaji si ndio watatumaliza??

Vyema Mkuu. Ila sisi wananchi tunachotaka ni Guarantee ya USTAWI WETU KWANZA! Sasa iwe under serikali 3, 2, 1 au majimbo, haijalishi. Hata kama wananchi watataka serikali 5 leo, lakini huko mbele zikashindwa ku-guarantee Ustawi wao, WATAZIPINGA japo walizitaka!
Upuuzi wa vyama vya siasa vimetu-switch wananchi tulio wengi kutanguliza Political wills zao, badala ya USTAWI WETU, ni janga kubwa! Leo wengi wanaotaka serikali 3 au 2 au majimbo ni kwa kuwa chama chake kinadai hivyo, hana muda wa kutathimini credibility yake katika kuleta USTAWI WAKE! Ni upu.mbavu! Kinachoendeshwa leo na vyama vyote vya siasa ni Political Movements (kwa tafsiri ya siasa mchezo mchafu), ambazo lengo lake ni ku-gain HISIA za watu si AKILI zao! Chochote wapo tayari kufanya ila tu wanapata Popularity ambayo under ushenzi uitwao Demokrasia ni muhimu sana. Chama makini cha siasa kingeendesha Welfare Movements, na automatically wangeteka AKILI za watu na si HISIA zao ambazo zipo tayari kubadilika kwa usiku mmoja tu! Pumbav.u! Tuache wafu wazikane! Lakini HATUTAKAA KIMYA MILELE! We are the Time, we will tell dem soon!
Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani! Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
CHADEMA walipendekeza kuwa na mfumo wa majimbo ikakataliwa na wananchi, wakauweka pending. Mfumo wa serikali tatu ndo ukakubaliwa. Shida iko wapi?

Shida ni kwamba pamoja na wananchi kukataa mfumo wa majimbo kama ulivyosema wewe mwenyewe, bado Chadema inatumia mfumo uliokataliwa na wananchi. Maana huwezi kuweka jambo pending wakati huo huo unalitekeleza.

Kama mfumo wa serikali tatu ndiyo ulikubaliwa basi Chadema waachane na utekelezaji wa sera yao ya majimbo.
 
....Kukiwa na serikali za majimbo ni kwamba hatutakuwa na RC 'mteuliwa' na Rais aliyeko Dar. Badala yake wananchi wa mkoa husika watapata nafasi ya kumchagua 'gavana' wao atakayesimamia matakwa yao na maendeleo yao. Watendaji wote watakaokuwa mkoani watawajibika kwa gavana ambaye atawajibishwa na wananchi waliomweka madarakani. Kwa maana hiyo shughuli za maendeleo zitasimamiwa kwa ukaribu zaidi kwani hakuna tena kusubiri 'amri' kutoka kwa mkuu wa kaya. Maana ingine ni kuwa ufisadi uliopamba moto na ubadhirifu vitaweza kudhibitiwa kirahisi zaidi iwapo watendaji wanajua ya kuwa uwepo wao unategemea ridhaa ya wananchi. Mathalani endapo wananchi wa mkoa fulani wana tatizo la Maji, Afisa wa Maji atapaswa kutoa majibu kwa wananchi na kueleza mikakati gani atakayochukua kuwapatia ufumbuzi. Serikali Kuu itakuwa msimamizi mkuu, itapanga sera za kitaifa kulingana na mipango mbalimbali itakayofikishwa huko kutoka kwenye majimbo badala ya kutoa amri na kutangaza sera majukwaani kama ifanyavyo sasa. Mfano mzuri ni huu mpango wa 'Big Results Now' ambao serikali imeutangaza, 'wateuliwa' Mawaziri wameupitisha, na pia mikoani maafisa elimu wameupitisha, walimu ambao ndio 'watekelezaji' hawakushirikishwa na sasa wanalazimishwa waukubali.

Kimsingi sikatai utawala wa majimbo, bali sioni mamtiki ya kuwepo kwa utawala wa majimbo halafu hapo hapo uwe na serikali tatu, yaani serikali ya mmungano chini ya Rais, na serikali ya Tanzania Bara na Zanzibar chini ya, tuseme mawaziri wakuu.

Kama shughuli za maendeleo zitasimamiwa na magavana, then kazi ya serikali kuu itakuwa tuu msimamizi mkuu na kupanga sera za kitaifa kulingana na mipango mbalimbali. Kama ni hivyo, serikali za bara na visiwani chini ya mawaziri wakuu itakuwa zitakuwa zinafanya kazi gani?
 
huu ni mtizamo wako na wala si msimamo wa chama ,,,

Kuuliza maswali kumbe nako ni mtazamo?

chadema ni chama makini na kinaongozwa na viongozi makini,,,,tumalize kwanza mchakato wakatiba unaohusu taifa kwa ujumla,,,,ilo ndilo la msingi kwanza,,,

Sera ya Chadema ya utawala wa majimbo siyo ya msingi? Sera ya majimbo haihusu taifa kwa ujumla?

Unaposema kuwa "chadema ni chama makini na kinaongozwa na viongozi makini" huna tofauti saaana na wale wanaosema kuwa "serikali chini ya CCM ni sikivu sana".
 
Jaji Warioba alitoa ufafanuzi mzuri kuwa, 'wananchi hawataki majimbo, mkataba wala serikali mbili! Wanataka tatu'. Vyama vyote hapa vikubwa vilipoteza. Ni mbumbumbu ndo hawakuelewa

Vipi kama suala la serikali tatu likiingia kwenye katiba mpya, Chadema itakuwa na utawala wa majimbo kama ikifanikiwa kuchukuwa madaraka?
 
hiji chama ni uwezo wake ni sawa na vigango vya uko usukumani yaani vyama vya kusaidiana kwenye shida na raha sasa wao wanzani kwa kuwa wamefanikiwa huko na kutawala nchi wataweza ....CHAGA DEVELOPMENT MOSHI AND ARUSHA (CHADEMA) ..ni janga la kitaifa
 
umeuliza maswali ya msingi sana kwenye hoja yako hii EMT. lakini kwanza hebu tujaribu kutafakari kwa undani ni kitu gani ambacho wanachi wanataka wka sasa??

wananchi wanataka serikali 3 wao hawataki moja wala mbili wala serikali za majimbo, kama ndivyo wananchi wanavyotaka ni wazi kwamba matakwa yao ndio yatimie.

Kama wananchi wameamua hivyo kupitia maoni yao kwenye suala la katiba, Chadema waache ku-practice hiyo sera ya majimbo kama inavyofanya sasa? Otherwise, si watakuwa wana-practice sera ambayo imekataliwa na wananchi?

lakini kwa upande mwngine CDM walilenga gavana wa jimbo ndiye atakaye mreplace mbunge by so doing wabunge wapewe meno ya kuwawajaibisha watendaji wa serikali. to me hii ilikuwa inaniwia ngumu sana sana kuipatia picha itakavyokaa manake niliwaza kiutendaji wabunge wetu kwanza sio wachapa kazi ni watu wa maneno mengi pasipo utekelezaji na hapo hapo pia wabunge wetu zaid ya kujineemesha kwa kutaka maposho makubwa hawana jingine wanalo tusaidia sisi kama wananchi sasa leo hii wakipewa hayo mamlaka ya kiutedaji si ndio watatumaliza??

Sidhani kama moja ya dhumuni la sera hiyo ni ku-replance wabunge. Wabunge wangeendelea kuwepo lakini vyeo vya mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya, katibu tarafa ndivyo vingefutwa. Kwa mujibu wa sera hiyo, hawa ndiyo wanaofanya nchi iendeshwe na Ikulu Dar.
 
Nina hakika Serikali tatu inawezekana bila gharama za maslahi, na majinbo ndiyo hasa muondo wa msingi wa kujitawala toka iwepo dunia ya kidemokrasia.

Kwa hiyo, kuwe na serikali tatu na pia utawala wa majimbo? Moja ya misingi ya sera ya Chadema ya utawala wa majimbo ni kushusha na kugawa madaraka. Hii itafanya maamuzi yafanywe na kwenye ngazi za chini kuliko ilivyo sasa.

Lengo la utawala wa majimbo ni kuifanya serikali kuu ijishughulishe na mambo machahe. Serikali ya majimbo itawezesha pia wananchi kushiriki na kushirikishwa kwa karibu zaidi katika shughuli za maendeleo katika majimbo yao.

Hata hivyo, Chadema inaunga mkono kuwepo kwa serikali tatu. Kwa maana hiyo, pamoja na kuwepo kwa serikali ya majimbo, kutakuwepo pia na serikali tatu ambazo ni serikali ya muungano, serikali kuu bara na serikali visiwani.

Swali langu ni kwamba hizi serikali zoooote tatu zitakuwa zinafanya kazi gani kama tayari madara na maamuzi yameshapelekwa majimboni kupitia utawala wa majimbo?

Kama haya maswali yameshatolewa majibu mara nyingi, naomba unipatie hayo majibu au nifahamishe wapi naweza kupata hayo majibu.
 
Vipi kama suala la serikali tatu likiingia kwenye katiba mpya, Chadema itakuwa na utawala wa majimbo kama ikifanikiwa kuchukuwa madaraka?

Mkuu EMT nadhani hili kwa sasa kuna haja ya kuiweka pembeni na ndicho kinachooneka kufanywa na CDM.
Kizingiti ilikuwa ni Zanzibar na kwa sababu tutakuwa na Tanganyika basi Katiba yetu Mpya ya Jamhuri ya Watu wa Tanganyika itakuwa msahafu wetu ujao wa kutuwekea misingi ya Nchi imara yaani Serikali ya Majimbo ambayo mwisho wa siku hii Serikali inayopigiwa chapuo ya JMT itakufa kifo cha taratibu.

Tuwe na subira!
 
Last edited by a moderator:
Kabla sijajadili hoja zako unapaswa kwanza kuzingatia mambo mawili:


  1. Mfumo wa sasa wa Tawala za Mikoa upo kwa malengo ya kuendeleza maslahi ya kisiasa na sio malengo ya kiutawala(Adminstrative goals). Matokeo yake ni kudumaa kwa demokrasia nchini na chimbuko la ukiukwaji wa misingi huru na haki katika ulingo wa kisiasa
  2. Mfumo wa serikali za mitaa unathibiwa kisiasa na watawala mawakala wanaounda Tawala za mikoa.

Hoja dhidi ya Gharama za uendeshaji
Uanzishwaji wa mfumo wa majimbo utapunguza gharama za uendeshaji kwa misingi ifuatayo:

Kwanza, kitasisi, ofisi za kiutawala zitapungua kutoka 30 za mikoa ya leo kufikia vituo vya idadi ya majimbo yasiyozidi kumi na tatu

Pili, ofisi za wakuu wa wilaya, pamoja na ofisi za kitarafa zitafutwa kwasababu hazina tija kwa ustawi na maendeleo ya watanzania.

Tatu, majukumu mengi ya kiutendaji kisekta yatasimamiwa na kutekelezwa katika ngazi ya majimbo na kupunguza majukumu ya kiwizara.

Kwa kuzingatia muktadha huu Wakuu wa nchi wa pande zote mbili watasimamia majukumu ya jumla yanayohusu serikali zao ambapo kimfumo kutakuwa na wizara ambazo zitakuwa zinashughughulikia mambo yasiyo ya muungano.

Ndugu yangu EMT

Malengo makuu ya mfumo wa majimbo ni kuweka uongozi unaotokana na ridhaa ya wananchi kukidhi dhana ya demokrasia na utawala bora. Mfumo ambao utatambua umma wa wananchi kama chimbuko la mamlaka ya utawala na kutegemea utegemezi wa kifikra( Entitled Mentality), kiutendaji na kisera kutoka kwa serikali kuu(central government) kama ilivyo sasa. Serikali za mitaa zitakuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Mamlaka za majimbo.

Nadhani tatizo lako hapa ni hili neno "jimbo" ambalo kimsingi tunaweza liita "mkoa". Hapa unapaswa kuangalia Mfumo wa Uendeshaji na sio jina. Kama utakuwa bado hujaridhika ninaweza kuendelea kutanua wigo wa mjadala
 
Mkuu EMT nadhani hili kwa sasa kuna haja ya kuiweka pembeni na ndicho kinachooneka kufanywa na CDM.
Kizingiti ilikuwa ni Zanzibar na kwa sababu tutakuwa na Tanganyika basi Katiba yetu Mpya ya Jamhuri ya Watu wa Tanganyika itakuwa msahafu wetu ujao wa kutuwekea misingi ya Nchi imara yaani Serikali ya Majimbo ambayo mwisho wa siku hii Serikali inayopigiwa chapuo ya JMT itakufa kifo cha taratibu.

Tuwe na subira!

Kwa hiyo, wakati Tanzania Bara kutakuwa na utawala wa majimbo, Zanzibar hakutakuwa na utawala huo? Ndicho unachotaka kusema?
 
Tunaanza kwanza na serikali tatu, halafu ikipita tutakuwa na mchakato wa kutengeneza Katiba ya Tanganyika na hapo sera ya majimbo itaeleweka vizuri!!
 
Mkuu EMT, kuna sintonfahamu kubwa sana juu ya upi msimamo wa CDM kwenye hili suala la katiba mpya, ukiwa makini sana na kufuatilia mwenendo wa hawa wapinzani ni kuwa hawana msimamo madhubuti wanafuata wanachohakikisha ni kuwa wanaipinga misimamo ya CCM katika katiba mpya. Kutokana na hili CCM wamewashitukia na wanawaburuza kisawa sawa mfano ni pale CCM ilipopretend haiitaki serikali 3 ghafla tukawaona wana CDM wakizunguka Nchini na kuipraise rasimu. full vituko.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
Chadema ni chama cha mashetani mkuu.

Huyu Mbulula naye anahesabu kachangia hoja....
i better log off maana nikiendelea kusoma uharo kama huu nikutafuta lupango bila sababu.
adios.
 
Kabla sijajadili hoja zako unapaswa kwanza kuzingatia mambo mawili:


  1. Mfumo wa sasa wa Tawala za Mikoa upo kwa malengo ya kuendeleza maslahi ya kisiasa na sio malengo ya kiutawala(Adminstrative goals). Matokeo yake ni kudumaa kwa demokrasia nchini na chimbuko la ukiukwaji wa misingi huru na haki katika ulingo wa kisiasa
  2. Mfumo wa serikali za mitaa unathibiwa kisiasa na watawala mawakala wanaounda Tawala za mikoa.

Hoja dhidi ya Gharama za uendeshaji
Uanzishwaji wa mfumo wa majimbo utapunguza gharama za uendeshaji kwa misingi ifuatayo:

Kwanza, kitasisi, ofisi za kiutawala zitapungua kutoka 30 za mikoa ya leo kufikia vituo vya idadi ya majimbo yasiyozidi kumi na tatu

Pili, ofisi za wakuu wa wilaya, pamoja na ofisi za kitarafa zitafutwa kwasababu hazina tija kwa ustawi na maendeleo ya watanzania.

Tatu, majukumu mengi ya kiutendaji kisekta yatasimamiwa na kutekelezwa katika ngazi ya majimbo na kupunguza majukumu ya kiwizara.

Kwa kuzingatia muktadha huu Wakuu wa nchi wa pande zote mbili watasimamia majukumu ya jumla yanayohusu serikali zao ambapo kimfumo kutakuwa na wizara ambazo zitakuwa zinashughughulikia mambo yasiyo ya muungano.

Ndugu yangu EMT

Malengo makuu ya mfumo wa majimbo ni kuweka uongozi unaotokana na ridhaa ya wananchi kukidhi dhana ya demokrasia na utawala bora. Mfumo ambao utatambua umma wa wananchi kama chimbuko la mamlaka ya utawala na kutegemea utegemezi wa kifikra( Entitled Mentality), kiutendaji na kisera kutoka kwa serikali kuu(central government) kama ilivyo sasa. Serikali za mitaa zitakuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Mamlaka za majimbo.

Nadhani tatizo lako hapa ni hili neno "jimbo" ambalo kimsingi tunaweza liita "mkoa". Hapa unapaswa kuangalia Mfumo wa Uendeshaji na sio jina. Kama utakuwa bado hujaridhika ninaweza kuendelea kutanua wigo wa mjadala

Sikatai kuwa mfumo wa sasa wa tawala za mikoa una malengo ya kisiasa zaidi kuliko ya kiutawala na kimaendelea.

Sikatai kuwa mfumo wa tawala za mikoa unadhibitiwa kisiasa na watawala mawakala wanaounda tawala za mikoa.

Pia sikatai kuwa uanzishwaji wa mfumo wa majimbo utapunguza gharama za uendeshaji.

Vile vile sipingi malengo ya utawala wa majimbo.

Suala langu lipo kwenye how do you reconcile utawala wa majimbo na serikali tatu?

Chukulia, kwa mfano, madaraka ya magavana wa majimbo katika nchi kama Marekani au mawaziri wakuu wa majimbo ya Afrika ya Kusini.

Huoni kuwa madaraka ya wakuu wa serikali ya Bara na ile ya Zanzibar yatakuwa almost sawa na madaraka ya magavana wa majimbo?
 
Tunaanza kwanza na serikali tatu, halafu ikipita tutakuwa na mchakato wa kutengeneza Katiba ya Tanganyika na hapo sera ya majimbo itaeleweka vizuri!!

Kwa hiyo serikali ya majimbo itakuwa Bara tuu na siyo Zanzibar?
 
CHADEMA wanataka kuwe na serikali tatu. Wakati huo huo wanataka kuwe serikali ya majimbo. Kwa maana hiyo, kutakuwa na Rais wa Muungano na wakuu wawili wa serikali za Bara na Zanzibar. Pia kutakuwepo na gavana katika kila jimbo ambao watakuwa na mamlaka kamili kwenye majimbo yao.

Ukiondoa suala la gharama ambalo kwa demokrasia ni vyema kuzipitia kiutawala hii imekaa sawa? Utawala wa majimbo chini ya serikali tatu unawezekana? Dhana kuu ya sera ya serikali ya majimbo ni kuhamisha madaraka ya maamuzi kutoka kwa watu wachache na kuyarejesha mikononi mwa wananchi vijijini.

Kama ni hivyo, hizo serikali mbili za Bara na Zanzibar zitakazokuwa zinaongozwa na wakuu wawili zitakuwa zinafanya nini? Madaraka ya wakuu wa serikali hizo mbili hayatagongana na madaraka ya magavana wa majimbo? Kama serikali moja chini ya utawala wa majimbo haiwezekani, solution ni kuwa na utawala wa majimbo chini ya serikali tatu?

Serikali za majimbo ni tamu hasa mnapoamua kuwa na serikali moja kama ilivyo Marekani. Tatizo ni Wazanzibar ambao muungano wanautaka huku wakitaka kuwa na madaraka yao hapo hapo. Hiyo haiwezekani. Tukubali serikali tatu kwa sasa hasa ukizingatia matukio ya kidhalimu yanayotokea Zanzibar kwa sasa. Kuendelea kung'ang'ania serikali mbili hasa kwa wenzangu wa CCM kwa sasa ni kuendeleza maumivu kwa wakristo wanaoishi Zanzibar hasa ukizingatia maelezo yaliyotolewa na padri kutoka Zanzibar hivi karibuni. Tatizo lilipo kwenye CCM kwa sasa ni watu kukosa ajira na kudhani ukitoa maoni tofauti wa wakubwa ambao ni watu wachache tu hata kumi hawafiki basi mtu hawezi kupata ukuu wa wilaya au mkoa. Haya ni makosa makubwa, tutakuwa na kizazi ambacho hakitaweza kufikiri mbele itakuwaje.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Serikali za majimbo ni tamu hasa mnapoamua kuwa na serikali moja kama ilivyo Marekani. Tatizo ni Wazanzibar ambao muungano wanautaka huku wakitaka kuwa na madaraka yao hapo hapo. Hiyo haiwezekani. Tukubali serikali tatu kwa sasa hasa ukizingatia matukio ya kidhalimu yanayotokea Zanzibar kwa sasa. Kuendelea kung'ang'ania serikali mbili hasa kwa wenzangu wa CCM kwa sasa ni kuendeleza maumivu kwa wakristo wanaoishi Zanzibar hasa ukizingatia maelezo yaliyotolewa na padri kutoka Zanzibar hivi karibuni. Tatizo lilipo kwenye CCM kwa sasa ni watu kukosa ajira na kudhani ukitoa maoni tofauti wa wakubwa ambao ni watu wachache tu hata kumi hawafiki basi mtu hawezi kupata ukuu wa wilaya au mkoa. Haya ni makosa makubwa, tutakuwa na kizazi ambacho hakitaweza kufikiri mbele itakuwaje.
 
Kwa hiyo, kuwe na serikali tatu na pia utawala wa majimbo? Moja ya misingi ya sera ya Chadema ya utawala wa majimbo ni kushusha na kugawa madaraka. Hii itafanya maamuzi yafanywe na kwenye ngazi za chini kuliko ilivyo sasa.

Lengo la utawala wa majimbo ni kuifanya serikali kuu ijishughulishe na mambo machahe. Serikali ya majimbo itawezesha pia wananchi kushiriki na kushirikishwa kwa karibu zaidi katika shughuli za maendeleo katika majimbo yao.

Hata hivyo, Chadema inaunga mkono kuwepo kwa serikali tatu. Kwa maana hiyo, pamoja na kuwepo kwa serikali ya majimbo, kutakuwepo pia na serikali tatu ambazo ni serikali ya muungano, serikali kuu bara na serikali visiwani.

Swali langu ni kwamba hizi serikali zoooote tatu zitakuwa zinafanya kazi gani kama tayari madara na maamuzi yameshapelekwa majimboni kupitia utawala wa majimbo?

Kama haya maswali yameshatolewa majibu mara nyingi, naomba unipatie hayo majibu au nifahamishe wapi naweza kupata hayo majibu.

Serikali za Majimbo ni Sera ya Chadema itakapoungwa mkono kushika madaraka.

Serikali tatu ni mapendekezo yaliyopo mezani ambayo wote tunashiriki kuyajadiri na kuyatolea maamuzi bila kujali itikadi zetu.

Nakukumbusha tu sera ya CCM ni UJAMAA na KUJITGEMEA. Tumekuwa wajamaa lini na tunajitegemea kivipi?

Hoja yako mezani naiona kama ya kichochezi kwa sababu suala la majimbo halipo kwenye mjadala wa sasa kuhusu katiba. Suala la serikali tatu ndilo suala mezani tujadili.

Narudia kwa hali ya sasa nafarijika na maoni ya Katiba kuhusu serikali tatu na hasa ya ikiwemo serikali HALISI YA TANGANYIKA.
 
Kitendawili: Ili upate wachangiaji wengi kwenye uzi wako hapa JF ni lazima ukitaje Chama Gani????

Mkuu hilo liko wazi,Kama vile ukitaka uuze gazeti ni lazima uandike habari zake...!
 
Back
Top Bottom