CHADEMA wanataka kuwe na serikali tatu. Wakati huo huo wanataka kuwe serikali ya majimbo. Kwa maana hiyo, kutakuwa na Rais wa Muungano na wakuu wawili wa serikali za Bara na Zanzibar. Pia kutakuwepo na gavana katika kila jimbo ambao watakuwa na mamlaka kamili kwenye majimbo yao.
Ukiondoa suala la gharama ambalo kwa demokrasia ni vyema kuzipitia kiutawala hii imekaa sawa? Utawala wa majimbo chini ya serikali tatu unawezekana? Dhana kuu ya sera ya serikali ya majimbo ni kuhamisha madaraka ya maamuzi kutoka kwa watu wachache na kuyarejesha mikononi mwa wananchi vijijini.
Kama ni hivyo, hizo serikali mbili za Bara na Zanzibar zitakazokuwa zinaongozwa na wakuu wawili zitakuwa zinafanya nini? Madaraka ya wakuu wa serikali hizo mbili hayatagongana na madaraka ya magavana wa majimbo? Kama serikali moja chini ya utawala wa majimbo haiwezekani, solution ni kuwa na utawala wa majimbo chini ya serikali tatu?
Binafsi nadhani Chadema walipokuja na hoja ya majimbo, hawakutarajia kwamba baadae, hoja ya serikali tatu ingepokelewa kwa mikono miwili na umma; Nadhani (sina uhakika) Chadema wali amini kwamba kuivunja 'unitary system' iliyopo isingekuwa kitu kirahisi, sasa kwa vile nia yao kama chama ni kutafuta ufanisi zaidi ndani ya mfumo uliopo, basi wakaona kwamba sera ya majimbo ingekuja na jibu ambapo madaraka na maamuzi juu ya uendeshaji wa serikali pamoja na rasilimali za wananchi, masuala haya (maamuzi na madaraka) yanasogea karibu zaidi na wananchi, badala ya kuwa centralized kama sasa ambapo manufaa kwa wananchi hayaonekani;
Katika mazingira ya sasa ambapo hoja ya Tanganyika inazidi kupamba moto, kuna umuhimu wa Chadema kujipanga vizuri ili wasionekane kwamba wanachanganya wananchi kwani ni jambo rahisi sana kwa viongozi wa CCM kubomoa hoja ya serikali tatu iwapo itaunganishwa na hoja ya serikali ya majimbo, hasa katika muktadha wa muungano kama ulivyoainisha hapo juu ambapo kwa kweli its impractical in a multitude of ways;
That said and done, haina maana kwamba taifa haliwezi kuwa na federal government, provincial governments and local governments kwa wakati mmoja kwani mafanikio ya federalism duniani (USA, Canada na Australia) wote wanafuata mfumo wa namna hii na wamekuwa na ufanisi wa hali ya juu katika kuboresha maisha ya wananchi wao, na ni sababu kubwa kwanini mataifa mengi yanakimbilia mfumo wa shirikisho vis a vis unitary system of governance; Tukichukulia mfano wa Marekani, taifa hili lina serikali zaidi ya hamsini (50) – kwa mfano, kuna federal government yenye katiba yake, na pia kuna 50 states, kila moja ikiwa na Katiba zake; Hii ni nje ya serikali za mitaa ambazo pia zipo marekani, na zipo zaidi ya serikali za mitaa 30,000 (elfu thelathini); Tukiingia Canada, they have ten provinces, each with its own government, kwahiyo ukijumlisha na serikali kuu, Canada ina serikali sio chini ya kumi na moja; Tukienda Australia, kule kuna six provinces , hivyo kufanya jumla ya serikali kuwa sio chini ya saba; Kwa maana hii, shirikisho la serikali tatu, nne, tano, kumi.... sio tatizo, suala la maana ni je, nani ni washirika wa shirikisho husika? Lengo lao ni kufanikisha nini? Wapo tayari ku surrender mambo gani kwa shirikisho husika? Vinginevyo wananchi katika taifa lolote lile huwa tayari kugharamia mfumo wowote ambao haulazimishwi kwao bali unaotokana na matakwa yao baada ya kuridhika juu ya ufanisi wa mfumo husika;
Nimalizie kwa kusema kwamba - kama Chadema inakabaliwa na changamoto kubwa katika mjadala unaoendelea, basi zaidi ni katika kutetea hoja juu ya mfumo wa shirikisho la serikali tatu unaofuata sera ya majimbo; Hoja ya Chadema inaweza kuwa practical kwa njia tatu:
- Kwanza iwapo Zanzibar 'kwa hiyari yake' itaamua to surrender safari yake towards full autonomy and self determination na badala yake kukubali kutambulika kama moja ya majimbo ya "Tanzania"; Hata hivyo, chini ya utaratibu huu, haitakuwa tena serikali tatu, bali kuu moja na nyingine kadhaa za majimbo ya tanganyika na majimbo ya zanzibar (aidha kama jimbo moja au kama mawili - Pemba na Unguja); Chini ya utaratibu huu, Zanzibar kama jimbo pamoja na majimbo mengine ya Tanganyika (lets say seven provinces?) kutakuwepo na distribution of power kwa majimbo husika, with each of the spheres (majimbo) having 'constitutionally' given powers and functions kama ilivyo kwa majimbo ya Marekani, n.k; Chini ya mfumo huu, the federal government will have powers of over sight over provincial governments (Za Tanganyika na Zanzibar), & provincial governments will have power of oversight on municipal governments;
- Pili, iwapo Tanganyika na Zanzibar zitaamua kwa hiyari kuungana, huku wakikubaliana kwamba mamlaka halisi yabakie katika nchi moja moja binafsi; Katika mfumo huu, serikali kuu (ya muungano) haitakuwa na nguvu; Mfano mzuri ni mfumo wa European Union ambapo nchi binafsi kama vile Ufaransa, Ujerumani, Uingereza, Uholanzi, Italia, Ureno, n.k zina nguvu ya kufanya maamuzi ya mwisho na sio bunge la Jumuiya ya Ulaya au Watendaji wake;
- Tatu, iwapo Muungano utavunjika, hivyo Tanganyika to pursue mfumo wa majimbo kwa urahisi zaidi;
Nje ya sura hizi tatu, binafsi sioni jinsi gani Chadema wanaweza kutetea Sera ya majimbo katika muktadha wa muungano; Vinginevyo ningependa kuelimishwa zaidi juu ya hili;