EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,347
- Thread starter
- #41
Serikali za majimbo ni tamu hasa mnapoamua kuwa na serikali moja kama ilivyo Marekani. Tatizo ni Wazanzibar ambao muungano wanautaka huku wakitaka kuwa na madaraka yao hapo hapo. Hiyo haiwezekani. Tukubali serikali tatu kwa sasa hasa ukizingatia matukio ya kidhalimu yanayotokea Zanzibar kwa sasa. Kuendelea kung'ang'ania serikali mbili hasa kwa wenzangu wa CCM kwa sasa ni kuendeleza maumivu kwa wakristo wanaoishi Zanzibar hasa ukizingatia maelezo yaliyotolewa na padri kutoka Zanzibar hivi karibuni. Tatizo lilipo kwenye CCM kwa sasa ni watu kukosa ajira na kudhani ukitoa maoni tofauti wa wakubwa ambao ni watu wachache tu hata kumi hawafiki basi mtu hawezi kupata ukuu wa wilaya au mkoa. Haya ni makosa makubwa, tutakuwa na kizazi ambacho hakitaweza kufikiri mbele itakuwaje.
Kwa hiyo sera ya Chadema ya majimbo umewekwa kapuni effectively mpaka hapo muungano utakapovunjika?