CHADEMA (Odinga) vs CCM (Uhuru) siasa za nje!

CHADEMA (Odinga) vs CCM (Uhuru) siasa za nje!

Ni lini CHADEMA wametangaza kumuunga mkono Odinga au Kenyata au CCM wametangaza lini mbona mnapenda kuzusha mambo na kujiingiza kwenye siasa za watu.....mambo ya kenya waachieni wakenya wenyewe mara huyu hivi yule vilee Watanzania bana ya kwenu yamewashinda mnaanza umbea

........

CCM walitangaza kumuunga Raila mkono kupitia kwa Magufuli kitu ambacho Wenje alipinga sana akisema kama Tanzania ina side na Raila, uhusiano wetu na Kenya utakuwaje pindi akishinda mtu mwingine zaidi ya Raila.

Ssasa ni lini tena Chadema walimuunga mkono Raila mtu ambaye walipinga alipoungwa mkono na Magufuli?
 
Uhuru ana mtazamo unaofanania sera za chadema

kukuza uchumi kwa ushirikishwaji wananchi kuanzia mashinani


......

Duh..!!Chadema siwawezi mshaanza kujirudisha polepole kwa uhuru..
Sasa kama siasa ya Uhuru ni sawa na ya Chadema iweje mkamkampenia Kibaki?au mlipoona mikutano yake inajaza watu mkadhani ndo ameshapita?.
 
Sina tatizo na Wakenya lakini ukweli ni kwamba siasa zao ni tofauti kabisa na inavyodhaniwa.

Magufuli na Rostam wanampigia upatu Odinga hali wengine wanasema CCM wanamkubali Kenyatta na CHADEMA wanamkubali Odinga kitu ambacho mimi sikiamini.

Kwa namna ninavyoijua CCM huenda wamesapoti pande zote mbili ndiyo maana nina msimamo tofauti.Hata kama atashinda Odinga au Kenyatta hakuna uhusiano wa moja kwa moja na CHADEMA au CCM!
 
sijui utajificha wapi?unaropoka ropoka tu,haya chadema ya kenya imeangukia pua,CDM ya tanzania ijiandae
 
John Pombe Magufuli alikwenda kuzindua kampeni za Odinga na kumpigia debe, je ndani ya CCM yuko katika nafasi gani? Je ni hatua zipi za kinidhamu anastahili kuchukuliwa na CCM?!

......

John Pombe Magufuli anaonekana live ktk clip hii ya ODM Conference kuanzia sekundeya 10 ya clip hii ya Video

ODM National Delegates Conference
Published on 7 Dec 2012Raila endorsed as ODM'S Presidential candidate
Prime minister Raila Odinga has officially received his ODM party's nod to run for president in the forthcoming elections.

While accepting his nomination in a highly attended ODM national delegates confrence at Kasarani gymnasium,


source: K24TV Kenya ya youtube
 
Last edited by a moderator:
Ni ukweli usiotiliwa shaka kuwa CCM inainjinia uchaguzi wa Kenya, na ipo upande wa Uhuru mmoja wa wagombea urais wa Kenya.

Vivyo hivyo chama kikuu cha upinzani nchini CHADEMA, kimejikita katika siasa za kimataifa kwa hapo Kenya huku karata yake kikiitupa miguuni mwa Raila Odinga mmoja wa wagombea anaepewa nafasi kubw ya kushinda kupitia muungano wa vyam ndugu.

Vita hii tunaiangaza kama ni yamapambano ya CHADEMA na CCM kuelekea 2015 hasa kila mmoja akisafisha njia ya kuungwa mkono kumataifa.

Ikiwa ni hivyo tayari ccm na CHADEMA kila mmoja ashashinda kete moja moja, kwanza ni CHADEMA Zambia kwa bwana Satta, na CCM Congo kwa kijana Kabila ambako dhahiri utawala unakula huku umeshikilia sahani mkononi kwani hakuna tumaini la kuweka mezani chakula chini ya M23.

Je ni CHADEMA (Odinga) ama CCM (Uhuru)


Karata yangu naitua kwa CHADEMA.


......

KAMANDA TUJUZE KAMA WEWE NI msemaji wa CHADEMA "MNYIKA" AU CCM "NAPE"
 
Dalili ya anguko la chadema 2015 uhuru kachukua nchi kudadadadeki ikulu full mafegi
 
[h=4]Kenya Population by Ethnic Affiliation - Main Tribes[/h]Kikuyu tribe – 6,622,576
Luhya tribe - 5,338,666
Kalenjin tribe – 4,967,328
Luo tribe – 4,044,440
Kamba tribe – 3,893,157
Somali tribe – 2,385,572
Kisii tribe – 2,205,669
Mijikenda tribe – 1,960,574
Meru tribe -1,658,108
Turkana tribe – 988,592
Maasai tribe - 841,622
Teso tribe – 338,833
Embu tribe – 324,092
Taita tribe – 273,519
Kuria tribe – 260,401
Samburu tribe – 237,179
Tharaka tribe – 175,905
Mbeere – 168,155
Borana – 161,399
Basuba – 139,271
Swahili – 110,614
Gabra – 89,515
Orma – 66,275
Rendile – 60,437
Tatizo la ukabila sio sana kama mnavyofikiri.

Kenya Population | Kenya
 
Acha unafiki hivyo ni vyama vipo Kenya asa ccm na chadema wanaingiaje! Ushindi wa uraisi wa Kenya upo mikononi mwa Wakeny,ataeshinda tutakuwa nae
 
mmhh hapo hakuna cha uccm wala ucdm ....jubilee ni jubilee na cord ni cord
 

Duh..!!Chadema siwawezi mshaanza kujirudisha polepole kwa uhuru..
Sasa kama siasa ya Uhuru ni sawa na ya Chadema iweje mkamkampenia Kibaki?au mlipoona mikutano yake inajaza watu mkadhani ndo ameshapita?.
Mwai tena!!,hiyo ya kuungwa mkono kivyama ni porojo tu

zimetokana na historia zaidi za wagombea hao
 
The problem with you guys ni kwamba hamfahamu hapa Afrika kuwa mpinzani anakuwa mwenza wako kabla hajaingia madarakani na akishaingia si mwenzako tena bali ni mwenza wa hasimu wako....!! Hata kama Raila yupo damudamu na CHADEMA, unazani ataendelea kuwa hivyo akishaingia madarakani ili ajiingize kwenye mgogoro na serikali ya CCM?! Katika Afrika, serikali ya nchi moja ku-support oppostion of neighboring country(in any way), will always create diplomatic conflict btn the countries! Hakuna nchi Afrika ambae inaweza kukaribisha jambo kama hilo unless hizo nchi tayari ziwe tayari zina mgogoro kati yao. So, to kuct story short, leo hii Raila akishinda, nyie mwenza wenu ni Uhuru and no longer Raila...open your eyes!

greater thnker!
 
Thread hii ni sawa na watoto wamekaa pembeni ya barabara wantambishiana magari yanayopita," gari hii ya kwangu ona inavyokimbia".
 
CCM ni makini sana, wala hawakutamka kuhusu uungaji mkono kwa mgombea yeyote; CHADEMA kutokana na kukosa ukomavu na busara wamejiingiza kichwa kichwa kumuunga mkono ODINGA, jioni ya leo watakula jeuri yao na kupata pigo la kisiasa tukielekea uchaguzi 2014 na 2015

Hebu tusaidie, ni wapi CHADEMA wamesema wanamuunga mkono Odinga?
 
Thread hii ni sawa na watoto wamekaa pembeni ya barabara wantambishiana magari yanayopita," gari hii ya kwangu ona inavyokimbia".

Mkuu umenifanya nicheke sana. Nakumbuka tumecheza mchezo wa kuwahi magari. Wakati mwingine mpaka kugombana kwa sababu mwenzako ameliwahi gari "lako". Hakika hiki ki thread ni cha kipuuzi...
 
Back
Top Bottom