Nimefurahishwa na kitu kimoja kwamba walau sasa demokrasia inakomaa Tanzania.Wananchi wamefumbuka na wanaelewa mbivu na mbichi.Wakati wa kudanganya watu umepita kwani vijana wanazidi kupata elimu ya uraia.
Niseme wazi kwa hapa ilipofikia ni vigumu Chadema kusambaratika.Ni kwa nini nasema hivyo.Nakumbuka miaka ile ya 90 wakati NCCR wakiwa na nguvu kubwa,pale role model alikuwa anaonekana mtu mmoja tu Augustine Lyatonga Mrema basi! Wafuasi wake walifanya chochote kisa Mrema kasema.Wafuasi wake walifikia kumbeba kama maiti!!!
Chadema ni tofauti sana.Hakuna mtu maarufu pale bali chama ndicho maarufu.Kama mwanademokrasia niwapongeze viongozi wa chadema kwa kuijenga chadema kama taasisi.Chadema leo anaweza kuondoka mtu yeyote na chama kikabaki imara sana.Angalieni mfano mdogo tu mauaji ya Nyamongo.Alienda kule Godbless Lema wanasiasa wakasema maneno mengi sana kwamba Lema anachochea vurugu kule,alivyoenda Marando na Tundu Lissu wakasema afadhali Lema kuliko hawa!!! Walisema Slaa asipokuwa bungeni chadema imekufa na wananchi hawatapata mtetezi tena walipoingia kina Mdee,Mnyika,Zitto,Lema na Wenje wakasema afadhali ya Slaa.Wakati wapiganaji wa chadema wakiwa bungeni huku nje Slaa anaongoza mashambulizi makali mikoani akiwa na akina Mpendazoe,Abdallah Safari,Marando,Mwita Mwikabe,Wilfred Lwakatare,Benson Kigaila na wengine siwamalizi kuwataja.
Hatimaye demokrasia imekua na ni vigumu sana kuimaliza Chadema..utamfunga nani uimalize nguvu? Labda wote uwapeleke gerezani kitu ambacho hakiwezekani.
Nimekosa la kusema ndio maana naiona Chadema kama timu maarufu ya mpira ya REAL MADRID.....
Niseme wazi kwa hapa ilipofikia ni vigumu Chadema kusambaratika.Ni kwa nini nasema hivyo.Nakumbuka miaka ile ya 90 wakati NCCR wakiwa na nguvu kubwa,pale role model alikuwa anaonekana mtu mmoja tu Augustine Lyatonga Mrema basi! Wafuasi wake walifanya chochote kisa Mrema kasema.Wafuasi wake walifikia kumbeba kama maiti!!!
Chadema ni tofauti sana.Hakuna mtu maarufu pale bali chama ndicho maarufu.Kama mwanademokrasia niwapongeze viongozi wa chadema kwa kuijenga chadema kama taasisi.Chadema leo anaweza kuondoka mtu yeyote na chama kikabaki imara sana.Angalieni mfano mdogo tu mauaji ya Nyamongo.Alienda kule Godbless Lema wanasiasa wakasema maneno mengi sana kwamba Lema anachochea vurugu kule,alivyoenda Marando na Tundu Lissu wakasema afadhali Lema kuliko hawa!!! Walisema Slaa asipokuwa bungeni chadema imekufa na wananchi hawatapata mtetezi tena walipoingia kina Mdee,Mnyika,Zitto,Lema na Wenje wakasema afadhali ya Slaa.Wakati wapiganaji wa chadema wakiwa bungeni huku nje Slaa anaongoza mashambulizi makali mikoani akiwa na akina Mpendazoe,Abdallah Safari,Marando,Mwita Mwikabe,Wilfred Lwakatare,Benson Kigaila na wengine siwamalizi kuwataja.
Hatimaye demokrasia imekua na ni vigumu sana kuimaliza Chadema..utamfunga nani uimalize nguvu? Labda wote uwapeleke gerezani kitu ambacho hakiwezekani.
Nimekosa la kusema ndio maana naiona Chadema kama timu maarufu ya mpira ya REAL MADRID.....