Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,556
- 272,296
Hii ni baada ya kampeni yao ndogo sana na ya muda mfupi ya kuhamasisha wananchi kususia uchaguzi feki wa serikali za mitaa kuungwa mkono na wananchi kwa zaidi ya 90%, hii ni rekodi.
Kwa mfano, msimamizi mmoja wa kituo cha uchaguzi jijini Dar es salaam ametoa siri kwamba kati ya watu zaidi ya 500 waliojiandikisha, waliopiga kura hawakufika 50, hii ni pamoja na wale wanaojifanya wanaccm, maana ya jambo hili ni kwamba ccm imekataliwa hata na wanaojiita wanachama wake yenyewe, hii ni hatua kubwa sana na ya kujivunia kwa wapinzani, maana sasa ni wazi kwamba wamefanikiwa mipango yao ya kupenya kwenye ngome za ccm na hivyo kujitengenezea mtaji wa baadaye.
Hakika Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana!
======
Maoni ya wadau
Kwa mfano, msimamizi mmoja wa kituo cha uchaguzi jijini Dar es salaam ametoa siri kwamba kati ya watu zaidi ya 500 waliojiandikisha, waliopiga kura hawakufika 50, hii ni pamoja na wale wanaojifanya wanaccm, maana ya jambo hili ni kwamba ccm imekataliwa hata na wanaojiita wanachama wake yenyewe, hii ni hatua kubwa sana na ya kujivunia kwa wapinzani, maana sasa ni wazi kwamba wamefanikiwa mipango yao ya kupenya kwenye ngome za ccm na hivyo kujitengenezea mtaji wa baadaye.
Hakika Utukufu wa Mungu ni wa ajabu sana!
======
Maoni ya wadau
Mngekuwa mnafanya mambo yenu kisayansi, hii ilikuwa ni fursa yenu nzuri sana ya kuanzia kampeni zenu, kuanzia sasa na kwenda mbele.
Mngekuwa mmejipanga vizuri kunasa namba sahihi ya:
- waTanzania waliojiandikisha kupiga kura
- waTanzania waliojitokeza kupiga kura
- sababu hasa zilizosababisha kuwepo upungufu, kama namba zenu hizo zitawaonyesha hivyo
- ni maeneo yapi hasa ya nchi yanayohitaji kulengwa kwa karibu na ufuatiliaji wa mara kwa mara
- ni viongozi (watu) gani hasa kwenye jamii mnaotakiwa kuwalenga ili kazi yenu ifane, n.k,. n.k.
Haya yote yangewasaidia kuelekeza nguvu zenu huko huko wananchi wanakoelekea ili kuwasaidia kujipanga vizuri kukabili yajayo.
Kwa bahati mbaya sana Erythro, mipango yenu bado mnaifanya kishaglabagara na kama kubahatisha tu, kama unavyotueleza katika mada yako hii.
Namba za hayo unayosema hapo zipo wapi na wapi?
Kazi ya kufanya siasa ni aina ya sayansi fulani. Inazo taratibu zake, sio kurukia tu mambo.
Kuna wakati, miaka michache iliyopita niliwaona kama mmeanza kuelekea huko, lakini hapa katikati, mmeonyesha kuvurugwa sana, na zile hatua za mwanzo mlizokuwa mmezianza zote zimepotea.
Ajabu ni kwamba, ruzuku yenu iliongezeka, na kila mtu angetegemea muitumie vizuri kuwafundisha vijana wenu wafanye kazi zao kisayansi, - matokeo yanaonyesha kinyume cha hapo!
Hata kuajiri ma-'consultant', nguli wa mambo haya kwa muda tu pia imewawia vigumu? Raslimali zenu mmezitawanya wakati ambapo mlitakiwa mzitumie kwa makini sana wakati huu ambao mabavu yanatumika kuwamaliza.
Haya maguvu mngeweza kuyapiku kwa kutumia sayansi, huku mkitumia akili zaidi.
Ona sasa mnavyoendeshwa!
