CHADEMA na Vitega Uchumi Vyake - Ni vipi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Chama cha Demokrasia na Maendeleo kama vilivyo vyama vingine bila ya shaka kimekuwa na mipango ya vitega uchumi ili kiweze kujiendesha na kufadhili shughuli zake mbalimbali bila ya kutegemea sana ruzuku au misaada ya wafadhili. Je, Chama hiki sasa hivi kina miradi gani kitega uchumi, yenye kuingiza faida gani, na inasimamiwaje? Au ndio "hatuna fedha ya kutosha, ruzuku yenyewe kidogo, na CCM wao wanajichotea mabilioni".

Je, Chadema imeweza kuanzisha sekondari moja ya Chama ikajionesha kuwa ni nzuri na ikashindanishwa na sekondari nyingine binafsi na za serikali?

Je, Chadema imeweza kuanzisha Kliniki au hospitali fulani ya Chama kwa ajili ya wananchi n.k

Je, Chadema imeshikiri vipi katika harakati za kusafisha jiji la Dar na kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu kwa kutoa mafunzo n.k?

Je, Chadema imeweza kujenga jengo lolote ambalo ni la kisasa na wakaweza kulipangisha kama kitega uchumi?

Je, Chadema wameweza kuanzisha kampuni ya kibiashara ambayo iko chini ya Chama na kuonesha jinsi wanaweza kusimamia miradi hiyo?

Je, CHadema ina vitega uchumi vipi kama Chama vinavyoonesha uwezo wa kusimamia miradi, kupanga, na kudhibiti mapato na matumizi zaidi ya fedha zinazoingia kwenye chama kupitia michango, ruzuku na misaada?
 
Mzee,wats behind the curtain??I can spot ur fully loaded missiles towards CHADEMA!Nway,hope ur questions have some answers.Watakuja kuyajibu wenye majibu.
 
Mzee,wats behind the curtain??I can spot ur fully loaded missiles towards CHADEMA!Nway,hope ur questions have some answers.Watakuja kuyajibu wenye majibu.

kuna msemo mmoja husema "chuma hunoa chuma..".. usijiumize kichwa ndugu yangu. Dhahabu hupitishwa kwenye tanuru ili ang'ae vinginevyo itabakia jiwe gumugumu tu na isiyo na thamani yake halisi!
 
Vitega uchumi vya nini? chama cha siasa...au chadema imeshakuwa investements company
 
Vitega uchumi vya nini? chama cha siasa...au chadema imeshakuwa investements company


ah yeah!? unafikiri vyama havina vitega uchumi; chama kinachojiendesha kwa ruzuku, misaada na ada tu kinajinyima uwezo chenyewe! Swali hili pia lingeulizwa kwa CUF vile vile!
 
lakini kaka unajua hiyo si inatokana na kiongozi mwenye VISION?

dont tell me you expected anything serious from Freeman Mbowe ambaye hataki kuwa clean na open kuhusu allegations kuwa alifanya GROSS ACADEMIC MISCONDUCT kule Hull University

Sasa Mwenyekiti wa chama hataki kuwa open kuhusu hili what makes you think atakuwa clean on Vitega uchumi na sources zao of funding?
 
ah yeah!? unafikiri vyama havina vitega uchumi; chama kinachojiendesha kwa ruzuku, misaada na ada tu kinajinyima uwezo chenyewe! Swali hili pia lingeulizwa kwa CUF vile vile!
Ulishawauliza CUF na Chadema wakwambia hawana..vitega uchumi..??
 
Hebu tuangalie na kwa wenzetu walotuzidi kama Marekani? Je DEMOCRATIC ama REPUBLICAN wana vitega uchumi? Kama ni kweli hakuna shida. Pia tujiulize vitega uchumi ilivyonavyo CCM ni vya kwake kweli ama iliviteka? Mfano mmoja ni Uwanja wa CCM Kirumba wazee wetu walikuwa wanachangia kwa lazima, hapo naweza kusema ni wa CCM? Pia unapotaka kuanzisha kitega uchumi si lazima uwe na mtaji? Je huo mtaji utaupata wapi? au ndo mambo ya kuingia ubia? Je wabia wakiwa mafisadi? hicho kitakuwa chama kweli au balaa.
 
Vitega uchumi vya vyama vya siasa ni watu madhubuti na makini ktk utendaji. Biashara ni mwiko kwani haya sii makampuni ya kibiashara na ndio maana kuna mswaada wa kutenganisha biashara na siasa. Kama ni suala la usimamizi, CHADEMA labda wapewe jukumu la kukusanya na kuisimamia mojawapo ya kodi zetu mfano ya foroza au VAT tuone kama watashindwa...!
 
kwanza kiongozi wao aite press conference aweke wazi kuhusu huu uvumi unaoendelea kuwa alijaribu kununua cheti toka kwa yule jamaa aliyemuuzia lile gari
 
Mzee Mwanakijiji, please give them a break! yes they are still infants usiwafananishe na CCM na vitegauchumi wao ambao Sisi wazamani wote tumechangia kwa lazima kwa kukatwa toka mishahara yetu enzi za chama kimoja.

Kama serikali ilikubali kuivunja NBC ili kuweka uwanja sawa wa ushindani kwenye sekta ya mabenki, tulipoanza mfumo wa vyama vingi, CCM ilitakiwa kusurender mali zote ilizohodhi kwa lazima, vyama vyote vianze moja kwenye uwanja sawa wa ushindani.

Hizi mechi za ushindani kugombea kisu cha kula keki ya taifa huku mmoja amekamata kwenye mpini mwingine ashike kwenye makali halafu mvutane...

Ni mpaka pale watakapojitokeza wanasheria mahiri kama kina Shivji, wakaishitaki CCM irudishe mali zote iliuzopora kwa watanzania ili kuweka playing ground level, vinginevyo...CCM itatawala milele!.
 
lakini kaka unajua hiyo si inatokana na kiongozi mwenye VISION?

dont tell me you expected anything serious from Freeman Mbowe ambaye hataki kuwa clean na open kuhusu allegations kuwa alifanya GROSS ACADEMIC MISCONDUCT kule Hull University

Sasa Mwenyekiti wa chama hataki kuwa open kuhusu hili what makes you think atakuwa clean on Vitega uchumi na sources zao of funding?

Chadema ni zaidi ya Mwenyekiti; Chadema ni chama.. nimeuliza suala la Chama. Katibu Mkuu anaweza kujibu kwani ndiye mtendaji mkuu... Ya Mbowe na shule yake namuachia yeye na walimu wake! Maanake tukienda huko itabidi tujiulize inakuwaje Rais na Mwenyekiti wa CCM anaweka madarakani watu walioghushi vyeti na kuwapa madaraka makubwa na hapo itakuwa ni kuzunguka ukuti ukuti!
 
Hebu tuangalie na kwa wenzetu walotuzidi kama Marekani? Je DEMOCRATIC ama REPUBLICAN wana vitega uchumi? Kama ni kweli hakuna shida.
ndiyo wanavyo!

Pia tujiulize vitega uchumi ilivyonavyo CCM ni vya kwake kweli ama iliviteka?

Irrelevant!

Mfano mmoja ni Uwanja wa CCM Kirumba wazee wetu walikuwa wanachangia kwa lazima, hapo naweza kusema ni wa CCM?

Kama siyo wangejitokeza watu kushtaki kuudai urudishwe kwa umma; hawajajitokeza so.. yes ni wa CCM de facto.
Pia unapotaka kuanzisha kitega uchumi si lazima uwe na mtaji? Je huo mtaji utaupata wapi?

kwani mtu akitaka kushinda uchaguzi si lazima apate kura? Sasa kura zinapatikana vipi kwa kuteremshwa mbinguni kama mana jangwani? Kama hawana mtaji wametafuta wakakosa au wanasubiri kudra?

au ndo mambo ya kuingia ubia? Je wabia wakiwa mafisadi? hicho kitakuwa chama kweli au balaa.

Na wasipokuwa mafisadi je?
 
Vitega uchumi vya vyama vya siasa ni watu madhubuti na makini ktk utendaji. Biashara ni mwiko kwani haya sii makampuni ya kibiashara na ndio maana kuna mswaada wa kutenganisha biashara na siasa.

Huo mswada ni kinyume na Katiba; Vitega uchumi ni juhudi za chama kujipatia mapato ya kuendeshea shughuli na programu zake mbalimbali ambazo si lazima ziwe za kisiasa na kujiweka katika mazingira ya uhuru zaidi. Vinginevyo ndio mnakutana na mambo haya ya Kagoda na wenzake!

[/quote]Kama ni suala la usimamizi, CHADEMA labda wapewe jukumu la kukusanya na kuisimamia mojawapo ya kodi zetu mfano ya foroza au VAT tuone kama watashindwa...![/QUOTE]

Wapewe kwa sababu wanastahili kwa namna gani?
 
Mzee Mwanakijiji, please give them a break!

Are you kidding me? a break from what?

yes they are still infants usiwafananishe na CCM na vitegauchumi wao ambao Sisi wazamani wote tumechangia kwa lazima kwa kukatwa toka mishahara yetu enzi za chama kimoja.

Kama ni wachanga kwanini wanataka kupewa madaraka makubwa ya kuongoza nchi? Kama ni wachanga basi waachwe wakue kwanza!


Kama serikali ilikubali kuivunja NBC ili kuweka uwanja sawa wa ushindani kwenye sekta ya mabenki, tulipoanza mfumo wa vyama vingi, CCM ilitakiwa kusurender mali zote ilizohodhi kwa lazima, vyama vyote vianze moja kwenye uwanja sawa wa ushindani.

Kuna mtu amelalamika hilo au kushinikiza hilo likashindikana zaidi ya kutuonesha ukweli ambao wengi tumeujua miaka nenda rudi?

Hizi mechi za ushindani kugombea kisu cha kula keki ya taifa huku mmoja amekamata kwenye mpini mwingine ashike kwenye makali halafu mvutane...

Inategemea nani amevaa glovu kati yao!


Ni mpaka pale watakapojitokeza wanasheria mahiri kama kina Shivji, wakaishitaki CCM irudishe mali zote iliuzopora kwa watanzania ili kuweka playing ground level, vinginevyo...CCM itatawala milele!.

Yaani hadi wanasheria "mahiri" wajitokeze? Huko Chadema hakuna wanasheria wa aina hiyo! Leo hii imefunguliwa kesi ya Kikatiba ya kupinga sheria ya Madini ya 1998 na kampuni binafsi ya uwakili, Chadema imejiunga kwenye kesi hiyo ikiwa na maslahi ya kisiasa? Hapana..! why?
 
Maswali mazuri kwa Chadema..naamini wana nia ya ya kukua na kuwa chama bora. Kuna mambo ya msingi ambayo wanatakiwa watafutie majawabu.Moja kubwa ni hili la vitega uchumi. Haya mambo ya kusubiri watu waendeshe chama kwa fedha za mifukoni mwao ndo baadaye wanafanya chama kama ni NGO zao.
MMKJ maswali yako yako relevant kwao ili waumize vichwa vyao kidogo.
 
mzee mwanakijiji leo umegonga kwenyewe haswa, hiyo ndiyo sababu moja wapo kubwa,inayokosesha vyama vya upinzani kura, wengi wanaamini kutokana na ccm kuwa na miradi ya maendeleo mingi, basi hata kula kwao kutakuwa kwa nafuu, kuliko vyama vingine visivyo na miradi ya maendeleo,wakipewa itabidi wale kwanza.
 
mzee mwanakijiji leo umegonga kwenyewe haswa, hiyo ndiyo sababu moja wapo kubwa,inayokosesha vyama vya upinzani kura, wengi wanaamini kutokana na ccm kuwa na miradi ya maendeleo mingi, basi hata kula kwao kutakuwa kwa nafuu, kuliko vyama vingine visivyo na miradi ya maendeleo,wakipewa itabidi wale kwanza.

hivi wakiingia madarakani na kuenza kutengeneza au kutekeleza sera zitakazoimarisha Chadema kama chama na kuweza kupata nafasi ya "kujipatia" tufweza twa mkataba fulani tutawashangaa?

Kama Chadema imekopeshwa fedha kutoka kwa wafadhili wake wa ndani (wanachama n.k) je itazirudisha fedha hizo wakiwa madarakani?

Hivi Chadema imeshindwa kuanzisha gazeti la wiki au la kila siku kama Uhuru or something au hiyo nayo ni "haliwezekani kwa sababu hatuna fedha"!?
 
Back
Top Bottom