CHADEMA na ubunge 2020

Mkuu tayari wana wagombea ubunge wao ,orodha anayo mwenyekiti Mbowe kim Il Sung kama humlambi viatu sahau ubunge kupitia Chadema,akina Sepetunga nao sijui tayari wameshatumikishwa ,Chadema ina mwenyewe ,wengine wote ni akina pangu pakavu tia mchuzi
Usipayuke sana nenda kasome kwanza taratibu mpya za chama chenu cha ndio. CCM ina mwenyewe.
 
Wenyewe wanasema "Chadema wana gain kila uchaguzi." Na pia hawana "hofu they will make it."

Ninaambatanisha ushahidi toka kwa Waterloo hapa chini.
2005 CCM 80%, 2010 CCM 61%, 2015 CCM 54%, 2020 CCM .....load..
NB. Haya ni matokeo baada ya kamati za ufundi za ccm ikiwepo tume ya taifa ya uchaguzi.
 
2005 CCM 80%, 2010 CCM 61%, 2015 CCM 54%, 2020 CCM .....load..
NB. Haya ni matokeo baada ya kamati za ufundi za ccm ikiwepo tume ya taifa ya uchaguzi.
Haya, shauri yako.
 
Umesema vizuri kabisa. Magufuli aliteua makada kushika nafasi za ukurugenzi wa Halmashauri ukifika uchaguzi akatangazwa ambaye hajashinda wataanza kulalamika eti wasimamizi ni makada. Wakati mwingine sielewi huu upinzani. Uchaguzi ujao A kutoka upinzani anashinda anatangazwa B wa CCM sasa andamana kumjaribu hapo ndo utajua.
 
Hatutishiki maana hizi dalili zinaletwa na vijana wa Lumumba. Adui yako muombee njaa.
Chadema inachana mawimbi tusikimbiane tu hapa hiyo 2020
nakupa heko kwa huo moyo wa chuma
 
Wanasubir ikifika 2019 ndio waanze sijui sheria na wagombea Wa kuungaunga
 
Bunge lipi? Bunge la wengi wape. Hovyo! Wewe CHADEMA iache tu. Pilipili usoila yakuwashia nini?
 

Hitimisho zuri sana kwenye Nchi inayo jinadi kuwa ni ya kidemokrasia..
 
2005 CCM 80%, 2010 CCM 61%, 2015 CCM 54%, 2020 CCM .....load..
NB. Haya ni matokeo baada ya kamati za ufundi za ccm ikiwepo tume ya taifa ya uchaguzi.

Na Geshi ra Porisi..
 
Hii ni challenge na wapinzani wasipodai katiba mpya 2020 kuna uwezekano tusipate hta diwani mmoja nchi nzima
 
Mnazunguka sana shida ni katiba kwa 2015 tulikuwa na uwezo kupata wabunge wengi sana hta hao 45 walipita kwa nguvu ya umma tu tusingeambulia hata mmoja
 
Shida rasimu ya warioba na ilizuiwa na magamba ssa mlitaka wapinzani wafanyeje??? Washikw mitutu??? Hata kma tutamsimaisha magufuli wenu kma mgombea wa UKAWA 2020 hawezi shinda nakuhakikishia!!! Shida ya upinzani sio sera wala ofisi shida ni TUME ....... mana hta 2015 tulikuwa na kila kitu cha kutuwezesha kushinda ila tukaanguka sembuse 2020?? Shida sio ofisi sijui nini mambo yote rasimu ya warioba ambayo ilizuiwa na maccm wenzio
 
Hayawezekanu bila katiba mpya...... hta tusimamishe malaika huwezi fikisha wabunge 100 ccm anakuangalia tu!!! Tusidanganyane hapa....... kelele ziwe tume huru na rasimu ya warioba ila ofisi sijui wagombea hata tukiwapata bado hawawezi tangazwa mshindi
 
..kwa maoni yako unadhani ni fikra/jambo gani ambalo CDM wanatakiwa kupambana nalo sasa hivi?

Hapo nina mawazo yangu; lakini nawaachia wao kujibu hasa. Nadhani ni fikra zinazotakiwa kuwa forward looking.

..my observation ni kwamba Mzee haamini ktk demokrasia ya vyama vingi. Haamini ktk uhuru wa mawazo. Hapendi uhuru wa wananchi kukusanyika freely au kuji express kwa njia ya maandamano.

Chukulia kuwa hilo ni kweli; kama upinzani wanaitikiaje? Hapa ndipo ilipo changamoto.
 
Upinzani wa Tanazania nao inabidi wawe creative aisee. La sivyo watakuwa ni wapinzani daima na hawatokuja kushika madaraka...iwe bungeni au ikulu.

You nailed it! its about creativity. Angalia wanavyofanya Bungeni na reaction yao. Yaani vitu vile vile vinawavuruga kirahisi, majibizano yale yale na hujasikia wabunge wa upinzani wanafanya nini kwenye majimbo yao ukiondoa occasional misaada ya ambulances, vitu abmavyo hata wabunge wa CCM huwa wanavifanya.
 
Rasimu ya Warioba ilitokana na mchakato haramu ulioanzishwa ndani ya CCM. Ilikuwaje wapinzani walidandia kitu amabcho kilikuwa wazi - kwa baadhi yetu - kuwa hakiendi popote?
 
Rasimu ya Warioba ilitokana na mchakato haramu ulioanzishwa ndani ya CCM. Ilikuwaje wapinzani walidandia kitu amabcho kilikuwa wazi - kwa baadhi yetu - kuwa hakiendi popote?
Mkuu upinzani ulidai katiba 2010 na kikwete hakuwa ameweka kwenye ilani ya ccm!! Ssa huo mchakato vp ulikuwa wa ccm?? Mbona tume ya warioba ilikuwa imejaa wazalendo wa akina kabudi polepole (kabla ya uteuzi) baregu ramadhan n.k na walifanya kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ssa ulitaka wapinzani wasiunge mkono wakato tume ilikuwa huru kabisa!!!!

Mkuu shida ni hawa ma-ccm yanafanya kila nia usiku na mchana upinzani usifanikiwe. Ndio maana nikasema sahvi katiba mpya kwanza ifumue limfumo lao la chama dola ndio tuanze kufikiria hta kufikisha wabunge 150 wa majimboni maana hayo unayosema 2015 yalikuwepo yote we had money,people,capacity,resources,support and numbers kwa ufupi we wea perfect to go 100% ila mbona bado ccm ilitangazwa????

Mchawi sio chadema au sera cjui mgombea urais MCHAWI NI KATIBA...... wote tudai hilo sio ofisi wala mgombea urais wala wabunge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…