Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,602
- 830,313
Tunaendea kwenye uchaguzi mkuu nchi mwishoni mwa mwaka huu kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu
Tunafanya hivyo kwakuwa tunaamini katika demokrasia na uongozi wa kisiasa.
Ni kwa muktadha huo ndio tunapata vyama vya siasa vitakavyopambana ili kushinda uchaguzi na hatimaye kuchukua madaraka ya nchi na kuongoza.
Tuna vyama vingi vya siasa, lakini vilivyo hai na mwelekeo wa kupambana kwenye sanduku la kura ni CHADEMA/UKAWA na ccm! Hapa ndio kuna mtifuano.
CCM kimekuwa chama tawala tangu Uhuru, kikafanya mazuri mengi mwanzoni lakini kadiri kilivyozidi kuwa kikongwe kikasahau misingi yake na kupoteza dira kabisa, kimebaki kuwa chama butu kisichoweza kuwa na sauti yoyote ya kukemea na kusimama kwenye misingi kwa watu wake! Lakini ndani yake kukiwa na watu wenye uwezo wa kufanya hivyo japo wanakosa nafasi.
Sasa uchaguzi unapokaribia ndio kinazinduka na kuanza kujitutumua ilihali kishachelewa mno! Rushwa imetamalaki, huduma za jamii zimedumaa, watendaji wamefubaa na mifumo ya uongozi na utawala bora vimeparaganyika kabisa, kila mtu anaangalia anapata nini kwenye nini.
Kuna hawa watu wawili ambao at least wana uelekeo wa kuirudisha nchi kwenye mstari wake, kuirudisha mifumo kwenye utaratibu wake, kuleta uwajibikaji serikalini na kila mahali.
Watu hawa wawili CHADEMA/ UKAWA NA LOWASSA ndio homa ya ccm kwasasa wanamfahamu vyema Lowassa hacheki na nyani na wanajua atafanya nini akiingia ikulu, ataleta kilio kikubwa kwa wengi, ana nguvu uwezo na uthubutu wa kufanya hivyo.
CHADEMA hawatofautiani na Lowassa watafanya kama atakavyofanya Lowassa kuirudisha nchi kwenye mstari, CHADEMA inajulikana vyema kwa ccm hawana utani wala mchezo na wanataka kuithibitishia dunia na wanaccm kuwa wanaweza hapa kutakuwa na kilio.
Kwahiyo kwasasa CCM imebanwa kotekote haijui ideal na CHADEMA au Lowassa hakuna mwenye afadhali mboga moto, ugali moto!
Chama Tawala kiko njiapanda.
Tunafanya hivyo kwakuwa tunaamini katika demokrasia na uongozi wa kisiasa.
Ni kwa muktadha huo ndio tunapata vyama vya siasa vitakavyopambana ili kushinda uchaguzi na hatimaye kuchukua madaraka ya nchi na kuongoza.
Tuna vyama vingi vya siasa, lakini vilivyo hai na mwelekeo wa kupambana kwenye sanduku la kura ni CHADEMA/UKAWA na ccm! Hapa ndio kuna mtifuano.
CCM kimekuwa chama tawala tangu Uhuru, kikafanya mazuri mengi mwanzoni lakini kadiri kilivyozidi kuwa kikongwe kikasahau misingi yake na kupoteza dira kabisa, kimebaki kuwa chama butu kisichoweza kuwa na sauti yoyote ya kukemea na kusimama kwenye misingi kwa watu wake! Lakini ndani yake kukiwa na watu wenye uwezo wa kufanya hivyo japo wanakosa nafasi.
Sasa uchaguzi unapokaribia ndio kinazinduka na kuanza kujitutumua ilihali kishachelewa mno! Rushwa imetamalaki, huduma za jamii zimedumaa, watendaji wamefubaa na mifumo ya uongozi na utawala bora vimeparaganyika kabisa, kila mtu anaangalia anapata nini kwenye nini.
Kuna hawa watu wawili ambao at least wana uelekeo wa kuirudisha nchi kwenye mstari wake, kuirudisha mifumo kwenye utaratibu wake, kuleta uwajibikaji serikalini na kila mahali.
Watu hawa wawili CHADEMA/ UKAWA NA LOWASSA ndio homa ya ccm kwasasa wanamfahamu vyema Lowassa hacheki na nyani na wanajua atafanya nini akiingia ikulu, ataleta kilio kikubwa kwa wengi, ana nguvu uwezo na uthubutu wa kufanya hivyo.
CHADEMA hawatofautiani na Lowassa watafanya kama atakavyofanya Lowassa kuirudisha nchi kwenye mstari, CHADEMA inajulikana vyema kwa ccm hawana utani wala mchezo na wanataka kuithibitishia dunia na wanaccm kuwa wanaweza hapa kutakuwa na kilio.
Kwahiyo kwasasa CCM imebanwa kotekote haijui ideal na CHADEMA au Lowassa hakuna mwenye afadhali mboga moto, ugali moto!
Chama Tawala kiko njiapanda.