leo nataka tukumbushana wana JF. Hivi mnakumbukua chadema waliamua kuondoka bungeni na kumuacha mhe. Rais akilihutubia bunge? Wakadai hawamtambui!! Siku chache baadae wakarudi bungeni kuendelea kujadili hotuba ya rais. Majuzi walitoka nje ya bunge kususia muswada wa katiba. Siku chache baadae wakaenda ikulu kuongea na rais kuhusu mswada huohuo walioukimbia bungeni. Hivi, hawa wenzetu na tabia zao za kususa, tukiwapa nchi wataweza ? CDM jifunzeni kuwa wavumilivu