Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT, mkishindwa kuwa kitu kimoja na kuachiana majimbo mtawafaidisha CCM

Huu muungano kwenye kura za urais na mgombea urais ndipo penye walakini.

Kiukweli kwangu Membe sioni influence yake kabisa ukiacha hiyo mikoa ya kusini, sasa kipi bora;

(a) Kumsimamisha Membe asaidie wagombea ubunge mikoa ya kusini ambayo hatuna uhakika kama kweli ana hiyo influence?

Au

(b) Chadema imsimamishe mgombea urais wake ambae inaamini anaungwa mkono na kundi kubwa la watu Tanzania nzima kwa ujumla, na sio kanda fulani pekee?

Mleta mada umejaribu kusisitiza kwenye umoja ni vizuri, lakini pia tuangalie kwa jicho la pili nguvu za wagombea hasa wa Urais kutoka vyama vyote viwili, tusilazimishe tu bora fulani ana jina basi apewe hiyo nafasi, napenda hapa tutazame zaidi nguvu/uungwaji mkono wa wagombea wa hivyo vyama viwili.
Membe hana ushawishi wowote zaidi ya wapiga Kura wachache pale Mtama na wengi wao kule ni ccm kumbuka Nape atagombea pia
 
siku zote umoja ni nguvu ila haiwezekani kupata umoja wa vyama vya upinzani kwa nchi maskini , yenye watu wenye njaa na iliyoharibiwa mfumo wake wa elimu kwa kujazwa siasa ya kipumbavu ya ujamaa na kujitegemea my foot!

Muungano wa watu maskini huwa ni wa muda, wenye mashaka, huwa ni wa kinafki , wa kibinafsi na wa kimaslahi zaidi, na katika hali hii ngumu ya kiuchumi wanasiasa wanapopigania matumbo yao ni ngumu mno kwa wao kuungana!

ila itapendeza mno kama Membe ataenda ACT akajijenge kisiasa na kuanza safari ya kuutafuta urais. Huyu mzee namshangaa kwanini hatangazi kujiunga upinzani na muda unakwenda sababu sisiem hawamtaki ni mtu asiekubali baadhi ya taratibu za chama

kwa akili zangu naamini tukiangalia haki tu bila kuhusa mengine Membe kafukuzwa sisiem bila kosa lolote, kudai kwake demokrasia ndani ya chama kwa kutaka kumchallenge boss wao kumemponza!

asichokijua Membe ni kuwa alikuwa katika genge lenye watu wengi wenye local education sasa yeye vile kwenda kwenda ulaya akadhani na wenzake wana akili ya kizungu kumbe hola, wote ni wa hapa hapa wenye mawazo mgando ya zidumu fikra za mwenyekiti!!
 
Huu muungano umeingia shubiri Mara baada ya zitto kumtamani mwanachama Wa ccm aje aokoe jahazi LA kugombea urais kupitia Act kisha muungano huo.Zitto kwa hili kapotoka sana, membe aweza karibishwa upinzani ila sio kwa kugombea urais.
Anzisha chama chako bro Lungwe
 
Chadema na ACT hawawezi kabisa kushirikiana,kutokaba na historia ya vyama hivyo,wanachoweza kufanya ni kuishi kwa kuvumiliana,na kuukubali ukweli kuwa kwao kushirikiana ni kama mbingu na ardhi
 
Sijui nini kinaendelea kati ya CHADEMA na ACT juu ya kushirikiana katika uchaguzi mkuu wa baadae mwaka huu, ila napenda tu kuwatahadharisha kuwa wakishindwa kukaa pamoja na kuja na mpango mkakati wa pamoja juu ya namna bora ya kushirikiana katika uchaguzi huu,basi watakaofaidika na hali hii watakuwa ni CCM katika baadhi ya maeneo ambayo ACT watakuwa na nguvu na CHADEMA nao pia watakuwa na nguvu hata kama watakuwa wanazidiana kwa kiasi fulani.

Zanzibar
Huko ni bora CHADEMA wawaunge mkono ACT kwasababu ujio wa Maalim Seif umeipa nguvu ACT hivyo ni bora CHADEMA wawaunge mkono kuliko kugombea alafu wagawane kura ingawa hata pasipo kuungana, bado ACT itashinda kulinganisha na CHADEMA. Tutambue kuwa adui yetu mkubwa wa kisiasa ni CCM na si chama kingine chochote kile cha siasa.

View attachment 1498622

View attachment 1498597

kigoma
Katika mikoa ambayo ACT na CHADEMA wanaweza kugawana kura na matokeo yakawa ni wote kukosa kama siyo kupunguza majimbo ya kwenda upinzani,basi Kigoma inaweza kuwa ni mojawapo, hivyo ni vizuri washirikiane katika kusimamisha wagombea kwa maana ya kuachiana majimbo na kata za uchaguzi vinginevyo itakula kwao.

Mikoa ya kusini
Iwapo Membe atajiunga ACT bila kujali atagombea uraisi kupitia ACT au laa,kitendo tu cha Membe kujiunga ACT kitaipa nguvu ACT na kuongeza ushindani wa kisiasa baina ya vyama vitatu:CCM,ACT na CHADEMA.Kwa maana hiyo,wapinzani wakishindwa kuungana,CCM inaweza kufaidika ingawa ACT bado inaweza kushinda hata ikisimama peke yake ila hasara itakuja katika kura za mgombea uraisi iwapo hivi vyama kila kimoja kitasimamisha mgombea wake.

Ukiacha mikoa hiyo niliyoitaja pamoja na Zanzibar,athari za wapinzani kutoachiana majimbo na kata za uchaguzi zinaweza kuonekana pia katika maeneo mengine machache kama kwenye mikoa ya Tabora na Tanga, na lazima ieleweka athari za kugawana kura zitaweza hata kuathiri wagombea uraisi ikitokea kila chama kitasimamisha mgombea wake.

Tanzania kwa ujumla
Iwapo Membe kweli atajiunga ACT kama dalili zinavyoonyesha,basi ni dhahiri Membe atakuja na kundi kubwa la wana-CCM waliko nyuma yake nchi nzima;hivyo, iwapo wapinzani hawataungana na ACT wakamsimamisha Membe kama mgombea wao wa uraisi, hii maana yake ni kuwa wapinzani wanaenda kugawana kura za uraisi na hili litakuwa ni pigo kubwa sana kwa upinzani.

Jambo lingine:hata kama watakuwa wamechelewa kuungana kisheria,swala la wao kushirikiana kwa kuachiana majimbo na kuamua kuwapigia debe wagombea wao haliwezi kuwa ni kosa kisheria zaidi tu ya kuhitaji dhamira ya kisiasa kutoka wahusika.

Ukweli ni kwamba,hata pasipo vyama hivi kuungana,CCM na wagombea wake ndio inayostahili kushika mkia kwenye matokeo ya uchaguzi ila ndio hiyo tena bado kuna baadhi ya watanzania wenzetu hawajielewi.

Muda wa nusu karne na zaidi kama umewashinda kubadili maisha ya watanzania,sioni ni sababu gani ya kuendelea kuwapa nafasi ya kuendelea kubaki madarakani.

CHADEMA mkijiona mna nguvu na mnaweza kusimama kivyenu katika kila sehemu ya nchi hii,basi matokeo yake mtakuja kuyaona;halikadhalika kwa ACT-Wazalendo.

Nukuu muhimu za wanasiasa zinazoendana na mada hii:


Wananchi wa Tanzania wanaotaka mabadiliko hawatatusamehe viongozi wa vyama makini vya upinzani hapa nchini iwapo tutashindwa kuweka maslahi yetu binafsi pembeni na kuunda ushirikiano utakaowaongoza Watanzania kuiondoa CCM madarakani. Wakati ni Huu! Wakati ni Sasa-Ismail Jussa on twitter.

Ni wajibu wetu sote kuonyesha dhamira zenu za kweli kwamba tunahitaji coalition. Wananchi wanafahamu kwamba wapo ambao wqnafanyabiashara katika hizi siasa. Nakubaliana na wewe Kaka Ismail Jussa kwamba hili lazima tusimame na tuhesabiwe-Patrick Ole Sosopi on twitter.

Wananchi wa Tanzania wanaotaka mabadiliko hawatatusamehe viongozi wa vyama makini vya upinzani hapa nchini iwapo tutashindwa kuweka maslahi yetu binafsi pembeni na kuunda ushirikiano utakaowaongoza Watanzania kuiondoa CCM madarakani. Ninaamini TUNAWEZA na TUTAWEZA-Zitto Kabwe on twitter.
Wewe Salary Slip ni mchumia tumbo tu, unataka Chadema waunge mkono mtoto wa shetani kuwa mgombea wa urais ?

Membe hana ushawishi wowote wa kisiasa zaidi ya kuwa mpiga kelele tu unafikiri kusini Membe anaushawishi kuliko wale wanacuf walioinyanyasa ccm mwaka 2015?

Unataka CHADEMA yenye wanachama millions kadhaa iwaachie ACT ambayo haina hata wanachama hivi unaakili kweli wewe ? Unajua jasho walilotumia CHADEMA kujenga chama waje wajiue kwa kukijenga ACT kwa mikono yao wenyewe?

Kama mnampenda Membe mfuateni huko ACT tuachieni CHADEMA kama hatuna mgombea tutamsimamisha mwanachama yeyote siyo Membe.
 
Huwa sisomi sana nyuzi zako lakini kwa hili nakuunga mkono. Kuna mijitu io CDM bado inaamini wao wanaimarika kuliko wakati wowote ilhali ni mbaya kupita maelezo. Mtu kama Yeriko Nyerere hataki muungano wa CDN na ACT kwa kuwa tu ana ugomvi na Zitto sasa watu kama hawa hawafai hata kuwasikiliza. Leo nakubaliana na wewe mkuu.
Kuhusu suala la Zitto kumchukua Membe, mimi nasema tatizo ni Lissu. Laiti kama Lissu angekuwa na uhakika wa kuja Tanzania na kugombea kwa tiketi ya CHADEMA nna uhakika Zitto ataachana na huo mpango wa kumchukua Membe.
Zitto yupo tayari kushirikiana na CHADEMA lakini wakati huo huo nae awe anajenga chama chake hivyo si kosa yeye kumchukua Membe ni kutaka kuongeza uungwaji mkono wa chama chake.
LISSU AWE NA UHAKIKA WA KUJA KUGOMBEA KWA TIKETI YA UPINZANI NNA UHAKIKA ZITTO ATAACHANA NA MEMBE.
Lissu anakuja tarehe 28 July
 
Wewe Salary Slip ni mchumia tumbo tu, unataka Chadema waunge mkono mtoto wa shetani kuwa mgombea wa urais ?

Membe hana ushawishi wowote wa kisiasa zaidi ya kuwa mpiga kelele tu unafikiri kusini Membe anaushawishi kuliko wale wanacuf walioinyanyasa ccm mwaka 2015?

Unataka CHADEMA yenye wanachama millions kadhaa iwaachie ACT ambayo haina hata wanachama hivi unaakili kweli wewe ? Unajua jasho walilotumia CHADEMA kujenga chama waje wajiue kwa kukijenga ACT kwa mikono yao wenyewe?

Kama mnampenda Membe mfuateni huko ACT tuachieni CHADEMA kama hatuna mgombea tutamsimamisha mwanachama yeyote siyo Membe.
Huu ndio ukweli ndugu
 
Membe hana “kundi kubwa la wanaCCM”. Ile ya Lowassa ilikuwa exceptional. Atapata shock kubwa. Just wait and see. Now that wanaCcm wanajua modus operandi ya JPM (mzee wa visasi bila kupoteza muda), hakuna mwanaCCM serious anayeweza kujitokeza hadharani na kumfuata Membe huko anakotaka kwenda.

Hongera CHADEMA kwa kuepuka makosa ya mwaka 2015. Hata Zitto analijua hilo ila anafanya kubahatisha tu atleast aokote majimbo kadhaa
 
Membe huyu alikuwa mwizi kama wengine na hakuwahi kusaidia kupata hiyo tume huru anayoisema. Leo bila aibu anapretend kuimba nyimbo mnazozipenda na baadhi ya watu wanaanza kumpigia makofi na mnamuona kama vile ni mkombozi wa wapinzani

Hatari sana!
 
Huu muungano umeingia shubiri Mara baada ya zitto kumtamani mwanachama Wa ccm aje aokoe jahazi LA kugombea urais kupitia Act kisha muungano huo.Zitto kwa hili kapotoka sana, membe aweza karibishwa upinzani ila sio kwa kugombea urais.
Unafikili Zitto angefanyaje wakati Bernard Membe alikuwa na hisa ndani ACT Wazalendo tangia kuanzishwa kwake.
 
Membe huyu alikuwa mwizi kama wengine na hakuwahi kusaidia kupata hiyo tume huru anayoisema. Leo bila aibu anapretend kuimba nyimbo mnazozipenda na baadhi ya watu wanaanza kumpigia makofi na mnamuona kama vile ni mkombozi wa wapinzani

Hatari sana!
Ndiyo unafiki wa wanasiasa wa ccm kazi yao kubwa ni kutafuta fursa ya kuiba Mali za umma tu.
 
Wewe Salary Slip ni mchumia tumbo tu, unataka Chadema waunge mkono mtoto wa shetani kuwa mgombea wa urais ?

Membe hana ushawishi wowote wa kisiasa zaidi ya kuwa mpiga kelele tu unafikiri kusini Membe anaushawishi kuliko wale wanacuf walioinyanyasa ccm mwaka 2015?

Unataka CHADEMA yenye wanachama millions kadhaa iwaachie ACT ambayo haina hata wanachama hivi unaakili kweli wewe ? Unajua jasho walilotumia CHADEMA kujenga chama waje wajiue kwa kukijenga ACT kwa mikono yao wenyewe?

Kama mnampenda Membe mfuateni huko ACT tuachieni CHADEMA kama hatuna mgombea tutamsimamisha mwanachama yeyote siyo Membe.
We lofa kabila!Uwezo wake wa kuelewa kilichoandikwa ni mdogo sana.
 
Back
Top Bottom