Kingine kinachotia Huruma ni huu ushabiki usiokuwa na kichwa wala miguu,yani inatia huruma lakini mwisho wa siku ni aibu ukikuta namna watu wanavyozungumza juu ya uchaguzi wa mwaka 2015 namna ambavyo CCM itashindwa na CHADEMA kama una roho ndogo unaweza kukimbia na kuamua kuachana na siasa na kama wewe ni mwanaccm unawez pia kuamua kukihama chama!
Kwanza binafsi sitaki kuamini kwamba CCM itashinda ama itashindwa kwenye uchaguzi mkuu ujao ama CHADEMA itashinda ama kushindwa,nasema hivyo kwa sababu kwa ushabiki ulioko hivi sasa unaweza kuwa ni sumu kwa CCM na faida kwa CDM,au faida kwa CCM na Sumu kwa CDM!.Kilichopo na hasa kwa wale wanaoonekana wako upinzani wamejaa ushabiki mtupu badala ya dhamira ya kweli kutoka moyoni.
Hata hiovyo wapo ambao wana dhamira ya kweli na wamekusudia kufanya kweli na hata leo hii ukiwaambia lazima kinaeleweka na hata baada ya miaka kumi kweli wako Serious!,lakini kundi kubwa ukiliangalia na kulichunguza kwa makini unagundua kwamba ni wanafiki wanafuata upepo.
Lakini ukiniambia kura zioige leo CCM bado itashinda lakini si kwa ushindi mkubwa kwa sababu wale wanaoshabikia bila kuwa na moyo wa dhati watapiga kura zao lakini kwa kusema hebu ngoja tujaribu,na hapo ndipo utakapokuwa mwanzo wa kuinyima kura CDM kwa sababu watu wa namna hiyo ni rahisi kubadili mawazo,ogopa sana mtu ambaye yeye kazi yake siku zote ni kusema ndio mzee hafnyi tathmini yoyote.
Hili jambo nimelifanyia utafiti kwa muda mrefu sana,kwamba CCM inaonekana kama vile mnyonge lakini ina watu wake ambao ni wa ukweli mtupu,lakini upinzani na hasa CDM wanaonekana wana kundi kubwa la watu nyuma lakini kundi ambalo halina maamuzi ya mwisho,badala yake maamuzi yao yanakuja kuamuliwa na lile kundi la wachache ndiyo maana mwisho wa siku malalamiko yanatokea.
Nina mifano hai miingi sana ambayo nimewahi kuishuhudia na hasa kwenye hizi chaguzi ndogo,jambo ambalo wakai mwingine linatia hasira kwamba ule upande ambao ulikuwa unaona kila siku shamrashamra nyingi pamoja na maandamano yanayoungwa mkono na maelfu ya watu tena kila kundi,lakini mwisho wa siku ndilo linakuja kushindwa inauma sana.
Pengine yawezekana watu wameanza kubadilika kwa sababu nimeangalia chaguzi ndogo kama mbili hivi za hivi karibuni ambazo watu wamefanya maamuzi kama ambavyo taswira ilikuwa ikijionyesha tangu mwanzo,ingawa nazo ni katika maeneo ya watu ambao wanaonekana ni kabila moja ama kabila filani lina wingi wa watu!!,kwa hiyo wakati wa maamuzi wnafanya maamuzi kama familia!!
Yote kwa yote kaka Nape ni vyema ninyi nyote mkaendelea na mikakati yenu ya kuwatumikia watanzania kwa moyo wa dhati,vinginevyo 2015 mnaweza kujikuta mkiwa chama pinzani,lakini kwa wapinzani hususani CDM ambacho hakuna ubishi kwamba ndiye baba wa upinzani hivi sasa nchini,waendeleze juhudi za kuwaelimisha watu wao na kuwa na misimamo,kuba kuwaondoa uoga na kuwa na uelewa wa nini wanapaswa kufanya,vinginevyo yatakuja yaleyale ya 2010 ya kuibiwa kura,mara sijui nani kafanya nini>