CHADEMA mnadanganywa, namba hazidanganyagi

Hata CCM hawana demokrasia ndani ya chama chao! Wanabadili Mwenyekiti pale tu urais unapobadilishwa kwa mwingine, ndiyo baada ya miaka kumi. Katiba ingebadilika na urais kuwa wa vipindi viwili vya miaka saba saba uenyekiti ungedumu miaka hiyohiyo!
Tumeshuhudia wanachama wakipigwa mkwara walipojitokeza kugombea katikati ya mhula wa urais! Mbaya zaidi demokrasia ndani ya CCM imeyeyuka kabisa sasa zaidi ya kipindi chochote! Mwenyekiti wa sasa aliweka hadharani nia ya " kuwapoteza" waasi ndani ya chama!
Halafu kuna mtu anabana pua na kuushutumu upinzani kwa kukosa demokrasia ndani ya vyama!
 
Mheshimiwa naona tunashindwa kabisa kuelewana. Kwa hiyo kwa vile ccm hamna democracy basi na Chadema nao inabidi wafanye hivyo Hivyo?
 
Lbd n kweli lakini msingi wa hoja yangu n Je ni kweli upinzn ulipiga hatua uchaguzi Mkuu 2015 au walirudi nyuma zaidi (kitakwimu lakini)

Ki mahesabu CHADEMA na UKAWA walipiga hatua- Walisonga mbele kwa kiwango kikubwa kutoka chini ya asilimia 30 uchaguguzi wa mwaka 2010 hadi kufikia karibu asilimia 40.

Pamoja na ukweli huu ninakusifu kwa moyo wa dhati kabisa kwamba umefirikiri na ndio maana ni rahisi kukuonyesha umekosea wapi. Hesabu ni zaidi ya namba kwa maana ya namba.

Hoja ya msingi hapa ni nani ni chachu ya mafanikio haya ambayo hayajakidhi haja? Marafiki na mashabiki wa Mhe. Lowasa, huamini kuwa mafanikio haya yameletwa naye. Tunaweza kusema ni kweli kama nia ya CHADEMA ilikuwa kuongeza asilimia kutoka chini ya 30% hadi kufikia chini kidogo ya aslimia 40 tu na sio ushindi wa kuongoza nchi.
Kwa maandalizi ya CHADEMA ilivyokuwa imeyafanya kwa miaka mitano, kushindwa kuunda serikali kuliwa ni kushindwa kuliko hitaji uwajibikaji au kwa mgombea binafsi au kwa baadhi ya watu. Na hoja ya kwamba tulifaulu ni katika kupotosha dhana ya uwajibikaji kwa makosa ya maamzi fulani au hata kwa kushindwa kuchukua maamzi fulani ambayo yangeleta ushindi zamu ijayo. Sioni kama tunayo maandalizi ya kukiri, ili tupate uhalali wa kuchuikua hatua mujarabu kwa ajili ya uchaguzi wa 2020.

Kwa kuchoka ambako wananchi wameichoka CCM, kwa kushindwa ambako CCM imeshindwa kuwaletea unafuu wananchi wa kawaida katika maisha yao ya kawaida, kwa majigambo yasiokuwa na tija ya utawala wa sasa, kuanzia Halmashauri za wilaya, Miji, Manispaa, majiji na serilkali kuu kwa ujumla wao, kwa uvurugaji wa mifumo ambayo imekuwa mihimili ya taifa letu unaofanywa na utawala wa sasa, CCM itaondoka endapo tutajipanga kidogo tu. CHADEMA ni chama chenye ITIKADI inayotekelzeka, kina falsafa inayoheshimu watu kama chanzo cha mamlaka. Hakuna mashaka ushindi upo jirani tu.
 
Points noticed mkuu
 
Yupo Kubenea kule
 
Mbona sikuoni ukijadili udhaifu wa ccm???
Au ndiyo ukuu was wilaya unakusumbua
We jamaa ni mgumu kuelewa. Umejuaje kama sijadili uozo na madudu yao ccm na vyama vingine. Mimi na wewe hatujuani sasa utathibitisha Vipi kama sijadili madudu ya Ccm? Tusifanywe mambumbu kiasi hichi na siasa za maji taka kiasi kwamba mtu hautaki chama chako kikosolewe hata kama wanakosea.
 
Weka basi na Uzi wa CCM
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…