CHADEMA mmeanza lini kuwaonea huruma CCM?

CHADEMA mmeanza lini kuwaonea huruma CCM?

Deo Corleone

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2011
Posts
17,038
Reaction score
13,467
CHADEMA wanapinga kura ya wazi wanatoa hoja kuwa CCM wanataka kuwadhibiti watakaopinga serikali 3 na wanasema CCM wakiwajua hao watawafukuzwa uanachama.

Swali langu linakuwa: CCM wakiwafukuza wanachama si itakuwa faida kwao?CHADEMA wana huruma na CCM KWELI?
 
Itakuwa hasara kwa Watanganyika na Wazanzibari kwani ni by the time wanafukuzwa tutakuwa hatuna serikali 3. wewe ulifundishwa na nina jinsi ya kutathmini mambo?
 
Najiuliza hivi mnyika anaogopa kusema hadharani kuwa anataka serikali mbili au tatu? hivi mbowe anaogopa kusema hadharani anataka serikali mbili au tatu? sasa huo uwazi wanaogopa wa nini?

Nilitegemea Mbowe kuwaunga mkono wabunge wa ccm kura ya wazi ili wananchi tujue mbivu na mbichi.
 
Mbona hao wabunge wa ccm zanzibar wanaoogopa kufukuzwa mbona waliungana pamoja na wacuf kusema mafuta isiwe ya muungano, kwa nini hawakuogopa kufukuzwa? angali Tanzania ilikuwa ikusua sua swala hilo. mbowe hapo anapotezwa na watu hao
 
Hivi ikitokea Gaidi Mwigulu akiropoka na kusema anataka serikali 3 na akafukuzwa CCM,hawa CHADEMA si watashangilia sana?
 
alama za mnafiki ni
1.........................?
2.........................!
3.........................!
4..........................!
5.........,...,............!
 
Mbona hao wabunge wa ccm zanzibar hutamka hadhari barazani kwao kuwa wanataka serikali tatu?mbona hata kificho kaandika barua kwa warioba iko wazi? Mbona kwenye kuandika katiba ya zanzibar hao wawakilishi wa zanzibar waliungana wakatunga moja? viongozi wa cdm wamekosea mi nilitaka kura ya wazi na bunge liwe live na kuwe na hansard za bunge kuwa kati ya wajumbe 600 ,kila mmjumbe kwa jina lake kujulikana alisema hivi.
 
CDM wameshapoteza dira kwenye siasa za Tanzania..
 
Itakuwa hasara kwa Watanganyika na Wazanzibari kwani ni by the time wanafukuzwa tutakuwa hatuna serikali 3. wewe ulifundishwa na nina jinsi ya kutathmini mambo?

Mkuu, uko sahihi ila utambue tu hapa wakurupukaji ni wengi tu. If he were using his faculty of thinking well, asingekuja na jibu hilo.
 
CDM wanapinga kura ya wazi wanatoa hoja kuwa CCM wanataka kuwadhibiti watakaopinga serikali 3 na wanasema CCM wakiwajua hao watawafukuzwa uanachama.
Swali langu linakuwa:CCM wakiwafukuza wanachama si itakuwa faida kwao?CDM wana huruma na CCM KWELI?
Kichwa chako hakiwezi kufikiria hasara ya kurudia uchaguzi? Hakifikirii pia hasara ya kukosa maamuzi ya wananchi kwa kuogopa CCM
 
katibu wa ccm zanzibar husema hadharani kuwa yeye anataka serikali mbili mbona hajadhuliwa, mbona wanaosema wanataka serikali 3 hawajadhuliwa huko zanzibar, masikani zote za ccm hutamka serikali mbili hazijaguswa.Hivi Mbowe hajiulizi kificho alishinda vipi kama wajumbe wa ccm znz na bara wako tofauti? Hao sio watu tofauti
 
Kichwa chako hakiwezi kufikiria hasara ya kurudia uchaguzi? Hakifikirii pia hasara ya kukosa maamuzi ya wananchi kwa kuogopa CCM

hakuna kurudia uchaguzi, haya mambo yako wazi, wana ccm znz hawataki muungano wa serikali mbili alafu wanaogopa kusema kwa ccm makao makuu. ipigwe kura ya wazi watu wawajue
 
Mkuu, uko sahihi ila utambue tu hapa wakurupukaji ni wengi tu.
Kwani CDM wameambiwa na Wabunge wangapi wa CCM kuwa wao wanataka 3 govts so Wawatetee wapige kura ya siri?Vipi kama itapita ya Siri na zkapita 2 govts?
 
Nilitegema maana wanaosema serikali mbili wana hoja zao na wanaosema serikali tatu wanahoja zao. hoja hizo ziongelewe hadharani na kila mjumbe kutoa sababu ya hoja yake ndio demokrasia sio uchawi au kamari ya kufanya kwa kificho kificho.
 
kichwa chako hakiwezi kufikiria hasara ya kurudia uchaguzi? Hakifikirii pia hasara ya kukosa maamuzi ya wananchi kwa kuogopa ccm

vipi kama itapita kura ya siri na cdm watashindwa na serikali zao 3 wanazopigania?
 
CDM na Mbowe watakuwa amewadhulumu wa tanzania kama itapita kura ya siri alafu serikali mbili zipitishwe bila kujua nani kakubali na nani kakataa hiyo ni mbaya na wananchi hatutajua wa kumpongeza na kumuhukumu.

Hata Biblia husema yali yaliyo ya kweli huwekwa nuruni. serikali mbili ni mbovu zianikeni kuwa hazifai by hoja.
 
Nani kasema tunawaonea huruma CCM ?

1. Tunawaonea huruma wananchi wanaotaka serikali tatu lakini CCM wanataka kulazimisha serikali mbili kwa kutumia wingi wa wabunge wao !

2. Tunajua kuna wabunge wa CCM ambao kama sisi wanataka kusimamia maslahi ya wananchi ila wanaogopa uongozi wa CCM

3. Sisi na hao CCM (wanaotetea maslahi ya wananchi) tunashare interest moja i.e. tuna lengo moja, ambalo ni serikali tatu kama wananchi wanavyotaka. Hivyo ni interest yetu kuwatetea hawa ili wawe huru kutetea maslahi ya wananchi kwani wakifanikiwa kutetea maslahi ya wananchi na sisi tutakuwa tumefanikiwa !

CDM wanapinga kura ya wazi wanatoa hoja kuwa CCM wanataka kuwadhibiti watakaopinga serikali 3 na wanasema CCM wakiwajua hao watawafukuzwa uanachama.
Swali langu linakuwa:CCM wakiwafukuza wanachama si itakuwa faida kwao?CDM wana huruma na CCM KWELI?
 
kura ya siri inatoa mianya mikubwa ya rushwa bila kujua yupi msaliti.
 
Back
Top Bottom