Yes nakubaliana na baadhi ya mambo unayosema. Mimi ninaamini kwamba kura ya siri au ya wazi zote zinakidhi matakwa ya kidemokrasia ! Na kuna faida zipo kwa kupiga kura za wazi na baadhi umezitaja hapa. Hata hivyo ninaamini kura za wazi zitafanya baadhi ya wajumbe (especially wa CCM) wapige kinyume na vile ambavyo wangependa kupiga. Kwa sababu hiyo naona kura ya siri ndio muafaka kwani cha muhimu zaidi kwetu ni maamuzi sahihi zaidi ya kujua mtu gani alifanya maamuzi gani !
Kwa maneno mengine nikiambiwa nichague maamuzi sahihi au kujua nani amefanya maamuzi gani (in case siwezi kuvipata vyote kwa pamoja) nitachagua maamuzi sahihi !. Na ndio maana natetea kura ya siri !
Wananchi tutawajibu kwamba CCM wamewadharau kwa kubadilisha maamuzi yao kinyemela. Na hii tunaweza kuisema bila kumumunya maneno, kwani katika kubadilisha kutoka serikali 3 kwenda 2, hilo haliwezi kufanyika kwa kificho, litabadilishwa hadharani, na litatetewa hadharani, na watakaofanya hivyo...ofcourse watakuwa CCM !
uko sawa. niseme tu kwamba ccm znz wanataka serikali mbili zinafaida kubwa kwao na wanalielewa hilo, wananchi wao wengi hawataki.nielezee kidogo :nchi za afrika ni masikini kote afrika maji,umeme ,barabara,afya ni huduma za kusuasua sasa kwa znz viongozi wanautabia ya kusingizia kila jambo muungano,kiasi cha wananchi kujua tatizo lao ni moja tu muungano hiyo wanataka uondoe au zije serikali 3. sasa ukifanya kwa siri kwanza unakuwa umedumisha ulaji wa wana ccm znz , pili umekuwa umedumisha uwakilishi wao huko visiwani maana wataenda kuimba wimbo ule ule tulikuwa wachache wabara wengi wakapitisha.
waweke wazi kwani sababu si zipo zisemwe. sio uchawi kwamba unataka mbili bila sababu au tatu bila sababu.mambo yawe wazi.