CHADEMA mjitafakari msiwabeze wahamaji, wana hoja za msingi. Adui wenu mkuu sio CCM! Lazima mbadilike

CCM wamefanikiwa kutengeneza wapinzani from within ili kupunguza nguvu ya upinzani wa nje ambao ni uncontrollable ....wanazi wa Chadema wanapenda kushangilia kila mwenye hoja kinyume na serikali na kuwapa umaarufu wa bure badala ya kujua hoja ni ipi na msimamo wa chama ni upi ili upande wowote hata kama ni serikali wakiwa na hoja ambayo ni agenda yao wanaungana nao ....haiwezekani mkawa mnapinga agenda zote za serikali ....ipo siku nchi itavamiwa na mtaipinga serikali kutuma jeshi dhidi ya wavamizi ...

..hivi Waganda walioshangilia wakati Tz imeivamia nchi yao, na kuwaita askari wa JWTZ "wakombozi", walikuwa siyo wazalendo au wenye nia mbaya na nchi yao?

NB.

..hata ccm wanautaratibu wa kupinga hata yale mazuri yanayofanywa au kupendekezwa na cdm.

..tumefika mahali cdm wanatoa ushahidi mzuri kabisa kuhusu matukio ya rushwa halafu watuhumiwa wanapandishwa vyeo.
 
Umekosea mayalla adui mkuu wa upinzani ni FISIEM Hawa wengine ni wamekumbwa na mifadhaiko hawawezi na hawatoweza kuiyumbisha cdm. Kaondoka kigogo slaa je umekionaje chama kimeyumba?

Chama hakiwezi kuendelea kwa kununua wanachama ona fisiem wanavohangaika kaondoka Nyalandu tazama idadi ya wanaowarubuni imefikia ngapiii... ukipata jibu hapo ndo ujue Nyalandu ananguvu ya idadi hiyo wanayonunua mpaka ifikie idadi YA MAUMIVU YA KUKIMBIWA na MH. NYALANDU nnaimani NYALANDU atakuwa mbali na hawatomfikia.

watambue kuwa kila kichwa watakachofika bei ndio sawa na gharama ya kumrudisha NYALANDU kama fisiem watammaind.
Kwaiyo mpka leo hujui kama chama kimeyumba kuondoka slaa pole
 
at first place.CHADEMA haikupaswa kamwe kuanza kujilinda kuhusu tuhuma za ufisadi.Technically ni kosa kubwa sana

..kweli cdm walifanya makosa kumfanya Lowassa mgombea wao.

..hoja yangu ni kwamba ndani ya ccm kuna mafisadi kibao. Lakini ccm wana ujasiri wa kuishambulia cdm kwa hoja ya ufisadi.

..katika mazingira hayo, cdm nao hawapaswi kuwa na kigugumizi kuwashambulia ccm kwa ufisadi.

NB.

..ccm hawapingi rushwa hata kidogo. Na ushahidi ni jinsi walivyowahonga madiwani wa cdm Arusha.
 
Ilihoja yako iwe na mashiko inabidi tujadili kwa kina aina ya watu wanaohama. Je, hao kweli ni watu? Je, wanasababu za msingi za kuhama? Hivi kweli mtu mwenye akili timamu anaweza kuhama kutoka CCM - Chadema -NCCR -CDM -CCM!!!! Na hivi vyama vyote alishatukana mitusi yote duniani eti siku anarudi tena anakusifia unafurahi, unapiga makofi!!

Isitoshe wengi wanaohama walikuwa viongozi. Hatukuwai kusikia hata siku 1 wakilaumu au pinga chama kwenye vikao vya ndani. Heri hata tungesikiwa umpigana na kiongozi mwenzako!! Mara zote walikuwa wakisifia chama. Je, hii tuiiteje, busara, hekima, uvumilivu au upumbavu na ujinga?. Hata hicho chama unachokimbilia kilianzishwa na watu walipigana kwa nguvu zao zote kukabiliana na changamoto, leo unaibuka eti chama hii kinzuri sana!!!

Hivi mtu ambaye aliwahi hongwa rushwa ya laki 2 tu akahama chama leo kaahidiwa Ukatibu mkuu au ukurugenzi atakataaa?? Tusiumize vichwa na watu kama hawa. Yuko wapi mzee aliyejifananisha na Drogba kila chama akienda anafiti?
 
Never, unataka kusema tanzania hii kuna anayeyaona hayo, never, ni njaa zinawasukuma kuondoka. Mbaya katika Tanzania hii ni Lowasa, Fisadi kuliko wote ni Lowasa (kama kweli tuhuma ni ya kweli). Nakuapia kama hawatapata wilaya na mikoa, watarudi Chadema. Usilete shallow analysis, hawa wanahama baada ya Magufuli kusema atahakikisha anaua upinzani. Njia moja wapo ni kuwanunua (madiwani), sasa anaona wenye njaa kama Kafulila, atawapa vyeo.... etc. Petro, akiwapa vyeo utasemaje? Time will tell. Yule binti tayari ni waziri, na akina kafulila and Co. Ltd wanategemea watafanyiwa hivyo.

Mkuu, "with all due respect" upinzani wa Chadema hauna nguvu sana kwa sasa maana yale yote walokuwa wakiyapigania, serikali chini ya CCM ndiyo inayatekeleza.

Chadema waache kutumia matukio kama sera zao na mikakati ya kutaka kugombea kuingia Ikulu.

Waanze upya kwa kuhakikisha wabunge wanaonekana wanafanya kazi waliyochaguliwa kuifanya.

Waje na sera mbadala na zionekane ni sera zipi ambazo zinakuwa ni zaidi ya zile zinazotekelezwa sasa na CCM na serikali yake.

Usitaje sera kama haki ya kufanya mikutano au kubomolewa nyumba zilizo ndani ya hifadhi ya barabara, hizo siyo sera bali ni hoja ambazo kamwe hazitasikilizwa na wananchi ambao huchambua hoja hizo.

Kama mwananchi anaona barabara inapaswa kupanuliwa kupitia ndani ya hifadhi yake na ni kweli amejenga ndani ya hifadhi basi ni lazima nyumba hiyo ivunjwe na apishe bila kutegemea kulipwa fidia yoyote.

Unapotaja sera Chadema ina sera zipi kuhusu Uchumi, viwanda, teknolojia, miundombinu, ajira, elimu, kilimo na kadhalika.

Unakuja na sera mbadala au "alternatives" unaweka wazi wananchi wanapima ingawa hakuna guarantee ya kuzikiubali kama zile zilizopo zinatekelezwa kwa kasi ya ajabu.

Mkishindwa kwenye uchaguzi mnapika sera zingine na zingine na hata baadae mnapata zile sera ambazo zinauzika kwa wapiga kura na huenda mkashinda uchaguzi.

Leo hii karibu nusu ya wabunge wa upinzani hawaenekani majimboni kwao, na hii ni kasoro kubwa sana kimkakati kwa Chadema ambayo ndiyo inawagharimu.

Pili, Dr Slaa ndiye alikuwa katibu mkuu wenu makini sana na hoja yake kwamba hawezi kula matapishi kwa kumkaribisha Edward Lowasa Chadema ni ya kuizingatia sana.

Vinginevyo ntaendelea kuamini kuwa Edward Lowasa, Fredirick Sumaye na mzee Kingunge Ngombale Mwiru wamehamia Chadema kukidhoofisha zaidi kuliko kukiimarisha.

Wakimaliza kazi hiyo basi mwenyekiti Mbowe atakuwa na wakati mgumu sana.

Naamini hayati Mwalimu Nyerere hakutaka kabisa vyama vya siasa lakini kwa kuwa hakuona faida ya kuendelea kuvikatalia akaamua kuvuruhusu mwaka 1992 na wengi hapa akiwemo Pasco tuliona huo ujio wa hivi vyama.

Lakini alifanya hivo kwa malengo kwamba ni lazima vyama hivi huko mbele visiwe na meno makali na hata vikiota meno makali basi wapo mafundi ya kuyapunguza.

Ndiyo maana Chadema inapaswa kuwa makini na utaratibu wake wa kukaribisha wanachama wapya hasa wale wanaohamia kutoka CCM ambao hakuna ushahidi kama wamerusisha kadi za vyama vyao.

Je, tunajua kama profesa Kitila Mkumbo au, bwana Katambi na wenzao kama walirudisha kadi za CCM walizokuwa nazo kabla hawajahamia Chadema kutoka CCM?

Jibu ni hapana.

Kama kweli Chadema ilitaka kuimarika kikwelikweli basi Freeman Mbiwe alipaswa kumpisha Edward Lowasa awe mwenyekiti wa chama ambapo angalau angeweka usawa katika majukwaa kama mtu "mzito" ingawa bado asingeweza kujisafisha na tuhuma za ufisadi.

Nafikiri utanielewa hapo.
 
..kweli cdm walifanya makosa kumfanya Lowassa mgombea wao.

..hoja yangu ni kwamba ndani ya ccm kuna mafisadi kibao. Lakini ccm wana ujasiri wa kuishambulia cdm kwa hoja ya ufisadi.

..katika mazingira hayo, cdm nao hawapaswi kuwa na kigugumizi kuwashambulia ccm kwa ufisadi.

NB.

..ccm hawapingi rushwa hata kidogo. Na ushahidi ni jinsi walivyowahonga madiwani wa cdm Arusha.

Kwa mtazamo wangu naona CHADEMA wajitafakari..warudi kwenye drawing board

Unajua kwenye hizi siasa unahitaji Differentiation

Bila kuwa na tofauti na CCM ...Utashindwa kusema bora mimi CHADEMA kuliko wale CCM
 
CC
Mkuu, "with all due respect" upinzani wa Chadema hauna nguvu sana kwa sasa maana yale yote walokuwa wakiyapigania, serikali chini ya CCM ndiyo inayatekeleza.

Chadema waache kutumia matukio kama sera zao na mikakati ya kutaka kugombea kuingia Ikulu.

Waanze upya kwa kuhakikisha wabunge wanaonekana wanafanya kazi waliyochaguliwa kuifanya.

Waje na sera mbadala na zionekane ni sera zipi ambazo zinakuwa ni zaidi ya zile zinazotekelezwa sasa na CCM na serikali yake.

Usitaje sera kama haki ya kufanya mikutano au kubomolewa nyumba zilizo ndani ya hifadhi ya barabara, hizo siyo sera bali ni hoja ambazo kamwe hazitasikilizwa na wananchi ambao huchambua hoja hizo.

Kama mwananchi anaona barabara inapaswa kupanuliwa kupitia ndani ya hifadhi yake na ni kweli amejenga ndani ya hifadhi basi ni lazima nyumba hiyo ivunjwe na apishe bila kutegemea kulipwa fidia yoyote.

Unapotaja sera Chadema ina sera zipi kuhusu Uchumi, viwanda, teknolojia, miundombinu, ajira, elimu, kilimo na kadhalika.

Unakuja na sera mbadala au "alternatives" unaweka wazi wananchi wanapima inagwa hakuna guarantee ya kuzikiubali kama zile zilizopo zinatekelezwa kwa kasi ya ajabu.

Mkishundwa kwenye uchaguzi mnapika sera zingine na zingine na hata baadae mnapata zile sera ambazo zinauzika kwa wapiga kura na huenda mkashinda uchaguzi.

Leo hii karibu nusu ya wabunge wa upinzani hawaenekani majimboni kwao, na hii ni kasoro kubwa sana kimkakati kwa Chadema ambayo ndiyo inawagharimu.

Pili, Dr Slaa ndiye alikuwa katibu mkuu wenu makini sana na hoja yake kwamba hawezi kula matapishi kwa kumkaribisha Edward Lowasa Chadema ni ya kuizingatia sana.

Vinginevyo ntaendelea kuamini kuwa Edward Lowasa, Fredirick Sumaye na mzee Kingunge Ngombale Mwiru wamehamia Chadema kukidhoofisha zaidi kuliko kukiimarisha.

Wakimaliza kazi hiyo basi mwenyekiti Mbowe atakuwa na wakati mgumu sana.

Naamini hayati Mwalimu Nyerere hakutaka kabisa vyama vya siasa lakini kwa kuwa hakuona faida ya kuendelea kuvikatalia akaamua kuvuruhusu mwaka 1992 na wengi hapa akiwemo Pasco tuliona huo ujio wa hivi vyama.

Lakini alifanya hivo kwa malengo kwamba ni lazima vyama hivi huko mbele visiwe na meno makali na hata vikiota meno makali basi wapo mafundi ya kuyapunguza.

Ndiyo maana Chadema inapaswa kuwa makini na utaratibu wake wa kukaribisha wanachama wapya hasa wale wanaohamia kutoka CCM ambao hakuna ushahidi kama wamerusisha kadi za vyama vyao.

Je, tunajua kama profesa Kitila Mkumbo au, bwana Katambi na wenzao kama walirudisha kadi za CCM walizokuwa nazo kabla hawajahamia Chadema kutoka CCM?

Jibu ni hapana.

Kama kweli Chadema ilitaka kuimarika kikwelikweli basi Freeman Mbiwe alipaswa kumpisha Edward Lowasa awe mwenyekiti wa chama ambapo angalau angeweka usawa katika majukwaa kama mtu "mzito" ingawa bado asingeweza kujisafisha na tuhuma za ufisadi.

Nafikiri utanielewa hapo.
CCM ilikuja na sera gani mbadala? Unaangalia weak point ya mpinzani wako unamgonga hapo hapo. matukio ya kuvunja haki za binadamu ni muhimu sana kupata wanachama na kuungwa mkono.......................
 
CC

CCM ilikuja na sera gani mbadala? Unaangalia weak point ya mpinzani wako unamgonga hapo hapo. matukio ya kuvunja haki za binadamu ni muhimu sana kupata wanachama na kuungwa mkono.......................

"Off course", sera za CCM ni zilezile lakini zilikuwa hazitekelezwi kwa vitendo na wananchi tukaona na badala yake tunafahamu kilichokuwa kinafanyika.

Yaani serikali zilizopita zilikuwa zilikuwa na makubwa zaidi ya mapato yake.

Hivyo fedha zilizokuwa ziende kwenye maendeleo hazikuwepo.

Sera hizohizo na ilani ya uchaguzi ileile ya mwaka 2015 ndizo zinazofanyiwa kazi kwa sasa na serikali ya awamu ya tano chini ya raisi John Magufuli.

Na hilo halina ubishi kwani tunashuhudia utekelezwaji wake.
 
Wanasemaga anayekueleza ukweli ndiye akupendaye,nadhani Chadema wamekusikia.Kaka Paschal naomba kutofautiana kidogo sana na wewe,uchaguzi wa mwaka 2015 hautakuwa rahisi " ki hivyo",sababu naogopa kuzitoa hapa nisije kupimwa UTI kaka.
 
"Off course", sera za CCM ni zilezile lakini zilikuwa hazitekelezwi kwa vitendo na wananchi tukaona na badala yake tunafahamu kilichokuwa kinafanyika.

Sera hizohizo na ilani ya uchaguzi ileile ya mwaka 2015 ndizo zinazofanyiwa kazi kwa sasa na serikali ya awamu ya tanoi chini ya raisi John Magufuli.

Na hilo halina ubishi kwani tunashuhudia utekelezwaji wake.

..kwa hapa naomba msaada.

..najua kuna ilani ya ccm.

..lakini sera za ccm ni zipi ?

..pia sina uhakika kama ccm wana itikadi tena.

..majuzi nilimsikia mbunge wa ccm akilalamika kuwa serekali ya Magufuli inataka kuirudisha nchi kwenye "ujamaa"!!

Cc The Valiant
 
..kwa hapa naomba msaada.

..najua kuna ilani ya ccm.

..lakini sera za ccm ni zipi ?

..pia sina uhakika kama ccm wana itikadi tena.

..majuzi nilimsikia mbunge wa ccm akilalamika kuwa serekali ya Magufuli inataka kuirudisha nchi kwenye "ujamaa"!!

Cc The Valiant

Ilani au manifesto ni mwongozo wa wapi chama kinaelekea yaani kwa mfano dira ya maendeleo ya CCM ni ya 2010-2020 halafu kuna 2015-2025.

Hivyo CCM katika dira yake imekusudia kupambana na mambo manne:

1. Kuondoa Umaskini
2. Kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana.
3. Kuondoa tatizo la Rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma.
4. Kudumisha Amani na ulinzi pamoja na usalama wa wananchi na mali zao.

Hivyo ni dira na inatekelezwa.

Kwa mfano Ilani kuu ya uchaguzi 2005 na 2010 ilikuwa ni Kasi mpya, Ari Mpya na Nguvu Mpya iliishia wapi? Maisha bora kwa kila mtanzania tunafahamu kilichototokea.

Sera ni mipango ya Serikali inayoundwa chini ya CCM kama dola ambapo ndiyo inaona sera ya viwanda, miundombinu kama barabara zinajengwa, Uchumi, sera za madini na nishati, sera ya elimu na sera ya kilimo na uzalishaji.

Itikadi yaweza kubadilika kulingana na mtazamo wa kiongozi aliepo madarakani maana hata huko Uchina raisi Xi anafanya mabadiliko kulingana na mahitaji yake na chama.

Hivyo kwa kuwa taifa letu bado linapiga hatua za maendeleo, basi itakadi yaweza kubakia kuwa ya ujamaa na kujitegemea kulingana na utelekezaji wa sera kama ya elimu bure ambapo serikali inalipia gharama za elimu ili kumkomboa mtoto asome na afahamu kusoma na kuandika.

China bado inacheza na itikadi hiyo huku ikikaribisha mabepari lakini ambao wapo tayari kufuata masharti ya China.
 
Kwa taarifa yenu Chadema ipo vizuri sana kuliko wakati mwingine wowote ule..

Pamoja na kuandamwa na vyombo vya Dola...

Kunyimwa uwanja sawa na uhuru wa kujieleza...

Chadema ipo na itaendelea kuwepo...
 
Back
Top Bottom