CHADEMA, Ludovick Rwezahula anaangamia mahabusu, utu uko wapi?

CHADEMA, Ludovick Rwezahula anaangamia mahabusu, utu uko wapi?

Status
Not open for further replies.
Mkuu, unataka kusema muda wote huo bado tu hajajua kuwa kijana yuko mahabusu, tena amekongoroka vibaya! CHADEMA imuangalie jamani, kiubinadamu tu.

Koma!Anapata kile anachostahil,mwambie chemba aliyemtuma akamtoe.ENDELEA NA WW KUWATUMIKIA MAGAMBA LAKINI KUMBUKA HAWAKAWII KUKUTOSA.
 
Tuliambiwa Rudovick haishi gerezani kwani hakuna ushahidi unaothibitisha yeye kuwa mahabusu.

Si kweli mkuu, kijana yuko gerezani ananyea debe tu. Inasikitisha sana kwa hatua aliyofikia.
 
Ajira apewe na ccm, kazi awafanyie ccm, mshahara alipwe na cdm? mbona majanga!
 
Ludo ni rafiki ake na lwakatare na ni private secretary wa slaa

Mbona Mna Force CDM Wakamtoe, Mna Huruma Sana????
Kama vp Nenden Mkamtoe Ninyi hata Ma Didas Mu Mpe Kabisa
 
Ludo ametumiwa sana na chadema km mpelelezi hususan kujua ukubalikaji wa viongozi wao kwa jamii

Mkuu, hiyo iwe fundisho kwa vijana wengine walio bega kwa bega na CDM, kwani hawawezi kujua hamta yao wenda yaweza kuwakuta haya haya Ludo.
 
Kwani mahakama imelazimisha kwamba dhamana lazima ifanywe na chadema??
 
Kijana wa Bavicha katelekezwa, Chadema mna jopo la wanasheria msaidieni huyu kijana.
 
mwosha huoshwa.
mtoa mada unajifanya kinyonga kwanini nyie magamba msimmwekee dhamana?
kwani masharti yake yanataka mwanachadema ndio amdhamini?
mwache akae huko baadae atatubu makosa yake yote..
 
kama kweli unauchungu kwanini usiende kumtolea dhamana? kinacho mtafuna ni usaliti wake. na kitu nilichokuwa nadhani na kinanipa yawezekana kuwa ni kweli. huyu jamaa inaonesha alishiriki moja kwa moja kumpiga kibanda, na hivyo kuepuka damu zilizo kuwa zimemrukia, akavua nguo kisha akadai amnyang'anywa mpaka nguo. wakumuomba kumtolea dhamana ni mwigulu.
CCM wamemgeuza jamaa kama toilet paper, na walichokuwa wakikikuthudia kuhusu ugaidi hawajafanikiwa. Usimuhusishe Dr. slaa na usaliti!

Ipo siku na wewe yaweza kukukuta kama haya tuwe na huruma na tuthamini mchango wake ktk chama.
 
Ajira apewe na ccm, kazi awafanyie ccm, mshahara alipwe na cdm? mbona majanga!

Mkuu, inaonekana hujui au unavika upofu kuhusu uchakalikaji wa kijana Ludo kwa CDM.

Kijana Ludo kwa Dr Slaa alikuwa ni lulu, kijana aliaminiwa na Dr Slaa mpaka akamfanya private secretary.

Kwanini wamteme hivi?
 
Mkuu, inaonekana hujui au unavika upofu kuhusu uchakalikaji wa kijana Ludo kwa CDM.

Kijana Ludo kwa Dr Slaa alikuwa ni lulu, kijana aliaminiwa na Dr Slaa mpaka akamfanya private secretary.

Kwanini wamteme hivi?


Kama Big g, utamu wake umeisha. Km unadhan utamu bado upo, iokote na ui-chew.
 
CHADEMA wanahusikaje na dhamana ya Ludovick wakati boss wake ni Mwigulu? Huu uzi wako ulitakiwa umuulize Mwigulu kuwa mbona kamtosa mtu wake?
 
Kwani mahakama imelazimisha kwamba dhamana lazima ifanywe na chadema??

Mkuu, ndugu zake hawana uwezo halafu ukizingatia wengi wao wako Bukoba, katika hali kama hiyo, ni ngumu kuweza kumtolea kijana Ludo dhamana hata kuja tu mahakamani inashindikana.

Dr Slaa alikuwa kama baba kwa Ludo, kwanini asilifanye hili suala kama lake na akamsaidia kijana anaengamia mahabusu. Dr Slaa awe na roho ya utu na akumbuke fadhira zote za kijana huyu katika kumtumikia. Jamani, ni utu tu.
 
du umenikumbusha alikuwa anatumiwa money kwa m-pesa ...amuulize imekuwaje tena hasaidiwi?
 
Wenye utu hapo na wanaopaswa kulaumiwa ni maccm wakiongozwa na mwigulu nchemba kwani hao ndio waliomsababishia huyo dogo matatizo yote hayo kwa njaaaaaaaaaa
 
Dah inasikitisha sana we hav to think before. Nitabaki tu kuwa neutral mambo haya ni magum sana. Siasa ni mchezo mchafu.
 
WanaJF!

Leo ni siku ya kesi ya bwana Lwakatare kusikilizwa kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, lakini kesi imehairishwa mpaka July 22, 2013.

Pamoja na hayo, mshitakiwa na.2 bwana Ludovick Rwezaura ameshindwa kupata dhamana kwa sababu ya kutokamilika kwa nyaraka za dhamana, ingawa dhamana yake iko wazi kabisa.

Bwana Ludovick akiwa nje ya mahakama, ameonekana akiwa mnyonge na alikuwa akilia sana kwa uchungu huku akilalamika ndugu zake (ambao hawakufika mahakamani) hawafatilii dhamana yake.

Kwa hali kama hiyo, kijana Ludovick anaendelea kusota gerezani na kuzidi kuangamia, kwani wote sisi ni wanaadamu na tunajua makali ya maisha ya gerezani.

Rai yangu kwa CHADEMA; haijarishi kijana Ludovick kama alikuwa mwajiriwa wa CHADEMA kimkataba ama alikuwa volunteer, jambo la msingi ni kwamba alikuwa ana kitumikia CHADEMA kwa moyo wake wote na nguvu zake zote. Ludovick alijitoa kwa CHADEMA kwa namna yake, ni kijana ambae alikuwa bega kwa bega na Dr Slaa kiutendaji na vile vile alikuwa kama mtoto kwa Dr Slaa.

Katika hali kama hiyo sikutarajia kama CHADEMA kinaweza kumtema na kumkataa kabisa bwana Ludovick Rwezaura. Kwani wote tunafahamu kuwa, kosa aliadhibiwi kwa ubaya, bali kosa dawa yake kukosolewa. Sasa kwanini CHADEMA wana muadhibu kijana Ludovick kwa ubaya? kwanini wasimsaidie hata kwa dhamana ili aweze kutoka kwenye 'jehanamu' ya duniani?

Maamuzi haya ya kumtupa mkono kijana Ludovick katika hali hii mbaya inayo mkabili, inajenga wasiwasi mkubwa kwa vijana wengi walio CHADEMA juu ya hatma yao endapo wakikosea jambo. Je, chama kitawasaidia kwa lolote? Ni wakati vijana wakawa makini sana na namna ambavyo CHADEMA na viongozi wake wana shughulikia nidhamu na makosa ya wanachama wao, hiki anacho fanyiwa Ludovick, hakina tofauti sana na walicho fanyiwa Juliana Shonza na Mtela Mwampamba.

View attachment 101283Kijana Ludovick akionekana amenyong'onyea leo mahakamani, pembeni yake ni bwana Lwakatare wakiwa na askari magereza.


Mwambieni bosi Mwigulu na Nape wenu akafute ile kesi kama mnahuruma sana..........

Mnajifanya sahizi mnahuruma wakati mnawafungulia kesi ya ugaidi mlikuwa hamujui, Lwakatare alikuwa anaumwa kisukari pamoja na hivyo mkamfungulia mashtaka ya kigaidi kinyume na sheria, leo ndiyo mnaona huruma.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom