CHADEMA, Lowassa apewe onyo mara moja

CHADEMA, Lowassa apewe onyo mara moja

Chadema ilikuwepo kabla ya Lowassa kuhama CCM, na tena ilikuwa ni chama imara, pendwa na chenye nguvu na ushawishi wa kutosha, hasa katika miji mikubwa ya Tanzania.

Hata Ukawa iliasisiswa kabla ya Lowassa kukatwa na kuhamia CDM. Kwa misingi hii hamna mtu anayeweza kuja na takwimu halisia eti bila Lowassa mambo yangekuwaje UKAWA?? Kama yupo azilete.

Hoja yangu ni hii;
Lowassa mpaka sasa amegeuza kila aina ya mafanikio ya UKAWA kuwa yake binafsi na kujinasibu kuwa yeye ndo ameyaleta. Amekuwa akijinasibu kwa kauli za kujisifia binafsi kana kwamba Chadema na Ukawa havikuepo na yeye ndo alikuja kiuasisi Chadema na muungano wa Ukawa.

Kauli za Lowassa zinakiweka chama mikononi mwake, na si mikononi mwa wanachama waliosumbuka kukijenga chama hiki kwa machozi, jasho, damu, vifo, njaa, na kudhalilishwa na Nguvu za Dola.

Mfano wa kauli za Lowassa;
  1. "Nimewawezesha wapinzani kufikisha wabunge zaidi ya 100, tukiweka na viti maalum"
  2. "Nimewasaidia kushikilia jiji la Dar es salaam"
  3. "Nitagombea 2020, najiandaa na uchaguzi mkuu "
  4. "Nimeufanya upinzani kuwa na nguvu kuliko wakati wowote"
Na nyingine nyingi zenye utata!

Swali ni je, kwanini hizi "nime" zisiwe "chama kime"? Halafu toka lini Lowassa amefuta taratibu za kumpata mgombea urais ndani ya chama na kujihakikishia nafasi ya kugombea uchaguzi mkuu 2020??

Lowassa apewe onyo, na afunzwe kuwa siasa ni collective and intergrated efforts na sio One man show or else mtwambie kama amekabidhiwa chama mikononi mwake, na lini ilifanyika hivyo.
Mnaye huyo.
Na sasa anasema atagombea 2020, sijui kwa kuchaguliwa vipi kwenye chama kugombea nafasi hiyo, itakayofanyika miaka mitano baadaye.
Au mlifanya uchaguzi usingizini!!!!!
 
Ngojeni dawa iwaingie.

Tulipowaambia jamaa ni mbinafsi mulitubeza na kutona vikaragosi, sasa kelele za nini?

Na bado, siku ata tamka "Mnyika na Nassari wafutwe uwanachama" ndio akili zitawakaa sawa.
 
..
Swali ni je, kwanini hizi "nime" zisiwe "chama kime"? Halafu toka lini Lowassa amefuta taratibu za kumpata mgombea urais ndani ya chama na kujihakikishia nafasi ya kugombea uchaguzi mkuu 2020??...
Tupitie na kauli hizi pia:
  • Chagua Magufuli (sio chagua CCM)
  • Serikali ya Magufuli ni ya Viwanda (sio serikali ya CCM ni ya viwanda)
  • Magufuli 4 Change
 
Chadema ilikuwepo kabla ya Lowassa kuhama CCM, na tena ilikuwa ni chama imara, pendwa na chenye nguvu na ushawishi wa kutosha, hasa katika miji mikubwa ya Tanzania.

Hata Ukawa iliasisiswa kabla ya Lowassa kukatwa na kuhamia CDM. Kwa misingi hii hamna mtu anayeweza kuja na takwimu halisia eti bila Lowassa mambo yangekuwaje UKAWA?? Kama yupo azilete.

Hoja yangu ni hii;
Lowassa mpaka sasa amegeuza kila aina ya mafanikio ya UKAWA kuwa yake binafsi na kujinasibu kuwa yeye ndo ameyaleta. Amekuwa akijinasibu kwa kauli za kujisifia binafsi kana kwamba Chadema na Ukawa havikuepo na yeye ndo alikuja kiuasisi Chadema na muungano wa Ukawa.

Kauli za Lowassa zinakiweka chama mikononi mwake, na si mikononi mwa wanachama waliosumbuka kukijenga chama hiki kwa machozi, jasho, damu, vifo, njaa, na kudhalilishwa na Nguvu za Dola.

Mfano wa kauli za Lowassa;
  1. "Nimewawezesha wapinzani kufikisha wabunge zaidi ya 100, tukiweka na viti maalum"
  2. "Nimewasaidia kushikilia jiji la Dar es salaam"
  3. "Nitagombea 2020, najiandaa na uchaguzi mkuu "
  4. "Nimeufanya upinzani kuwa na nguvu kuliko wakati wowote"
Na nyingine nyingi zenye utata!

Swali ni je, kwanini hizi "nime" zisiwe "chama kime"? Halafu toka lini Lowassa amefuta taratibu za kumpata mgombea urais ndani ya chama na kujihakikishia nafasi ya kugombea uchaguzi mkuu 2020??

Lowassa apewe onyo, na afunzwe kuwa siasa ni collective and intergrated efforts na sio One man show or else mtwambie kama amekabidhiwa chama mikononi mwake, na lini ilifanyika hivyo.
Umeandika Sana lakini yanabaki Kuwa mawazo yako na yanaheshimiwa
 
Yaani nyinyi wa upande wa dola mnatoa povu kama mmepigwa kipepsi kitandani. Mbona anayoboronga JPM hamsemi nakuu Magufuli for Change siyo CCM for change. Serikali ya Magufuliu itafanya ---- siyo serikali ya CCM itafanya ------. Chagua Magufuli siyo CCM. Kwa nini iwe nongwa kwa mtu kueleza aliyonayo, anayoyafanya na ushahidi upo?

Matatizo ya utumwa wa akili uliosimikwa na CCM. Mleta mada Lowasa na kauli zake kama ilivyo kwa JPM SIYO ISSUE HIZO ISSUE NIFACTS ON THE GROUND. Elimu bure si issue kwanza bure aghali. Kuna elimu elimu elimu siyo bora elimu.
 
Hawez kuwa chadema huyu . Kada wa chadema anayejitambua Hawez andika hivyo .
Wewee! usifikiri kila mwana chadema ni Nyumbu km ww, wengine wanajitambua.

Huyo SONGOKA, humu si mgeni, ni mchadema aliekunywa maji ya bendera lkn inaonekana jamaa anajitambua.

Tofauti yake na nyinyi manyumbu wengine, mwenzenu anasimamia anachokiamini wakati nyinyi munafuata tu kisa kiongozi flani kasema.
 
Acha

acha hizo Lowasa apewe Onyo la nini? ww badala ya kuhangaikia kipato chako na familia yako unashinda kukariri kauli za Lowasa tu, huna cha kufanya? Chadema hawana shida na kauli hizo wali hazina Tatizo mda huu watu wapo busy kumuandaa katibu mkuu wa chama.
Wanapata mgombea 2020 katibu hakuna
Kweli CDM vituko
 
Yaani nyinyi wa upande wa dola mnatoa povu kama mmepigwa kipepsi kitandani. Mbona anayoboronga JPM hamsemi nakuu Magufuli for Change siyo CCM for change. Serikali ya Magufuliu itafanya ---- siyo serikali ya CCM itafanya ------. Chagua Magufuli siyo CCM. Kwa nini iwe nongwa kwa mtu kueleza aliyonayo, anayoyafanya na ushahidi upo?

Matatizo ya utumwa wa akili uliosimikwa na CCM. Mleta mada Lowasa na kauli zake kama ilivyo kwa JPM SIYO ISSUE HIZO ISSUE NIFACTS ON THE GROUND. Elimu bure si issue kwanza bure aghali. Kuna elimu elimu elimu siyo bora elimu.
Shida ni pale cdm inapobanwa kwenye hoja kukimbilia kujifananisha na ccm......
 
mkuu hiki ni chama cha wanachama wote, na sio mtu mmoja, anayoyafanya LOWASA ndo yaleyale aliyofanya ZITO; ya kujifanya kila zuri wewe ndo umelileta.

Mwaka 2012 nilibandika hapa uzi wenye kichwa cha habari (NAIBU KATIBU MKUU) nikikemea unafiki wa zitto kujibinafshia chama na kuwataka viongozi wamtimue, wengi mlishambulia hivihivi buta baadaye hii ikawa hoja yenu kuu.

natoa angalizo : Tabia hii haikubaliki
Zitto tofauti na Lowassa
Zitto hatoki kaskazini
Zitto hana pessa
Zitto hajainunua cdm
 
Kufukuzwa hapana ila kauli za "nime" kwa kweli kitaasisi sio nzuri. Ni za kutaka kujiinua na kujipa utukufu badala ya kumwacha Mungu mwenyewe akuinue. Ni kauli za akina Zitto hizi na kwa mbaali Slaa alikuwa pia na katabia ka aina hiyo; yapasa aziache mara moja.
Mlitaka asemeje wakati mmemuuzia chama
Mnapenda pesa zake, Tulieni
 
Shida ni pale cdm inapobanwa kwenye hoja kukimbilia kujifananisha na ccm......
Rejea bandiko langu; wewe unachoita hoja kwangu mwenye kuelewa ni viroja. Una uypungufu wa elimu elimu elimu na umezoea hivyo ujinga ujinga ujinga.
 
Mh rais Ngoyai yupo sahihi, wewe waongozwa chuki tu, aliyoyasema ni kweli tupu, lini upanzani ulishawahi kuongoza halmashauri? Na lini upinzani wamekuwa Na idadi kubwa ya wAbunge mjengoni, hebu pungezi kumuwaza lowassa mtapata kansa vichwani mwenu
Basi mwambieni aunde chama chake aongoze zaidi mwaka 2020
 
Back
Top Bottom