Wadau Jf;
Kuna tonyo nimemegewa usiku huu kuwa haya Ma-sisiem kwa woga wao yamepeleka kikosi rasmi toka dar, toka vituo mbalimbali vya policcm dar kuweka kambi chalinze ili kuhakikisha 'mtoto wa mfalme haadhiriki' na anashinda kwa 'kishindo'. Hii ni breaking nimeipokea toka kwa class-mate wangu aliye askari anayefanyia kituo cha Wazo, kanihakikishia kuwa kikosi rasmi kilichounganisha polisisiem toka wazo, kunduchi, oyster bay na wengineo wapo chalinze usiku huu kucha ..eti kwa kazi rasmi ya kuhalikisha mfalme mdogo Riz1 hashindwi...aliongea kwa kuilalamikia ccm, kanihakikishia naye yupo chalinze usiku huu! Nilipomcheki na mdau mwingine wa kambi ya kunduchi kaniambia wapo mbali jiji, wapo chalinze wamepewa Kazi huko usiku huu!
Mtaamini sasa kuwa CCM ni debe tupu kwa kiwango gani, lakini kwa wale wanaokesha hapa jamvini jf kuitetea kwa ajili ya kuganga njaa na buku 7 za Lumumba hawatasita kunyanyua kope na kuanza kuimba! . Mambo yao hayooo!
, ukweli ni kuwa haya ma-ccm yapo ktk ukingo mbaya, hawajiamini, hawaamini yeyote na kutokana na udhalimu wao hawaamini hata wale inaowaweka ktk majukumu mfano mawakala wao, wasimmizi wa uchaguzi na hata baadhi ya polisi wa serikali yao! Kweli hii hatari
..tena hatari kweli...ndio maana kura ya siri kwao ni moto wa jehanam na wamejaa woga hakuna picha.
..Ni jambo lililonishangaza sana na naomb wadau engine walio na marafiki askari wa baadhi ya vituo nilivyotaja wawadodose wataafiki ukweli huu.
Mbaya zaidi kesho baada ya kura za wizi, magumashi na feki nyingi...ma-ccm yatatangaza kushinda kwa kishindo na tume ya uchaguzi inathibitisha ufidhuli huu...nyang'au! Nchi hii kubaki chini ya ccm ni kuishi jehanamu ukiwa hai..wizi na uozo mtupu!
Nawasilisha..