Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,217
- 128,979
- Toka Jumapili nipo hapa Kilosa, hakuna Chadema presence kabisa, yaani hata Madiwani wote ni wa CCM, I mean ni vigumu sana kwetu CCM kutawala bila kukumbushwa mapungufu yetu na Chadema sasa wanapokuwa hawapo kabisa mara nyingi inapelekea Viongozi wetu wa CCM kujisahau.
- Halafu inakuja hoja yangu ya msingi, Vipi Chadema kumpeleka Slaa DC Washington badala ya kumleta huku Kilosa aje ajaribu kufungua matawi? I mean Tawi la Kilosa si linaweza kuwa muhimu kwa Chadema kuliko tawi la wanachama wanne la DC Washington/USA? Chadema ni muhimu sana mkaangalia priorities zenu kwa sababu hii no moja ya changamoto kubwa inayowatesa sana ya kukimbilia kuanzisha matawi ambayo ni fruitless huko nja na kwa gharama kubwa kuliko kuhangaikia hapa Bongo kwa gharama ndogo na yenye matokeo ya kura kwa chama chenu.
Le Mutuz
Mkuu Wille, kati ya mambo ambayo mimi ninakukubali ni pale unapokuwa mkweli, kama hapo kwenye bold!. Kumbe ni kweli CCM imejisahau, japo sikubaliani na wewe kuwa ni lazima kukumbushwa na Chadema tuu, no, hata sisi ambao hatuna vyama tumekuwa tunaikumbusha CCM ila kwa vile ni Chadema tuu ndio inayowakosesha usingizi, then kukumbushwa kwenu ni na Chadema tuu!.
Hili la ushauri wako kwa Chadema kuhusu priorities nalo ni la kweli, ila japo mimi sio Chadema, ila naamini lengo la ziara ya Dr. kule sio tuu kufungua matawi, kama kuna ufunguzi wa matawi, itakuwa ni just one of!.
Kwangu mimi kuelekea uchaguzi wa 2015, issue sio CCM ina matawi mangapi au Chadema ina matawi mangapi mahali, kwa sababu wanaopiga kura sio CCM au Chadema bali ni wananchi!. Ili chama fulani kishinde, kinategemea mwamko wa watu husika kujitambua na kupiga kura wakiwa na informed decision wanakipigia chama gani na kwa sababu zipi!.
Unaweza kushangaa hapo Kilosa hakuna tawi hata moja la Chadema, ukafanyika uchaguzi, Chadema ikasimamisha mgombea na akachaguliwa!.
Hii ni kutokana na kwenye baadhi ya maeneo, CCM imekuwa ikichaguliwa kwa mazoea tuu, huku asilimia kubwa zaidi ya wapiga kura wakiwa wamejilalia zao!. Hawa waliolala wakiamka ni hatari sana!. Ndio maana nawaona watu wakipita huku na kule kuwahimiza watu waendelee kulala, huku wengine wakipita huko na huku wakiwaamsha!. Japo amsha amsha haijaipitia Kilosa, kuna uwezekano wakaamka tuu hata kwa kele za jirani!.
Niliwahi kusema humu kuwa kwenye baadhi ya maeneo, CCM imechokwa mpaka basi, kiasi kwamba hata Chadema wakisimamisha jiwe, jiwe litachaguliwa!. Hii ni changamoto kwa Chadema, hata kama haina tawi, kuhakikisha chaguzi zijazo, inasimamisha wagombea kila kitongoji, kila kata, kila tarafa, kila kijiji, kila wilaya, na kila jimbo na ikitokea hakuna mwanachama hata mmoja, basi kisimamishe tuu hata jiwe, liandikwe Chadema!, nakuhakikishia jiwe litapita!.
Uchahuzi uliopita, waliojiandikisha kupiga kura ni milioni 20, waliojitokeza ni milioni 8 na CCM imechaguliwa na kura milioni 6 tuu!. Wale milioni 12 ambao hawakujitokeza, ni ama wamelala, ama wamekata kabisa tamaa kuwa hata ufanye nini CCM itapita tuu, hivyo kuamua kutojisumbua kwenda kupiga kura, bora wajilalie zao!. Hawa 12 ambao hawakupiga kura ndio hatari zaidi kuliko wale 6 waliopigia kura CCM, kwa sababu wakiamka na kujiunga na wale wawili, watakuwa ni 14!, hivyo kiukweli, bora kuendeleza hiyo kazi mzuri ya kuwasisitiza waendelee kulala ndio salama ya CCM 2015!, wakiamka, au hata kuamshwa tuu na kelele za majirani, kiukweli Wile, uchaguzi wa 2015, CCM kazi mnayo!.
Pasco.