CHADEMA kukutana na wanahabari leo mchana

CHADEMA kukutana na wanahabari leo mchana

Yaliotoke kule upande mwingine upande huu nao unayainga ama kweli mkubwa ni mkubwa tu .
 
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimempitisha Grace Tendeya Mvanda, kuwa mgombea wake katika kinyang'anyiro cha ubunge katika jimbo la Kalenga, mkoani Iringa.

Grace Mvanda alikuwa mtu wa pili katika kinyang'anyiro cha kura za maoni jimboni humo. Aliyeshika nafasi ya kwanza alikuwa ni Lucas Sinkala Mwenda (31) ambaye Kamati Kuu haikupitisha jina lake.

Mwenda ni mhitimu wa Shahada ya Kwanza ya Sheria na sasa anataka kujiunga na Mafunzo ya Sheria kwa vitendo.

Uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga umepangwa kufanyika 16 Machi 2014. Uchaguzi huu unatokana na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Dk. William Mgimwa kufariki dunia miezi miwili iliyopita nchini Afrika Kusini.

Taarifa za ndani ya kikao zinasema, Kamati Kuu ilijadili kwa kina majina ya wagombea wote wa nafasi hiyo; huku wajumbe wakipata nafasi ya kuwahoji kila mgombea aliyekuwa anatafuta nafasi ya kupeperusha bendera ya chama.

Hatimaye Grace Masha, kwa kutumia ripoti za interejensia ya chama na vigezo vingine, aliteuliwa kuwakilisha chama katika kinyang'anyiro hicho.

Miongoni mwa vigezo vilivyotumika, ni kwamba mwanamama huyo aliwahi kugombea ubunge katika jimbo hilo mwaka 2005 kupitia chama cha Jahazi Asilia. Alishindwa.

Lakini alishika nafasi ya pili nyuma ya mgombea wa CCM. Taarifa zinasema, pamoja na kwamba JAHAZI Asilia hakikuwapo jimboni humo na mkoa wa Iringa kwa ujumla, lakini alifanikiwa kujinyakulia kura 13.500.

"Hii inaonyesha mgombea huyo anakubalika," anaeleza Tundu Lissu, Mwanasheria mkuu wa chama hicho.

Lucas Sinkala Mwenda, alikubaliana kwa moyo mmoja na maamuzi ya Kamati na ameahidi kutoa ushirikiano kwa mgombea na kukisaidia chama chake kushinda
.
 
Ina maana yule mwanasheria wamembadilisha?tatizo ni nini?
 
Vipi suala la ubaguzi wa kijinsia katika eneo hilo limeangaliwa vizuri? Ili lisije kuwa sababu ya kushindwa mgombea wetu.
 
Nahisi Baregu anaweza kufukuzwa kutokana na msimamo wake juu ya ZZK. Maana yeye Kama Prof wa Siasa anaona swala la ZZK lilipaswa kuchukuliwa kwa uangalifu mkubwa Huku busara ikitawala!
 
Sasa kma waliyajua hayo zile kura za maoni walupiga za nnn????
 
Mkuu, we ndo hujutambui

wasiwasi wangu ni kwamba ipo siku tunaweza kumpata mtu kama wewe akawa rais. Tutajuta kama tunavyo juta sasa.mpaka 2015 TMBO WOTE WATAKUWA WAMEUAWA,Lakini rais anasema wauaji anawajua vizuri tena kwa namba lakini kuchukua hatu mmh. Wauzaji wa madawa ya kulevya anawajua vizuri lakini kuchukua hatua mmh! Wezi wa EPE anawajua vizuri lakini kuchukua hatua mmh! Wanawake wametukomoaje? maana ndio walio mchagua. mpaka 2015 kule mstuni watabaki digidigi tu labda na nyoka wadogodogo. Lakini utawasikia wenyewe wakisema huyu ndio BONGE LA PRESIDA!! Hivi huwa mna mu enjoy au huwa mko serious?
 
Naona Nyumbu wa Lumumba wakiongozwa na Lizaboni na MSALANI wamevamia thread kwa Speed kubwa sana.
Hawa Ma Punguani siwaonagi kabisa katika nyuzi zile Nyuzi zinavyoonyesha Serikali ilivyo kinara katika Ujangili wa kuua tembo na Faru.
Hawa ndo wale watu walioko ndani wanapiga soga tuu huku Nyumba yao inaungua wakati kuna watu kutoka mbali kabisa wanapiga kelele kuwastua kuwa Nyumba yao inaungua.
Hawa watu ni wa Kupuuzwa na kuonewa huruma kwa kuwa bado hawaja Jitambua.
Teh!teh!teh ccm bana!
 
Last edited by a moderator:
watueleze matumizi ya ruzuku ya chama, watueleze operation chopa ilitumia shillings ngapi, watueleze kwa nini wameshindwa vibaya uchaguzi wa udiwani kwa kupata kata tatu tu, ..

kutumia chopa inawauma sana lumumba mbon ujangili hauwaumi hivi
 
Sasa kma waliyajua hayo zile kura za maoni walupiga za nnn????

Walitaka kulipana Posho,wanachama wamemchagua mwanasheria,Uongozi wanamtaka Mwanamke,kwani waliomchagua huyo mwanasheria hawajui kama uyo mama yupo,na aligombea kupitia Jahazi....yale yale ya Mama makinda kuwa Spika
 
Iringa mwaka 2010, wanachama wa CCM walimchagua Fredrick Mwakalebela, KK ya CCM, ikamuondoa na kumuweka mama Mbega. Je! CCM ni Role model wa vyama vingine? nauliza tu lakini.
 
Wanataka kutuambia watatupia chopa kumi Kalenga

Kutoka moyoni ninaipenda sana cdm, yaani haya maneno yenu yakipuuzi yanatuongezea munkari tu, hapa ushirombo maisha ni full V tu yaani sign of VICTORY, tunaishukuru cdm ndo mkombozi wetu, sasa hv mama,baba,dada zangu,wajomba,shangaz wooooooote huwa nawaambia maovu ya ccm,wanaichukia mbaya,nawaambia tuthubutu hata kuiadhibu tuitoe madarakani ili wawe na adabu,kama bibi yangu amejua uozo wa ccm,je wewe Chris lukosi vp? Najua una maslahi binafsi kuitetea ccm,pole,lakin najua moyon mwako ni cdm full
 
Iringa mwaka 2010, wanachama wa CCM walimchagua Fredrick Mwakalebela, KK ya CCM, ikamuondoa na kumuweka mama Mbega. Je! CCM ni Role model wa vyama vingine? nauliza tu lakini.

sijui ile kesi ya kutoa rushwa wazi wazi iliyomkabili yeye na mkewe imeishia wapi ?
 
Back
Top Bottom