CHADEMA kujazana mahakamani ili kurekodi mwenendo wa kesi kwa lengo la kupotosha jamii na kutengeneza chuki dhidi ya mahakama siyo sawa

Kwa nchi za wenzetu hiyo kesi kwa masirahi ya umma ingekuwa inaonyeshwa live runingani Ila hapa kwetu tunatakiwa tuachane nayo tukafanye kazi,Kama bunge tu jaturuhusiwi sembuse kesi!
 
Sioni kama kulikuwa na uwongo wowote kwa wanaoripoti. Toka kesi ianze, wanapowasilisha vielelezo, watoaji wa taarifa huwa wanasema, "shahidi anasoma maelezo yaliyopo kwenye vielelezo". Ujue shahidi anaposoma maelezo anaenda haraka sana, tofauti na anapohojiwa ambapo maelezo anayoyatoa, anaenda taratibu ili jaji aweze kuandika. Maelezo ya kwenye vielelezo, jaji haandiki maana maelezo atayakuta kwenye vielelezo.
 
Mkuu sisi tunafatilia tu mwenendo wala siyo kazi yetu kuhukumu ILA tunalohoji ni kwa nini huyo msamalia mwena aliyejitolea kuacha kazi ya kutafuta riziki atumpe mwenendo nusu nusu?! Lengo lake ni nini? Kwa maoni yangu lengo ni kuyumbisha mtazamo wa jamii kuwa upande wa mashitaka hauna ushahidi dhidi ya Mbowe na wenzake
Tunashukuru wewe umetuletea jumbe hizo kwa ukamilifu wake.

Sasa tujadili kwa maslahi ya taifa letu kama wananchi huru,

Kwako wewe kuna mahali ktka jumbe hizo umeona neno hata moja linaloashiria kuwa walikuwa wakipanga ugaidi? Maana jumbe hizi ndiyo msingi mkuu wa ushahidi tulioambiwa na Siro kuwa upo ushahidi wa kutosha.

Kama hii Ndiyo msingi wa ushahidi basi, kuna shida ktk jeshi la polisi.
 
Wewe anzi yako utupe update za mahakamani ila yule anajitahidi simjui hanijui ila kongole kwake
 
Mkuu hivi uko CHADEMA ulinzi wa mtu mkubwa kama Mbowe si ungetangazwa wazi tu

sijakuelewa mkuu unaweza kurudia tena kama hutajali?
Mbona huwa hatuoni mkitangaza nafasi za kazi za usalama wa taifa wanaomlinda Rais?
Ushawahi kujua namna wanavyorecruit hao watu?
The same reason,Mbowe akitangaza nafasi za walinzi binafsi,TISS haishindwi kupenyeza watu wao nao wakaombe!
Kama ujuavyo Kwa nchi hii,vyombo vya Dola vipo kuihudumia na kuipambania CCM!
 
Mbona mwandishi anarukaru. Hii hapa iko mwananchi ila hapa hamna

Taarifa ya Uchunguzi:

Shahidi: 13/8/2020 Maabara ya uchunguzi wa Kisayansi ikipokea barua na vielelezo simu nane pamoja na simu card zake kwa ajili ya uchunguzi kubaini Mawasiliano kupitia mitandao ya kijamii Kama vule Whatsapp, Telegram, unumbe mfupi na kupiga nakupigiwa katika namba za simu zilizotangulia, usajili wa namba hizo na Mawasiliano mengine

Kisha shahidi anasoma matokeo ya uchunguzi wake.

Shahidi: Katika uchunguzi huo shahidi anabainisha jinsi namba za simu hizo ambazo amebainisha usajili wake kuwa ni za baadhi ya washtakiwa, hususan Mbowe pamoja na shahidi mtarajiwa wa Jamhuri, Luten Denis Urio, wakijadiliana kuhusu kuwapata vijana ambao wengine wametajwa miongoni mwa washtakiwa.

Shahidi: Ripoti ya uchunguzi huo inabainisha muda wa mawasiliano hayo kupitia mitandao ya kijamii, zote ujumbe mfupi wa maneno, kupiga na kupokea simu na miamala ya fedha huku mmoja akimtahadharisha mwingine kuwa asiwe anatumia namba yake binafsi kwa masuala ya pesa

Wakati Shahidi anaendelea kusoma taarifa hizo, Jaji anahoji kama kuna kusoma taarifa zote hizo na hasa viambatanisho. Anashauri isomwe ripoti ya uchunguzi na wakili Hilla anamuongoza kwenye maneo muhimu ya uchunguzi.

Shahidi anabainisha mawasiliano Kati ya Mbowe na Denis Urio kuanzia Januari 2020 jinsi walivyotafutana kwa njia ya ujumbe wa mitandao na ujumbe na call kupitia telegram na ujumbe wa maneno

Shahidi: 20/7/2020 saa 1:59 asubuhi kupitia telegram Mbowe anasema kaka wale mtu tatu au nne ni muhimu sana siku zimekwisha.

Shahidi: Baadaye alipiga simu kwa telegram

Shahidi: Saa 1:45 asubuhi Denis alimpigia Mbowe

Shahidi: Saa 1:47'46 Mbowe alimpigia Denis

Shahidi: 20/7/2020 saa 2;20 Denis amtumia Mbowe ujumbe, bro kuna memba wawili mmoja yuko Tunduma anashughulika na mabasi ya safari za nje na mwingine yuko Dodoma

Shahidi:Mboye baadaye simu siyo salama

Shahidi: Baadaye Mbowe atuma ujumbe hao wawili kuanzia siyombaya na hawawezi kutelekezwa wameshakwanbia mahitaki yao

Shahidi: Denis anamtumia Mbowe ujumbe mmoja kazaliwa 1980

Shahidi: Baadaye Denis ujumbe kwa Mbowe nitumie nauli ya kwenda nao Moro

Shahidi: Mbowe anajibu hakuna tatizo, kiasi gani

Shahidi: Denis anajibu laki 5

Shahidi: Saa 2:21:48, Mbowe anajibu sawa kaka

Shahidi: 2:22:29 Denis kwa Mbowe Nashukuru nitakujibu jioni

Shahidi: Denis usiwe unatumia namba yako binafsi kutuma pesa tumia wakala au mtu mwingine

Shahidi: Mbowe Ok

Shahidi: 27/7/2020. Denis yule jamaa anayefanya kazi Yard ameshafika

Shahidi: Yule mtu wa Tunduma anakaribia Moro

Shahidi: Denis Ila Kuna maswali wanauliza kuhusu malazi na mishahara yao.

Shahidi: Baadaye Denis ampigia Mbowe

Shahidi: 22/7/2020 : 6:26 Denis ampigia Mbowe

Shahidi: 2/7/2020 saa 6: Denis Shikamoo mkuu wale vijana tayari niko nao nimekutana nao na wako tayari kwa kazi

Shahidi: Denis naomba unipe utaratibu wao

Shahidi: Mbowe 7:38 Denis amtumia Mbowe kuwa wamekuja Dar anaomba nauli na mahali pa kukutana

Shahidi: 22/7/2020 saa7:51 Denis kwa nauli na chakula kwa wote ni Sh200.000

Shahidi: Mbowe natuma namba gani

Shahidi: Denis 0787555200

Shahidi: Mbowe ni namba ya nani?

Denis: Namba yangu

Shahidi: Denis uliyotumia juzi

Shahidi: Denis Lakini wewe usitumie namba yako

Shahidi: Mbowe: Ok

Shahidi: Mbowe wakiwa around Mlandizi watume sms wanafika muda gani nitatuma gari kuwapokea Ubungo

Shahidi: Denis: niwape namba gani muweze kuwasiliana?

Shahidi: Siku hiyo 3 Mbowe namba ninayotumia unumbe ni ya dereva wangu wamtafute yeye

Shahidi: Denis sawa, nitumie hiyo namba baadaye Denis

Shahidi: Tayari nimeipata

Shahidi: Denis: Nashukuru nimeelewa nitawapa hiyo namba.

Shahidi: Saa 12:20 jioni Denis: Tayari wameshaondoka wanakaribia Ruvu

Shahidi: Denis wale vijana wengine nimewapata Mwanza, Mtwara na Dodoma

Shahidi: Denis: Naomba kushauri uwe unanitumia fedha za kutosha kwa ajili ya ku-mobilize

Shahidi: Mbowe: kaka bado niko kamati kuu tuma ujumbe please.

Shahidi: Denis: Kuna MSG nilizokutumia kuhusu wale vijana wengine ambao wako tayari.

Shahidi: 13/7/2020 Denis: Naomba rejea msg zangu za jana usiku

Shahidi: 23/7/2020 saa 1:03 jioni Urio anapokea ujumbe wenye jina la Mohamed Abdillahi Ling'wenya

Shahidi: Urio: Mbona hujatuma majina na picha ya Adamoo ( Adamu Hassan Kasekwa, mshtakiwa wa pili?

Shahidi: Baadaye Urio apokea picha nyingine Kisha ujumbe usemao Adamu Hassan Kasekwa

Baada ya shahidi kumaliza kusoma ripoti hizo wakili Hilla anaomba ahirisho.

Jaji Tiganga anaahirisha kesi hiyo hadi saa 7:55 mchana huu ili upande wa mashtaka uendelee kumuongoza shahidi wake kutoa ushahidi wake.

Mahakama imerejea kwaajili Shahdi kuendelea kuhojiwa na wakili wwa serikali Piusi Hilla.

Shahidi: Baada ya kumaliza kufanya uchunguzi vielelezo hivi nilivifunga na kufihifadhi sikuviona tena hadi jana Ijumaa Januari 17.

Shahidi: Ijumaa iliyopita nilipigiwa simu na Inspekta Swilla kutakiwa kuja kutoa ushahidi kuhusiana na uchunguzi niliofanya.

Shahidi: Nilienda kuangalia kwenye register ya maabara ili kufahamu na Jumatatu tuliwasiliana aliniletea vielelezo.

Shahidi: Vielelezo hivyo ni simu nane na kwakuwa nilizifanyia kazi kwa kuangalia stika zilizokuwa kwenye simu zile…..

Shahidi: Hali ya vielelezo hivyo niliona jina langu na juu ya bahasha ilikuwa imeandikwa kwa makapeni.

Shahidi: Nilivihifadhi kwenye begi langu kwaajili ya usalama na kuja navyo mahakamani kwa ajili ya kuvitolea ushahidi.

Shahidi: Lakini jana kutokana na changamoto ya kiafya, nilirudi navyo na kwenda kuvihifadhi ofisini Kitengo cha uchunguzi wa kisayansi katika makao Makuu ya Polisi ya zamani na leo
Hii hawaiandiki wala hawapendi ijulikane hivyo

Wao wamekariri neno...moja tu Mchongo.

Ahsante@comte kwa kunyoosha mistari.

Kwenye ili Updates yao wamekiruka hiki kipengele chote kinachomhusu Mbowe !
 
Mleta mada sikui umewaza ninini hadi kuweka hili bandiko!
Watu kwenda mahakamani kusikiliza kesi ya mpendwa wao itatengenezaje chuki dhidi ya mahakama?
Nilitamani kuona andiko lako kuelezea lakini siaona!
 
Mbona mwandishi anarukaru. Hii hapa iko mwananchi ila hapa hamna

Taarifa ya Uchunguzi:
Bado katika haya maelezo yote sijaona kiashiria chochote kile cha ugaidi! Zaidi tu ya mawasiliano baina ya watu wawili katika kusafirisha watu kutoka eneo moja kwenda lingine.

Hakuna sehemu imetolewa sababu ya kuwasafirisha! Zaidi tu ya mvutano! Watuhumiwa na upande wa utetezi kwa ujumla wakisema walisafirishwa kwa ajili ya VIP proyection, huku upande wa serikali/mashtaka wakilazimisha ni kwa sababu za kigaidi.

By the way, kama hii kesi haina harufu ya mchongo kwa namna yoyote ile, mbona huyo Dennis Urio haonekani mahakamani? Au zamu yake ya kutoa ushahidi kwa upande wa mashtaka bado haijafika?
 
JUMBE fupi za maneno (meseji), zinazodaiwa kuwa za Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na baadhi ya washtakiwa wenzake, katika kesi ya ugaidi inayowakabili, zimesomwa kwenye Mahakama Kuu, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Haihitaji uwe wakili msomi kugundua hii kesi siyo ya ugaidi wala uhujumu uchumi. Hii ni kesi ya kupotezeana tu muda kupitia vyombo vya dola.

Maelezo yote yamejaa stori za kawaida, tena za watu waliosafirishwa kwenda sehemu nyingine kwa ajili ya kumlinda mtu aliye mtumia mtu wa kati kuwatafuta.

Ni aibu kwa serikali kupoteza hela za walipa kodi kwa mambo ya kipuuzi kama haya.
 
Bado katika haya maelezo yote sijaona kiashiria chochote kile cha ugaidi! Zaidi tu ya mawasiliano baina ya watu wawili katika kusafirisha watu kutoka eneo moja kwenda lingine.

Hakuna sehemu imetolewa sababu ya kuwasafirisha! Zaidi tu ya mvutano! Watuhumiwa na upande wa utetezi kwa ujumla wakisema walisafirishwa kwa ajili ya VIP proyection, huku upande wa serikali/mashtaka wakilazimisha ni kwa sababu za kigaidi.

By the way, kama hii kesi haina harufu ya mchongo kwa namna yoyote ile, mbona huyo Dennis Urio haonekani mahakamani? Au zamu yake ya kutoa ushahidi kwa upande wa mashtaka bado haijafika?
Mkuu sijui mengine mnayatoa wapi- hoja yangu siyo tujadili kuhusu nani mkweli na ni nani muungo. Hoja yangu ni kwa nini mleta update alete taarifa nusunusu- anaficha nini? Ni kitu gani hataki tukijue? na KWA NINI?
 
Hii hawaiandiki wala hawapendi ijulikane hivyo

Wao wamekariri neno...moja tu Mchongo.

Ahsante@comte kwa kunyoosha mistari.

Kwenye ili Updates yao wamekiruka hiki kipengele chote kinachomhusu Mbowe !
Mkuu wakumbuke wapenda ukweli bado tupo humu-siyo CHADEMA siyo CCM ila wapenda UKWELI
 
Mkuu sijui mengine mnayatoa wapi- hoja yangu siyo tujadili kuhusu nani mkweli na ni nani muungo. Hoja yangu ni kwa nini mleta update alete taarifa nusunusu- anaficha nini? Ni kitu gani hataki tukijue? na KWA NINI?
Basi jibu ni hili hapa; Analeta nusunusu hizo taarifa kwa sababu ya utashi wake tu. Maana amejitolea, na hatumlipi. Hata akiamua kutoleta kabisa, bado hatuna cha kumfanya. Sisi wengine tunamshukuru hata kwa hicho kidogo anacho tuletea humu jukwaani.
 
Mbona huwa hatuoni mkitangaza nafasi za kazi za usalama wa taifa wanaomlinda Rais?
Ushawahi kujua namna wanavyorecruit hao watu?
The same reason,Mbowe akitangaza nafasi za walinzi binafsi,TISS haishindwi kupenyeza watu wao nao wakaombe!
Kama ujuavyo Kwa nchi hii,vyombo vya Dola vipo kuihudumia na kuipambania CCM!
Sikujua- na yaho ndiyo madhara ya kutaka kuishi Kidola wakati huna dola
 
Tunashukuru wewe umetuletea jumbe hizo kwa ukamilifu wake.

Sasa tujadili kwa maslahi ya taifa letu kama wananchi huru,

Kwako wewe kuna mahali ktka jumbe hizo umeona neno hata moja linaloashiria kuwa walikuwa wakipanga ugaidi? Maana jumbe hizi ndiyo msingi mkuu wa ushahidi tulioambiwa na Siro kuwa upo ushahidi wa kutosha.

Kama hii Ndiyo msingi wa ushahidi basi, kuna shida ktk jeshi la polisi.
Mimi siyo mahakama wala hakimu- wewe baki na hukumu yako ila ikitolewa yenyewe na wenyewe usilie
 
Basi jibu ni hili hapa; Analeta nusunusu hizo taarifa kwa sababu ya utashi wake tu. Maana amejitolea, na hatumlipi. Hata akiamua kutoleta kabisa, bado hatuna cha kumfanya. Sisi wengine tunamshukuru hata kwa hicho kidogo anacho tuletea humu jukwaani.
Na unaona ni sawa?
 
Basi jibu ni hili hapa; Analeta nusunusu hizo taarifa kwa sababu ya utashi wake tu. Maana amejitolea, na hatumlipi. Hata akiamua kutoleta kabisa, bado hatuna cha kumfanya. Sisi wengine tunamshukuru hata kwa hicho kidogo anacho tuletea humu jukwaani.
Na unaona ni sawa?
 
Sikujua- na yaho ndiyo madhara ya kutaka kuishi Kidola wakati huna dola
Hayo mambo yapo!Mbona kina mond,harmonize Wana walinzi kibao tu!!
Issue ni kuwa Mbowe ni mwanasiasa Tena mpinzani!Kuwa mpinzani imara nchi hii ni risky sana!
 
Mleta mada sikui umewaza ninini hadi kuweka hili bandiko!
Watu kwenda mahakamani kusikiliza kesi ya mpendwa wao itatengenezaje chuki dhidi ya mahakama?
Nilitamani kuona andiko lako kuelezea lakini siaona!
Mkuu kwa uelewa wako hutakaa uelewe.
 
Back
Top Bottom