CHADEMA kinapotea rasmi chini ya Katibu Mkuu "mchina"

Dopas

JF-Expert Member
Aug 14, 2010
1,151
392
Ni maoni yangu tu wanaJF,

Kama ambavyo BAVICHA ilififia na kuzikwa alipotoka tu John Heche kama mwenye kiti wake, na kuchaguliwa chaguo la mwenyekiti, Protas.

Sasa tunashuhudia tena taratibu chama kikuu cha upinzani kikielekea shimoni baada ya chaguo la mwenye chama na mamvi kwa maslahi wayajuayo wao kuteuliwa katibu mkuu, aka "katibu mkuu mchina".

Inasikitisha sana chama tulichokipenda sana kikifa kwa uzembe au kwa maslahi binafsi.

CHADEMA kilikuwa chama hadi Julai mwaka jana, kabla hakijageuzwa kuwa taasisi ya kibiashara.

Lakini hata naibu katibu mkuu Salum Mwalimu alijitahidi sana kukiongoza chama katika kipindi kigumu cha mpito kuelekea uchaguzi mkuu hadi alipotolewa kwa mizengwe wanayojua Mbowe na Lowassa na kuja na chaguo lao ambalo hata hakuna anayejua walikomtoa.

Binafsi nilitegemea huyu kijana shujaa Salum Mwalimu angeteuliwa katibu mkuu.

Haidhuru, lakini tangu uteuzi wa katibu mkuu wao hadi leo tunashuhudia kifo kikikinyemelea CHADEMA.

RIP CHADEMA.

Tutamkumbuka sana Dr. Slaa na Salum mwalimu. Mungu awalinde.
 
Kwi kwi kwi kwi mtoa mada amesahau kwamba baada ya uchaguzi wa mwaka Jana CHADEMA sasa ina madiwani wengi, wabunge wengi na mameya wengi kupita miaka yote iliyopita kwi kwi kwi kwi kwi kwi chama ndiyo kinazidi kuwa na nguvu zaidi kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi
 
Lumumba mna tabu mmesahau Dar inaongozwa na Ukawa sasa huyo Makonda asipoangalia utendaji wake utakua mgumu maana Ukawa tunatekeleza ilani yetu sasa
 
Kwi kwi kwi kwi mtoa mada amesahau kwamba baada ya uchaguzi wa mwaka Jana chadema sasa ina madiwani wengi, wabunge wengi na mameya wengi kupita miaka yote iliyopita kwi kwi kwi kwi kwi kwi chama ndiyo kinazidi kuwa na nguvu zaidi kwi kwi kwi kwi kwi kwi kwi
Ni kweli hayo unayoyasema. Lakini hayo yamepatikana baada ya msingi alioweka Dr. Slaa kama katibu mkuu, na msingi ule aliendeleza naibu katibu Mkuu Salum Mwalimu. Niambie tangu uteuzi wa katibu mkuu wa saa kipi kinaonesha mwelekeo wa matumaini mapya? Hayo yote unayoongelea muda si mrefu kwa hali jinsi ilivyoanza kuonekana, yatabaki hadithi. Labda wabunge maarufu kina Lisu wafanye juhudi binafsi ya kujibakiza mjengoni. Lakini wale goigoi wote wanaotegemea nguvu ya chama iwe wabunge au madiwani wasahau kabisa.
 
Lumumba mna tabu mmesahau Dar inaongozwa na Ukawa sasa huyo Makonda asipoangalia utendaji wake utakua mgumu maana Ukawa tunatekeleza ilani yetu sasa
Muda utakuja kukuambia, kama ni suala la buku 7 au ni ukweli. Ukweli lazima utaonekana hata kama utachelewa kuonekana kwaajili ya mizengwe. Subiri mkuu. Binafsi siipendi hata kidogo CCM na madudu yake. Lakini mbaya zaidi CHADEMA ambayo kilikuwa matumaini, kimeuzwa. Maumivu makubwa.
 
Ni kweli hayo unayoyasema. Lakini hayo yamepatikana baada ya msingi alioweka Dr. Slaa kama katibu mkuu, na msingi ule aliendeleza naibu katibu Mkuu Salum Mwalimu. Niambie tangu uteuzi wa katibu mkuu wa saa kipi kinaonesha mwelekeo wa matumaini mapya? Hayo yote unayoongelea muda si mrefu kwa hali jinsi ilivyoanza kuonekana, yatabaki hadithi. Labda wabunge maarufu kina Lisu wafanye juhudi binafsi ya kujibakiza mjengoni. Lakini wale goigoi wote wanaotegemea nguvu ya chama iwe wabunge au madiwani wasahau kabisa.
Ngoja nikanywe bia kwi kwi kwi kwi kwivkwi
 
Nadhani makatibu wa vyama vyote wapo kimya sana, Mzee Kinana ndiyo simsikii kabisa, Mwigamba nae kimya, ADC, UDP, PPT et al sijui kama vina makatibu wakuu. Maalim Seif peke yake ndiyo katibu anaesikika.

Hata hivyo kutosikika siyo kigezo cha ufanisi.
 
Unajua kazi za katibu mkuu sio kupiga domo ni utendaji huyo msaliti Slaa alienunuliwa kwa vipande 30 tushamsahau siku nyingi
 
Unajua kazi za katibu mkuu sio kupiga domo ni utendaji huyo msaliti slaa alienunuliwa kwa vipande 30 tushamsahau siku nyingi
Kama Dr. Slaa na Salum Mwalimu kwa kipindi tajwa walikijenga chama kwa kupiga domo, basi nayo ni sawa. La msingi ni kuelewa kuwa mfa maji haachi kutapata. Naona sasa maji yawafikia shingoni. Ukimya wa katibu mkuu mpya kama ndo style ya kujenga chama au kama ndiyo kupwaya kwenyewe time will tell.
Dr. Slaa hataweza kusahauliwa na wapenda CHADEMA, isipokuwa hao waliokifanya chama kama taasisi ya biashara.
 
Ni maoni yangu tu wanaJF,

Kama ambavyo BAVICHA ilififia na kuzikwa alipotoka tu John Heche kama mwenye kiti wake, na kuchaguliwa chaguo la mwenyekiti, Protas.

Sasa tunashuhudia tena taratibu chama kikuu cha upinzani kikielekea shimoni baada ya chaguo la mwenye chama na mamvi kwa maslahi wayajuayo wao kuteuliwa katibu mkuu, aka "katibu mkuu mchina".

Inasikitisha sana chama tulichokipenda sana kikifa kwa uzembe au kwa maslahi binafsi.

CHADEMA kilikuwa chama hadi Julai mwaka jana, kabla hakijageuzwa kuwa taasisi ya kibiashara.

Lakini hata naibu katibu mkuu Salum Mwalimu alijitahidi sana kukiongoza chama katika kipindi kigumu cha mpito kuelekea uchaguzi mkuu hadi alipotolewa kwa mizengwe wanayojua Mbowe na Lowassa na kuja na chaguo lao ambalo hata hakuna anayejua walikomtoa.

Binafsi nilitegemea huyu kijana shujaa Salum Mwalimu angeteuliwa katibu mkuu.

Haidhuru, lakini tangu uteuzi wa katibu mkuu wao hadi leo tunashuhudia kifo kikikinyemelea CHADEMA.

RIP CHADEMA.

Tutamkumbuka sana Dr. Slaa na Salum mwalimu. Mungu awalinde.


Mtoa mada mlitaka CHADEMA wafanyeje ndio mjue kiko strong (waandamane, wacheze disco, waingie msituni au walie????!!! )

Waambie Lumumba ndio wenye serikali mliopora wawatumikie wananchi msitafute mchawi . UKWELI MCHUNGU SANA ni kuwa mafanikio kidogo waliopata CHADEMA umewatia kiwewe nyumba ya kijani.
 
Peroject ya buku 7 Lumumba kitakuwa ni historia mara tu Magufuli atakapochaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama.. Muanze kutafuta ajira sehemu nyingine..
 
Nadhani makatibu wa vyama vyote wapo kimya sana, Mzee Kinana ndiyo simsikii kabisa, Mwigamba nae kimya, ADC, UDP, PPT et al sijui kama vina makatibu wakuu. Maalim Seif peke yake ndiyo katibu anaesikika.

Hata hivyo kutosikika siyo kigezo cha ufanisi.
Maalim ni mwenye chama
 
Kazi ya dr mashinji, nikumlindia mbowe uwenyekiti, asije kutokea mtu anaitaka hiyo nafasi akapita kwa haki, huku boss wake akijigawia ruzuku
 
Unajua kazi za katibu mkuu sio kupiga domo ni utendaji huyo msaliti slaa alienunuliwa kwa vipande 30 tushamsahau siku nyingi
We shika adabu yako.....ole wako nikusikie unamuita slaa msaliti....jinga sana wewe.
 
Back
Top Bottom