CHADEMA kina wanachama wangapi?

 
Kutokana na mfumo wa RUSHWA, wanachama wa CCM huwa wanaongezeka kipindi cha uchaguzi wa ndani, kumpata mgombea ubunge na udiwani,

Kadi huwa zinagawiwa, sio tu bure na hela juu, unapewa kadi na msimbazi wawili au mmoja kulingana na ulivyo ili umpigie kura kwenye kura za maoni

niliwahi kuwa katibu wa UVCCM tawi, na hili ni tatizo lililo nifanya nitoke CCM, baada ya kutokubaliana na huo mfumo
 
CHADEMA kinaonekana kuwa chama kisichojali sana kuwa na wanachama wengi bali wafia chama. Niliongea na mtu wangu pale CDM ili tufungue tawi nikaomba anisaidie kupata kadi kama hamsini hivi mana nilishaoganise wapenzi tufungue tawi. jamaa aliniambia jambo la maana sana alisema falsaa ya chama ni kuwa na wanachama wafia chama na si kuuza mikadi ama kuwa na wanachama kwa kusikiliza hotuba mkutano mmoja. CHADEMA inatamani zaidi kuwa na wafia chama. Sasa unaweza jijibu mwenyewe CCM , ACT na CHADEMA nani mwenye wafia chama wengi? Je humu jf ,face book nani ana wafia chama wengi ? wale wasiotaka chama chao kiguswe hata na jambo la kweli wapo kupigania tu hao ndio washindi na ni vigumu kuwajenga
 
 
Kwa Takwim Zilizofanywa Na Chadema Ni Msingi, Na Data Zilizopo Kwa Katibu Mkuu Taifa, Chadema Imeweka Lekodi Afrika Kwa Kuwa Na Wanachama Wengi Kikiongoza Tanzania Kwa Kuwa Na Wanachama Zaidi Ya Milion 10, Huku Ccm Kikishuka Kutoka Wanachama Milioni Tano Mpaka Milion Tatu Na Upuzi, Hii Ni Kutokana Na Chadema Kusimika Viongozi Toka Ngazi Ya Ubalozi Mpaka Taifa, Na Watu Walijitokeza Kugombea Ubunge Mwaka Huu, Zaidi Ya Elfu Nne NChi Nzima,
 
Hivi kwa nchi yetu kuwa mwanachama wa chama cha siasa ni lazima kuwa na kadi? Je kuichangia chama bila kuwa na kadi ni kosa? Kwa ufahamisho tu...Marekani ina wapiga kura zaidi ya milioni mia moja (>100,000,000) lakini idadi ya wenye kadi za chama hawazidi milioni tatu (<3,000,000) sawa na asilimia tatu (<3%). Kadi inatakiwa pale tu unapotaka kugombea uongozi ama ndani ya chama au kwenye chaguzi mbali mbali za uongozi serikalini. Kwa mfano wengi wanaoitwa "Democrats" asilimia zaidi ya tisini (>90%) si wanachama kwa maana ya kuwa na kadi, ni washabiki tu. Umuhimu wa kuwa na kadi ya chama hapa Tanzania ulikuwa ni wakati wa mfumo wa chama kimoja ambapo kadi ilikuwa ni kama paspoti ya kupata huduma za kijamii.
 

Embu washauri ACT labda watakuelewa
 
Habari.
Si vibaya kujua haya ni wajibu wa kila Mwanachama wa Chama cha Siasa kujua idadi kamili ya wanachama nchi Nzima.

Je Chadema Ukawa kwa ujumla ina wanachama wangapi hadi hivi sasa?
 
Matokeo ya kula za maoni ndan ya CHADEMA ambayo yanaendelea kutolewa yanahashilia kuwa chama bado kinahitaji kuongeza nguvu ya kusajili wanachama wapya .

Mtu anashinda kwa kula 88 na kula zilizopgwa ni zaid ya kula mia moja ukizngatia jimbo lina wapiga kula zaid ya 50000.

2010 vita ya CCM ndani kwa ndani ilichangia sana CHADEMA ikazoa Wabunge katika maeneo ya mijini kama Dar na Iringa.

Kuna umuhimu wa chama kuzidi kusajili watu ili kuwa na safari ya uhakika.
 

Attachments

  • 1437449099608.jpg
    31.7 KB · Views: 913
  • 1437449147792.jpg
    34.1 KB · Views: 781
  • 1437449176267.jpg
    37.8 KB · Views: 777
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…