CHADEMA itashinda kwa kishindo Arumeru - Dr Slaa

CHADEMA itashinda kwa kishindo Arumeru - Dr Slaa

Umesoma shule gani wewe?
Ulipata division ngapi o-level?
Vmimi napata wakati mgumu unapomuuliza mwenzako" kiingeleza alifaulu" badala ya kusema kiingereza, sasa na wewe kiswahili ulifaulu?
 
Niseme hivi, kama kuna mti kakwamba kumalizia ka-kibanda kake pengine mabati yamepungua au hela ya koleo imekuwa tabu basi apige kambi Arumeru Mashariki mapema! Zitamwagwa hela za kufa mtu pale.

Na ningependa sana kuamini Dr Slaa anajua sakarasi zinatakavyochezwa. Kama 2010 Sumari alishinda bila ya kufanya campaign yeye binafsi leo hii mwanae itakuwaje? Hii ngoma bana itakuwa ngumu sana na ukiingiza vile vita vya kimeru ndio kabisa.

Umefilisika mawazo ndugu!
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amewahakikishia wapenzi na wanachama wa CHADEMA kwamba chama hicho kitashinda kwa kishindo katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Arumeru Mashariki utakaofanyika hivi karibuni.Dr Slaa amesema chama chake kina nguvu kubwa jimboni humo na katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010 chama chake kilifungua matawi 69 yaliyo hai mpaka leo katika kila kona ya jimbo hilo.
Dr Slaa amesema CHADEMA ilijifunza mengi katika jimbo la Igunga na kutahadharisha vitendo vya ugawaji rushwa kurubuni wapiga kura kamwe havitavumiliwa Arumeru.Pia alisema chama chake kimejipanga kutoa elimu kubwa ya uraia kwa wananchi wa Arumeru mashariki kupitia kampeni mara zitakapozinduliwa.Dr Slaa ameahidi kampeni safi na za kistaarabu.

SOURCE:MTANZANIA

Alisema maneno hayo hayo uzini.
Lakin matokeo ndio jibu la yote.

 
Hata Uzini Slaa alisema CDM itashinda kwa kishindo!!!
Labda nako CCM walichakachua matokeo!!

Mkuu haya ya Uzini Dr. Slaa hajayasema, ni wewe tu ndiyo unataka kuudanganya uma wa kitaanzania, mimi nilikuwa pale kwenye uzinduzi, hali halisi tuliiona, na kibaya zaidi C** wakaanza propaganda ya Udini, kwa kweli inatia hasira sana.
wapiga kura wakatishwa kuwa sasa Ukristo ndiyo unatia nanga Bambi - Uzini, kweli C** hawakututendea haki na siku ya siku Raza akapewa ushindi ambao ulijengwa kwa misingi ya udini.

Siku yaja hapo ndugu zetu Zanzibari watakapojitambua. ni jambo la
 
Kauli za. Mtu Kama dr Slaa siyo mpya hapa Tanzania bado hatujasahau elimu bure, saruji 5000 na mabati 5000. Tangu Bunge likutane hakuna mbunge wa Chadema aliewahi kuleta hoja ya namna ya kufikia malengo hayo ya Chadema. Inaonekana ulikuwa uongo wa Slaa kuwahadaa watanzania wamuchague, na kuliwa. Sasa ameanza tena Arumeru ni la chadema . Mwaka jana alishindwa naSumari bila campaign. Kamanda wake feki alianza campain kwenye msiba utadhani alizikwa mnyama pale! Wameru walioshuhudia unyama ule pale akheri wachague ili wapate nini zaidi ya mandamano?

Nadhani katika watu wanaotumia makalio kurikiri wewe ni mmoja wao! Wabunge wa CHADEMA watapelekaje hoja bungeni ya kutekeleza ilani yao wakati hawapo madarakani?
 
Pale CCM wakamweke Mzee Kingunge labda watashinda..Zaidi ya hapo kulaladek..Natamani kazi ianze kesho
 
Alisema maneno hayo hayo uzini.
Lakin matokeo ndio jibu la yote.


Cha msingi wananchi wa Arumeru watambue utu wao na waepuke fitna zote za udini kama tulivyoshuhudia kule Uzini na Igunga
 
Back
Top Bottom