CHADEMA itabaki kuwa CHADEMA tu

CHADEMA itabaki kuwa CHADEMA tu

Tindo, umelirudia hili mara kwa mara, kiasi kwamba inanibidi niheshimu fikra na pengine hata kuanza kushawishika jambo husika lifikiriwe na kujadiriwa ndani ya chama na Mbowe mwenyewe asilionee kinyongo. Ninapata taabu sana kuitetea hoja yako, lakini haina maana kwamba sioni mantki ndani yake.

Na wazo hili linatokana na uamini kwamba CHADEMA ni chama cha watu wengi wenye msimamo wa pamoja kuhusu chama chao.

Watu hawa ndio wenye uwezo wa kuamua, kama Mbowe aendelee kuongoza chama chao, au awekwe kiongozi mwingine.

Hii haitakuwa na maana kwamba Mbowe ameshindwa kuongoza, (bali litakuwa ni hitaji la kuleta mawazo mapya ndani ya chama)? Hili ni swali.

Je, uwepo wa Mbowe unazuia mawazo mapya? Hao wenye mawazo mapya yenye manufaa makubwa lakini wakashindwa kuyawasilisha ndani ya chama kwa vile sio viongozi wakuu wa chama, ni mawazo ya namna gani hayo; na hawa viongozi wana commitment kiasi gani ndani ya chama chao?

Wanachama wa CHADEMA wanawafahamu vizuri viongozi wao kuliko sisi tulio nje ya chama.
Kwa kuunga mkono msimamo wako; je kukiitishwa uchaguzi wawachague viongozi na wakataka Mbowe aendelee kuwa kiongozi wao bado utaona wamekosea? Kwa bahati nzuri msimamo wako juu ya swali hilo pia unajulikana!

Tatizo juu ya hili kufanyika sasa pia linajulikana. Sio wakati sahihi kufanya hivyo; na watasambaratishwa wasijue ni nini kimewatokea. Wewe hili huliamini kuwa linawezekana kutokea!

Kutaka Mbowe ajitoe katika uongozi, hasa wakati huu, wazo hilo sio la kuitakia mema CHADEMA na nchi kwa ujumla.

CHADEMA kama wanata mabadiliko, wakati sahihi wa kufanya mabadiliko hayo sio sasa, itabidi wasubiri baada ya 2020.

Mkuu nashukuru sana kwa kunitendea haki. Ukijaribu kuangalia michango yangu kwa cdm haina shaka kwamba naikubali cdm na pia naitaka mema cdm kama chama. Hata msimamo wangu kuhusu Lowassa uko wazi na wala sikuyumba mpaka majuzi anaondoka cdm.

Tuje kwenye hili la Mbowe, ukweli ni kuwa Mbowe ni jabali hasa na mhimili halisi wa cdm, lakini hili suala la kwamba sio muda muafaka Mbowe kuachia madaraka silipendi sana kwani hata wakati wa JK ilisemwa hivyo hivyo. Wasiwasi wangu Mbowe anaweza kuendelea kuwa mwenyekiti kwa sababu hizi hizi za kwamba muda sio sahihi. Hivi ni kweli ndani ya cdm taasisi ni Mbowe tu ndio jasiri na wengine wote ni wadhaifu? Angalia post yangu namba 31 hasa post paragraph ya pili utapata ni kipi nasimamia.

Huenda Mbowe anaweza akachaguliwa tena na wanachama hilo sina shida nalo kwani ndio demokrasia, lakini wangalau akijadiliwa kutapatikana mabadiliko ya dhati. Kwa mfano huyo katibu mkuu kuna haja ya kuendelea kuwa na mtu wa hivyo wakati huu? Huoni kama tungekuwa na katibu mkuu imara Mbowe naye angezidi kuwa imara. Tuje kwenye mfano halisi mfano masahibu yaliyompata Lisu yangempata Mbowe na hata kufa Cdm ndio ingekufa? Tujue cdm ndio maisha yetu na ndio silaha yetu, iwapo leo tutashindwa hata kuhoji nafasi ya mwenyekiti wetu tutapata wapi nguvu ya kuhoji nguvu ya rais? Nashukuru sana Kalamu1 umejitosa kwenye hili, tusione aibu kuhoji uwajibikaji wa yoyote.
 
Hapana.
Inawezekana sana kuwemo viongozi imara sana ndani ya CHADEMA kama alivyo imara Mbowe, ila hawatambuliki kwa vile hawajajitokeza ili wapimwe uwezo wao na wanachama wenzao.
Ni kiasi tu, wakati mwafaka ukitimia, Mbowe na viongozi wenzake waweke utaratibu ili wanaotaka kujitokeza wapimwe wapewe fursa hiyo. Wakati wa kufanya hivyo si sasa.
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
 
Kama kumbukumbu yangu hainiangushi, nakuomba urejee wakati ule wa kampeni iliyokuwa inapangwa ya "UKUTA." Angalia watu waliokuwa wanapigia kelele nyingi sana UKUTA ifanyike bila kujali dalili za matokeo yake.
Sijui wakati huu tungekuwa tunasemaje!
Fafanua zaidi.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
Vuta pumzi, nadhani sasa unapost tu bila ya kuwaza unachopost!
Maneno haya niliyo'quote' hukuyapa fikra ya kutosha.
 
Vuta pumzi, nadhani sasa unapost tu bila ya kuwaza unachopost!
Maneno haya niliyo'quote' hukuyapa fikra ya kutosha.
Nimeyaelewa ndiyo maana nikajibu hivyo, gari inapoharibika huwezi kukimbilia kubadili injini.
 
Wakati ni ukuta kwa wote sio kwa Mbowe tu.

Kama wewe ni mfuatiliaji wa siasa za Chadema nafikiri viongozi wenye uwezo wa kuongoza Chadema unawajua kama huwajui itakuwa tunajadili bure, tupe angalau majina mawili yenye uwezo wa kuwa Mkiti Chadema, inawezekana tunasema wabadili for the sake ya kubadilisha kumbe hata wa kubadilisha hayupo.

Binafsi siwezi kudai UDP wamtoe Cheyo uenyekiti wakati sijui kama kuna mtu wa kumpokea Cheyo, ni wao ndio wanaojua uwezo wake.

Quinine katika watu ninaowaheshimu hapa jukwaani ww ni mmojawapo. Hii post yako inaisifu cdm kama taasisi imara, sasa taasisi imara isiyoweza kupata mwenyekiti zaidi ya Mbowe, tena humo ndani kuna wasomi kibao hapo unamaanisha nini boss?. Hivi Mbowe akifa hii leo ndio cdm haitakaa iwe na mwenyekiti!? Hapo cdm ikiitwa ni genge utakataa?
 
Tuje kwenye hili la Mbowe, ukweli ni kuwa Mbowe ni jabali hasa na mhimili halisi wa cdm, lakini hili suala la kwamba sio muda muafaka Mbowe kuachia madaraka silipendi sana kwani hata wakati wa JK ilisemwa hivyo hivyo
Sikujua kuwa kuna aliyesema muda haukuwa mwafaka kwa JK kuachia madaraka! Nilikuwa nimechoka sana na kusubiri aondoke.

Siyo sahihi kulinganisha kutoka kwa JK na Mbowe kwa aina zote unazoweza kuzilinganisha.

Mimi ninakubaliana na wewe juu ya Mbowe na viongozi wenzake ndani ya chama, wakati utakaporuhusu; yaani baada ya uchaguzi mkuu wa 2020; CHADEMA waitishe uchaguzi wawapate viongozi wao.

Hili hawawezi wakalifanya wakati huu bila ya kuhatarisha usalama wa chama chao. CCM wana nyenzo zote wanazohitaji kuwavuruga na wasiweze hata kushiriki uchaguzi mwaka huu na mwakani.

Itashangaza sana kwa kiongozi yeyote kutoka CHADEMA kupigia kelele uchaguzi ndani ya chama wakati huu.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.

Quinine naona ni bora upumzike hii mada imekuwa nzito kwako, post ya mwenyekiti wa cdm ni post sensitive kuliko post ya urais!? Kama mtu alikuja akiwa na wiki 2 alipewa post ya kugombea urais itakuwa hiyo ya uenyekiti wa cdm? Kuna post sensitive nchi hii kuliko ya urais. Sikuwahi kujua kama ww ni mwepesi kiasi hiki, na ndio maana unaamini kwamba Mbowe tu ndio anaweza kuwa mwenyekiti cdm. Kama ni Mbowe tu ndio anaweza kuwa mwenyekiti ndani ya cdm basi hapo hamna chama boss.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
"Post ya Mkti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere"?

Nimeyaelewa ndiyo maana nikajibu hivyo, gari inapoharibika huwezi kukimbilia kubadili injini.

Viongozi na wanachama waliomo CHADEMA ni "watu wowote from nowhere?"

Basi sawa!
 
Quinine katika watu ninaowaheshimu hapa jukwaani ww ni mmojawapo. Hii post yako inaisifu cdm kama taasisi imara, sasa taasisi imara isiyoweza kupata mwenyekiti zaidi ya Mbowe, tena humo ndani kuna wasomi kibao hapo unamaanisha nini boss?. Hivi Mbowe akifa hii leo ndio cdm haitakaa iwe na mwenyekiti!? Hapo cdm ikiitwa ni genge utakataa?
Mkuu ndiyo maana nikasema tujaribu kuwa specific tuanze kujadili nani anaweza kuvaa viatu vya Mbowe siyo dhambi kuwajua kwa majina, mbona wenye uwezo wa kuwa makatibu wakuu makatibu wenezi wanaoweza wanatajwa kuwa Marcos Albanie, Heche, Msigwa, Malisa kwanini post ya Mkiti hatutaji?
 
Sikujua kuwa kuna aliyesema muda haukuwa mwafaka kwa JK kuachia madaraka! Nilikuwa nimechoka sana na kusubiri aondoke.

Siyo sahihi kulinganisha kutoka kwa JK na Mbowe kwa aina zote unazoweza kuzilinganisha.

Mimi ninakubaliana na wewe juu ya Mbowe na viongozi wenzake ndani ya chama, wakati utakaporuhusu; yaani baada ya uchaguzi mkuu wa 2020; CHADEMA waitishe uchaguzi wawapate viongozi wao.

Hili hawawezi wakalifanya wakati huu bila ya kuhatarisha usalama wa chama chao. CCM wana nyenzo zote wanazohitaji kuwavuruga na wasiweze hata kushiriki uchaguzi mwaka huu na mwakani.

Itashangaza sana kwa kiongozi yeyote kutoka CHADEMA kupigia kelele uchaguzi ndani ya chama wakati huu.

Kalamu1 usiwe mwepesi, ccm kama ni kuivuruga cdm imeshaivuruga na wala hawamuogopi Mbowe. Kama Mbowe kakaa ndani miezi minne itakuwa kuogopa huo uenyekiti wake? Cdm si inaporwa ushindi wake kwenye chaguzi kimachomacho na Mbowe akiwa mwenyekiti amefanyaje? Mali ngapi za Mbowe zimevurugwa na hana lolote alilofanya? Ukiniambia viongozi wa cdm hakuna anayetaka kugombea uwenyekiti nitakuelewa lakini sio kwamba Mbowe ndio mwenye uwezo kulingana na wakati wa sasa. Kama cdm ni taasisi basi utetezi wa kwamba Mbowe ndio anayefaa tu kwenye uenyekiti ni utani wa mchana kweupe.
 
Quinine naona ni bora upumzike hii mada imekuwa nzito kwako, post ya mwenyekiti wa cdm ni post sensitive kuliko post ya urais!? Kama mtu alikuja akiwa na wiki 2 alipewa post ya kugombea urais itakuwa hiyo ya uenyekiti wa cdm? Kuna post sensitive nchi hii kuliko ya urais. Sikuwahi kujua kama ww ni mwepesi kiasi hiki, na ndio maana unaamini kwamba Mbowe tu ndio anaweza kuwa mwenyekiti cdm. Kama ni Mbowe tu ndio anaweza kuwa mwenyekiti ndani ya cdm basi hapo hamna chama boss.
Niliyeanzisha mada ni mimi naijua uzito wake inawezekana wewe hujui hata lengo lake, hii mada ni pana nyie mmedandia sehemu ndogo sana ya mada husika 'uenyekiti wa Mbowe' na mimi naenda na nyie, akitokea mwingine tutajadili mafanikio ya Chadema nk, usichanganye mada kusema sensitive nalinganisha na posts ndani ya chama siyo nje ya chama, kwenye chama Mkiti ndiye kichwa cha chama.
 
Sikujua kuwa kuna aliyesema muda haukuwa mwafaka kwa JK kuachia madaraka! Nilikuwa nimechoka sana na kusubiri aondoke.

Siyo sahihi kulinganisha kutoka kwa JK na Mbowe kwa aina zote unazoweza kuzilinganisha.

Mimi ninakubaliana na wewe juu ya Mbowe na viongozi wenzake ndani ya chama, wakati utakaporuhusu; yaani baada ya uchaguzi mkuu wa 2020; CHADEMA waitishe uchaguzi wawapate viongozi wao.

Hili hawawezi wakalifanya wakati huu bila ya kuhatarisha usalama wa chama chao. CCM wana nyenzo zote wanazohitaji kuwavuruga na wasiweze hata kushiriki uchaguzi mwaka huu na mwakani.

Itashangaza sana kwa kiongozi yeyote kutoka CHADEMA kupigia kelele uchaguzi ndani ya chama wakati huu.
Kwani katiba inasemaje, si ni mwaka huu ndio wanapashwa kufanya uchaguzi, nafikiri uchaguzi wa mwisho wamefanya 2014 kama sikosei.

Na kwa hizi sheria za sasa zinazomfanya msajili kuwa Mungu mtu nahisi atawashinikiza wafanye kwa amri kutoka juu.
 
Mkuu ndiyo maana nikasema tujaribu kuwa specific tuanze kujadili nani anaweza kuvaa viatu vya Mbowe siyo dhambi kuwajua kwa majina, mbona wenye uwezo wa kuwa makatibu wakuu makatibu wenezi wanaoweza wanatajwa kuwa Marcos Albanie, Heche, Msigwa, Malisa kwanini post ya Mkiti hatutaji?

Anayeweza kuwa katibu mkuu anaweza kuwa mwenyekiti pia. Labda kama uniambie cdm haiendeshwi kama taasisi bali kama kampuni ya watu fulani ambayo vyanzo vyake vya mapato vinategemea mifuko ya hao matajiri. Hapa ninachokiona ni kwamba unapima upepo uone ni nani anatajwa kwenye nafasi hiyo. Kama Mbowe analeta pesa zake za mfukoni kuendesha chama una haki ya kusema hakuna anayeweza kuwa mwenyekiti kwani akiwa mwenyekiti inabidi aje na hela zake. Sasa kama cdm kinaendeshwa kwa fedha za mwenyekiti hapo ujue hamna chama kuna kundi la wajanja.
 
Niliyeanzisha mada ni mimi naijua uzito wake inawezekana wewe hujui hata lengo lake, hii mada ni pana nyie mmedandia sehemu ndogo sana ya mada husika 'uenyekiti wa Mbowe' na mimi naenda na nyie, akitokea mwingine tutajadili mafanikio ya Chadema nk, usichanganye mada kusema sensitive nalinganisha na posts ndani ya chama siyo nje ya chama, kwenye chama Mkiti ndiye kichwa cha chama.

Nikurahisishie kama hii mada ni nzito na ww tu ndio unaujua uzito wake basi huku jukwaani ulipoileta sio sehemu sahihi. Hapa umeleta mada ya ofisi jukwaani ambapo huku tuko huru hatujali mipaka ya huko ofisini kwenu. Siku nyingine mada ya huko ofisini bakini nayo ikija hapa tunaichambua bila woga wala mipaka. Unasema mada ni pana lakini wakati huohuo unaiwekea mipaka!! Mkuu kubali tu leo umejichanganya, kajipange upya sio wote ni wepesi kwa kiwango unachodhani.
 
Post ya Mkiti wa chama ni sensitive huwezi kumwachia mtu yeyote from nowhere lzm atambulike wanachama wamjue na awe groomed na viongozi. Kama hatambuliki basi hafai kuwa kiongozi.
QUININE hapa umepotoka sana, na kwa hoja unapaswa kuwaomba radhi wanachadema wote humu Jamvini.

Hivi Lowassa na JUMA Duni walikuwa wanachadema from somewhere ila wanachadema wengine ni from nowhere to deserve uenyekiti wa chama ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anayeweza kuwa katibu mkuu anaweza kuwa mwenyekiti pia. Labda kama uniambie cdm haiendeshwi kama taasisi bali kama kampuni ya watu fulani ambayo vyanzo vyake vya mapato vinategemea mifuko ya hao matajiri. Hapa ninachokiona ni kwamba unapima upepo uone ni nani anatajwa kwenye nafasi hiyo. Kama Mbowe analeta pesa zake za mfukoni kuendesha chama una haki ya kusema hakuna anayeweza kuwa mwenyekiti kwani akiwa mwenyekiti inabidi aje na hela zake. Sasa kama cdm kinaendeshwa kwa fedha za mwenyekiti hapo ujue hamna chama kuna kundi la wajanja.
Angalau sasa tunaanza kujuana rangi it was just a matter of time,
Nikurahisishie kama hii mada ni nzito na ww tu ndio unaujua uzito wake basi huku jukwaani ulipoileta sio sehemu sahihi. Hapa umeleta mada ya ofisi jukwaani ambapo huku tuko huru hatujali mipaka ya huko ofisini kwenu. Siku nyingine mada ya huko ofisini bakini nayo ikija hapa tunaichambua bila woga wala mipaka. Unasema mada ni pana lakini wakati huohuo unaiwekea mipaka!! Mkuu kubali tu leo umejichanganya, kajipange upya sio wote ni wepesi kwa kiwango unachodhani.
Tangu uanze kujadili point yako kuu ni Mbowe, huendi zaidi ya kuongelea Mbowe kakaa muda mrefu, umeshaeleweka ni muda wa kuwaachia wenye mawazo tofauti na Mbowe kuachia madaraka. Kwa heri if you don't mind.
 
QUININE hapa umepotoka sana, na kwa hoja unapaswa kuwaomba radhi wanachadema wote humu Jamvini.

Hivi Lowassa na JUMA Duni walikuwa wanachadema from somewhere ila wanachadema wengine ni from nowhere to deserve uenyekiti wa chama ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni mawazo yangu niombe radhi kutoa maoni yangu,

Lowassa na Duni waligombea wenyekiti?
 
Niliyeanzisha mada ni mimi naijua uzito wake inawezekana wewe hujui hata lengo lake, hii mada ni pana nyie mmedandia sehemu ndogo sana ya mada husika 'uenyekiti wa Mbowe' na mimi naenda na nyie, akitokea mwingine tutajadili mafanikio ya Chadema nk, usichanganye mada kusema sensitive nalinganisha na posts ndani ya chama siyo nje ya chama, kwenye chama Mkiti ndiye kichwa cha chama.
Kwahiyo kama tumedandia mada ulitaka uanzishe mada uchangie peke yako tu ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom