CHADEMA itabaki kuwa CHADEMA tu

CHADEMA itabaki kuwa CHADEMA tu

Kuwa mwanachama wa Chadema lazima u-risk kazi yako ref. Prof. Baregu, u-risk maisha yako ref. Tundu Lissu, u-risk biashara zako ref. Mbowe. Kama huna moyo wa kiuana mapinduzi, una tamaa ya utajiri, tamaa ya kazi serikalini, tamaa ya tenda Chadema siyo sehemu yako. Alikuwepo Dr. Slaa kaondoka mwenyewe, alikuja Lowassa na watu wake kaondoka na watu wake kaiacha Chadema na watu wake wasioyumba.


Mchambuzi huru mwana JF Quinine.
Baada ya Sumaye kumwaga manyanga nimeona nijikumbushe yanayoikumba Chadema kwa kukopi kupande changu hiki.
 
Mimi sisemi Mbowe apumzike uenyekiti kisa hilo kosa la Lowassa tu, bali ameshakaa madarakani kwenye nafasi ya uenyekiti zaidi ya miaka 15, hapo ndio dhana ya taasisi ingepata maana kwa kuchagua mwenyekiti mwingine. Jaribu kuangalia kiongozi mzuri ni ndani ya miaka kumi tu kwenye nafasi moja, lakini akizidi miaka kumi huanza kuongoza kwa mizengwe na maamuzi kama hayo ya kumpokea Lowassa. Hili wala halihitaji ubishani kwani ndio uhalisia. Mwisho kabisa wa ubora wa Mbowe ilikuwa ni 2015 hata kama cdm ingetoa rais, ukweli uwezo wake kwa sasa umefikia ukingoni.
Kama una charisma ya kutosha muda huu si sahihi Mbowe kuondoka!

Wengine hatujui watareact vipi wakiguswa Mali zao, maisha yao, ndugu zao etc, Mbowe kaguswa vyote hivyo na kafauru.

Hiki si kipindi cha majaribio japo naamini kuna watu wenye Uwezo kama au kuliko Mbowe ila kwa utawala huu, aslani tusijaribu.

Tumeona watu wanavyotishiwa na kuyield, kuuwawa au kuteswa na kunyong'onyea twende na Mbowe then huyu akitoka naye atoke, ila, team ya uongozi ya Mbowe inabidi ibadilike ili chama kizidi kusonga mbele!

CHADEMA ina nguvu zaidi ya CCM ukizingatia idadi ya wana chama lakini kinakuwa weak kwa kutokuwa na dola tuu! Na CCM wanajua hilo na wametumia mbinu zote kupenetrate wameshindwa!

Systemic change yeyote itaiingiza CHADEMA madarakani hapo ndipo watu watazidi kuishangaa charisma na Mwalimu Nyerere maana alitabiri tayari kuwa after CCM CHADEMA watachukua nchi!!
 
Kuna watu wanaifananisha Chadema na NCCR Mageuzi, wanaifananisha Chadema na CUF wengine wamefikia kuifananisha Chadema na ACT Wazalendo, hawako sahihi hawajui historia yake.

Chadema haikufika pale ilipo kwa kubebwa na vyombo vya dola imepambana kwa jasho la damu, haijafika hapo kwa kupata wanachama wa mkupuo wanachama wa mafuriko kama ilivyopata NCCR 1995 wakati Mrema alipohama CCM au kama ACT Wazalendo inavyopata wanachama wengi (Zanzibar) baada ya Maalimu Seif kuhama CUF. Chadema imewajenga wanachama na viongozi wake kutoka mashinani, wengi wa viongozi wake imewa groom yenyewe, Mnyika, Zitto, Mbowe, Mdee, Heche, Kafulila, Katambi nk.

Waliosahau historia ya Chadema naomba niwakumbushe kidogo. Mwaka 1994 Chadema ilikuwa na Madiwani 13 tu Tanzania nzima haikuwa na Halmashauri hata moja. Mwaka 1995 ilikuwa na Wabunge wanne (4). Mwaka 2000 ilipata Madiwani 45 tu nchi nzima. Kwa hiyo safari ya Chadema siyo ya kuangalia leo, yanayo wakuta ndugu zake ACT Wazalendo wao yaliwakuta zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Chadema ina wanachama wenye imani na damu ya demokrasia, wanaharakati, wanachama wake wengi siyo wanaofuata mtu, ina wanachama na wapenzi waliojitoa.

Kuwa mwanachama wa Chadema lazima u-risk kazi yako ref. Prof. Baregu, u-risk maisha yako ref. Tundu Lissu, u-risk biashara zako ref. Mbowe. Kama huna moyo wa kiuana mapinduzi, una tamaa ya utajiri, tamaa ya kazi serikalini, tamaa ya tenda Chadema siyo sehemu yako. Alikuwepo Dr. Slaa kaondoka mwenyewe, alikuja Lowassa na watu wake kaondoka na watu wake kaiacha Chadema na watu wake wasioyumba.

Chadema inajengwa na mfumo ambao unafika hadi vijijini kwenye mashina si rahisi kuuvunja, Chadema ya leo haina tofauti na Chama cha Mapinduzi CCM, imejengeka ki taasisi zaidi, CCM hata aondoke Magufuli itabaki kuwa CCM, vivyo hivyo Chadema hata aondoke Mbowe itabaki kuwa Chadema, si rahisi kuilinganisha na vyama vingine, vitakuja vitapata umaarufu na kama havitasimamia misingi vitaondoka na kuiacha Chadema.

Mchambuzi huru mwana JF Quinine.
Chadema imekwisha mwaka kesho 2020 huenda hata mbunge mmoja wakakosa
 
Aisee CDM haiingiliki nimeamini - CDM ni imani...huna imani hukai humo yaani utaondoka mwenyewe tena mchana mchana kweupe na magodoro yako kichwani !!
 
Ila Chadema inatakiwa kuondokana na mamluki kama ilivyo kwa Sumaye .

Chadema haiwezi kuchukua dola kwa kuendelea kuwategemea CCM.


Tunataka chadema mpya yenye watu wenye ushawishi ma uthubutu kama ilivyo kwa Lissu, Heche,Lema na Sugu ..

Watu Mbogo hawahitajiki Chadema kama mnataka kuchukua Dola..
kaka ille safu ya mashambulizi inarudi ile ile....mtaa wa saba salaam kwenu... mkishindwa hoja msikimbilie kuwaita police..
 
Chadema imekwisha mwaka kesho 2020 huenda hata mbunge mmoja wakakosa
Kwa uchafuzi wanaweza kukosa ila kwa uchaguzi Hata zaidi ya 70% watachaguliwa! Kwa akili yako unafikiri kwanini huyo bwana anaogopa uchaguzi?

Lubuva ilikuwa 10m vs 4m fikiri kwa kina utaelewa!
 
Kuna watu wanaifananisha Chadema na NCCR Mageuzi, wanaifananisha Chadema na CUF wengine wamefikia kuifananisha Chadema na ACT Wazalendo, hawako sahihi hawajui historia yake.

Chadema haikufika pale ilipo kwa kubebwa na vyombo vya dola imepambana kwa jasho la damu, haijafika hapo kwa kupata wanachama wa mkupuo wanachama wa mafuriko kama ilivyopata NCCR 1995 wakati Mrema alipohama CCM au kama ACT Wazalendo inavyopata wanachama wengi (Zanzibar) baada ya Maalimu Seif kuhama CUF. Chadema imewajenga wanachama na viongozi wake kutoka mashinani, wengi wa viongozi wake imewa groom yenyewe, Mnyika, Zitto, Mbowe, Mdee, Heche, Kafulila, Katambi nk.

Waliosahau historia ya Chadema naomba niwakumbushe kidogo. Mwaka 1994 Chadema ilikuwa na Madiwani 13 tu Tanzania nzima haikuwa na Halmashauri hata moja. Mwaka 1995 ilikuwa na Wabunge wanne (4). Mwaka 2000 ilipata Madiwani 45 tu nchi nzima. Kwa hiyo safari ya Chadema siyo ya kuangalia leo, yanayo wakuta ndugu zake ACT Wazalendo wao yaliwakuta zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Chadema ina wanachama wenye imani na damu ya demokrasia, wanaharakati, wanachama wake wengi siyo wanaofuata mtu, ina wanachama na wapenzi waliojitoa.

Kuwa mwanachama wa Chadema lazima u-risk kazi yako ref. Prof. Baregu, u-risk maisha yako ref. Tundu Lissu, u-risk biashara zako ref. Mbowe. Kama huna moyo wa kiuana mapinduzi, una tamaa ya utajiri, tamaa ya kazi serikalini, tamaa ya tenda Chadema siyo sehemu yako. Alikuwepo Dr. Slaa kaondoka mwenyewe, alikuja Lowassa na watu wake kaondoka na watu wake kaiacha Chadema na watu wake wasioyumba.

Chadema inajengwa na mfumo ambao unafika hadi vijijini kwenye mashina si rahisi kuuvunja, Chadema ya leo haina tofauti na Chama cha Mapinduzi CCM, imejengeka ki taasisi zaidi, CCM hata aondoke Magufuli itabaki kuwa CCM, vivyo hivyo Chadema hata aondoke Mbowe itabaki kuwa Chadema, si rahisi kuilinganisha na vyama vingine, vitakuja vitapata umaarufu na kama havitasimamia misingi vitaondoka na kuiacha Chadema.

Mchambuzi huru mwana JF Quinine.

Moments kama.hizi zinaleta nafasi ya kujitafakari. Sio vizuri kuzibeza
 
Mkuu mimi nina maoni mawili tu hapa:

Mosi, kitu kimoja kikubwa CHADEMA haina, ambacho nadhani ni muhimu kwa siasa za Afrika ni kuwa na wanachama watiifu ambao ni watu kutoka vyombo vya dola kama TISS, JWTZ, POLISI na Mahakama.

Hili ndilo linawabeba CCM na kuwapa kiburi cha kufanya watakavyo hapa nchini bila hata kuzingatia miiko ya kisheria.

CHADEMA kimejitahidi sana kufika vijijini kuliko vyama vingine vya upinzani. Lakini bahati mbaya sana ni kwamba chaguzi za Afrika hazifanikishwi kwa boski la kura peke yake, lazima mkono wa dola utumike tu.

Pili, kitu kingine kikubwa zaidi na muhimu ambacho CUF inacho ambacho vyama vingine vya upinzani havina ni kwamba CUF imewahi kufanikiwa kushika dola kule Zanzibar kwa nguvu zao wenyewe kabla hata ya UKAWA kuzaliwa.

Walifanikiwa kuunda Serikali ya Umoja ya Zanzibar na kutoa Makamu wa Raisi: Hivyo nadhani kwenye suala zima la uzoefu wa kiuongozi CUF watakuwa wako mbele kidogo ya CHADEMA. Pia mtandao wao kule visiwani ni mkubwa sana kuliko chama chochote cha upinzani hapa Tanzania.

Umetoa hoja nzuri na ya msingi sana. Mimi naomba kuchangia kwenye hili moja tu;

Kwamba, CHADEMA na vyama vilivyo nje ya dola kwa ujumla wanapaswa kuwa na watu (wanachama) watiifu ktk taasisi nyeti za umma (serikali) hususani TISS, JWTZ, POLISI na Mahakama...

Yes, nakubaliana na wewe 100% na ndiyo njia ya pekee kuwaondoa CCM madarakani....

SWALI NI; How?

Moja ya zana (tools & weapons) muhimu kuzitumia kufanikisha hili ni;

FEDHA

- Hii ndiyo silaha wanayotumia watawala wengi na vyama vyao ktk nchi za ki-Africa na dunia ya tatu kuhakikisha wanabaki madarakani....

- Wanahakikisha kuwa vyama vya upinzani vinakuwa dhaifu (weak) kiuchumi (kifedha) ili washindwe kujiimarisha na kuwa na ushawishi ktk jamii/watu...

- Na ndiyo maana ya hizi harakati zinazoendelea sasa za kununua wabunge, madiwani na wanachama wengine maarufu wa vyama hivi...

- Tukumbuke vyanzo vikuu vya fedha ndani ya vyama hivi ni RUZUKU toka serikalini na MICHANGO ya wanachama waaminifu....

- Binafsi niwapongeze CHADEMA kwani mpaka sasa kina umri wa takribani miaka 28 na graph yake ya ukuaji, inapanda tu pamoja na kupitia misukosuko mikubwa mara zote ktk chaguzi zote chini ya mfumo wa vyama vingi....

- Hata mwaka huu, wanaodhani vinginevyo, wanajidanganya. Kuna kila dalili na sababu kuwa, CHADEMA na UPINZANI kwa ujumla watazoa viti vingi sana kuanzia Udiwani hadi Ubunge....

- Na kwenye Urais, CCM wakae chonjo kwani pamoja na kuwa mazingira ya uchaguzi kwa akili na macho ya kibinadamu yanawapendelea (favour) wao, lakini lipo kosa watalifanya na ndiyo utakuwa mwisho wao...!!

SASA, KWANINI FEDHA? WATATOA WAPI FEDHA AMBAYO NDIYO POWER KATIKA SIASA?

- Ni rahisi tu kujua kuwa, FEDHA ndiyo inayowafanya TISS, JWTZ, POLISI na MAHAKAMA (majaji & mahakimu) kuwa royal kwa CCM...

- You want them to be raoyal to you, overtake what is being provided to them by your opponent...!!

- Kwa taarifa ya wote wasiojua, ni kuwa, moja ya kada za umma zenye upendeleo maalumu "kimaslahi na marupurupu" ya wazi kisheria na ya kificho ni hizi tajwa...

- Hii siyo kwa bahati mbaya. Ni kwa sababu moja tu, that is, "to maintain their royalty", kwa mtawala aliyepo madarakani - CCM..!!

NOW, WHAT SHOULD THEY DO?

1. Defenetely, hawana fedha. They are weak economically kama taasisi. Wanachoweza kufanya ni aidha kupata economic assistance toka nje wakati huohuo wawe na uwezo wa kuepa sheria za kifedha za nchi kwa sbb kwa utaratibu wa kawaida, hawawezi kukubaliwa kupokea fedha toka nje...!!

2. Kuitumia kikweli kweli slogan ya " PEOPLE'S POWER" ama kwa kiswahili "NGUVU YA UMMA" ili ku - organize "civil disobedience" dhidi ya utawala wa serikali wasiyoitaka. Sababu za kuwaambia watu, wakubaliane nazo na kisha wawaunge mkono lazima ziwe very CLEAR and GENUINE na kamwe zisiwe za kufikirika tu.....!

Lakini, ili hii ifanye kazi kwa ufasaha pasipo kuleta madhara (casualities), tunarudi palepale, kwamba, kuna ulazima ingalau wawe na ushawishi wa kiwango fulani kwenye vyombo hivi kama ikivyotokea Tunisia, Libya na Egypt...!

Huko ktk nchi hizi, ilifika mahali POLISI na jeshi wakawa upande wa umma. Wakakataa kuua watu....!

MUHIMU:

- Lazima tukubaliane kwa dhati kabisa kuwa, mpaka sasa utawala huu chini ya CCM ulishafeli kukidhi marajio ya wananchi kiuchumi na kijamii na kwa mantiki hii umeshajitegenezea mazingira yote ya kuondolewa madarakani...

- TISS, JWTZ, POLISI na MAHAKAMA wote wanalijua hili kwa ukamilifu wake. Lakini, kwa kuwa wanapata kila wanchohitaji kwa ajili ya maisha yao na familia zao, watakuwa watiifu tu kwa sbb hiyo na siyo kitu kingine..!!

- Vyama vilivyo nje ya mfumo wa serikali (upinzani) wakitumia fursa hii kwa usahihi na kwa umakini, wanaweza kuangusha mbuyu kwa kuusukuma kwa mikono tu bila kutumia greda....!!
 
CCM wanafikiri watatawala nchi milele...kwa kuanza tunaanza na Tume huru kwanza watake wasitake.
 
Mleta uzi uko sahihi sana kuhusu cdm. Ila cdm 2015 ilituangusha sana kwa tamaa ya viongozi wachache kukubali kuchukua asali ya Lowassa na kumpa nafasi adhimu mzee toka ccm aliyetaka urais tu bila kujali chama. Lile ni kosa la wazi na kubwa sana kufanywa na taasisi. Sikutegemea taasisi kubwa kama cdm ingeweza kufanya maamuzi mazito kwa kuchukua mgombea ambaye hata Mimi nisiyejua siasa nilijua kabisa ni kosa la dhahiri. Kwa kosa lile ni dhahiri Mbowe anapaswa kuachana na uenyekiti na kumuachia mtu mwingine ili tuanze upya.

Halafu cheo muhimu cha katibu mkuu ndani ya cdm kimepwaya mno kiasi kwamba kuendelea kuwa na katibu mkuu kama huyo ni kosa kubwa. Kwa sasa tunapaswa kuwa na katibu mkuu mtu kama Heche au Marcos Albanie. Huyo katibu mkuu wa sasa kachangia kuifubaza sana cdm.

Huna hoja. Huijui Chadema. Uko upande wa pili. Huwezi kuwa objective.
 
IMG_20200727_152411.jpg
 
Mleta uzi uko sahihi sana kuhusu cdm. Ila cdm 2015 ilituangusha sana kwa tamaa ya viongozi wachache kukubali kuchukua asali ya Lowassa na kumpa nafasi adhimu mzee toka ccm aliyetaka urais tu bila kujali chama. Lile ni kosa la wazi na kubwa sana kufanywa na taasisi. Sikutegemea taasisi kubwa kama cdm ingeweza kufanya maamuzi mazito kwa kuchukua mgombea ambaye hata Mimi nisiyejua siasa nilijua kabisa ni kosa la dhahiri. Kwa kosa lile ni dhahiri Mbowe anapaswa kuachana na uenyekiti na kumuachia mtu mwingine ili tuanze upya.

Halafu cheo muhimu cha katibu mkuu ndani ya cdm kimepwaya mno kiasi kwamba kuendelea kuwa na katibu mkuu kama huyo ni kosa kubwa. Kwa sasa tunapaswa kuwa na katibu mkuu mtu kama Heche au Marcos Albanie. Huyo katibu mkuu wa sasa kachangia kuifubaza sana cdm.
leta hoja yako acha kuzungukazunguka?? Unazingua tu.
 
Back
Top Bottom