Mkuu nilitarajia ungenipa majibu kwenye paragraph ya pili ili kunionyesha uimara wa Mbowe. Ila naona umechomoka kwa hoja zile zile za mahaba niue. Sitaki kukukwaza sana maana kipendacho roho. Chukua tu ujumbe wangu kwamba wakati ukuta.
Mkuu kama unachukulia kuhama kwa madiwani na wabunge kwenda CCM ni kushindwa kwa Mkiti basi huzijui siasa za Tanzania, hujui nguvu inayotumika, polisi, msajili, hazina, mahakama, bunge, pole sana, halafu kujenga ofisi siyo siasa ndugu unaweza kufanya siasa bila kujenga hata chumba, Nyerere alifanya siasa chini ya miembe.
Jisomee kidogo mafanikio ya Chadema isiyo na ofisi. COPY & PASTE from somewhere. Hoja kwa hoja.
TREND YA USHINDI YA CHADEMA
CHADEMA kimepta usajili wa kudumu 21.01.1993 baada ya hapo kilianza kushiriki uchaguzi wa SM na Madiwani mwaka 1994. Toka hapo hadi sasa ushindi wetu kwa Madiwani, Halmashauri, Wabunge na kura za Uraisi umekuwa hivi;
*Mwaka 1994*
1. Madiwani 13 Tanzania nzima
2. Hatukupata Halmashauri hata moja.
*Mwaka 1995*
1. Wabunge tulipata wanne (4). Kati ya hao watatu wa Majimbo na mmoja wa Viti Maalum ambao ni;
- Karatu (Dr Slaa)
- Rombo (Masumbuko Lamwai)
- Kigoma Mjini (Dr Wared Kaburu)
- Viti Maalum alikuwa Mary Kabigi wa Mbeya.
2. Uraisi
- Tuliwaunga Mkono NCCR Mageuzi (Mrema)
*Mwaka 2000*
1. Madiwani tulipata 45 nchi nzima
2. Halmashauri mbili (Karatu na Hai)
3. Wabunge watano. Majimbo manne na viti maalum mmoja.
- Karatu (Dr Slaa)
- Hai (Freeman Mbowe)
- Moshi Mjini (Marehemu Ndesamburo)
- Kigoma Mjini (Dr Wared Kaburu)
- Viti Maalum alikuwa Grace Kihwelu ambaye yuko hadi leo.
*Mwaka 2005*
1. Madiwani 102 nchi nzima.
2. Halmashauri mbili (Karatu na Moshi Manispaa)
3. Wabunge tulipata 11. Watano wa Majimbo na sita viti Maalum. Ambao walikuwa;
- Karatu (Dr Slaa)
- Moshi Mjini (Marehemu Ndesamburo)
- Kigoma Kaskazini (Zitto)
- Mpanda Kati (Said A. Arfi)
- Tarime (Chacha Wangwe)
- Viti maalum walikuwa 6 pamoja na Halima Mdee, Grace Kihwelu na wengine.
4. Uraisi Freeman Mbowe
- Tulipata kura 670,000/=
*Mwaka 2010*
1. Madiwani 589 Nchi nzima
2. Halmashauri 7
- Karatu
- Moshi Manispaa
- Hai
- Musoma Mjini
- Ukerewe
- Ilemela
- Kigoma Ujiji (50/50)
3. Wabunge 49
- Majimbo 24 (Ni pamoja na kina Msigwa, Wenje, Mnyika, Halima, etc)
- Viti Maalum 25 (pamoja na Kiwanga, Lyimo, Conchester, etc)
4. Uraisi (Dr Slaa)
- Kura 2,300,000
*Mwaka 2015*
1. Madiwani 1108. Nchi nzima
2. Halmashauri 25 nchi nzima.
- 22 tunaziongoza
- 3 wametupora CCM (Kilombero DC, Sumbawanga MC, Kyerwa DC)
3. Wabunge tumepata 74
- Majimbo 35 pamoja na Ndanda
- Viti Maalum 37
- Africa Mashariki 2
Kati ya hao wanaume 29 na wanawake 45.
4. Uraisi (Edward Lowassa)
- Tulipata kura 6,080,000
*Tukutane kwenye Msingi, Tuongeze ushindi. CHADEMA haijawahi kudumaa wala kushuka katika ushindi.