Mkuu nilitarajia unakuja na hoja za msingi kumbe unanibebea hoja nyepesi hivyo? Hiyo kwamba Nyerere alifanya siasa chini ya miembe mimi ndio nimekuwa nikiwajibu wanaccm hapa jukwaani toka 2013 walipokuwa wanaibeza cdm kutokuwa na ofisi. Hivi unaweza kukabidhiwa watoto uwaongoze kisha leo kapotea mmoja, kesho mwingine, na mtondogoo hivyo hivyo kisha useme bado una uwezo wa kuwaongoza? Hayo mafanikio ndio hayo ninayokuambia kilele cha Mbowe kwenye mafanikio ilikuwa 2015, kwa mtu asiyejijali bali kuamini taasisi angepisha mwingine. Haidhuru basi angesema uchaguzi ujao hatagombea ili kutoa nafasi kwa mwanachama mwingine. Narudia tena, wakati ukuta.
Tindo, umelirudia hili mara kwa mara, kiasi kwamba inanibidi niheshimu fikra na pengine hata kuanza kushawishika jambo husika lifikiriwe na kujadiriwa ndani ya chama na Mbowe mwenyewe asilionee kinyongo. Ninapata taabu sana kuitetea hoja yako, lakini haina maana kwamba sioni mantki ndani yake.
Na wazo hili linatokana na uamini kwamba CHADEMA ni chama cha watu wengi wenye msimamo wa pamoja kuhusu chama chao.
Watu hawa ndio wenye uwezo wa kuamua, kama Mbowe aendelee kuongoza chama chao, au awekwe kiongozi mwingine.
Hii haitakuwa na maana kwamba Mbowe ameshindwa kuongoza, (bali litakuwa ni hitaji la kuleta mawazo mapya ndani ya chama)? Hili ni swali.
Je, uwepo wa Mbowe unazuia mawazo mapya? Hao wenye mawazo mapya yenye manufaa makubwa lakini wakashindwa kuyawasilisha ndani ya chama kwa vile sio viongozi wakuu wa chama, ni mawazo ya namna gani hayo; na hawa viongozi wana commitment kiasi gani ndani ya chama chao?
Wanachama wa CHADEMA wanawafahamu vizuri viongozi wao kuliko sisi tulio nje ya chama.
Kwa kuunga mkono msimamo wako; je kukiitishwa uchaguzi wawachague viongozi na wakataka Mbowe aendelee kuwa kiongozi wao bado utaona wamekosea? Kwa bahati nzuri msimamo wako juu ya swali hilo pia unajulikana!
Tatizo juu ya hili kufanyika sasa pia linajulikana. Sio wakati sahihi kufanya hivyo; na watasambaratishwa wasijue ni nini kimewatokea. Wewe hili huliamini kuwa linawezekana kutokea!
Kutaka Mbowe ajitoe katika uongozi, hasa wakati huu, wazo hilo sio la kuitakia mema CHADEMA na nchi kwa ujumla.
CHADEMA kama wanata mabadiliko, wakati sahihi wa kufanya mabadiliko hayo sio sasa, itabidi wasubiri baada ya 2020.