Maishamapya
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 1,279
- 375
We Prudence kama alivyo kaka yako Padre Privatus na kaka yako Primus ni wazuri sana wa kujenga hoja watu wa Ibwera kule aragwe.
Lakini kwa hili Classmate wangu imekupuruchuka.
Kwani lazima ujue kuwa kazi ya Vyama vya Upinzani ni kuizindua na kuikosoa Serikali iliyopo madarakani kwa nia na madhumuni ya kufanya nchi iende sawia. Kwa hiyo Serikali yoyote iliyo makini ni ile inayochambua kauli za wapinzani na zile wanazoziona zinawakwaza wananchi basi inaweka kipaumbele katika kuzitatua.
Mfano mdogo ni issue ya katiba mpya. hata kule Kenya utaiona upinzani ndio ulioshinikiza na serikali ikakubali na baadae wamepata katiba mpya. Si rahisi kwa Serikali yenyewe na chama chake kutaka katiba mpya sababu kubwa katiba hiyo mara nyingi ina kipendelea chama tawala.
Kwa hiyo Upnzani si dhambi na ni wajibu wao kuikosoa serikali pale inapokosea.
Nyegera waitu
Kwangu mimi alichokisema Prudence na unachokisema havina tofauti.