- Source #1
- View Source #1
Heche kweli kichekesho! Kila siku makelele kama generator ya kijijini, kumbe walikuwa wanapiga porojo tu! Walisema hawashiriki uchaguzi, leo wanatuma maombi kwa mbwembwe. Wanafiki wakuu, walitaka huruma kumbe walikuwa wanatafuta nafasi! Acheni maigizo, wananchi si wajinga.
- Tunachokijua
- John Heche makamu mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) alizungumza na wananchi Juni 30, 2025. Katika mkutano huo Heche alizungumzia masuala tofauti ikiwemo suala la kuhitaji mabadiliko ya uchaguzi.
Madai
Juni 30, 2025 kumekuwa na grafiki inayosambazwa katika baadhi ya mitandao ya kijamii ikiwemo X huku ikiwa na utambulisho wa chombo cha habari cha Jambo TV. Grafiki hiyo imeambatana na picha ya John Heche na ujumbe unaosomeka “HECHE: CHADEMA TUMESHATUMA MAOMBI YA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU KWA MSAJILI”
Uhalisia wa madai hayo
JamiiCheck imefuatilia uhalisia wa taarifa hiyo na kubaini kuwa si ya kweli. Katika hotuba aliyoitoa John Heche Juni 30, 2025, Makamu huyo alizungumza mambo mbalimbali yanayoeneldela nchini ikiwemo kupotea kwa watu, kutekwa na mwenenndo wa hali ya uchumi.
Ufuatiliaji wa kina uliofanywa na JamiiCheck kwa kufuatilia hotuba hiyo imebaini kuwa maneno hayo ya kuwa CHADEMA wameshatuma maombi ya kushiriki uchaguzi mkuu wa kwa msajili wa vyama.
Mbali na mambo mengine Heche alibainisha kuwa serikali inatamani viongozi wa chama hicho waende kusujudu kwao lakini wao wamekataa. Pia amesisitiza kuwa wamekataa kushiriki katika uchaguzi usio sawa na wa haki
“Tumekataa kuwa sehemu ya uchaguzi wenye unajisi. Tunaisihi serikali na tunaendelea kuisihi serikali ifanye mabadiliko kwenye mifumo ya uchaguzi” - John Heche
April 12 Kaimu Katibu mkuu wa CHADEMA, John Mnyika kupitia ukurasa wake wa X alisema kuwa hatoenda kusaini fomu za maadili ya uchaguzi wakihimiza mabadiliko katika mifumo ya uchaguzi, jambo ambalo liliwanyima wao sifa za kushiriki uchaguzi mkuu 2025.
JamiiCheck imefuatilia pia na kubaini kuwa grafiki zinazotumika kusambaza taarifa hizo hazijatolewa wala kuchapishwa na Jambo TV katika kurasa zao rasmi za mitandao ya kijamii hivyo ni za kughushi.