CHADEMA imekuwa dampo la CCM

CHADEMA imekuwa dampo la CCM

Nianze kwa kuwasalim wakuu
Kwanza kabisa sina kadi ya chama chochote bali ni mtanzania ninayefuatilia siasa za nchi yangu kwa undani.

Katika kila taifa kuna aina mbili za kuimarisha upinzani
Njia ya kwanza ni kwa upinzani kuombea kumeguka kwa chama tawala hasa ukizingatia kuwa nchi yetu ilikuwa na chama kimoja

Mifano ya njia hii iko mingi lakini wa karibu kabisa ni nchini Kenya

Njia ya pili ni kwa wale waliozaliwa katika mfumo wa vyama vingi na wakaelewa kwa nn wapo upande pinzani na chama tawala
Njia zote zinategemeana na lengo ni moja tuu katika kuuimarisha upinzani kwani upinza imara utoa nafasi ya chama tawala kujikosoa

Napendelea tanzania tuwe na upinzani imara lakini si upinzani huu unaofanywa na chama kikuu cha upinzani CHADEMA
Ni ukweli usiopingika kuwa kila mtu ana haki ya kuwa mwanachama wa chama chochote pasi kuvunja sheria na katiba ya nchi, lakini sasa CHADEMA wamekuwa watumwa wa makandokando ya CCM

Hii inaonesha kuwa chama kikubwa cha Upinzani hakina uwezo wa kutengeneza watu wake mpaka itegemee makando ya chama tawala

Hii halitatupa upinzani mzuri hivyi pia chama tawala kitakuwa legelege kwani hakitaweza kujitathimini

Upinzani imara ndio msingi wa nchi imara na si upinzani wa kutegemea makandokando

Kwani hayo makandokando hayataweza kamwe kujitofautisha na kule watokapo
Asanteni
 
mwanzo kabla ya 1992 hao wapinzani walikuwa vyama gani? kama walitoka ccm basi kila mmoja ana uhuru kuendelea kuchagua chama akipendacho
 
Trum alikuwa Republican akahamia Democratic, akawa Independent na mwishoe akarudi Republican.
Nikawaida sana mtu kuhama chama, sema huku bongo ushamba mwingi.

Anyway hii inatokana na siasa changa ukichangia na huu utamaduni wa demokrasia tulio urithi kwa wazungu.
Hakuna tulicholithi kwa wazungu hapo, yaani nachukia sana.
 
Betony unategemea utawapata wapi wanachama wasio na chama??
Si kwamba napinga chama kutegemea wanachama toka chama kingine hapana
Ni kwamba chama kikuu cha Upinzani kwa zaidi ya miaka hii ishirini ya vyama vingi kiatakiwa kiwe na uwezo wa kuweza kutengeneza wanachama wake na si kutegemea makandokando ya vyama vingine
 
mwanzo kabla ya 1992 hao wapinzani walikuwa vyama gani? kama walitoka ccm basi kila mmoja ana uhuru kuendelea kuchagua chama akipendacho
Ni zaidi ya miaka ishirini sasa
Kutegemea makandokando hakukutofautishi na pal yalipotoka
 
Siasa ni kama mpira huwezi kuniambia Ronaldo kwenda Real Madrid eti Madrid ni dambo la Manchester United.Je Lowassa akirudi CCM Kwa hiyo CCM in dambo la chadema?
 
Siasa ni kama mpira huwezi kuniambia Ronaldo kwenda Real Madrid eti Madrid ni dambo la Manchester United.Je Lowassa akirudi CCM Kwa hiyo CCM in dambo la chadema?
Wema asingekamatwa na bangi, angehamia chadema?

Lowasa asingekuwa fisadi na kukatwa angehamia chadema??
 
Naomba kueleweshwa tu kama chadema ni chama cha wahalifu au la.

Kila anayetuhumiwa ndani ya ccm kwa uhalifu uwe ni ufisadi au dawa za kulevya utamsikia anakimbilia chadema.

Ni vema Chadema mkajitafakari kabla ya Watanzania kufanya uamuzi juu yenu mwaka 2020 na kujikuta hampati hata 5% ya wapiga kura wote.

Si kila ndege huliwa la hasha wengine wana sumu kali.
 
Kuhama chama hakuna mwanachama anayekatazwa yaan vyama ni kama timu za mpira....kumbuka machali moses kaamia ccm mbn hamjasema matapishi
 
Huyo LOWASA ni CCM aliyekatwa but kufika chadema akafanywa mungu mtu na kupewa madaraka at the expense of wakongwe waliojenga chama, its a lower version bcz ccm hawawez kujiendesha kihovyohovyo kama chadema.

Huwez kujiita bora kuliko mm wakati unakula nilivyovitapika.

Kabla hawajapewa madaraka wanatakiwa wajithathmin wenyewe kama wameweza kujiendesha wao kama wao bcz haiwezekan kufanyia majaribio nchi . jinsi mboe anavyoiendesha chadema syo tofaut sana na jnsi Rwanda inavyojiendesha af eti unakuja na Hoja ya ukuta.

Its a lower of CCM bcz Lowasa aliifanya Chadema chaguo la pili na mpango wake ulikuwa CCM, na hapa inajionyesha yeye sio Chadema na amereveal kuwa CCM is a higher version of Chadema, na yy sio chadema real but n maslahi.

Chomoka upinzan af kuwa neutral af uchambue upinzan, hii itakusaidia kuondoa mihemuko.

Chadema is a lower version of CCM.
Quoted from JF member...
Juzi juzi ccm IMEVUNA wana CHADEMA zaidi ya elfu 1. Ccm ni dampo la CHADEMA
 
Kuhama chama hakuna mwanachama anayekatazwa yaan vyama ni kama timu za mpira....kumbuka machali moses kaamia ccm mbn hamjasema matapishi
Chama kina katiba, pia kina miiko ya viongozi.

Je leo hii chadema watakuwa na ubavu wa kutoka mbele na kukemea ufisadi?

Leo hii chadema wana ubavu wa kukemea wauza madawa ya kulevya??
 
Tangia kuondoka kwa Dr Slaa, Chadema imeacha misingi yake!, sasa hivi kinaongozwa bila kanuni, taratibu na miiko ya chama.

Sasa hivi mafisadi, wachawi, wauza madawa ya kulevya wote watajiunga chadema kwa shangwe na vigelegele bila shida yoyote. !!

Kipindi cha Dr Slaa mtu yoyote mwenye tuhuma za ufisadi na uuzaji wa dawa za kulevya asingeweza kukimbilia chadema.
Mfamaji.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom