CHADEMA imekuwa dampo la CCM

CHADEMA imekuwa dampo la CCM

Ningeshangaa wiki kuisha bila jina la lowasa kutajwa
 
Wanaokwenda ccm inajulikana ni njaa huwa inawaandama, ila kwa chadema tena hasa miaka ya karibuni wanaoingia ni watu wa hovyo zaidi.....mafisadi, wachawi, makahaba, madawa ya kulevya nk
Hahhahaa...iddi azani naye vipi hahaha na wengine akina rizimoko hahaha hao ni akina nani ...mapadri au hahha ...akina daudi bashite ...na mafisad wengine waliojificha tunaowajua ....hahahah
 
Nakupinga mtoa mada umekurupuka, CCM kuanzia TANU ninaijua na CHADEMA ninaijua, sasa nikuambie faida ya kuwa mwanachama wa CHADEMA:-


Ukizielewa vyema falsafa za CHADEMA utapata faida zifuatazo;
1.Kujitegemea
CHADEMA inawafundisha wafuasi wake kuwa na fikra za kujitegemea hawaendekezi mambo ya ombaomba kama CCM ,chama cha CCM wanachama wake no ombaomba hadi inatia kinyaa ndio maana hawaishi kuomba mahindi ya njaa.

2.ELIMU
Wana CHADEMA ni watu wanaojitambua, wameelimika, kuna msukumo mkubwa kujielimisha ili uwe mwanachama mahili wa CHADEMA kunyume na CCM elimu haipewi msukumo wowote ndio maana akina Livingstine Lusinde naye ni mbunge, zaidi ya nusu ya bunge wa CCM ni mambumbumbu.

3.SAREZAO(MAGWANDA)

Sare zao walizochagua ni nguo bora sana khaki aina ya cadet au khaki Amerika, nguo ambazo zamani ulikuwa huwezi kuzipata mpaka upate schorship uende nje, wakizishona na kuzivaa zinawapendeza kabisa na unaweza kuzivaa sehemu yoyote . vijana ambao bado hawana nundu nguo hizo zinawapendeza sana, tofauti na sare za CCM huwezi kushona bali hugawiwa tu kutokana na mambo yao ya kupenda kwa sadala, huwa wanafanya kugawiana tu, SARE za CHADEMA hununuliwa na wenyewe bei ya chini kabisa ni shs 70000 wakati sare za CCM ni wastati wa shs 5000 na unaweza kugawia kijiji kizima

Na mengine mengi tu CHADEMA imeifunika CCM japo kuwa ni chama kongwe lakini hakina ubunifu.
 
Na wanaopokelewa kila siku ccm wakitokea Chadema wao unawazungumziaje?
Ccm ya sasa haipokei makapi..hao wengine wamerudi tu walikotoka..na hawajapokelewa kwa mbwembwe zozote kama mlivyompokea wema..mpeni kitengo cha itikadi na uenezi..atawafaa sana
 
CHADEMA wanaweza kuwa na mapungufu (ambayo kimsingi wananayo) lakini CCM na serikali yake ni waovu, hasa kwa kukiuka haki za raia wake. Uchaguzi uliopita Magufuli alipiganiwa sana na watu, matokeo yake tunaona "giza" tu, hakuna tumaini. Kwa hiyo wanao hama wanawakilisha mitazazamo na nia ya watanzania wengi waliokatishwa tamaa.
 
Kibstec hayo ni maoni yako tu,sasa chadema imeimarika sana kuliko muda mwingine wowote ule tangu kianze,ndiyo maana ccm wameanza kuvuruga watendaji wakuu wa chadema ili wasiendelee na kuimarisha chama,mzee anapiga issue za chinichini sana.
 
Kulisoma andiko la Mbumbumbu ni kazi sana, sasa Kama CCM kilizaliwa siku nyingi na tulikua kwenye one part system wewe unafikiri wanachama wapya wa byama vya upinzani watatoka wapi kama sio CCM? Dr Slaa alihamia Chadema akitokea wapi?Huelewi kitu unaboronga tu kwa sa sababu una ID JF.
 
Kibstec hayo ni maoni yako tu,sasa chadema imeimarika sana kuliko muda mwingine wowote ule tangu kianze,ndiyo maana ccm wameanza kuvuruga watendaji wakuu wa chadema ili wasiendelee na kuimarisha chama,mzee anapiga issue za chinichini sana.
Kimeimarika?????chama kina kosa hata OFISI ya maana......Nisikukatalie ya kuwa CHADEMA imeimalika kupita wakati wowote lakini ni KWENYE SUALA LA UFISADI.....
 
Kinondoni ndio wilaya inayoongoza kwa utumiaji wa mihadarati ,uhuni,Ushoga na kila kitu kibaya ukikosa sehemu au wilaya nyingine Tanganyika utakipata kinondoni na Mitaa ya Ufipa kinondoni ndio makao makuu ya tasisi ya kisiasa so siwezi shangaa leo washukukiwa wote wa mihadarati wakiamia kwenye hyo taasisi



Nasikia mtaa wa ufipa imegeuzwa kuwa sober house .
 
Kwahiyo Dk slaa alikuwa anazuia watu kujiunga chamani? Kuna msemo ubmnasema "Umetisha" lakini wewe "UMETISHWA" pole yako!!!!
Ilikuwà lazima ujitathmini mara mbili..enzi hizo ukiwa Kiongozi wa chadema unaonekana Kiongozi wa taifa..chadema ilikuwa inatoa matamko yanayoishi..chadema ile iliibomoa kabisa ccm..enzi zile matamko ya chadema yalikusanya taifa zima..wasomi, wahadhiri wa vyuo vikuu, viongozi wa Dini, wanachuo na wengine..leo hii kweli inaenda kujikumbatia kwenye koti la wema sepetu..kweli !!!? ama kweli hujafa hujaumbika
 
Sasa unafikiri ccm ndiyo wako salama kwenye ufisadi?? wote ni wapigaji tu,ofisi wanayo ndiyo maana wanafanya kazi zao.
 
Kinondoni ndio wilaya inayoongoza kwa utumiaji wa mihadarati ,uhuni,Ushoga na kila kitu kibaya ukikosa sehemu au wilaya nyingine Tanganyika utakipata kinondoni na Mitaa ya Ufipa kinondoni ndio makao makuu ya tasisi ya kisiasa so siwezi shangaa leo washukukiwa wote wa mihadarati wakiamia kwenye hyo taasisi
Na hiyo kinondoni ipo chini ya Serikali ya CCM tangia uhuru
 
Tangia kuondoka kwa Dr Slaa, Chadema imeacha misingi yake!, sasa hivi kinaongozwa bila kanuni, taratibu na miiko ya chama.

Sasa hivi mafisadi, wachawi, wauza madawa ya kulevya wote watajiunga chadema kwa shangwe na vigelegele bila shida yoyote. !!

Kipindi cha Dr Slaa mtu yoyote mwenye tuhuma za ufisadi na uuzaji wa dawa za kulevya asingeweza kukimbilia chadema.
Hakuna lolote ccm inaenda kuanguka, ss huku mwanza tulikuwa tunampenda magufuli pamoja na ccm lkn saivi hakuna tena, hali mbaya ya kiuchumi mala tunasikia na kuona watu wakionewa na kudhalilishwa ovyo ni ubabe tu, wabunge wetu wanadharauliwa, mahakama nayo kama imekandamizwa, na system yote ime pooza, Tulikuwa hatumpendi Lowassa lkn hakika tutamchagua tu
 
Tangia kuondoka kwa Dr Slaa, Chadema imeacha misingi yake!, sasa hivi kinaongozwa bila kanuni, taratibu na miiko ya chama.

Sasa hivi mafisadi, wachawi, wauza madawa ya kulevya wote watajiunga chadema kwa shangwe na vigelegele bila shida yoyote. !!

Kipindi cha Dr Slaa mtu yoyote mwenye tuhuma za ufisadi na uuzaji wa dawa za kulevya asingeweza kukimbilia chadema.
Wanachagua nadhani. Kweli watampokea Makonda akishatimuliwa CCM?
 
Wema ameenda kwa deal maalum
Wanashindwa elewa CCM kuna WATU wana akili BALAA......hapo tuna mtuma WEMA akachekee na MBOWE vizuri...Then siku mbowe anashtuka hana CHAKE.....WEMA huyo CCM
Wameshindwa elewa kwanini WEMA ameenda CHADEMA mapema hivyo......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom