Cha msingi kama chadema inataka IRUDI vizuri inaibidi ijifunge mkanda kisawasawa kwa kujisafisha na safari hii waondoe ule ukanda ili propaganda zisipate nafasi
Ukanda utaondokaje wakati Kanda zingine Wanachama wenye uwezo hawajitokezi kugombea? Hivi umejiuliza kwenye mikoa ya Kusini, kati, kanda ya Ziwa ni kiongozi gani ambaye unahisi anaweza kuchukua uongozi wa Juu ndani ya CDM? Nipe mfano kwa kuwataja majina.
Pia niambie kwanini ndani ya CCM mawaziri wakuu wengi wametoka Mkoa wa Arusha kuliko mikoa mingine na mingine haijatoa kabisa? Mfano: Sokoine, Lowasa, Sumaye,Msuya
Pia niambie ni Mbunge gani wa kanda nyingine mwenye influence kubwa ndani ya Mkoa, Jimbo ukiacha wale Wabunge wa Kaskazini?
Niambie ni majimbo gani yaliyopo Tz bara ambako mpinzani ameweza kushinda kwa vipindi vitatu mfululizo ukiacha yale ya kaskazini?
Niambie ni kiongozi gani wa ccm au cdm au cuf ambaye ana nguvu kwenye kanda yake akasimama kwenye kugombea Urais na Mkoa wake acha kanda ikamsapoti kwa kumpa KURA nyingi.
Niambie kwanini wakaskazini wamejaa kwenye Ngazi za Juu za serikali, mashirika ya umma na binafsi Tz nzima kushinda kanda zingine?
Kwanini wanasheria wakubwa na maarufu wengi wanat kaskazini?
Na mengine mengi siwezi kuyaorodhesha hapa.
Hivi unategemea Mwenyekiti/Katibu Mkuu wa CDM atoke Dodoma wakati uyo kiongozi hana uwezo wa kushinda hata Udiwani kwa uchaguzi mmoja? Halafu aende kuwaambia watu wa Moshi mchagueni huyu awe Mbunge wakati yeye mwenyewe ameshindwa nyumbani kwake.
Jamani tuache masihara kuongoza chama cha Upinzani Tanzania na kufikia mafanikio ya CDM au CUF ni kazi kubwa sana nakumbuka OSCAR KAMBONA alijitahidi sana kuijenga TADEA Mkoani Ruvuma lakini hakuthaminiwa na kusapotiwa na wana Ruvuma hakuwahi hata kushinda UDIWANI au ujumbe.
Vyama vya Upinzani kutengeneza Ngome sehemu unayokubalika ni kete Muhimu sana na si CDM tu hata CUF wamejikita Pemba, CDM kaskazini na hata ACT wamejikita pale Kigoma.
Cha msingi ni kuwashauri Wasomi na watu wenye uwezo na ushawishi wajiunge na Vyama vya Upinzani au waanzishe na kutengeneza ngome kwenye maeneo yao wanayokubalika.