Wahenga walinena kuwa nyota njema huonekana asubuhi, vile vile pia nyota mbaya huonekana asubuhi.
Chadema tumeweza kufanya haya kwa nchi yetu kwa muda mfupi Sana mara tu baada ya Lowasa kujiunga na chama chetu,.
Hata kabla ya kushika dola chadema tumekuwa na ujasiri wa kuifanyia haya nchi yetu pendwa Tanzania.
1. Kutetea kila aina ya wakwepa kodi
2. Kutetea na kupokea kila aina ya fisadi wa nchi hii
3. Kupinga watu wasilipe kodi.
4.Kutetea wauza madawa ya kulevya na kuwakumbatia kwenye chamá chetu.
5. Kupinga hadharani viroba visifungiwe, hivyo kuhamasisha Viana waendelee kutumia viroba.
6. Kupinga serikali kubana matumizi ,ikiwemo kujenga hosteli za bei nafuu pale UDSM.
7. Kupinga serikali kuzuia safari za nje.
Maana yake sisi tukishika dola, watu watasafiri nje kama wanavyotaka.
8. Kupinga mkandarasi aliyechelewesha kwa makusudi mradi wa maji Lindi asinyang'anywe passport .
Hivyo sisi tukiingia madarakani wakandarasi hata wakichelewesha mradi itakuwa poa tu.
9. Tumeweza kushangilia hadharani kila polisi wanapouawa na majambazi
10. Tumeweza kuwachangia pesa watu wanao tukana matusi mitandaoni ili wasiende jela.
11. Tumeweza kutetea wazembe kazini, na kuwakumbatia wote waliotumbuliwa.
Swali la kujiuliza kama tumeweza kufanya haya kabla ya kushika dola, je tukishika dola itakuwaje??
Haya ndio yatatokea Tanzania ikiwa ccm itaondoka madarakani na chadema kuchukua nchi.