Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
Mfumo wa kuchangisha fedha kwa SMS wazua mjadala
MKAKATI mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa kuanzisha mfumo wa kiteknolojia kuchangisha fedha na kusajili wanachama, utakaokiwezesha kupata mamilioni ya wanachama kupitia simu zao za mkononi, umekitisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuibua mjadala miongoni mwa watendaji wake.
Habari ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM, jijini Dar es Salaam, zilisema kuwa mara baada ya CHADEMA kutangaza kuzindua mfumo huo wa kisasa, baadhi ya watendaji wa idara ya uenezi walijadili kwa kina faida za mkakati huo na kukiri kwamba unaweza kukijenga zaidi chama hicho na kukusanya mabilioni ya fedha za kampeni.
Kwa mujibu wa habari hizo, CCM ilikuwa na mkakati wa aina hiyo ambao ulitarajiwa kuzinduliwa mwakani, miezi michache kabla ya Uchaguzi Mkuu, hivyo walikiri kuwa CHADEMA imewazidi ujanja kwa kuwahi kuzindua mpango huo kabla yao.
Watendaji wa ofisi ndogo tulijadili sana suala hili, kwa kweli kama mpango huo utafanikiwa kwa wananchi kuunga mkono, hakika CHADEMA haitashikika mwakani, alisema mmoja wa viongozi wa idara hiyo kwa sharti la kutotaja jina lake.
Mbali ya watendaji hao, baadhi ya wabunge wa CCM, waliozungumza na Tanzania Daima kuhusu mkakati huo, waliipongeza CHADEMA kwamba imezungukwa na vijana wadogo, lakini wabunifu.
CHADEMA ina vijana wadogo, lakini wana akili na wabunifu. Watu wa aina hiyo ndio wanaofaa kukaa makao makuu ya chama chetu, ila tuna bahati mbaya tumezungukwa na wazee, kazi yao ni kupiga majungu kwa Katibu Mkuu Yusuf Makamba muda wote ili awape pesa, hawana kitu kipya cha kubuni, hii ni dunia nyingine, lazima tuwe wabunifu, alisema mmoja wa wabunge wa CCM kutoka mkoani Mbeya.
Hivi karibuni, CHADEMA iliweka historia ya kuwa chama cha kwanza si tu hapa nchini, bali pia barani Afrika kwa kuanzisha mfumo huo unaotumiwa na vyama vya siasa katika nchi zilizoendelea za bara la Ulaya na Marekani.
Mpango huo unaotumia teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama), ulizinduliwa na Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe aliyechaguliwa tena kuongoza kwa miaka mingine mitano.
Mfumo huo ambao unatarajiwa kuanza kazi wiki hii, utamwezesha pia kila mwanachama wa CHADEMA, shabiki na wananchi wote, kukichangia sh 300 kila mwezi, kusaidia harakati zake za kujiimarisha na kukusanya fedha za kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwakani.
Mbowe ambaye ndiye mwaasisi wa mpango huo, alisema utakiwezesha chama hicho kuwa na oganaizesheni ya kiteknolojia, sambamba na oganaizesheni yake ya sasa ya matawi na vikao vyake vyake vya kichama.
Alisema ili mtu aweze kuichangia fedha CHADEMA na kuwa mwanachama wa chama hicho kama akipenda, itampasa kutuma ujumbe mfupi wa simu yake ya mkononi (SMS), bila kujali aina ya mtandao anaotumia, wenye neno CHADEMA, kwenda namba 15710 na baada ya kufanya hivyo, atakuwa akikatwa sh 300 kila mwezi.
Mbowe alisema baada ya ujumbe huo, mwanaharakati huyo atapewa fursa ya kuwa mwanachama wa CHADEMA kama anapenda na atakuwa akitumiwa taarifa mbalimbali za chama hicho mara kwa mara kupitia simu yake ya mkononi. Akitaka kuchangia zaidi ya sh 300 ndani ya mwezi mmoja, anapaswa kutuma neno CHADEMA mara nyingi atakavyo na kwa kufanya hivyo, atakuwa akikatwa sh 300 kila wakati kadri apendavyo kwa mwezi huo, alisema Mbowe. Kwa mujibu wa Mbowe, chini ya mpango huo, CHADEMA inataweza kuongeza mamilioni ya wanachama kila mwezi kutoka kwenye wanachama 900,000 iliowaandikisha kwa utaratibu wa kawaida wa kadi za uanachama, kwani imelenga kupata angalau watu milioni tatu watakaokuwa
MKAKATI mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa kuanzisha mfumo wa kiteknolojia kuchangisha fedha na kusajili wanachama, utakaokiwezesha kupata mamilioni ya wanachama kupitia simu zao za mkononi, umekitisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuibua mjadala miongoni mwa watendaji wake.
Habari ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM, jijini Dar es Salaam, zilisema kuwa mara baada ya CHADEMA kutangaza kuzindua mfumo huo wa kisasa, baadhi ya watendaji wa idara ya uenezi walijadili kwa kina faida za mkakati huo na kukiri kwamba unaweza kukijenga zaidi chama hicho na kukusanya mabilioni ya fedha za kampeni.
Kwa mujibu wa habari hizo, CCM ilikuwa na mkakati wa aina hiyo ambao ulitarajiwa kuzinduliwa mwakani, miezi michache kabla ya Uchaguzi Mkuu, hivyo walikiri kuwa CHADEMA imewazidi ujanja kwa kuwahi kuzindua mpango huo kabla yao.
Watendaji wa ofisi ndogo tulijadili sana suala hili, kwa kweli kama mpango huo utafanikiwa kwa wananchi kuunga mkono, hakika CHADEMA haitashikika mwakani, alisema mmoja wa viongozi wa idara hiyo kwa sharti la kutotaja jina lake.
Mbali ya watendaji hao, baadhi ya wabunge wa CCM, waliozungumza na Tanzania Daima kuhusu mkakati huo, waliipongeza CHADEMA kwamba imezungukwa na vijana wadogo, lakini wabunifu.
CHADEMA ina vijana wadogo, lakini wana akili na wabunifu. Watu wa aina hiyo ndio wanaofaa kukaa makao makuu ya chama chetu, ila tuna bahati mbaya tumezungukwa na wazee, kazi yao ni kupiga majungu kwa Katibu Mkuu Yusuf Makamba muda wote ili awape pesa, hawana kitu kipya cha kubuni, hii ni dunia nyingine, lazima tuwe wabunifu, alisema mmoja wa wabunge wa CCM kutoka mkoani Mbeya.
Hivi karibuni, CHADEMA iliweka historia ya kuwa chama cha kwanza si tu hapa nchini, bali pia barani Afrika kwa kuanzisha mfumo huo unaotumiwa na vyama vya siasa katika nchi zilizoendelea za bara la Ulaya na Marekani.
Mpango huo unaotumia teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama), ulizinduliwa na Mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe aliyechaguliwa tena kuongoza kwa miaka mingine mitano.
Mfumo huo ambao unatarajiwa kuanza kazi wiki hii, utamwezesha pia kila mwanachama wa CHADEMA, shabiki na wananchi wote, kukichangia sh 300 kila mwezi, kusaidia harakati zake za kujiimarisha na kukusanya fedha za kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwakani.
Mbowe ambaye ndiye mwaasisi wa mpango huo, alisema utakiwezesha chama hicho kuwa na oganaizesheni ya kiteknolojia, sambamba na oganaizesheni yake ya sasa ya matawi na vikao vyake vyake vya kichama.
Alisema ili mtu aweze kuichangia fedha CHADEMA na kuwa mwanachama wa chama hicho kama akipenda, itampasa kutuma ujumbe mfupi wa simu yake ya mkononi (SMS), bila kujali aina ya mtandao anaotumia, wenye neno CHADEMA, kwenda namba 15710 na baada ya kufanya hivyo, atakuwa akikatwa sh 300 kila mwezi.
Mbowe alisema baada ya ujumbe huo, mwanaharakati huyo atapewa fursa ya kuwa mwanachama wa CHADEMA kama anapenda na atakuwa akitumiwa taarifa mbalimbali za chama hicho mara kwa mara kupitia simu yake ya mkononi. Akitaka kuchangia zaidi ya sh 300 ndani ya mwezi mmoja, anapaswa kutuma neno CHADEMA mara nyingi atakavyo na kwa kufanya hivyo, atakuwa akikatwa sh 300 kila wakati kadri apendavyo kwa mwezi huo, alisema Mbowe. Kwa mujibu wa Mbowe, chini ya mpango huo, CHADEMA inataweza kuongeza mamilioni ya wanachama kila mwezi kutoka kwenye wanachama 900,000 iliowaandikisha kwa utaratibu wa kawaida wa kadi za uanachama, kwani imelenga kupata angalau watu milioni tatu watakaokuwa