CHADEMA iitishe maandamano ya shinikizo?

CHADEMA iitishe maandamano ya shinikizo?

JK aliwahi kusema mgao wa umeme utakuwa historia.......sijui kama anaweza kusema haya maneno leo hadharani. Shame on him
Tatizo la JK amemuweka Waziri weak sana pale...hawezi kitu...nafikiri angeondolewa wizarani akawekwa mtu strong tungepata umeme?
 
Wapinzani wa kweli wenye historia ya kuandamana, kupigwa, kuuliwa, kufungwa, kuwa wakimbizi nk ni CUF.

Ushauri wako utakuwa na maana sana kama utaelekezwa kwa CUF, lakini for obvious reasons huna guts hizo kwani hao "hawafungamani na wewe" kwa namna yeyote ile.

Chadema ni sehemu ya CCM umeona lini Mbowe akipigwa walau kibao let alone bomu la machozi na FFU?

Stop beating around the bush, kuna tofauti kubwa kati ya siasa za mwembe Yanga na siasa za kweli.

Kalagabagho!
 
Wapinzani wa kweli wenye historia ya kuandamana, kupigwa, kuuliwa, kufungwa, kuwa wakimbizi nk ni CUF. !


si kweli; ni Mrema ndiyo anahistoria hiyo! Seif alipigwa lini mabomu. Kila kikiungua yeye anakimbilia UK au mahali fulani! lini umesikia Seif kaandamana kupinga lolote?

Kuhusu Chadema though yawezekana uko sahihi. Nasubiri kusikia mwitikio wao Jumatatu na hapo ndipo tutajua kama ni chama relevant au tuwafute katika matumaini ya watu! For sometime now I have been leaning towards the later.
 
Wapinzani wa kweli wenye historia ya kuandamana, kupigwa, kuuliwa, kufungwa, kuwa wakimbizi nk ni CUF.

Ushauri wako utakuwa na maana sana kama utaelekezwa kwa CUF, lakini for obvious reasons huna guts hizo kwani hao "hawafungamani na wewe" kwa namna yeyote ile.

Chadema ni sehemu ya CCM umeona lini Mbowe akipigwa walau kibao let alone bomu la machozi na FFU?

Stop beating around the bush, kuna tofauti kubwa kati ya siasa za mwembe Yanga na siasa za kweli.

Kalagabagho!

Ha ha ha ..... duuh, bonge la dongo....! Hii umeua mazee. Mtu wewe nuksi kweri kweri!! lol
 
si kweli; ni Mrema ndiyo anahistoria hiyo! Seif alipigwa lini mabomu. Kila kikiungua yeye anakimbilia UK au mahali fulani! lini umesikia Seif kaandamana kupinga lolote?

Kuhusu Chadema though yawezekana uko sahihi. Nasubiri kusikia mwitikio wao Jumatatu na hapo ndipo tutajua kama ni chama relevant au tuwafute katika matumaini ya watu! For sometime now I have been leaning towards the later.


Bahati mbaya Seif sio Mwenyekiti wa CUF. Mwenyekiti wa CUF ni Profesa Ibrahim Lipumba ambaye alishiriki maandamano ya January 27 2001, akipigwa na kuvunjwa mkono na Polisi na hatimae kufunguliwa kesi.

Hata hivyo hoja yako inahusu chama kufanya maandamano na sio kiongozi fulani kushiriki maandamano. Kwa muktadha huo chama cha CUF kimekuwa mstari wa mbele katika kufanya maandamano ya kudai haki mara kwa mara.

Chama chako cha Chadema hawana historia hiyo, zaidi ya kufanya maandamano ya kumbukumbu ya kifo cha Nyerere, ambayo washiriki hawakufika hata 100!
 
si kweli; ni Mrema ndiyo anahistoria hiyo! Seif alipigwa lini mabomu. Kila kikiungua yeye anakimbilia UK au mahali fulani! lini umesikia Seif kaandamana kupinga lolote?

Kuhusu Chadema though yawezekana uko sahihi. Nasubiri kusikia mwitikio wao Jumatatu na hapo ndipo tutajua kama ni chama relevant au tuwafute katika matumaini ya watu! For sometime now I have been leaning towards the later.
Nakumbuka hata Prof.Lipumba kachezea sana kichapo cha 'Fanya Fujo Uone'
 
Tatizo la JK amemuweka Waziri weak sana pale...hawezi kitu...nafikiri angeondolewa wizarani akawekwa mtu strong tungepata umeme?


Ngeleja alikuwa mfanyakazi wa RA kule vodacom kabla ya kumpeleka kugombea ubunge Sengerema, alipopata ubunge RA akamwambia Jakaya ampeleke kwenye wizara ya Nishati na Madini ili aweze kufanya vituvyake! Kwahiyo ni nguvu ya RA ndiyo imemuweka Ngeleja pale na sidhani Jakaya kwa hivi sasa mambo yalivyomzidi kama ana ubavu wa kuweza kumtoa huyu kilaza pale! Hili giza totolo tunalo kwa muda mrefu sana ujao.
 
Bahati mbaya Seif sio Mwenyekiti wa CUF. Mwenyekiti wa CUF ni Profesa Ibrahim Lipumba ambaye alishiriki maandamano ya January 27 2001, akipigwa na kuvunjwa mkono na Polisi na hatimae kufunguliwa kesi.

mwanzoni hukusema "CUF" maana yake ni "Mwenyekiti"!

Hata hivyo hoja yako inahusu chama kufanya maandamano na sio kiongozi fulani kushiriki maandamano. Kwa muktadha huo chama cha CUF kimekuwa mstari wa mbele katika kufanya maandamano ya kudai haki mara kwa mara.

vile vile NCCR!

Chama chako cha Chadema hawana historia hiyo,

hicho chama ulinipa wewe!

zaidi ya kufanya maandamano ya kumbukumbu ya kifo cha Nyerere, ambayo washiriki hawakufika hata 100!

kwani kufanya kitu inatakiwa washiriki wafikie wangapi; Ingekuwa wingi ndio kigezo basi CCM inaongoza maana mafisadi waliojazana ndani yake inapita idadi!
 
mwanzoni hukusema "CUF" maana yake ni "Mwenyekiti"!

Hata sasa hivi sijasema "CUF" ni "Mwenyekiti" paragraph ya pili nimesema hivi;


Hata hivyo hoja yako inahusu chama kufanya maandamano na sio kiongozi fulani kushiriki maandamano. Kwa muktadha huo chama cha CUF kimekuwa mstari wa mbele katika kufanya maandamano ya kudai haki mara kwa mara.


vile vile NCCR!

What abt Chadema?

hicho chama ulinipa wewe!

Leo unawakana eeeh!
 
Kushinikiza Dowans itaifishwe, Ngeleja ajiuzulu na kujijenga kisiasa na kiuongozi kuelekea uchaguzi wa mitaa? Wanangojea upendelem gani kwa Mungu au hadi awateremshie magunia ya kura?

Mwanakijiji kwa mara nyingine tena umeonesha Upeo wako wa kupima mambo.....Hichi kitu ulichoandika leo ni "Golden Chance" kwa chama chochote cha siasa cha Upinzani kinachotafuta support ya watu...Viongozi wa Upinzani ni Waoga!!.....Hii peke yake ndio nafasi ya wazi ya kuandamana kwa amani na maandamano hayo yakapata Mwitikio mkubwa wa Wananchi.Wajiandae kuwaambia wananchi watafanya nini ili kuondoa Tatizo hili sugu.

Tatizo hili la Umeme linamgusa kila Mtanzania leo hii...Na kwa kiasi kikubwa Watanzania wameujua Upuuzi wa Viongozi wetu katika kutatua Tatizo la Umeme,kila mtu analalamika hali iliyopo sasa.....Kwa kuwa ni Upuuzi na kutokujali kwa Viongozi wetu...Sioni Tatizo Opposition wakaitumia hali hii kujijenga Kisiasa!

"Kila kitu sasa kinaamuliwa kisiasa,hata issues zinazotaka uamuzi wa kitaalamu zinangoja wanasiasa watoe matamko yao,ndio maana sishangai wataalamu (wasomi) wanataka kazi za siasa ili wakatoe majibu rahisi kwa maswali magumu!"
 
Leo unawakana eeeh!

lini niliwakubali kuwa ni chama changu! the burden of proof is on you! Na ukinionesha mahali popote ambapo nimewahi kukubali kwa kauli yangu moja kwa moja au kuashiria kuwa chadema ni chama changu nitakuomba radhi na kukiri kuzuga watu. Go ahead show the audience that at anytime in the past 4 years I have ever identified myself with Chadema as a political party of my affiliation.
 
lini niliwakubali kuwa ni chama changu! the burden of proof is on you! Na ukinionesha mahali popote ambapo nimewahi kukubali kwa kauli yangu moja kwa moja au kuashiria kuwa chadema ni chama changu nitakuomba radhi na kukiri kuzuga watu. Go ahead show the audience that at anytime in the past 4 years I have ever identified myself with Chadema as a political party of my affiliation.

Hiyo mipovu iliyokutoka hapo juu ni ushahidi tosha kuwa wewe ni Chadema damu.

Unataka ushahidi gani mwingine?
 
Hiyo mipovu iliyokutoka hapo juu ni ushahidi tosha kuwa wewe ni Chadema damu.

Unataka ushahidi gani mwingine?

hahahah.. well. hoja siyo rahisi hivyo.. ni rahisi kutoa madai bila kuweza kuyatetea na badala ya kujibu hoja mtu anabakia kuwa na vihoja.. mimi si mtu wa ghadhabu na siongozwi na vionjo namna hiyo.. I'm a rational being always in control of faculties. I don't lose temper kama hivyo. Ningekuwa mtu kama Makamba au Chiligati labda! -
 
Kama ilivyo rahisi ku drop names like Makamba na Chiligati bila kutetea kwa hoja.

Kweli hoja si rahisi hivyo...
 
Kama ilivyo rahisi ku drop names like Makamba na Chiligati bila kutetea kwa hoja.

Kweli hoja si rahisi hivyo...

hhahaha.. kwamba Makamba na Chiligati ni watu wa jazba mbona halina ubishi sana isipokuwa kwa watu wasiowajua. Well... kwa vile umeshindwa kuonesha mahali popote kuwa mimi chama changu ni Chadema.. inathibitisha tu ni jinsi gani hisia na vionjo vinavyosukuma fikra zako.
 
Nashauri CHADEMA na CUF washirkiane kuandaa wananchi kuandamana kushinikiza hatua za haraka zichukuliwe kuhakikisha mgawo wa TANESCO hauendelei. Vyama vingine vya upinzani vikishiriki,mambo yatanoga zaidi.

Mhe. Zitto ameonyesha katika uchambuzi wake kwamba madhara kwa uchumi kwa jumla yatadhihirika siku za karibuni. Pia kodi ya Serikali itapungua sana. Kwa upande wa huduma za kijamii ni kwamba hospitali nyingi haziwezi kufanya matibabu kama umeme haupatikani kwa hakika. Vyuo vikuu na shule nyingi wanategemea umeme na stand-by generators ni vyombo adimu na aghali.

Wafanyakazi wa viwandani na wajasiriamali wadogo wadogo wenye viwanda kama vya SIDO wengi wanategemea umeme wa TANESCO. Wote wahamasishwe na waelimishwe kwamba ni lazima wachukue hatua sasa kuishinikiza Serikali ili Tanesco wasiendelee na mgawo.

Serikali ina jukumu la kuhakikisha wananchi wake wanaendelea kuishi, na maisha yao yanaboreshwa kama ahadi zilivyotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi.

Serikali huru haiwezi kutishiwa na kampuni kama IPTL, eti hakuna kupata nishati ya umeme hadi hapo kesi itakapoamuliwa. Kampuni hiyo hiyo inategemea mitambo yake ipate ulinzi toka serikalini.

Serikali huru (sovereign) ina jukumu la kulinda na kuhifadhi maisha ya wananchi wake na haiwezi kukubali vitisho vinavyolazimisha uamuzi fulani (ransom). Serikali huru inaweza kuchukua hatua za kidharura kulinda na kuhifadhi maisha ya wananchi wake, hata kama kufanya hivyo kutakuwa ni kinyume na sheria ya kawaida. Hatua kama hiyo itachukuliwa kama ni dharura za kivita, ambapo sheria inaweza kuwekwa kando.

Kwa misingi hiyo IPTL inaweza kuagizwa kuwasha mitambo yake na kuzalisha umeme mara moja, na Dowans inaweza kutaifishwa. Mitambo hii iko nchini na inahifadhiwa na dola. Haiwezi hata kuondolewa nchini bila kuwa na idhini ya serikali.

Vyama hivi vya upinzani viungane vishinikize Serikali ili Watanzania tuepuke madhara na shida zinazosababishwa na mgawo wa TANESCO.
 
hhahaha.. kwamba Makamba na Chiligati ni watu wa jazba mbona halina ubishi sana isipokuwa kwa watu wasiowajua. Well... kwa vile umeshindwa kuonesha mahali popote kuwa mimi chama changu ni Chadema.. inathibitisha tu ni jinsi gani hisia na vionjo vinavyosukuma fikra zako.

Unataka ushahidi gani zaidi ulioonyesha mwenyewe hapo juu? Hakika hili halina ubishi isipokuwa kwa watu wasio kujua.
 
Unataka ushahidi gani zaidi ulioonyesha mwenyewe hapo juu? Hakika hili halina ubishi isipokuwa kwa watu wasio kujua.

mbona mipovu kibao mkuu masatu?

Si utoe tu ushahidi ulioombwa au kuomba msamaha kama vile ulivyomuomba Zitto juzi?
 
mbona mipovu kibao mkuu masatu?

Si utoe tu ushahidi ulioombwa au kuomba msamaha kama vile ulivyomuomba Zitto juzi?

Huo msamaha ni wachache wa kuuamini wasiomjua Masatu. Hiyo ilikuwa calculated preemptive strike dhidi ya Mh. Zitto in favour of Dowans!!
 
Back
Top Bottom