CHADEMA hujafa hujaumbika

CHADEMA hujafa hujaumbika

Philipo Mwakibinga

Senior Member
Joined
May 13, 2013
Posts
110
Reaction score
175
Ikumbukwe Prof. J ni mbunge mstaafu na mpaka sasa ni kiongozi wa Chadema (mwenyekiti wilaya ya Kilosa na mjumbe wa Baraza kuu na mkutano mkuu Taifa)

Sarakasi za Chadema zimepekekea Raia kuhoji mambo mengi sana.

Tena Bora wasingedandia treni mbele labda wasingeibua mijadala inayoendelea mitandaoni

1. Chadema walijiweka kando na Familia ya Jay, ni Kama kumsusa Jay kimtindo.

2. Chadema hawakwenda hata kumuona Jay hospitali. Ni Kama kumpuuza fulani hivi. Jana Jumamosi ndio tumewaona Suzan Lyimo, Kihwelu na Owenya ndio wameenda.

3. Chadema kama chama haijaonyesha namna yoyote ya kumchangia Jay matibabu, walitaka kujificha kwenye kivuli Cha malisa na Gifted heart wakasahau kuwa Malisa ni mwanachama tu na gifted heart ina members wa mirengo tofauti.

Gifted heart wamehimiza michango.

Wasanii wamekusanya michango.
ACT wamehimiza michango
CCM kupitia kwa Katibu Mkuu wake wameenda hospitali kumuona Jay.
Wizara ya afya imempa special care mgonjwa.

Mama Samia ameagiza serikali kugharamia matibabu.

Clouds media na viongozi wa dini wamefanya ibada maalum ya kumuombea Jay.

Chadema imefanya nini? Angalau hata hawa wabunge mnaowaita covid walijichangisha wakapeleka mchango wao kwa mgonjwa.

Kuna wakati huwa tunadanganywa kuwa wanaohama wananunuliwa' kumbe matendo ya viongozi ambayo kimsingi hayaendani na kile wanachokihubiri ndio kinachowakwaza watu. Inauma na kufikirisha sana!
 
Tuchukulie uko sahihi sana na hii ramli chonganishi, Profesa J ameporwa ubunge wake uchaguzi uliopita na yule kiongozi.

Hivyo Prof J alivuta hela yake yote ya kumaliza ubunge 200m. Je amepeleka wapi hela yote hiyo ndani ya mwaka mpaka mumgeuze mtaji wa siasa za kishamba?

Mnadhani mnaichonganisha cdm na wananchi, kumbe mnamuanika profesa J kuwa ni mfujaji wa Pesa. Kama alikuwa anapata 12m@month kwa muda wa miaka mitano, na mkono wa kwaheri wa 200m, iweje ndani ya mwaka ashindwe kujihudumia matibabu yake mpaka ageuzwe muhanga wa siasa za majitaka?

Ni hivi, kama mmegeuza mtaji wa kisiasa profesa J, basi mnamuanika tu kuwa ni mfujaji wa pesa akitegemea kusaidiwa kisa alikuwa mbunge wa cdm.
 
Naona ulikuwa getini muhimbili unawaangalia wanaoingia Uongo umebarikiwa ndio maana TEUZI HUPATI

20211219_102505.jpg


Sent from my SM-J600F using JamiiForums mobile app
 
Uongo unaokuaibisha utakusaidia nini ?
Jibu hoja kwa ushahidi kwamba hicho kinachodaiwa kutofanyika kwa Profesa J ni kweli au uongo kwa kuweka ushahidi sio kusema tu uongo hausaidii.

Wewe ni mmojawapo wa wazushi wazoefu wa kuleta mada za uzushi hapa JF.

Tuthibitishie it is not your own medicine.
 
Tatizo mnafanya siasa Hadi kwenye ugonjwa wa mtu. CHADEMA ilishakusanya million 22 na kukabidhi familia ya profesa j. CCM nayo ikaingia kichwa kichwa kufanya siasa kwenye ugonjwa wa mtu na kujifanya mwema wakati Lissu walikataa kumpa pesa ya matibabu.

Ushauri kwako wewe mpiga ramli unajiita mwakibinga ambaye unajifanya mwana CCM huku umekatwa mkia, kuwa mstaarabu usilete siasa kwenye ugonjwa wa mtu.
 
Mbona CHADEMA ilisha kusanya million 22 na kukabidhi kwa familia ya Prof j. Na pia CHADEMA walituma salamu za shukrani kwa wananchi waliohusika. Tatizo mnafanya siasa Hadi kwenye ugonjwa wa mtu. Mnatafuta Mambo madogo ili muishushe CHADEMA.
Chadema imekusanya wapi? Wakati hizo milioni 22 ni michango ya jumla ya wananchi wote ikiwepo elfu kumi yangu,na tulituma moja kwa moja kwenye namba ya simu ya mgonjwa,wewe wa wapi?
 
Tuchukulie uko sahihi sana na hii ramli chonganishi, Profesa J ameporwa ubunge wake uchaguzi uliopita na yule kiongozi dhalimu aliyeko motoni. Hivyo Prof J alivuta hela yake yote ya kumaliza ubunge 200m. Je amepeleka wapi hela yote hiyo ndani ya mwaka mpaka mumgeuze mtaji wa siasa za kishamba? Mnadhani mnaichonganisha cdm na wananchi, kumbe mnamuanika profesa J kuwa ni mfujaji wa Pesa. Kama alikuwa anapata 12m@ kwa muda wa miaka mitano, na mkono wa kwaheri wa 200m, iweje ndani ya mwaka ashindwe kujihudumia matibabu yake mpaka ageuzwe muhanga wa siasa za majitaka? Ni hivi, kama mmegeuza mtaji wa kisiasa profesa J, basi mnamuanika tu kuwa ni mfujaji wa pesa akitegemea kusaidiwa kisa alikuwa mbunge wa cdm.
Hapa una feli mkuu,
Kuna vitu ni kama sadaka mkuu huwa watu hawatizami mambo ya uwezo,

Mfano ipo misiba ya watu mashuhuri na matajiri wakubwa ambayo imezungukwa na watu wenye uwezo tu lakini bado watu masikini wakubwa wanatoa rambirambi.

Iko michango hutolewa kuonesha upamoja ama ishara ya upendo na sio kama unavyofikiri wewe mkuu.

CDM haipaswi kutizama uwezo wa mgonjwa kwenye hili bali ilipaswa kufanya jambo kwa J ili tu kuonesha upendo kwake.
 
Jibu hoja kwa ushahidi kwamba hicho kinachodaiwa kutofanyika kwa Profesa J ni kweli au uongo kwa kuweka ushahidi sio kusema tu uongo hausaidii.
Wewe ni mmojawapo wa wazushi wazoefu wa kuleta mada za uzushi hapa JF.
Tuthibitishie it is not your own medicine.
Sio wakati wote ni muda wakujibu ujinga.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Ikumbukwe Prof. J ni mbunge mstaafu na mpaka sasa ni kiongozi wa Chadema(mwenyekiti wilaya ya kilosa na mjumbe wa Baraza kuu na mkutano mkuu Taifa)
Sarakasi za Chadema zimepekekea Raia kuhoji mambo mengi Sana. Tena Bora wasingedandia treni mbele labda wasingeibua mijadala inayoendelea mitandaoni
1.chadema walijiweka kando na Familia ya Jay, ni Kama kumsusa Jay kimtindo.
2.chadema hawakwenda hata kumuona Jay hospitali. Ni Kama kumpuuza fulani hivi. Jana jmos ndo tumewaona suzan lyimo, Kihwelu na Owenya ndo wameenda.
3.chadema Kama chama haijaonyesha namna yoyote ya kumchangia Jay matibabu, walitaka kujificha kwenye kivuli Cha malisa na Gifted heart wakasahau kuwa malisa ni mwanachama tu na gifted heart ina members wa mirengo tofauti.
:::Gifted heart wamehimiza michango.
Wasanii wamekusanya michango.
AcT wamehimiza michango
Ccm kupitia kwa Katibu Mkuu wake wameenda hospitali kumuona Jay.
Wizara ya afya imempa special care mgonjwa.
Mama Samia ameagiza serikali kugharamia matibabu.
Clouds media na viongozi wa dini wamefanya ibada maalum ya kumuombea Jay.

Chadema imefanya nini? Angalau hata hawa wabunge mnaowaita covid walijichangisha wakapeleka mchango wao kwa mgonjwa.
Kuna wakati huwa tunadanganywa kuwa wanaohama wananunuliwa' kumbe matendo ya viongozi ambayo kimsingi hayaendani na kile wanachokihubiri ndio kinachowakwaza watu. Inauma na kufikirisha Sana!
Unadharirisha wanyakyusa. Huwa hawana sifa ya unafki, kujipendekeza ni wapenda haki.

Ni Wacha Mungu
 
Back
Top Bottom