CHADEMA hawajakaguliwa! #FACT


Ninatumaini mwisho wa yote tutaupata ukweli. Hivi CAG na Msajiri walikuwa hawaijui sheria hii. Kwa nini hawakuitekeleza mpaka Kamati ya Bunge ipige kelele. Kwa maelezo ya Zitto wawili hawa walikuwa na woga, je wafikiri walikuwa wakimwogopa nani hasa, ambaye ana nguvu juu yao?
 
Chadema ni chama kinachoendeshwa katika misingi ya kilaghai. Lengo kuu la Chadema ni kupata fursa ya kushika dola ili watafune mali ya umma.
Outdated single.

Umekua kasuku. Tangu lumumba wakukaririshe hiyo singo ndio basi tena.
 
Ndio nimesoma magazetini ila swali langu ni: ukaguzi huo uliendeshwa na nani? Maana mkaguzi ni CAG na anasema hajakagua chama hata kimoja. Inamaana ni internal audit na sio audit inayo pendekezwa na art 14. Au?
Sasa wewe mvunjaungo Mwali, kama CAG hajakagua hivyo vitabu vya hesabu vya CHADEMA kosa ni la nani hapo.

Umeambiwa Chadema walishapeleka hesabu zao kwa msajili, then msajili wa vyama ndio alitakiwa ku facilitate huo ukaguzi through CAG. Hakufanya hivyo. Mbona humlaumu, umekazania Chadema tu.

Na msimamo wa chadema unataka vyama vyote vikaguliwe hesabu zote sio ruzuku tu.

Vipi kuhusu ccm ambayo bado haijapeleka hesabu zake hata huko kwa msajili tu, unaizungumziaje.

Can you balance your propaganda by giving answers to those questions?
 
Last edited by a moderator:

Tembelea thread hii hapa:-

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-msajili-na-cag-wawajibike-9.html#post7596177
 

Sheria nayo inachanganya. Vyama vya siasa vinatakiwa kuwasilisha mahesabu Yao yaliyokaguliwa kwa Msajiri. Anayakagua ni CAG! Kawaida ni kuwa unawasilisha Statement of Accounts kwa Mkaguzi ili azikague. Akishakagua anawasilisha kunakotakiwa - kwa serikali anapeleka kwa Rais anayewasilisha Bungeni. Nilifikiri kwa vyama vya siasa isingekuwa tofauti sana, angeziwasilisha kwa Msajiri ili awapelekee akina Zitto.

Inawezekana mchanganyo huu ndio unasababisha matatizo. Hakuna sehemu katika sheria hiyo inayowataka kupeleka mahesabu kwa CAG, ila tu kwamba wapeleke mahesabu yaliyokaguliwa naye kwa Msajiri. CAG naye hajaona umhimu wa kufuatilia na kuweka utaratibu mzuri wa jinsi ya kufanya ukaguzi huo. Hivyo basi kwa maoni yangu, Msajiri na CAG wanahusika zaidi na udhaifu huu kuliko hata vyama vya siasa.
 
Mwita Maranya haya mambo waachie wataalamu wewe nenda mtaa Ufipa ukahesabu misukule iliyosaini leo katika kitabu cha mahudhurio

Unawrza kuitaja hiyo misukule japo mitano tu@ Mingoi
 
Last edited by a moderator:
hapa ni sawa na stori ya mzazi mwalimu na mwanafunzi ....yale yale madudu...

cag anatakiwa akaguwe mahesabu ya mashirika yote pamoja na vyama vya siasa hajafanya
 

kumbuka kwa mawazo yangu, CDM waliwasilisha kwa CAG proper books of accounts, internally audited, kwa msajili, ili sasa, kupata maelekezo namna gani watakaguliwa na CAG na utaratibu wa malipo. haya yangefanyiwa kazi na Tendwa ina maana hatua ya kukaguliwa na CAG ndiyo ingefuata. Je hatukumbuki mara nyingi msajili aliyepita Tendwa alikuwa anatishia kukifuta CDM, unadhani kk hali ya kawaida angewatendea haki katika mambo ya msingi kama haya? je mmesahau hata CDM walishawahi kusema hawana imani naye, je mliwahi kuwauliza kwann? mie kama mwananchi naona hili lilikuwa limewkwa kama bomu kutafuta kuidhoofisha CDM kwa wakati huu

ukweli utabaki pale pale, Msajili wa Vyama ndiye huwasiliana na CAG/polisi/wengineo kupata maelekezo kuhusu jambo la vyama vyote kisha msajili kuviandikia vyama kuvijulisha suala na jinsi ya kulitekeleza

haya tuwaachie wenye vyama
 


Mkuu, nakubaliana na wewe 100%. Ndo maana nikasema kuwa, kuwasilisha mahesabu kwa Msajiri wa vyama si kuwa ndo hesabu zimekaguliwa (FACT). Pia, ni kweli, hili ni la CAG kueleza kwa nini hajakagua hizo hesabu!.
 
...samahani, mimi nilidhani wanaokagua wamesomea kazi yao? una maana wakaguzi ni aina ya NasDaz?
Issue ni kwamba utakagua vipi michango wakati hufahamu ilikusanywa kiasi gani?!! Sasa kama hufahamu mapato ni kiasi gani, utakagua vipi hata kama una wewe ni GWIJI wa Ukaguzi wa Hesabu? Kuna receipts zinazotolewa kwenye mikutano ya kisiasa pale wanachama na mashabiki wanapochangia vyama vyao?
 
...sasa si wakague ndio watueleze hayo unayoyasema? kwa hiyo unataka ruzuku zote zisikaguliwe kwa sababu michango haina receipts? wataalam wanajua jinsi ya kuriport vitu visivyo na receipts na watatoa recommendations zao what to do in future.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…