CHADEMA dhaifu dhidi ya CCM mpya na imara!

CHADEMA dhaifu dhidi ya CCM mpya na imara!

ACHANA TUU NA KUTOMALIZA HUO UDAKTARI BINGWA WA NUSU KAPUTI, NA HATA KWENYE MIGOMO YA MADAKTARI HAKUWA NA USHAWISHI WOWOTE, NASHANGAA MBOWE NA JINA LAKE LA MFUKONI, KINGUNGE YUKO WAPI MBONA HAMKEMEI MWENYEKITI WAKE ALIEKUJA NA JINA LA MFUKONI , TENA JINA AMBALO HALINA USHAWISHIIII WOWOTE! CHADEMA CHAMA KINACHOKUFAAA! NOO- KILICHOKUFAAA , MAANA KINAJIFICHA KWENYE KICHAKAA KIMOJA KINAITWA UKAWA!!!
 
chadema wanateua mtaalamu wa migomo wanadhani ndiyo tiba wakumbuke watanzania wanataka maendeleo siyo migomo.

Lakini tukumbuke kwamba watanzania tumekua tukikubali kila kitu hata kama sio sahihi na kusababisha mikataba mingi ya kifisadi, uhujumu uchumi uliokithiri na watuhumiwa wengi kutochuliwa hatua stahiki. Haya ni madhara ya utamaduni tulijengewa kukubali kila kitu hata kama sio sawa .

Tumekosa ujasiri wa kusimamia haki kwa hofu tuliyojengewa na mfumo m bovu.
 
Wasalaam...

Kwa furaha kabisa napenda kusema kuwa mimi nilikuwa PRO CDM au PRO Slaa kabla ya gia za angani kupanguliwa.


Nasikitika sana kuona Gia za Angani zilivyopelekea maafa makubwa ya kisiasa ya Chama cha upinzani kilichovumilia mikikimikiki mikubwa kutoka kwa CCM kwa miaka takribani 20 lakini kikaufyata mkia ndani ya kipindi cha chini ya mwezi mmoja kwa mwanaCCM aliyekatwa na CCM.

Hayo ni masikitiko ya wengi hasa hasa kwa wale wanaoitwa Chadema Asilia.

Uteuzi wa katibu mkuu wa 'MAJARIBIO' wa Chadema ni kituko kingine cha kisiasa nchini baada ya kile cha kupokea yule aliyeimbwa kama fisadi na kumfanya kuwa mgombea wao,Namuita katibu mkuu wa majaribio kwa kuwa ni wazi ndani ya kipindi cha muda mfupi tu mwenyekiti Itabidi arejee tena akiwa na jina la katibu mkuu haswa mwenye haiba,weledi,uzoefu,ushawishi na msimamo unaoendana na ukatibu mkuu sio tu wa chama cha siasa bali wa Chama cha siasa kinachoendesha siasa za kiharakati.

Ni katibu mkuu wa majaribio kwa kuwa kasi iliyofikiwa na Chadema kipindi Dr Slaa akiwa katibu mkuu ilikuwa ni kasi yakipekee...ilikuwa ni kasi iliyowaamsha CCM na kuja na operesheni vua gamba....ilikuwa ni kasi ya kufa mtu iliyofanya CCM ibadili safu za uongozi....
ilikuwa ni kasi ya ajabu iliyomfanya Kinana na Nape waanze utalii wa ndani!!

Kiufupi naweza kusema Dr Slaa ali-set standards ndani ya Chadema kiasi cha kuanza kuona makatibu wakuu wa Chadema wakiongea ama wakitenda mithili ya Dr Slaa.

Inawezekana Mbowe amemuweka katibu mkuu kwa jicho la ukanda yaani akijaribu kuiteka kanda ya ziwa....ingawa aliyemuweka hana ushawishi wowote katika kanda hiyo.

Inawezekana Mbowe amemuweka Msomi ili avute wasomo lakino pia ni ukweli usiopingika kuwa jamaa hana ushawishi kwa wasomi wa kada yake,hana ushawishi wa kitaasisi ya usomi mithili ya alivyo Baregu au Kitila Mkumbo.

yaani CV yake inataka kulazimishia usomi wakati sio msomi kihivyo!...Nimepenyezewa kuwa hata huo udaktari bingwa alioundika kwenye CV yake hakufanikiwa kuumaliza(MMED ANAESTHESIOLOGY)

Chadema imepiga gia nyingine ya anga na itaangukia pua kama ilivyoangukia pua oktoba 2015.

Kwa bahati mbaya sana wakati Chadema inafanya majaribio ya SG ,CCM inazidi kubebwa na jeshi la mtu mmoja ambaye ni mwenyekiti mtarajiwa JPJM.

Yaani ungeniuliza ni kipindi gani chadema walitakiwa kufanya majaribio basi ningesema ni vipindi vyote ila isiwe kipindi hiki cha Magufuli.

VIATU VYA DR SLAA HAVIVALIKI!!!!

Sasa pilipili ya shamba inakuwashia nini??Kama CDM inakufa kwanini usiende kushereheka??
 
Hii inaonyesha ni jinsi gani CHADEMA haina viongozi wenye mvuto nje ya kanda ya Kaskazini.

Mbowe alikuwa hana ujanja mwingine zaidi ya kupata mtu ambaye hatoki kanda ya Kaskazini ili kupunguza dhana iliyojengwa kuhusu CHADEMA

Fikiria Mbowe ameangaza kote na akaona huyu ni bora kuliko waliopo.

Huyu Katibu Mkuu anafaa kuwa mkuu wa kitengo ndani ya CHADEMA lakini sio Katibu Mkuu.

Kwako wewe hana mvuto kwa wlaiomteua anawafaa.Kaa mbali na huyo jamaa humuwezi.Yale majina yenu mliyojipangia naona yamewafanya muweweseke sana.Poleni sana.
 
chadema wanateua mtaalamu wa migomo wanadhani ndiyo tiba wakumbuke watanzania wanataka maendeleo siyo migomo.
Vicent anazidi kupata wapinzani kila kona. Nasubiri kwa hamu maoni ya Tundu Lissu

Labda kwa wanaccm lakini waliomchagua wamemkubali.NAjua Lizabon kichwani kwako ulimuweka Sumaye na Marando nk nk,jina lilivyokuja umekuwa mdogo kama piriton.Jamani waachieni wenyewe.Nyumba yao ikibomoka nyie inawahusu nini??

Wanasema adui usimuombee njaa bali maisha marefu ili aone utakavyobarikiwa,mie nadhani mngeiombea CDM maisha marefu ili tuone ukomavu wa CCM.

Kwa mlipofikia mnatia aibu
 
Yaani huyo katibu mkuu wa Chadema anaweza kupelekwa puta na Shaka A Shaka yule wa UVCCM
Hat hivyo umesema kweli katika andiko lako...ni dhairi ulikuwa shabiki wa mtu siyo chama na ndiyo maana unafikiri kuwa CCM imeimarika kwa sababu ya mtu mmoja! Halikadhalika nafikiri sasa siasa za kiuanaharakati za Slaa hazitafua dafu kwa sababu CCM "wameshazijulia" na ukitaka angalia uteuzi wa watendaji wa jeshi la mtu mmoja - ni mwendo wa uanaharakati ndani ya utendaji. Uongozi si kujulikana kwa jina bali kujua kujenga mfumo na kuwatumia watu kuteñda.
 
Baba wa familia, ukivamiwa nyumbani kwako utajitutumua kuitetea familia yako hata kama mvamizi kakuzidi nguvu. Kama ukishindwa na kukaa kimya maana yake familia yako haitakuamini tena kama mtetezi wao. Chadema imeshindwa kabisa kujitetea yenyewe pale viongozi wake wote walipowekwa ndani bila kujali kama ni waheshimiwa wabunge. Chadema wamezidiwa akili hata na walemavu ambao haki zao zikichezewa wanalala na kufunga barabara mpaka kieleweke. Sasa kama chama hakiwezi kujitetea chenyewe kitawezaje kutetea haki za watanzania wenye Imani nacho…..very strange .... Chadema siyo chama
 
Ni chama chenye busara sana. Tutaandamana muda sahihi utakapofika sio anapotaka magu.
 


Yeah! Chadema siyo chama.

Next!

Baba wa familia, ukivamiwa nyumbani kwako utajitutumua kuitetea familia yako hata kama mvamizi kakuzidi nguvu. Kama ukishindwa na kukaa kimya maana yake familia yako haitakuamini tena kama mtetezi wao. Chadema imeshindwa kabisa kujitetea yenyewe pale viongozi wake wote walipowekwa ndani bila kujali kama ni waheshimiwa wabunge. Chadema wamezidiwa akili hata na walemavu ambao haki zao zikichezewa wanalala na kufunga barabara mpaka kieleweke. Sasa kama chama hakiwezi kujitetea chenyewe kitawezaje kutetea haki za watanzania wenye Imani nacho…..very strange .... Chadema siyo chama
 
Wewe ni bwege kuliko bwege wote niliowahi kuwasikia! Na ni mchochezi pia!
Zito Kabwe anazunguka akifanya mikutano Manyara na kwingine lakini hawekwi ndani.
Wewe unachochea hapa ukitaka Mbowe afurukute kama mkuu wa kaya ili wapate chance ya kumakwilina???
Ndiyo maana ya kuleta uchokozi?
Nyie mnadhani kuwa watu wanawapenda sana lakini ukweli ni kwamba hasira zimewafika wengi kooni. So you better shut up!
 
Kumbe unadhani ukionea watu kwa kuwa wewe ni rais basi utaonekani hodari sana mbele ya watu?
Mark my words. It is just the opposite. Ni rais mwoga ambayw labda hata hakushinda kura ndiyo anafanya hayo!!!!
 
Mbona mnaogopa kucheza fair play......mikutano,mandamano mnafanya nyie tu wenzenu wakifanya mnawasweka ndani...
Hapo muoga nani sasa?

Ova
 
Serekali inawalazimisha viongozi wa chadema waunge mkono maandamano hilo mbowe kashaliona kimyaa kinamaana kubwa...

Subiri 264 ipite mtisikia matamko ya chadema.
 
Back
Top Bottom