Tatizo kubwa mtu akishazoea MAKESI KESI, basi hata jambo ambalo ni la kimsingi yeye ni kwenda mahakamani tu kufanya KESI.Wanabodi
Declaration of interest. Paskali sio mwanachama, mfuasi, mshabiki wa chama chochote cha siasa, bali ni Mtanzania Mzalendo wa nchi yake anayetanguliza mbele maslahi ya taifa kwa kutoa mawazo, maoni na mapendekezo yake freely kwa ukweli daima bila kujali ukweli huo utamfurahisha nani au utamuumiza nani, kwa sababu ukweli ni ukweli tuu na utasisima mpaka mwisho.
Naomba kukiri kupandisha bandiko hili kutokana na bandiko hili
Kiukweli kama hili litafanyika, Chadema kitakuwa ni chama cha ajabu sana! . Kinapeleka mahakamani issue ndogo ambayo sio issue kabisa ya kisheria bali ni kikanuni tuu!, lakini kumetokea very serious issues za kukanyagwa kwa katiba ambako ndiko haswa kungehitaji legal interpretation Chadema inakupiga kwa kuunda UKUTA na kuhamashisha mandam ano na mikutano nchi mzima!.
Spika is right, kati ya wabunge 9, watatu ni wanawake. CCM ina nafasi 6 imepeleka wanawake 6 na wanaume 6. Opposition wana nafasi 3, walipaswa kupeleka wagombea angalau 6 ambapo 3 wanaume, 3 wanawake.
Hata kama kati ya nafasi 9 za Tanzania wanawake ni watatu na tayari CCM inao wanawake watatu, wanaochagua wabunge wa EALA ni Bunge la JMT na sio CCM, hivyo hiyo haki ya female represention lazima ionekana kwa vyama vyote ili wabunge wa Bunge la JMT wawe na choice to choose from all parties na sio kulazimishwa kuwakumbatia wagombea wa CCM.
Nadhani Chadema wanamtegemea sana Lisu kwenye legal interpretation, yes Lisu ni mwanasheria mzuri, nguli na mbobezi ila sio mzuri saana kivile kwenye kanuni, udhaifu wa Lisu ulionekana wakati wa muswada wa katiba aliwaingiza chaka opposition wote kama nilivyo eleza hapa
Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!
Hivyo kama ndiye aliyewashauri Chadema waende mahakamani kupinga uchaguzi wa EALA wakati uchaguzi ni leo, the anawaingiza tena chaka.
The best thing to do kwa Chadema ni kufuata tuu sheria, taratibu na kanuni, kwa Chadema kurekebisha makosa katika muda waliopewa.
Japo ni kweli Mahakama ndio chombo rasmi cha kutoa legal interpretation nchini Tanzania hivyo Chadema kinaitumia haki hiyo, kwanza wakamilishe taratibu na kanuni za kibunge kwa kufuata maelekezo ya Spika wakati wakijaribu kusimamisha uchaguzi huo mahakamani, kwa sababu uwepo wa wagombea kutoka Chadema sio prerequisite ya kufanyika kwa uchaguzi huo.
Mahakama haitausimamisha uchaguzi huo kwa respect ya the principles of separation of powers kutoingilia Mhimili wa Bunge, na hata wakiusimamisha , bado uchaguzi utafanyi kwa Mhimili wa Bunge hautakubali kuingiliwa na Mahakama, hivyo Chadema wata loose big time.
Hawajifunzi kwa CUF ambao ni loosers, CUF walipotangaza kususia uchaguzi wa marudio Zanzibar walidhani uchaguzi ungeshindikana, amini usiamini saa hizi Maalim anajuta, anautamani hata ule umakamo! .
Kiukweli Chadema ni chama cha ajabu sana, kinakimbilia mahakani kutafuta legal redress kwenye trivia issue ndogo tuu za kanuni, halafu very serious issues kama kuvunjwa kwa katiba na rais wa JMT, wao ndio wana deal nayo kwa kuunda UKUTA na kupanga maandamano na mikutano nchi nzima?!.
Katiba imetoa uhuru kwa vyama vya siasa kukutana na kufanya mikutano ya kisiasa. Ametokea mtu aliyeapa kuilinda katiba lakini akaikanyaga. This is very serious allegations ambazo ndizo zingehitaji haswa a legal redress, kutoka kwa mabingwa na wabobezi wa sheria.
Nilijitahidi kutafuta Gwiji wa Sheria na Katiba, Prof. Issa Shivji, Agoma Kuzungumzia Dhana ya Udikiteta/Uvunjifu Katiba!
Chadema walipounda UKUTA kupinga udikiteta, niliwauliza hivi katiba ikikiukwa solution yake ni kufanya maandamano na mikutano? .Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!
Mwaka 2014 wakati tukisubiria uchaguzi wa 2015, niliwahi kutoa ushauri wa bure kwa Chadema kuhusu udikiteta CHADEMA Ikipewa Nchi, October 2015, Hakuna Hatari Kugeuka Utawala wa Kidikteta? Nauliza Tuu!
Halafu watu kama hawa ndio watujie ile 2020 kuwaomba Watanzania wawakabidhi nchi?!.
Pia nilishauri
Kuelekea 2015: CHADEMA Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!
Uchaguzi wa Mwaka 2015 Chadema ilikuwa ina stand better chances kuchukua nchi only if Chadema wangezitia hili
Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target, Adui Mkubwa sio CCM Bali ni .....!
Hivyo wote wenye matumaini ya mageuzi Tanzania, wana very high expectations na Chadema, as a leeder on opposition atakaye kwenda kuipumzisha CCM, lakini unfortunately and very sad kwa nchi yetu Tanzania, Chadema ina wa let down kwa issues kama hizi za kijinga kijinga zinazoipotezea muda Chadema kushinda mahakamani kufunga na kufungua, 2020 hiyo hapo.
CCM iliishachokwa siku nyingi, kuna watu kibao wangependa kuipiga chini CCM hata kesho, wakiwemo CCM wenyewe, tatizo ni waikabidhi nchi kwa nani? .
Tanzania bado hatuna kabisa a serious opposition ya kuiangusha CCM 2020, hivyo kwa Watanzania wengi hata 2020 wataingia kwenye uchaguzi wakiwa faced na two choices, in between the two devils, you choose the lesser! .
Niliwahi kusema mahali kuwa CCM ni li zimwi na Watanzania wengi wanajua wakiwemo wana CCM wenyewe, lakini unapokuwa faced na mazimwi mawili, unachagua zimwi likujualo, better a devil you know than you don't know, sasa kama mambo ya Chadema ndio kama haya kwenye mambo madogo madogo, tutegemee nini 2020? .
Nawatakia Bunge jema.
Jumanne njema.
Paskali
Kwa lugha nyingine mtu huyo hu enjoy MAKESI.
Prerequisite ya kiongozi mzuri ni UTULIVU before he acts or reacts for that matter.Na si KUKURUPUKA na kukimbiza mambo. Acha tusubiri kesi!