CHADEMA chama bora mwaka 2008: Tujifunze toka kwao

- CCM ooha Chadema, taifa linakwenda chini mkuu kuna hoja muhimu za taifa sasa hivi badala ya hizi nyepesi nyepesi!, hivi umesikia kwua kuna wanafunzi wengi wamepasi primary lakini hawana shule za kwenda form one?

Hapa FMES umezungumza point kubwa sana. Inasikitisha kusikia maelfu ya watoto wa Kitanzania ambao wamepasi mitihani yao ya darasa la saba lakini kutokananna upungufu wa madarasa hawataendelea na masomo yao ya secondary. Idadi ya watoto hawa kwa nchi nzima inaweza kuzidi 300,000 hawa no watoto wengi sana kuacha wazagae hivi hivi tu.

Wakati huo huo tunaachia 'wawekezaji' wachukue 97% ya rasilimali zetu!!! Mimi kwa maoni yangu yale mabilioni ya EPA kama kweli yamerudishwa basi yaelekezwe katika kujenga madarasa na kuwaendeleza waalimu katika mikoa yote ya nchi yetu ili tusisikie tena hili la maelfu ya Wanafunzi wa shule za msingi waliopasi wanakosa nafasi za kuendelea na masomo kutokana na ukosefu wa madarasa. Huu ni uzembe wa hali ya juu sana.
 
Dr Slaa, nimefurahi kukuona hapa ukumbini ukisoma michango mbali mbali katika hii thread. Naomba pia kama inawezekana utwambie nini kilichojiri mpaka mkapoteza mgombea wenu Mbeya vijijini. Yalikuwa ni makosa tu ya kibinadamu au kuna uzembe ambao ulitokea mahali. Je, CHADEMA itajiandaa vipi kuhakikisha makosa kama hayo au mengineyo ambayo yanaweza kusababisha wagombea wenu kutoruhusiwa kushiriki katika chaguzi za siku za usoni.

Shukrani.
 
Ndugu yangu Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu

Umetoa mawazo mazuri lakini nadahni swali lako kuhus uteuzi wa wabunge wa viti maalumu ni vizuri ukaangalia katiba ya CHADEMA. Nijuavyo mimi ni kuwa suala hilo walishalijadili sana ndani ya chama na hata kufanya mabadiliko ya katiba kuhusiana na hilo….

Kuhusu maamuzi ya matumizi na mikopo sidhani kama kuhusisha wanachama wote inawezekana na kama feasible. Kuna baadhi ya majukumu ya kiutendaji yanapasa kushughulikiwa na sekretariati kwa ajili ya ufanisi. Wanachama wanakuwa na nafasi ya kuchagua viongozi na kupitisha sera na kwa kupitia viongozi waliowachagua ndio wanapaswa kuhusika katika utekelezaji wa sera na maazimio yaliyoptishwa na viongozi waliowachagua…

Nakubaliana nawe kabisa suala la kupanua wigo wa ushirikiano wa vyama hadi kwa wanachama. Itakuwa vizuri kama hivi vyama vitakuwa vinafanya mikutano ya pamoja. Hii itasaidia sana kujenga kuaminiana kati ya vyama hivi kuliko kuacha hili kwa viongozi pekee ambao ni ama hawaaminiani ama wanaoneana wivu…..

Tanzanianjema

Ninapozungumzia wanachama si maanishi wote waitwe kwa pamoja kwenye maamuzi lkn kuwe na protocal ya kujadili kwa mfano matawini then wanatuma kwamba wao wanataka nini kupitia wawakilishi wao.Hiyo ndiyo demokrasia.
Mfano swala la kutumia helicopter kwenye chaguzi lingefaa lijadiliwe mapema na wanachama matawini kabla uongozi wa juu hawajaamua kwani uchaguzi upo kwenye kalenda na si swala la kukurupuka,hivyo kama kuna mpango wa kutumia helicopter na kukopa fedha wanachama ni vyema wakajulishwa mapema na wakapewa fursa kujadili kwenye ngazi zao na kupeleka maamuzi yao kupitia wawakilishi na hili litapanua wigo wa uwazi ktk uendeshaji chama.
 
Tuweke VIGEZO ambavyo vitatuongoza katika kupima ni CHAMA kipi BORA kwa mwaka 2008. Baadhi ya vigezo hivyo ni:
1.Demokrasia ndani ya CHAMA kwa mujibu wa KATIBA yao na ya NCHI;
2.Uongozi wa pamoja;
3.Siasa na SERA za CHAMA husika na utekelezaji wake;
4.Ulinzi na usimamizi wa rasilimali za CHAMA na za NCHI;
5.Ukuaji wa CHAMA katika Nchi.
 
Wildcate,
Mkuu chama bora ni kile kinachotetea maslahi ya taifa..Ni kile kinachowakilisha mawazo ya wananchi walio wengi. Ni kile kinachopanga sera zake kwa manufaa ya taifa na sio ndani ya chama. Ni kile kinachotukuza uhuru na amani kwa wananchi wake na kuwapa tumaini la maisha bora..

Hivyo uimara wa chama ndani ya majengo yao haiwezi kuwa mfano bora kwetu kwa sababu hizi ni sifa za Udikteta...tawala zote za madikteta ndizo huwa na sifa za lazima kwa kutumia maguvu inabidi wananchi wakubali. Ni wakati wa saadam tumeona wananchi wakimchagua kwa kura asilimia 90, ni wakati wa Ujamaa tumemchagua Nyerere kwa kura asilimia 99 kwa sababu mfumo mzima ulijengwa kumtazama mtu mmoja asiyekuwa na mshindani...
 
MkamaP,
nadhani Eric amekujibu vizuri labda mimi nifafanue zaidi.
Aloyafanya Kikwete ni kinyume cha matakwa ya wanachama au chama CCM.. Kuna watu wacheche sana wanaounga mkono Kikwete ktk maswala yote ikiwa ni pamoja na swala la Lowassa, kuvunja baraza la Mawaziri, Kuwapeleka mahakamani kina Jeetu, Mramba na Yona..Kila siku tunaona michango ya watu humu wakilaani kukamatwa kwa hao na wengine..
Kwa hiyo kama maswala haya yote yangepigiwa kura ndani ya chama Kikwete angeungana na watu wachache sana niliowataja hapo nyuma..

Wakati maswala yote yanayohusiana na Zitto pamoja na Dr. Slaa ni maswala ambayo kwanza yamepitishwa na chama mbali na kuwakilishwa na watajwa hao..kifupi mambo yote yaliyofanywa na Zitto, Dr. Slaa Mnyika na wengine yamepata baraka za chama na pengine sio watu waliokuwa nataarifa za awali isipokuwa wamependekezwa kusimamisha hoja Bungeni..Kumbuka tu Chadema ina wabunge watano (5) tu wa kuchaguliwa na kati yao wawili ni mfano mzuri wa nini wabunge wanatakiwa kusimamia..

Kisha swala hapa ni swala la mwaka hadi mwaka. Hili sio swala la Ushindani kama Simba na Yanga kiasi tuseme timu bora ni ile iliyochukua kombe! Hakuna mashindano ya mwaka.. labda hizo chaguzi ndogo nazo pia sio ubora wa chama..Tunazungumzia Ubora wa chama kulingana na mazuri waliyoyafanya kama chama mwaka 2008...
Kwa mfano, Ukitazama mapungufu yaliyoandika mkuu Kazi ndio kipimo cha Utu.. utagundua kwamba ni mapungufu ambayo yapo vyama vyote..Hakuna kasoro hata moja aliyoitaja ambayo huwezi kuikuta CCM, CUF, NCCR au vyama vinginevyo..

Mkuu Mkandara, sidhani kuwa una data zozote zinazoonyesha kuwa Kikwete haungwi mkono na wenzake ndani ya CCM katika kushughulikia mafisadi. Nasema hivyo kwasababu sijasikia kauli zozote za wanachama wake wakipinga jitihada hizo zaidi ya zile zinazounga mkono.

Mimi ningeunga mkono hoja ya CHADEMA kuwa chama bora zaidi kama hoja ingeainisha mafanikio kwa mapana zaidi. Kama ingetolewa tathmini ya idadi kubwa ya uungwaji mkono (kwa kupata wanachama zaidi) ama kuonyesha makisio ya maandalizi yanayoeleweka zaidi kuhusiana na jinsi wanavyotegemea kushinda chaguzi zijazo. Nimesikitishwa kusikia kuwa mgombea wao Mbeya ameshindwa kula kiapo kama inavyotakiwa. Hiyo inadhihirisha tu kuwa hawako tayari kushinda chaguzi kama lilivyo kusudio la kuundwa kwa chama hicho.

Siamini kuwa kazi ya Chama cha siasa ni kuisimamia serikali. Maamini kuwa kazi yake ni kupata wanachama wengi iwezekanavyo na kushinda uchaguzi kila inapotakikana. Nadhani ndio maana wachangiaji wengi wanashindwa kukubaliana na hoja kuwa CHADEMA inastahili kuwa chama bora zaidi kwa mwaka 2008. Operation za CHADEMA sio mafanikio, ni jitihada. Matokeo ya jitihada hizo ndio zinazoweza kuwa mafanikio.

Nakubali kuwa CHADEMA imetoa msisimko mkubwa kulinganisha na vyama vingine vya upinzani kisiasa katika kipindi husika (mwaka 2008). Ila hiyo haitoshi kukipa nafasi ya ubora kuliko vyama vyote (CCM ikiwepo).

Bado jitihada zinahitajika kukifanya kiwe bora zaidi. Ushindi uko kwenye kura. Na wananchi ndio waamuzi. Kazi kwenu wana CHADEMA.
 
- Mkuu Tanzanianjema, naona kabla sikaujibu hapa Mkulu Balatanda, ameniwahi na kukupa darasa zito sana, kwamba tuache uyanga na simba maana taifa linadidimia hata ubingwa wa EAC tu unatushinda lakini tunalilia yanga ohhh simba,

- CCM ooha Chadema, taifa linakwenda chini mkuu kuna hoja muhimu za taifa sasa hivi badala ya hizi nyepesi nyepesi!, hivi umesikia kwua kuna wanafunzi wengi wamepasi primary lakini hawana shule za kwenda form one?

FMES, heshima kwako.

Ni kweli taifa linadidimia,na tuko hapa kutokana kuwa na taasisi dhaifu za kisiasa, zilizokosa uwezo wa kutambua na kuyapa ufumbuzi haya maswala mchomo.

Tunaweza kujadili maswala mazito kile siku lakini kama taasisi zetu za kisiasa hazina uwezo au nia ya kupokea masuala haya na kufanyia kazi, mijadala yetu itakuwa haileti matokeo tarajiwa.

Mjadala huu si wa "usimba na Yanga", hapa tunajaribu kuimarisha taasisi za kisiasa. Tunatambua mazuri waliofanya. iwapo kipo chama kilichofanya vema zaidi ya CHADEMA kwa mwaka 2008 kitajwe .

Ikiwa tunataka kuimirisha vyama vyetu ni vyema basi tukaanza kutambua pale wanapofanya vyema kuliko kuwekeza katika kukosoa tu, Hasa tukitambua mengi wanayofanya wengine hatuwezi kuthubutu.
 
Mkuu Mkandara, sidhani kuwa una data zozote zinazoonyesha kuwa Kikwete haungwi mkono na wenzake ndani ya CCM katika kushughulikia mafisadi. Nasema hivyo kwasababu sijasikia kauli zozote za wanachama wake wakipinga jitihada hizo zaidi ya zile zinazounga mkono.

Mimi ningeunga mkono hoja ya CHADEMA kuwa chama bora zaidi kama hoja ingeainisha mafanikio kwa mapana zaidi. Kama ingetolewa tathmini ya idadi kubwa ya uungwaji mkono (kwa kupata wanachama zaidi) ama kuonyesha makisio ya maandalizi yanayoeleweka zaidi kuhusiana na jinsi wanavyotegemea kushinda chaguzi zijazo. Nimesikitishwa kusikia kuwa mgombea wao Mbeya ameshindwa kula kiapo kama inavyotakiwa. Hiyo inadhihirisha tu kuwa hawako tayari kushinda chaguzi kama lilivyo kusudio la kuundwa kwa chama hicho.

Siamini kuwa kazi ya Chama cha siasa ni kuisimamia serikali. Maamini kuwa kazi yake ni kupata wanachama wengi iwezekanavyo na kushinda uchaguzi kila inapotakikana. Nadhani ndio maana wachangiaji wengi wanashindwa kukubaliana na hoja kuwa CHADEMA inastahili kuwa chama bora zaidi kwa mwaka 2008. Operation za CHADEMA sio mafanikio, ni jitihada. Matokeo ya jitihada hizo ndio zinazoweza kuwa mafanikio.

Nakubali kuwa CHADEMA imetoa msisimko mkubwa kulinganisha na vyama vingine vya upinzani kisiasa katika kipindi husika (mwaka 2008). Ila hiyo haitoshi kukipa nafasi ya ubora kuliko vyama vyote (CCM ikiwepo).

Bado jitihada zinahitajika kukifanya kiwe bora zaidi. Ushindi uko kwenye kura. Na wananchi ndio waamuzi. Kazi kwenu wana CHADEMA.

Ndugu yangu Recta:
1. Chama kinasubiri kushika uongozi kina jukumu la kuiwajibisha serekali hasa mda ule kinapokuwa hamna uchaguzi.Ndio maana Bungeni tuna mawaziri kivuli.Vyama lazima vitoe mbadala na kuwa "watchdogs"

2. Wakati ambapo hakuna uchaguzi nguvu ya chama inajionyesha katika namna ambavyo kinawafikiwa wananchi, kuweza kuibua masula yenye kulinda maslahi ya taifa na shughuli za kiuenezi.Tatizo hatuna kura za maoni za mara kwa mara zingetusaidia kuonyesha viwango vya kukubalika miongoni mwa vyama.

3. Ushindi wa Tarime ni kipimo kizuri na kilelezo cha kukubalikwa kwa chama haswa ukizingatia rekodi za chaguzi ndogo. Suala la mbeya ni kweli ni doa kubwa lakini haliwezi kubadilisha rangi nzima ya bahari ya mafanikio ya CHADEMA kwa mwaka 2008. Wanachama wengi sana wanadelea kuvunwa katika operesheni sangara.

4. Ni kweli wanachofanya CHADEMA NI"jitihada". Zinapaswa kutambuliwa. Maana wamefanikiwa kutafsiri majukumu ya chama cha upinzani kunapokuwa hamna uchaguzi. Mwaka huu tuna uchaguzi wa serekali za mitaa utasaidia kutoa picha kamili ya matokeo ya jitihada hizi.

5. Ikiwa CHADEMA haistahili kuwa chama bora nani anastahili?
 
Ndugu yangu Recta:
1. Chama kinasubiri kushika uongozi kina jukumu la kuiwajibisha serekali hasa mda ule kinapokuwa hamna uchaguzi.Ndio maana Bungeni tuna mawaziri kivuli.Vyama lazima vitoe mbadala na kuwa "watchdogs"

2. Wakati ambapo hakuna uchaguzi nguvu ya chama inajionyesha katika namna ambavyo kinawafikiwa wananchi, kuweza kuibua masula yenye kulinda maslahi ya taifa na shughuli za kiuenezi.Tatizo hatuna kura za maoni za mara kwa mara zingetusaidia kuonyesha viwango vya kukubalika miongoni mwa vyama.

3. Ushindi wa Tarime ni kipimo kizuri na kilelezo cha kukubalikwa kwa chama haswa ukizingatia rekodi za chaguzi ndogo. Suala la mbeya ni kweli ni doa kubwa lakini haliwezi kubadilisha rangi nzima ya bahari ya mafanikio ya CHADEMA kwa mwaka 2008. Wanachama wengi sana wanadelea kuvunwa katika operesheni sangara.

4. Ni kweli wanachofanya CHADEMA NI"jitihada". Zinapaswa kutambuliwa. Maana wamefanikiwa kutafsiri majukumu ya chama cha upinzani kunapokuwa hamna uchaguzi. Mwaka huu tuna uchaguzi wa serekali za mitaa utasaidia kutoa picha kamili ya matokeo ya jitihada hizi.

5. Ikiwa CHADEMA haistahili kuwa chama bora nani anastahili?

Mkuu Eric, ni vigumu kusema chama gani ni bora kuliko kingine. Ili kusema kuweza kusema chama bora zaidi ni kipi, inahitajika tathmini makini zaidi ya uliyoitoa mwanzo wa mada hii. Tathmini uliyoitoa inaelezea mambo machache makubwa yaliyofanywa na CHADEMA mwaka 2008, na wala haitoshi kukipa chama hicho sifa ya kuwa bora zaidi. Mimi sina chama ninachoweza kukipa sifa hiyo. Wanaoweza kutoa tathmini za kutosha wanaweza kunishawishi.

Ushindi wa Tarime umevuta hisia kubwa. Ila kwa maoni yangu ulikuwa ushindi dhahiri. Doa kubwa katika kushindwa hata kukidhi matakwa ya uchaguzi linachafua bahari (kama unavyoiita) ya mafanikio yoyote yaliyopatikana. Nilitarajia CHADEMA ingefanikiwa kupata ushindi pia Mbeya. Kwakuwa hilo sasa haliwezekani, basi tusubiri matokeo ya serikali za mitaa, kama unavyosema. Ila bado kazi ni kubwa kwa CHADEMA kushinda kama unavyotarajia. Maana, sina uhakika na uwezo uliojengwa wa kushinda kwa kiasi kikubwa katika chaguzi hizo. Inawezekana CHADEMA ikapata viti vingine vichache zaidi, ila sio vingi kama unavyotarajia.
 
Chadema Chama Bora 2008

I congratulate Eric Ongara for a well researched, balanced review of Chadema's performance in 2008. And I dare say that Kibunango's rash remarks disqualify him as a "Senior Expert Member" of JF.

Inspite of the fact that Chadema's nominee for the Mbeya Vijijini constituency seemed to have been over-confident and ignored the strict letter of the law on Uchaguzi, I trust Chadema will continue with the Sangara Campaign. It should also bear in mind that its detractors will always find whatever loopholes exist in their Chadema's acts and utterances in order to stall the march to genuine democracy. Its candidates must therefore strictly follow the word and letter of the law, esp. when seeking nominations which may unseat the mafisadi and their cohorts.

Although Bubu Ataka Kusema is not a Member of Chadema, he has spoken well. I join him in urging Zitto, Slaa, Mbowe, Mnyika and the other members of Kizazi Kipya to maintain the tempo in imparting and infusing courage to the people of Tanzania so that they decide what is good for them inspite the manipulations and manouvres of chama tawala. Ensure that 2009 becomes even a better year than 2008 for Chadema. Hakuna Kulala Mpaka Kieleweke.




Kilasara (Junior Member, JF)
 
Yaani mtu mmoja anatoka huko alikotoka na kuja kusema Chadema chama bora,na vigezo vyake vya ajabu ajabu! Ni lazima nitamwona kuwa yupo ndotoni tu!

Basi watakuwa wamajitahidi, maana pamoja na kudaiwa kuwa na UKABILA na mwenyekiti wao kutumia funds za ruzuku kwa madie ya kujilipa madeni yanadaiwa hayana kichwa wala miguu na bado wameibuka kidede?, KAZI ipo.

Au kwakuwa WAMEKOMBOA JIMBO walilokuwa WAMELISHIKILIA?

Swali la msingi ni vigezo vilivyotumika mpaka kikawa hivyo.
 
Recta,
Umezungumzia kuhusu Uhakika wa Kikwete kuungwa mkono ndani ya CCM...
Mkuu labda hujanisoma vizuri swala langu.. NI hivi kama rais wetu akiwa kiti cha Ikulu ameweza kuwashusha viongozi kibao na wengine kuwa mahakamani lakini anapovaa magwanda yake ya Chama yaani CCM tunamwona akifuata taratibu za chama chake - KUBEBANA..

Sasa ktk swlaa la Utawala mzima kuna hata viongozi wa vyama vya Upinzani wamempa kura zao ktk swala la Mafisadi na wengine wanaona haitoshi bado..hivyo pengine hawaoni kama kafanya kitu.. Hii haina maana kwamba Kikwete as The President has done nothing na ndio maana tunaweza kusema Kikwete amefanikiwa zaidi ktk kipindi chake kuliko Mkapa au Mkapa alifanikiwa zaidi kuliko Kikwete.. NI vipimo vya watu hawa kama marais na sio chama CCM.
Binafsi sasa hivi sina wasiwasi tena na Kikwete naona anafanya mambo ingawa taratibu sio kwa kasi mpya!..amerudisha tumaini langu sana kwa sababu mimi naamini kabisa kwamba Tanzania haiwezi kupiga hatua mbele kama Ufisadi hautashughulikiwa. Kwa kila hatua moja mbele tutarudi nyuma hatua mbili nyuma, kuna wenzangu wengine wanaona tofauti kuwa mafisadi sio tatizo ila uwezo wetu kuzalisha..

Anyway, kama kuna wajumbe wa CCM wanaomuunga mkono Kikwete kuchukua hatua ndani ya chama ingekwisha fanyika isipokuwa ni watu wachache sana na pengine hawana nguvu kabisa..Kukipandisha chart chama CCM ktk Ubora, ni pale watakapo fanya mambo ambayo ni BORA kwa wananchi.. Hao kina Mramba washtakiwa bado wanaendelea na Ujumbe, Ubunge na kadhalika wakati wewe hapo Recta ukikisiwa tu kuwa una scandal kazini acha kufikishwa mahakamani huna kazi U will be fired or suspended..na kama ni daktari basi liseni yako itafungiwa hadi pale maamuzi ya mahakama yatakapo toa hukumu ya kesi yako, iweje hawa mafisadi bado ni wawakilishi na wajumbe wa chama kama kweli tunataka kupima Ubora wa chama hiki CCM.
 
Recta,
Umezungumzia kuhusu Uhakika wa Kikwete kuungwa mkono ndani ya CCM...
Mkuu labda hujanisoma vizuri swala langu.. NI hivi kama rais wetu akiwa kiti cha Ikulu ameweza kuwashusha viongozi kibao na wengine kuwa mahakamani lakini anapovaa magwanda yake ya Chama yaani CCM tunamwona akifuata taratibu za chama chake - KUBEBANA..

Sasa ktk swlaa la Utawala mzima kuna hata viongozi wa vyama vya Upinzani wamempa kura zao ktk swala la Mafisadi na wengine wanaona haitoshi bado..hivyo pengine hawaoni kama kafanya kitu.. Hii haina maana kwamba Kikwete as The President has done nothing na ndio maana tunaweza kusema Kikwete amefanikiwa zaidi ktk kipindi chake kuliko Mkapa au Mkapa alifanikiwa zaidi kuliko Kikwete.. NI vipimo vya watu hawa kama marais na sio chama CCM.
Binafsi sasa hivi sina wasiwasi tena na Kikwete naona anafanya mambo ingawa taratibu sio kwa kasi mpya!..amerudisha tumaini langu sana kwa sababu mimi naamini kabisa kwamba Tanzania haiwezi kupiga hatua mbele kama Ufisadi hautashughulikiwa. Kwa kila hatua moja mbele tutarudi nyuma hatua mbili nyuma, kuna wenzangu wengine wanaona tofauti kuwa mafisadi sio tatizo ila uwezo wetu kuzalisha..

Anyway, kama kuna wajumbe wa CCM wanaomuunga mkono Kikwete kuchukua hatua ndani ya chama ingekwisha fanyika isipokuwa ni watu wachache sana na pengine hawana nguvu kabisa..Kukipandisha chart chama CCM ktk Ubora, ni pale watakapo fanya mambo ambayo ni BORA kwa wananchi.. Hao kina Mramba washtakiwa bado wanaendelea na Ujumbe, Ubunge na kadhalika wakati wewe hapo Recta ukikisiwa tu kuwa una scandal kazini acha kufikishwa mahakamani huna kazi U will be fired or suspended..na kama ni daktari basi liseni yako itafungiwa hadi pale maamuzi ya mahakama yatakapo toa hukumu ya kesi yako, iweje hawa mafisadi bado ni wawakilishi na wajumbe wa chama kama kweli tunataka kupima Ubora wa chama hiki CCM.
 
Anyway, kama kuna wajumbe wa CCM wanaomuunga mkono Kikwete kuchukua hatua ndani ya chama ingekwisha fanyika isipokuwa ni watu wachache sana na pengine hawana nguvu kabisa..Kukipandisha chart chama CCM ktk Ubora, ni pale watakapo fanya mambo ambayo ni BORA kwa wananchi.. Hao kina Mramba washtakiwa bado wanaendelea na Ujumbe, Ubunge na kadhalika wakati wewe hapo Recta ukikisiwa tu kuwa una scandal kazini acha kufikishwa mahakamani huna kazi U will be fired or suspended..na kama ni daktari basi liseni yako itafungiwa hadi pale maamuzi ya mahakama yatakapo toa hukumu ya kesi yako, iweje hawa mafisadi bado ni wawakilishi na wajumbe wa chama kama kweli tunataka kupima Ubora wa chama hiki CCM.

Nakubaliana nawe kwa kiasi kidogo Mkuu Mkandara.

Nadhani kinachoendelea ni ufuataji wa sheria na taratibu za utekelezaji wa kitaalamu unaotakiwa kufanywa na taasisi zinazohusika na kuchukua hatua za kuhakikisha Mafisadi wanashughulikiwa kwa usahihi. Mkuu utakubaliana na mimi kuwa Rais mwenye ustaarabu, hekima na anaejua wajibu wake, hawezi kuingilia utendaji wa wataalamu wake hasa kama anaona wanaendelea kutekeleza wajibu wao vizuri. Speed kubwa ya utekelezaji wa masuala yanayohusu haki, inaweza kuwanyima haki wahusika (washitaki/washitakiwa) katika utetezi mahakamani.

Mkuu Mkandara, natumaini pia unafahamu kuwa mtuhumiwa sio mkosefu mpaka itakapothibitishwa kuwa kweli alikosea. Kuna taratibu za kumsimamisha Mjumbe/Mbunge na hata Mfanyakazi kuzingatia sababu za kufanya hivyo. Ingekuwa taasisi anayoihudumia (Mjumbe/Mbunge) ndio inayomshitaki, ingebidi imsimamishe utumishi kwa sababu ya kuruhusu uchunguzi huru ama kuzuia uendelezo wa madhara anayotuhumiwa nayo ama sababu nyingine kama hizo. Naamini Sheria ina jinsi ya kuitumia (technicalities) ambazo zikikiukwa zinaweza kumnyima haki mshitakiwa ama mshitaki.
 
CHama kilicho bora ni kile ambacho kilishindwa kuwa na migogor mikobwa ya wao kwa wao.Rejea ugomvi mkuwa sana wa ndugu yangu Marehemu Chacha Wangwe na Mbowe ambao ulipelekea Mbowe kurudi kwa lazima Nchini baada ya kuona chama kinataka kupokonywa.

nakumbuka kilikuwa kipindi kibaya sana kwa mbowe sababu alikuwa tayari kehsafel shule baada ya kushindwa kusaidiwa na vijana wake kina ngurumo na Kitila.
 
sasa we kibunango naona unaleta ubishi tu kama alivyowahi kusema Mkapa unawivu wa kike wewe...!!

Mpaka sasa kama upo timamu kweli lazima ukubali CHADEMA ndiyo chama makini cha siasa nchini...sijui kikikua zaidi itakuwaje...

CCM inaringia pesa...lakini haina future...angalia vijana wake vilaza watupu..cheki vichwa vya maisha na siasa vilivyojaa katika CHADEMA wewe acha kupumua humu ati oohh nini chama makini ni CHADEMA tuuuu now!!!
 
MkamaP,
nadhani Eric amekujibu vizuri labda mimi nifafanue zaidi.
Aloyafanya Kikwete ni kinyume cha matakwa ya wanachama au chama CCM.. Kuna watu wacheche sana wanaounga mkono Kikwete ktk maswala yote ikiwa ni pamoja na swala la Lowassa, kuvunja baraza la Mawaziri, Kuwapeleka mahakamani kina Jeetu, Mramba na Yona..Kila siku tunaona michango ya watu humu wakilaani kukamatwa kwa hao na wengine..
Kwa hiyo kama maswala haya yote yangepigiwa kura ndani ya chama Kikwete angeungana na watu wachache sana niliowataja hapo nyuma..
Mkuu Mkandara nafikiri uko dunia nyingine.
Unahitaji ridhaa ya nani kumpeleka mhalifu kwa pilato?
Jamaa waendelee kufidsadi tu. Katika hili la kuwapeleka mahakamani wahujumu uchumi wacha mahakama iamue,na give JK the pat on the back he deserves bwana!
CHADEMA hata hivyo lazima kipongezwe kwa kupigia kelele suala hili la ufisadi ndani ya serikali, suala ambalo CCM imeshindwa kulishikia bango.
 
CHama kilicho bora ni kile ambacho kilishindwa kuwa na migogor mikobwa ya wao kwa wao.Rejea ugomvi mkuwa sana wa ndugu yangu Marehemu Chacha Wangwe na Mbowe ambao ulipelekea Mbowe kurudi kwa lazima Nchini baada ya kuona chama kinataka kupokonywa.

nakumbuka kilikuwa kipindi kibaya sana kwa mbowe sababu alikuwa tayari kehsafel shule baada ya kushindwa kusaidiwa na vijana wake kina ngurumo na Kitila.

Gembe unapaswa kuwa juu ya haya unayoyaandika hapa! Zilie ni Hitilafu za kawaida kwenye taasisi za kibinadamu. Mgogoro wa marehemu Wangwe ulikuzwa na watu wenye hofu na nia mbaya dhidi ya CHADEMA.

marehemu Wangwe alikuwa peke yake akishambulia viongozi wenzanke, tungeweza kuita mgogoro mkubwa kama ungefikia hatua ya kuleta mgawanyo ambao kweli ungetishia uhai wa chama kwa kukigawanya katika vipande viwili,hilo halikuwepo, watu waliendelea kufanya kazi kama kawaida. Haukuwa na athari kubwa ndani ya chama, bali nje uliumbwa na kukuzwa kwa minajili ya kufuraisha wapinzani wa CHADEMA.

Namna walivyoutatua suala la marehemu wangwe na kufauata taritibu za kichama na kufanya maamuzi ya kijasiri kumsimamisha mmoja wa viongozi wa juu ni kipimo cha uwezo wa kiuongozi.

Unaweza kulinganisha sakata la Nape Hatua zilizochukuliwa dhidi yake ndani ya UVCCM na NEC kushindwa kutoa ufumbuzi. Kama mgogoro mkubwa basi ni CCM ambapo tunaambiwa kuna timu inajiandaa kumn'goa JK 2010! Hii ndio mgogoro mikubwa maana inakipasua chama katikati!

Tena wakaamua kugeuza wagombea wa uchaguzi wa UVCCM chini juu, eti wa makamu wanakuwa wenyeviti na wenyeviti wanagombea umakamu! Huu ndio uongozi unaogopa kuyakabili mambo kama yalivyo.Unaamua kuyageuza ili uyaangalie kinyumenyume. Tena angalia sakata la wagombe wa UWT, na ya kufunga mwaka; CHADEMA wanaweza kuwa walitofautiana kimtazamo lakini hawakufikia hatua ya kutoleana nguo za ndani kama ilivyo kwa CCM mbeya.

Migogoro haipo CHADEMA,ingawa wapo ambao wangependa iwe hivyo. Na la pili ubora wa chama hujidhihirisha kwa kuangalia uwezo wa kuitatua, hasa ubora wa hatua zenyewe! Huu ndio ubora wa CHADEMA.
 
Back
Top Bottom