William Mshumbusi
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 1,792
- 2,421
- Thread starter
- #61
William,
inawezekana umeandika kwa jazba au kishabiki tu au hata kwa kutojua, hiyo ndiyo siasa unaangali upenyo unaoweza kuwafanya wananchi wakuelewe na unasimamia hapo na kwa Chadema naona wanafanikiwa, kila likitokea tatizo wanawaeleza wananchi na wananchi wanauona ukweli, huwezi kuwaeleza wanachi maneno tu bila kuwapa mifano. Ufisadi wanona, ndio chanzo cha huduma duni za kijamii, wanafunzi kufeli ni kwa sababu ya uongozi bomu! na mambo mengine mengi!
Kuhusu waziri kujiuzuru huku ni kuwajibika na kwa mtu mwenye busara matokeo mabovu kabisa miaka mitatu mfululizo anaachia ngazi mwenyewe bila hata kusubiri, na hapa ndipo tungepata mahala pa kuanzia kutatua tatizo. waziri amekuwepo kwa muda sasa kwenye wizara hiyo na matokeo mabovu sana katika nchi hii yametokea kipindi chake hivyo hana mbinu za kutatua matatizo ingawa anayajua na dawa yake ni yeye kupisha mtu mwingine mwenye uwezo;
Pia nikukumbushe kwamba Chadema wanafanya uchunguzi na utafiti wa mambo mengi sana na ndio maana wanaibua uvundo mwingi sana serikalini na ndiyo sababu ya nyie kuichukia zaidi Chadema kuliko vyama vingine vyote; wanatafiti wanakuja na tafiti makini bungeni mnazizima! wakienda kuwaeleza wananchi wenye nchi yao mnatumia polisi kuwazima, sasa unataka watumie mbunu zipi!?
Tusiwe Majuha jamani nchi yetu nzuri inateketea chini ya utawala wa ccm na sisi tumekaa kimya tu tukiangalia! kisa mimi ninapata kila kitu sina tatizo! huu ni ubinafsi tu! mamilioni ya watanzania wanaishi kwa shida na taabu wakati nchi yao tajiri sana, nchi inashindwa kutoa huduma bora za kijamii kwa wananchi wake! tukataeni mambo haya ndugu zangu! msikubali kutumiwa na hawa wafujaji wa mali za umma! hivi umeshaona hawa watu wanavyofuja mali za nchi hii! na hapa hatuongelei hao waliojuu tu hata waliochini ni tatizo, 60% ya fedha za serikali zinatumiwa kwa mambo ya hovyo kabisa kwa sababu hakuna mfumo mzuri wa kusimamia fedha na hakuna uwajibikaji, kila kitu ni chini ya kiwango, hatuko makini kuhakikisha fedha yetu inafanya kazi kwa tija na kwa viwango! tunafanya mizaha tu! kila mtu anapiga dili tu! tutabaki nyuma sana!
TUSIWE WABINAFSI TUAMKE TUTETEE JIMII NZIMA YA WATANZANIA.
ujumbe mzuri Je unamfikiaje na mtu asiyejua Jamii folumu na asiyehudhuria mikutano ya hadhara akiamini siasa ni ulongo.
Mbinu duni za kujieneza hizi