CHADEMA bado mno Kupambana na CCM

CHADEMA bado mno Kupambana na CCM

im happy kuwa deep inside u unaikubali chadema, dat z nice wape kura yako kila kitu kitaeleweka sera zipo na zinatekelezeka ndo maana magamba nyingine wanaziiba na kutekeleza. GO CDM
 
Umeandika vema na umetoa hoja yako ingawa na wewe huo utafiti wako wa hoja una ombwe la ushabiki so you are not a researcher kwa sababu umeweka ushabiki na si reasonable doubt, umeelezea matatizo pasi na searching a doubtful answer. kifupi umeenda nje ya mwiko mmoja mkuu; ''without reseach no opinion adherence''. This is the room of great thinkers, think.
 
Ndugu yangu hiki chama uwa hakikosolewi na chama cha Mitume.
Tunakubali makosa, sasa tunashughulika mpaka utakimbia makazi. Yaani ukiona bendera ya CDM utakuwa unakimbia. Muulize William.
 
Umeandika vema na umetoa hoja yako ingawa na wewe huo utafiti wako wa hoja una ombwe la ushabiki so you are not a researcher kwa sababu umeweka ushabiki na si reasonable doubt, umeelezea matatizo pasi na searching a doubtful answer. kifupi umeenda nje ya mwiko mmoja mkuu; ''without reseach no opinion adherence''. This is the room of great thinkers, think.
Kubali yaishe, si ni kuongeza M4C tu.
 
William Mshumbusi,badala ya kuilaumu CHADEMA hebu jifikirie umeifanyia nini nchi yako kulingana na maelezo yako.Inawezekana hata kelele hupigi basi nafuu hata CHADEMA wanapiga kelele kumuamsha mwenye nyumba usingizini.

Unaweza ukadhani kelele zipigwazo na CHADEMA hazina msingi lakini isingekuwa kelele hizo basi hata wewe usingekasirika na kutoa ujumbe wako ili tuujadili.

Kwangu mimi upinzani unaweza ukajengwa na kuamua kwa dhati kabisa kwamba tupunguze nguvu ya serikali kwa kubana nafasi za wabunge nyingi ziende kwa upinzani ili ule ujinga wa serikali wa waliokubali wameshinda utakwisha na yote ya ubadhirifu wa mali ya umma utapungua sababu mhimili mmoja wa kuibana serikali utakuwa na nguvu.Lakini kwenye hili vyama vyote vinapigania vipate rais hatutafika kule tunakoenda.

Sisi sote watanzania( mimi,wewe na yule) bila kujali itikadi ya vyama tunajukumu la kuiwezesha nchi yetu kutowachagua wale wote tunaowaona hawafai kuwa viongozi kwa sababu za wizi wa mali ya umma,udini,uwongo,unyanyasaji.na mengineyo.
 
Tuseme yote lakini roho yangu haitatulia, kwanza mpaka CCM iwe imetoka madarakani, maana walicho isha tufanya...basi tu...
 
Ndugu yangu hiki chama uwa hakikosolewi na chama cha Mitume.

Mtume mmoja tu ndie hataki kukosolewa, ukimkosea wafuasi wake watakushikisha adabu!!!
Wengine unawakosoa tu....labda ungesema..hakikosolewi kama mtume fulani!..
 
William Mshumbusi

Huu ni mgando wa mawazo hata kwa moto wa kuyeyushia chuma hauwez yeyusha..hiv unaposema wewe ni kiongoz kazi yako ni nin.,wewe kwa akil zako za manati ya mmbu unaona uongoz wako unasimamia na ku-provide vizur mahitaji ya watu,iyo mitihan alisahisha mwanafunzi au.,iyo migogoro katika jamii walianzisha nani kama walikuwa hawaipendi na mbaya zaidi kwa nin hawashughulik na miziz wanakimbilia matawi

...ukiona unapigwa mawe ujue watu wamekuchoka ni wiz wako ila ukipona hutaiba tena bali utatatua matatizo yako kwa kuangalia mzizi wake..
 
Last edited by a moderator:
Kiongozi form 4 unatarajia nini.Elimu ni muhimu jamani
 
mmetuchosha sasa always cdm, cdm.vyama vya siasa vipo 20 na zaidi why cdm, cdm kila mda aaaahhhhhhhhh
 
Mbinu za CHADEMA kujieneza haziridhishi na inaonekana wazi hakifanyii utafiti matatizo yaliyopo nchini na matatizo makubwa yaliyofichika.

Bali kuja kushinikiza maamuzi juu matokeo ya matokeo ya tafiti au taarifa zinazotolewa na vyombo vya selikali zinazoonesha madhaifu ya sekta fulani mifano:
Mushumbusi unadhani hiyo ni kazi ya CHADEMA! au chama chochote cha siasa? Chama kitakachofanya hivyo kitakuwa kinaisaidia CCM iendelee kuwa madarakani. Wewe mwenyewe umetaja masuala kama tisini hivi, maana yake huwezi kufanya tafiti tisini ili ubadilishe sera. Chama cha siasa kitapata wapi fedha za kufanya tafiti hizo? Kutokana na maelezo yako ni kuwa kinachotakiwa ni kukiondoa chama kilichopo madarakani ili Chama kingine kichukue nafasi ya kurekebisha hayo tisini uliyoainisha. CDM kwa mantiki hiyo kifanye kazi ya siasa ya kushinikiza CCM iachie ngazi ili washike dola na wakabiliane na changamoto zilizopo.
 
William,

inawezekana umeandika kwa jazba au kishabiki tu au hata kwa kutojua, hiyo ndiyo siasa unaangali upenyo unaoweza kuwafanya wananchi wakuelewe na unasimamia hapo na kwa Chadema naona wanafanikiwa, kila likitokea tatizo wanawaeleza wananchi na wananchi wanauona ukweli, huwezi kuwaeleza wanachi maneno tu bila kuwapa mifano. Ufisadi wanona, ndio chanzo cha huduma duni za kijamii, wanafunzi kufeli ni kwa sababu ya uongozi bomu! na mambo mengine mengi!

Kuhusu waziri kujiuzuru huku ni kuwajibika na kwa mtu mwenye busara matokeo mabovu kabisa miaka mitatu mfululizo anaachia ngazi mwenyewe bila hata kusubiri, na hapa ndipo tungepata mahala pa kuanzia kutatua tatizo. waziri amekuwepo kwa muda sasa kwenye wizara hiyo na matokeo mabovu sana katika nchi hii yametokea kipindi chake hivyo hana mbinu za kutatua matatizo ingawa anayajua na dawa yake ni yeye kupisha mtu mwingine mwenye uwezo;

Pia nikukumbushe kwamba Chadema wanafanya uchunguzi na utafiti wa mambo mengi sana na ndio maana wanaibua uvundo mwingi sana serikalini na ndiyo sababu ya nyie kuichukia zaidi Chadema kuliko vyama vingine vyote; wanatafiti wanakuja na tafiti makini bungeni mnazizima! wakienda kuwaeleza wananchi wenye nchi yao mnatumia polisi kuwazima, sasa unataka watumie mbunu zipi!?

Tusiwe Majuha jamani nchi yetu nzuri inateketea chini ya utawala wa ccm na sisi tumekaa kimya tu tukiangalia! kisa mimi ninapata kila kitu sina tatizo! huu ni ubinafsi tu! mamilioni ya watanzania wanaishi kwa shida na taabu wakati nchi yao tajiri sana, nchi inashindwa kutoa huduma bora za kijamii kwa wananchi wake! tukataeni mambo haya ndugu zangu! msikubali kutumiwa na hawa wafujaji wa mali za umma! hivi umeshaona hawa watu wanavyofuja mali za nchi hii! na hapa hatuongelei hao waliojuu tu hata waliochini ni tatizo, 60% ya fedha za serikali zinatumiwa kwa mambo ya hovyo kabisa kwa sababu hakuna mfumo mzuri wa kusimamia fedha na hakuna uwajibikaji, kila kitu ni chini ya kiwango, hatuko makini kuhakikisha fedha yetu inafanya kazi kwa tija na kwa viwango! tunafanya mizaha tu! kila mtu anapiga dili tu! tutabaki nyuma sana!

TUSIWE WABINAFSI TUAMKE TUTETEE JIMII NZIMA YA WATANZANIA.
 
  • Thanks
Reactions: Pai
Mushumbusi unadhani hiyo ni kazi ya CHADEMA! au chama chochote cha siasa? Chama kitakachofanya hivyo kitakuwa kinaisaidia CCM iendelee kuwa madarakani. Wewe mwenyewe umetaja masuala kama tisini hivi, maana yake huwezi kufanya tafiti tisini ili ubadilishe sera. Chama cha siasa kitapata wapi fedha za kufanya tafiti hizo? Kutokana na maelezo yako ni kuwa kinachotakiwa ni kukiondoa chama kilichopo madarakani ili Chama kingine kichukue nafasi ya kurekebisha hayo tisini uliyoainisha. CDM kwa mantiki hiyo kifanye kazi ya siasa ya kushinikiza CCM iachie ngazi ili washike dola na wakabiliane na changamoto zilizopo.

kidogo nimekuelewa lakini CHADEMA bado haijaibua kero nyingi kama chama kikuu cha upinzani zaidi ya kukoment juu ya tafiti na chunguzi za taasisi za kiserekali
 
hayo yote uliyoyasema ndio kinachofanywa na cdm,na wala sio kuparamia hija pekee,mfano usipojadili ripoti ya CAG,ambayo ni ya kitaalamu unataka wajadili nini,matatizo ya walimu,na miundo mibovu ya secta nyingine pamoja na uwajibikaji mbovu,ndicho kinachohubiliwa majukwaani na cdm,na wala sio kudandia hoja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom